Tuliowahi kufukuzwa kazi tukutane tupeane experience

Tuliowahi kufukuzwa kazi tukutane tupeane experience

mm sijawahi kufukuzwa,Ila niliwahi kubembelezwa ni resign nikasita kwa muda mrefu baadae nikaamua kukubali ku resign.Ilikuwa hiv ,baada ya kumalizia tu chuo,niliingia kitaa kusaka kazi,nikatumia wk 2 kuzurula mtaani na kibahasha changu Cha vyeti, world vision nilifika lkn wakanpa maneno ya kunifarj lkn nikaona hapa bila mtu sipat kaz nikaachana nao,Kama zali wk ya pili nikapewa mchongo Kuna project mpya shirika fulani hv Iina launch project mpya, iliitwa LEAD project donors wakiwa UK,jamaa Kama masihara wakanichukua kwa mkataba wa miaka 4,ilikuwa 2013yr hiyo,waka nipost mbeya nikagoma,wakanibembeleza weeee nikagoma nakumbuka tuligoma vituo watu 2,mm na jamaa mmoja kutoka tanga aliitwa Jonas,siku hiyo walipangiwa wote pamoja na jamaa angu,kasoro mm,wakaniambia Rudi baadae tutakupigia sm nikawaambia poa,kweli nikarudi zangu home,usiku saa tano manager wa mladi akanipigia sm,kuwa wamenipa iringa nikamwambia poa nitaenda,Nika join iringa,nikiwa kule nilikuwa situlii kila mala naingia internet kuchek mashirika mengine,maana nilijua private sector Kuna michezo michafu na rafu nyingi,muda wowote kinaweza kunuka.

nikiwa iringa 2014,nafasi za ajira zikatoka govt,fasta nikatuma maombi , interview tuliitwa arusha,mwaka huo nikaajiriwa govt mkoa wa mbeya,wilaya ya kyela,nikawakumbuka wazungu waliokuwa wananibembeleza niende mbeya na LEAD PROJECT,nikaona nimebugi Sana kuwagomea kipnd kile.ss nikawa napga govt na LEAD PROJECT,Ila kwa Siri ,boss wangu kule gvt sikumficha maana nilijua nisipompa mchongo kupga huku na kule itakuwa inshu,uzur boss alikuwa sosho Sana,akasema dogo piga kaz usjal,Ila ukiwa unachomoka hapa nipage taarifa,nikamwambia poa .

Sasa baada ya miez 3, LEAD PROJECT HQ,wakasanuliwa na jamaa mmoja tulikuwa nae pale iringa lead project,wakawa Wana nipigia masim kibao ni resign ,nikawakazia ,nilijua hawawez kunifukuza na tayari mkataba nilisha saini.

Niliendelea kupga Kaz huku na huku,Ila kero za masm zilikuwa Mara kwa Mara,wakiniuliza ume saini Kaz govt nawabishia nawaambia hapana ,hakuna kitu Kama hicho,wakiwatuma wakuda waje iringa Kuna jamaa yangu mwngine alikuwa best wa ukweli kwangu,akawa ana nitonya fasta yy alikuwa na ndg yake HQ dar so alikuwa anapata taarifa mapema za project kutoka HQ. Jamaa walichanganyikiwa kweli,kunifukuza hawawezi ,so wakabaki kunipiga saund ni resign.

Siku moja,nikatoka iringa ,kwenda mbeya kazn govt,asbh nikiwa kyela,nikapigiwa sm,kupokea jamaa akajitambulisha yy ni manager kampuni moja inaitwa utravet ,HQ zao ziko Kenya,kwa hapa tz ni Arusha ,akaniambia natakiwa kuripoti Arusha ndani ya siku 3, nisaini mkataba na utravet ,baada ya kusaini natakiwa kwenda Kenya pale Nairobi seminar ya 2wks,akaniambia ulituma email yako tangu mwaka Jana 2013 ,nikamwambia kweli,Basi jamaa akasisitiza hapa huta piga interview yoyote ,wameiona CV yangu hawana haja kunifanyia interview,ni kusaini mkataba na kukwea piga Nairobi kwa seminar,nikirudi Nita manage mkoa wa morogoro na Dodoma,usafr kila ktu poa.

Nikampigia jamaa angu mmoja ,Kama anawajua vizuri hawa utravet ,akaniambia jamaa Kama wamekuita nenda ,wako vzr Sana Tena Sana,Kuna vijipesa vya kipuuzi puuzi kibao .akanipa na contact ya best ake ambae alikuwa bado anapiga nao Kaz mkoa wa mwanza,aise nikabaki sijui Cha kuamua.Niko bado na mkataba na LEAD PROJECT,nimeajiliwa govt ndo kwanza Nina miez Kama 3,huku napewa offer na utravet .
Sijui huwa ni nini unapokuwa huna kazi utasota kupata kazi, ukiwa nayo tu ofa zingine za kazi zinakufuata.

Ndiyo hapo utaelewa kuwa mwenye nacho huongezewa.
 
Aisee hii thread imenigusa imebidi nijiunge na jamii forum baada ya kuwa guest kwa miaka takriban 7.
Ipo hivi mwaka 2014 nilimaliza chuo na kupata degree ya Marketing.basi bwana nikakaa home mpka 2015 mwezi ya tano nikapata kazi kwenye hoteli moja jina nitalificha five star kule Toure Drive Oysterbay Wahindi kibao tena wengine hawana vibali wanakuja tz hawajua kiingereza wala kiswahili na kuwekwa humohumo ndani ya hoteli hawatoki hata njee hadi mahitaji kama ya nguo wanaomba waswahili wawasaidie kununua kko mimi na degree ya marketing niliingizwa miezi mitatu wanione kama nafaa au la basi nikafanya kazi miezi mitatu kimya sioni dalili yoyote ya kutoswa siku ya siku ya kumaliza miezi mitatu naambiwa kwaheri nikauliza sababu sikupewa, aliyenifukuza hata si HR. ni mdada Msouth Afrika machozi yalinitoka nakujiona sina bahati. baadae nafata mshahara wangu maana mshahara wa tarehe 30 unalipwa tarehe 7 mwezi unaofata Hr mdada mswahili ananiambia wewe si ulimtolea njee Msouth wa kiume. dah,kusema ukweli huyo msouth wa kiume hakunitongoza ila alianza mazoea ya kishenzi nikamkazia .fast forward 2016 nikapata kazi mshahara mara tatu zaidi ya kule na baada ya miaka miwili nikaacha mwenyewe kujiajili na pesa kidogo nilisave huku nyingine Mr akinipiga tafu.
Lesson. usikatishwe na tamaa juu ya hawa binadamu maana kama ningebaki pale huenda ningechelewa kufika hapa nilipo.
Nb.kama itatokea umeenda sehemu za hoteli kubwa kubwa usiagize chakula chenye samaki,kuku,sambusa maaana mara nyingi huwa si fresh aisee ile hoteli ilikuwa ina samaki kwenye fridge wa miezi hadi 6 huwa si fresh kama unavyodhani bora ule kwa mama ntilie.
 
Aisee hii thread imenigusa imebidi nijiunge na jamii forum baada ya kuwa guest kwa miaka takriban 7.
Ipo hivi mwaka 2014 nilimaliza chuo na kupata degree ya Marketing.basi bwana nikakaa home mpka 2015 mwezi ya tano nikapata kazi kwenye hoteli moja jina nitalificha five star kule Toure Drive Oysterbay Wahindi kibao tena wengine hawana vibali wanakuja tz hawajua kiingereza wala kiswahili na kuwekwa humohumo ndani ya hoteli hawatoki hata njee hadi mahitaji kama ya nguo wanaomba waswahili wawasaidie kununua kko mimi na degree ya marketing niliingizwa miezi mitatu wanione kama nafaa au la basi nikafanya kazi miezi mitatu kimya sioni dalili yoyote ya kutoswa siku ya siku ya kumaliza miezi mitatu naambiwa kwaheri nikauliza sababu sikupewa, aliyenifukuza hata si HR. ni mdada Msouth Afrika machozi yalinitoka nakujiona sina bahati. baadae nafata mshahara wangu maana mshahara wa tarehe 30 unalipwa tarehe 7 mwezi unaofata Hr mdada mswahili ananiambia wewe si ulimtolea njee Msouth wa kiume. dah,kusema ukweli huyo msouth wa kiume hakunitongoza ila alianza mazoea ya kishenzi nikamkazia .fast forward 2016 nikapata kazi mshahara mara tatu zaidi ya kule na baada ya miaka miwili nikaacha mwenyewe kujiajili na pesa kidogo nilisave huku nyingine Mr akinipiga tafu.
Lesson. usikatishwe na tamaa juu ya hawa binadamu maana kama ningebaki pale huenda ningechelewa kufika hapa nilipo.
Nb.kama itatokea umeenda sehemu za hoteli kubwa kubwa usiagize chakula chenye samaki,kuku,sambusa maaana mara nyingi huwa si fresh aisee ile hoteli ilikuwa ina samaki kwenye fridge wa miezi hadi 6 huwa si fresh kama unavyodhani bora ule kwa mama ntilie.
Hapa mwisho uneongea nukta muhimu sana.
 
Aisee hii thread imenigusa imebidi nijiunge na jamii forum baada ya kuwa guest kwa miaka takriban 7.
Ipo hivi mwaka 2014 nilimaliza chuo na kupata degree ya Marketing.basi bwana nikakaa home mpka 2015 mwezi ya tano nikapata kazi kwenye hoteli moja jina nitalificha five star kule Toure Drive Oysterbay Wahindi kibao tena wengine hawana vibali wanakuja tz hawajua kiingereza wala kiswahili na kuwekwa humohumo ndani ya hoteli hawatoki hata njee hadi mahitaji kama ya nguo wanaomba waswahili wawasaidie kununua kko mimi na degree ya marketing niliingizwa miezi mitatu wanione kama nafaa au la basi nikafanya kazi miezi mitatu kimya sioni dalili yoyote ya kutoswa siku ya siku ya kumaliza miezi mitatu naambiwa kwaheri nikauliza sababu sikupewa, aliyenifukuza hata si HR. ni mdada Msouth Afrika machozi yalinitoka nakujiona sina bahati. baadae nafata mshahara wangu maana mshahara wa tarehe 30 unalipwa tarehe 7 mwezi unaofata Hr mdada mswahili ananiambia wewe si ulimtolea njee Msouth wa kiume. dah,kusema ukweli huyo msouth wa kiume hakunitongoza ila alianza mazoea ya kishenzi nikamkazia .fast forward 2016 nikapata kazi mshahara mara tatu zaidi ya kule na baada ya miaka miwili nikaacha mwenyewe kujiajili na pesa kidogo nilisave huku nyingine Mr akinipiga tafu.
Lesson. usikatishwe na tamaa juu ya hawa binadamu maana kama ningebaki pale huenda ningechelewa kufika hapa nilipo.
Nb.kama itatokea umeenda sehemu za hoteli kubwa kubwa usiagize chakula chenye samaki,kuku,sambusa maaana mara nyingi huwa si fresh aisee ile hoteli ilikuwa ina samaki kwenye fridge wa miezi hadi 6 huwa si fresh kama unavyodhani bora ule kwa mama ntilie.
Nimejifunza kitu aiseeee
 
Aisee hii thread imenigusa imebidi nijiunge na jamii forum baada ya kuwa guest kwa miaka takriban 7.
Ipo hivi mwaka 2014 nilimaliza chuo na kupata degree ya Marketing.basi bwana nikakaa home mpka 2015 mwezi ya tano nikapata kazi kwenye hoteli moja jina nitalificha five star kule Toure Drive Oysterbay Wahindi kibao tena wengine hawana vibali wanakuja tz hawajua kiingereza wala kiswahili na kuwekwa humohumo ndani ya hoteli hawatoki hata njee hadi mahitaji kama ya nguo wanaomba waswahili wawasaidie kununua kko mimi na degree ya marketing niliingizwa miezi mitatu wanione kama nafaa au la basi nikafanya kazi miezi mitatu kimya sioni dalili yoyote ya kutoswa siku ya siku ya kumaliza miezi mitatu naambiwa kwaheri nikauliza sababu sikupewa, aliyenifukuza hata si HR. ni mdada Msouth Afrika machozi yalinitoka nakujiona sina bahati. baadae nafata mshahara wangu maana mshahara wa tarehe 30 unalipwa tarehe 7 mwezi unaofata Hr mdada mswahili ananiambia wewe si ulimtolea njee Msouth wa kiume. dah,kusema ukweli huyo msouth wa kiume hakunitongoza ila alianza mazoea ya kishenzi nikamkazia .fast forward 2016 nikapata kazi mshahara mara tatu zaidi ya kule na baada ya miaka miwili nikaacha mwenyewe kujiajili na pesa kidogo nilisave huku nyingine Mr akinipiga tafu.
Lesson. usikatishwe na tamaa juu ya hawa binadamu maana kama ningebaki pale huenda ningechelewa kufika hapa nilipo.
Nb.kama itatokea umeenda sehemu za hoteli kubwa kubwa usiagize chakula chenye samaki,kuku,sambusa maaana mara nyingi huwa si fresh aisee ile hoteli ilikuwa ina samaki kwenye fridge wa miezi hadi 6 huwa si fresh kama unavyodhani bora ule kwa mama ntilie.
Haya mavyakula yanakaa kwenye freezer miez 8 ndo wanatuandalia eti buffet....[emoji848][emoji848]
 
Kuna hoteli niliwahi fanya kazi ya utunza bustani wakati nasubiri majibu ya form four. Nilivyomaliza chuo nikaambiwa wananitafuta wanataka mtu wa store, nikaenda, tukakubaliana mshahara, ilikua ni 180K kwa mwezi, basi ikawa mziki mshahara ila nikakaza.

Basi bwana baada ya almost mwaka nikaitwa na meneja wa waswahili akaniambia bwana ni hivi mimi naona wewe kukulipa hatuwezi. Kichwani najiongelesha "Hawa jamaa wananilipa 180K lakini wanaona ni kubwa walitarget wanilipe sh ngapi?"

Kauli ya mwisho nikasikia "Kwahiyo tumeona tukuache" basi mambo yakawa hivyo.
Sio kule ulikimbia baada ya boss kukuambia umfanyie massage?
 
Aisee nakumbuka ilikuwa mwaka 2014 nilipata kaz shule moja ya girls nilikuwa mchapa kaz sn boss alinipenda sn maana nilikuwa nafanya kaz ya records Mambo ya Ada na michango mingne lakini nilikuwa na faida nyngn Kama sekritari hayupo nilikuwa nasmamia show za kuchapa mitihani na Mambo mengine yote ya kuprint na kuchapa sasa alikuja mzungu mmoja mdada kaleta mtoto pale shulen na mi ndo nilikuwa napokea wanafunz nakagua kama wamelipa Ada na michango mingne Yan mi nilikuwa na uwezo hata wa Kimtoa nje mwanafunz ambaye hajakamilisha ada huyo mzungu alipofka akawa ananiangalia vile nachapa kazi kwa kila anayeingia na kutoka akanikubali sana sasa alinikubali zaid pale nilipomsaidia mtoto aliyekuja naye kuingia shulen wakati hakuwa amelipa ada kwan mzungu aliniomba nimpe rist ya ada halafu kesho atanipigia cm nikachukue pesa niitumbukze bank

Kwan ye muda wa kwenda bank amekosa kabisa basi bhana kweli kesho yake alinipa ile pesa lakin akaniulza nalipwa shs ngapi nikamwambia akasema nna mkataba nikamwambia hapana bs akanambia ana kampuni ya kukodisha magari anataka nikafanye kaz kwake anilipe mara mbili ya mshahara nnaolipwa shulen nikamwambia poa
kweli nilihamia huko kwa mzungu kimbembe kilikuwa hivi

Kumbe pale ofsn kulikuwa na mdada wa kimasai anaitwa joyce ndiye alitakiwa atoke pale ofsn ahamie kwny kitengo cha masoko na jamaa wengi madereva pale ofsn walikuwa hawampendi sn daaah aisee dada alikuwa na roho mbaya kama sura yake akawa anaenda kwa waganga ili nifukuzwe kazi maana hakupenda kutoka pale ofsn kwenda kwny masoko

Mara nikute kaz nilizofanya jana yakr zmefutwa kwny pc yan majanga tu boss nae akaanza kunichukia hatari bila sababu

Mdada akawa anaomba ruhusa hata ya wiki kumbe anaenda kwa waganga ili nifukuzwe kaz amlete rafiki yake ndo aje awe wa masoko ye arudi ofsn cha ajabu kaz hawez kabsa ila ni ana mdomo hatari mwisho wa sku nilichukia kbs kaz wkend ikiisha nakosa amani kabsa aisee nakumbuka bosi aliniita sku moja mbele ya huyo dada akawa ananifokea eti simuheshimu huyo dada mara huyo dada akawa anatamba eti tatzo mi smjui ye ni nani pale ofsn mmmh bosi akanambia natakiwa kumheshimu joyce sn kama bosi nilishangaa nmuheshimu kvp mbona sielewi aisee wakati ni binti tu kijana kama mimi au nmemkosea nn yan nikawa sjui kbs ndo nikpata taarifa kwa dereva mmoja kwmb joyce anasema mi nafanya sn kaz na bosi ananikubali sn sa uwenda mbele ya safari takuja kuwa mtu mkubwa sana ukizngatia nina elimu kubwa kuliko wafanyakaz wote na nna chapa kaz hatari

Siku moja niliitwa na bosi mbele ya wafanyakaz wote ilikuwa mwisho wa mwezi nashangaa nakabiziwa mshahara wangu by cash na kuambiwa sina kaz tena pale bila sababu za msingi skuumia sn maana nilishaona vitimbwi vya joyce ila niliwambia watu pale ofsn kama Mungu Aishivyo ikiwa nmefukuzwa kaz kisa joyce tena bila kosa lolote bs joyce hatomalza miezi miwili naye atatmuliwa kweli nilipata taarifa joyce alifukuzwa kwa aibu kubwa kwa kosa la kuitia hasara kampuni hata miezi miwili haikufka

Mengne ningesema wakuu baada ya kufukuzwa ilikuaje sema naogopa kuwachosha nyie acheni tu maisha haya maisha haya stasahau nilikuwa natembea kwa mguu toka goba mpk posta au mabibo hostel kwny internet kutafuta kaz nyngn online stasahau kabisa
Pole sana mkuu,
.. Waafirka sisi ni wapumbavu sana
 
Kiongozi hii thread yako imenikumbusha machungu Makubwa sana.

Nilivomaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza bn, nikapiga kazi miezi mitatu tu nikapandishwa hadhi kidogo bana. Kazi ikaendelea, baada ya Mwaka mmoja kuisha, Kiongozi mmojawapo katika ofisi yetu akapa nafasi ya kuajiriwa serikalini, kampuni ikanipa nafasi yake. Kumbe ile hali wenzangu ambao tulikuwa tunafanya nao kazi walichukia sana. Why me?

Sijawa na hili wale like, mdogo wangu akauugua, wadogo zangu wengine walikuwa wanasoma bado secondary, so ikabidi nichukue likizo ya siku 14 kwanza nikamuuguze, bahati mbaya haikuwa riziki akafariki. Baada ya kumaliza matanga, nilirejea kazini, lakn haikuisha hata mwezi mama akaugua.

Akapelekwa hospital, akawa anakaa na dada yangu, kila wikend lazima niwe huko, nikalazimika kumhamishia kwangu (getho) pamoja na sista, afu Mimi nikawa nalala kwa mpangaji mwezangu msela. Uguza weee, hadi hela ikakata. Kazi nikiwa naendelea nayo lakini.

Basi bana nakumbuka ilikuwa Tarehe 1/10 tukaenda kuchukua mshahara, nilivyofika kwa mhasibu akanipa mshahara wangu na barua. Kuifungua, eti nimeachishwa kazi!

Kosa silijui. Basi ile hela yote nikamtibia mama, lakini haikufua dafu. Nikauza kabati la nguo laki 100,000/, nikauza sofa langu elfu 70, latop hp, 150,000,, uza king'amzi na TV, na dish lake 170,00, friji 70,000 nikaendelea kumtibia mama. Nilivyoishiwa kabisa, mama akapona!

Basi tukarejea kijijini, nikaanza kulima nyanya. Nikipeleka maombi ya ualimu hata shule za kata nakataliwa! Naambiwa nitaitwa lakn siitwi. Nyanya hakuna wanunuzi. Ikabidi nianze kuvua samaki, lkn wapi.

Wale watumishi wenzangu hata hawapokei simu yangu, kila surauali sasa hainitoshi, mwonekano umeshazidi umri wangu halisi. Nimezeeka balaa.

Sema ndo hivo siku hazifanani, nilikuja kupata pa kujishikiza na maisha yanaendelea. Lakn ukweli kuamka bila kujua pa kwenda ni shida.
 
Kiongozi hii thread yako imenikumbusha machungu Makubwa sana.

Nilivomaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza bn, nikapiga kazi miezi mitatu tu nikapandishwa hadhi kidogo bana. Kazi ikaendelea, baada ya Mwaka mmoja kuisha, Kiongozi mmojawapo katika ofisi yetu akapa nafasi ya kuajiriwa serikalini, kampuni ikanipa nafasi yake. Kumbe ile hali wenzangu ambao tulikuwa tunafanya nao kazi walichukia sana. Why me?

Sijawa na hili wale like, mdogo wangu akauugua, wadogo zangu wengine walikuwa wanasoma bado secondary, so ikabidi nichukue likizo ya siku 14 kwanza nikamuuguze, bahati mbaya haikuwa riziki akafariki. Baada ya kumaliza matanga, nilirejea kazini, lakn haikuisha hata mwezi mama akaugua.

Akapelekwa hospital, akawa anakaa na dada yangu, kila wikend lazima niwe huko, nikalazimika kumhamishia kwangu (getho) pamoja na sista, afu Mimi nikawa nalala kwa mpangaji mwezangu msela. Uguza weee, hadi hela ikakata. Kazi nikiwa naendelea nayo lakini.

Basi bana nakumbuka ilikuwa Tarehe 1/10 tukaenda kuchukua mshahara, nilivyofika kwa mhasibu akanipa mshahara wangu na barua. Kuifungua, eti nimeachishwa kazi!

Kosa silijui. Basi ile hela yote nikamtibia mama, lakini haikufua dafu. Nikauza kabati la nguo laki 100,000/, nikauza sofa langu elfu 70, latop hp, 150,000,, uza king'amzi na TV, na dish lake 170,00, friji 70,000 nikaendelea kumtibia mama. Nilivyoishiwa kabisa, mama akapona!

Basi tukarejea kijijini, nikaanza kulima nyanya. Nikipeleka maombi ya ualimu hata shule za kata nakataliwa! Naambiwa nitaitwa lakn siitwi. Nyanya hakuna wanunuzi. Ikabidi nianze kuvua samaki, lkn wapi.

Wale watumishi wenzangu hata hawapokei simu yangu, kila surauali sasa hainitoshi, mwonekano umeshazidi umri wangu halisi. Nimezeeka balaa.

Sema ndo hivo siku hazifanani, nilikuja kupata pa kujishikiza na maisha yanaendelea. Lakn ukweli kuamka bila kujua pa kwenda ni shida.
Sasa sabb ya kufukuzwa ilikuwa ni nini?[emoji848]
 
Sasa sabb ya kufukuzwa ilikuwa ni nini?[emoji848]
Hadi leo sijui sababu witnessj. Nafikir kuna mjinga mmoja alikuwa ananichawia. Maana sikuwa na kosa lolote kabisa.

Bahati mbaya na hiyo taasisi yao ilishakufa , iliniuma sana kusikia wamefilisika, kwa sababu pamoja na kwamba walinifukuza bila kosa lolote lakini ni ukweli kwamba walinisaidia kupata pa kuanzia.
 
Mm nishafukuzwa kibabe huku mfukoni Nina eflu 2 ya nauli,bank Nina elf 28,na hapo ni ktkt ya mwez,mwisho wa mwez ninatakiwa ada ya mtt private school, nimepewa barua ya kufukuzwa nikasepa,baada ya kuhangaika miez km mitano nikapata kaz mkoa mwingine,kazi ya maana kinyama,mshahara kule nilipofukuzwa ulikua 480k,nikapata kazi ya mshahara 915k take home,baada ya miez mi5 nikarud hom kusalimia,nikaonana na wafanyakaz wenzangu wa mwanzo kule nilipofukuzwa,wengi wanapongeza kuwa eti nimependeza,nimenenepa na kunidadisi nafanya kaz wapi,Mara njiani nakutana na bosi wangu yupo ndani ya gari na wafanyakazi wengine km wa3 HV,bosi akamwambia drv wake asimamishe gar akaniita na kuniuliza eti nafanya kazi gani na wapi?,,

Mara eti dah maisha umeyapatia kweli,naona umependeza km vile MD wa kampuni flani HV,nikamjibu nafanya kazi za ndani kwa mama ako kisha nikasepa zangu,.mpuuzi sana yule jamaa,hadi Leo nafanya kazi hapo hapo na mshara umepanda hadi 1.25m,na ki IST nimenunua na mjengo wangu nimemalizia.ukifukuzwa kazi unapata muda mzuri wa kutafuta kazi nzur maana bila hivyo una relax na kikazi ulichonacho na madeni kila kona

Hilo jibu ulilompa boss wako mi hoi [emoji23]
 
Kuna mfanyakazi mmoja ameachishwa kazi baada ya kupata msiba watu wameenda kumpa pole kufika wakakuta mjengo wa maana
Alivyorudi kazini anaulizwa hela ya kujenga nyumba kama hii kaipata wapi

[emoji23] binadamu hatupendani mweeee
 
Alikuwa akiumia hata ukivaa nguo mpya ofisini wanamjua waliowahi fanya nae Kazi kabla.Kuna libosi limoja lilikuwa likiumia mkila kuku ofisini.Image mtu anaumia ukila kuku au kuvaaa nguo mpya ofisini atashindwa vipi kufurahi ukifukuzwa Kazi

Duu huo muda mpaka wa kuhesabiana nguo hadi ujue leo huyu kavaa nguo mpya watu huwa wanatoa wapi?
 
Back
Top Bottom