Tuliowahi kufukuzwa kazi tukutane tupeane experience

Tuliowahi kufukuzwa kazi tukutane tupeane experience

Duuhh 2019

2016 nimemaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza, 2017 nikapewa mkataba wa mwaka mmoja moja.

Wakati naingia mambo yalienda vema sn, ila mkuu wa kitengo alikua anapenda sifa KUPITA KIASI (Kila mtu kwake ni Hopeless) hili lilinifanya nipishane nae

2019 January yeye ndio akawa mkuu wa ofisi, aisee hapo niliipata,

1. Alisema nisipewe kazi yoyote
2. Alisema mimi sijui kazi kabisa( hii ilitokana kuna mradi tulipata, nikapewa mimi niufanyie kazi, sasa wakati umefika kwenye utekelezaji yeye ndio boss ko akaninyangaya akasema nimefanya kimakosa akauchukua yeye)
3.Akawa anasema mimi ni Hopeless
4. Anakuita mbele ya watu anakutukana sanaa daahh aisee nimedhalilika sana

Nikaanza kutafuta kazi kimya kimya, Nikapata tena kwenye taasisi ya watu tuliokua tunawahudumia "ilikuaje"

Walimuuliza mkuu wangu wa kitengo wa kipindi hiki ss "mbona xxx siku hizi hatumuoni" akajibu "dah sijui wana bifu gani na mkuu, maana hataki hata kumuona"

Jamaa wakanitafuta wakanipa mkataba wa kazi nikatulia, sasa nikaandika barua ya kusitisha mkataba huku namsubiri mkuu ajichanganye..

Akaingia kwenye 18, siku hiyo akaja reception kabisa kwa watu wanaokuja kumuona akaanza sifa zake

Akamuita HR na wenzie akasema kuna watu mkataba ukiisha wasionhezewe akaniita akaanza kunisema akasema sikuongezei mkataba, nikamwambia sihitaji

Nikaingia ofisini nikachukua barua, Nikamwambia wewe ni mbwa kama wengine unastahili kutupiwa chakula, NIKAMTUPIA BARUA YA KUSITISHA MKATABA NIKAMWAMBIA OKOTO UPELEKE MASIJALA. HAKUAMINI.

Hii ni Taasisi ya Serikali, mtu anaifanya yake
 
Duuhh 2019

2016 nimemaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza, 2017 nikapewa mkataba wa mwaka mmoja moja.

Wakati naingia mambo yalienda vema sn, ila mkuu wa kitengo alikua anapenda sifa KUPITA KIASI (Kila mtu kwake ni Hopeless) hili lilinifanya nipishane nae

2019 January yeye ndio akawa mkuu wa ofisi, aisee hapo niliipata,

1. Alisema nisipewe kazi yoyote
2. Alisema mimi sijui kazi kabisa( hii ilitokana kuna mradi tulipata, nikapewa mimi niufanyie kazi, sasa wakati umefika kwenye utekelezaji yeye ndio boss ko akaninyangaya akasema nimefanya kimakosa akauchukua yeye)
3.Akawa anasema mimi ni Hopeless
4. Anakuita mbele ya watu anakutukana sanaa daahh aisee nimedhalilika sana

Nikaanza kutafuta kazi kimya kimya, Nikapata tena kwenye taasisi ya watu tuliokua tunawahudumia "ilikuaje"

Walimuuliza mkuu wangu wa kitengo wa kipindi hiki ss "mbona xxx siku hizi hatumuoni" akajibu "dah sijui wana bifu gani na mkuu, maana hataki hata kumuona"

Jamaa wakanitafuta wakanipa mkataba wa kazi nikatulia, sasa nikaandika barua ya kusitisha mkataba huku namsubiri mkuu ajichanganye..

Akaingia kwenye 18, siku hiyo akaja reception kabisa kwa watu wanaokuja kumuona akaanza sifa zake

Akamuita HR na wenzie akasema kuna watu mkataba ukiisha wasionhezewe akaniita akaanza kunisema akasema sikuongezei mkataba, nikamwambia sihitaji

Nikaingia ofisini nikachukua barua, Nikamwambia wewe ni mbwa kama wengine unastahili kutupiwa chakula, NIKAMTUPIA BARUA YA KUSITISHA MKATABA NIKAMWAMBIA OKOTO UPELEKE MASIJALA. HAKUAMINI.

Hii ni Taasisi ya Serikali, mtu anaifanya yake
Saf sana
 
Duuhh 2019

2016 nimemaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza, 2017 nikapewa mkataba wa mwaka mmoja moja.

Wakati naingia mambo yalienda vema sn, ila mkuu wa kitengo alikua anapenda sifa KUPITA KIASI (Kila mtu kwake ni Hopeless) hili lilinifanya nipishane nae

2019 January yeye ndio akawa mkuu wa ofisi, aisee hapo niliipata,

1. Alisema nisipewe kazi yoyote
2. Alisema mimi sijui kazi kabisa( hii ilitokana kuna mradi tulipata, nikapewa mimi niufanyie kazi, sasa wakati umefika kwenye utekelezaji yeye ndio boss ko akaninyangaya akasema nimefanya kimakosa akauchukua yeye)
3.Akawa anasema mimi ni Hopeless
4. Anakuita mbele ya watu anakutukana sanaa daahh aisee nimedhalilika sana

Nikaanza kutafuta kazi kimya kimya, Nikapata tena kwenye taasisi ya watu tuliokua tunawahudumia "ilikuaje"

Walimuuliza mkuu wangu wa kitengo wa kipindi hiki ss "mbona xxx siku hizi hatumuoni" akajibu "dah sijui wana bifu gani na mkuu, maana hataki hata kumuona"

Jamaa wakanitafuta wakanipa mkataba wa kazi nikatulia, sasa nikaandika barua ya kusitisha mkataba huku namsubiri mkuu ajichanganye..

Akaingia kwenye 18, siku hiyo akaja reception kabisa kwa watu wanaokuja kumuona akaanza sifa zake

Akamuita HR na wenzie akasema kuna watu mkataba ukiisha wasionhezewe akaniita akaanza kunisema akasema sikuongezei mkataba, nikamwambia sihitaji

Nikaingia ofisini nikachukua barua, Nikamwambia wewe ni mbwa kama wengine unastahili kutupiwa chakula, NIKAMTUPIA BARUA YA KUSITISHA MKATABA NIKAMWAMBIA OKOTO UPELEKE MASIJALA. HAKUAMINI.

Hii ni Taasisi ya Serikali, mtu anaifanya yake
Nipe namba zake nimtukane potele pote
 
Kipindi Mkapa anaingia madarakani mabeberu walimshauri apunguze wafanyakazi wa serikali naye akakubali. Pale ofisini kulikua na watu wa IDM Mzumbe, IFM na sisi wa Mlimani (UDSM).
Kulikua na uhasama wa chini chini Kati yetu kwa upande mmoja na wale wa advanced diploma za IFM na IDM.
Waraka wa Chenkapa ukaja idarani kwamba baadhi ya watu wapunguzwe.
Aisee, aliye pewa kazi ya ku earmark watu wa kupunguzwa alikua mtu wa IDM. Hakufanya kosa, barua ya kwanza, ya pili ya tatu Ni yangu. Kipindi kile bar zinauza beer kuanzia saa mbili asubuhi, Basi nilizama bar moja kule mjini karibu na benki ya NMB.
Redundancy [emoji1][emoji1787]
 
Binadamu wana mambo.

Kuna bwana mdogo mmoja alifukuzwa kazi baada ya bosi kuona furniture alizonazo wakati anahamia nyumba ya kampuni. Nakumbuka yule mzee aliongea sana na kuanza kuuliza maswali kwetu bwana mdogo vitu ametoa wapi. Visa vikawa vingi, haukuisha mwezi akapigwa chini ila Mungu mwema dogo akapata kazi in two weeks maisha yakasonga.

Sema Mungu bwana ni wetu sote. Riziki anatoa pasipo upendeleo
 
Nimewahi fukuzwa brack kinyemelaa na wahindi mwak 2013 bila kujipanga vxr nilienda asbh Kama kawa cku ya mshahara na wale wanatoa mshahara cash kwamkono nilipo pokea tu cash yangu hapo hapo nikapewa na ya kutimuliwaa nikarud kijini mda kidg nikapata tanesco cjakah sawa nikatimuliwa Tena na hr kwakumfidhia meneja hayupo bas aliyepewa kukaimu wakanipitisha HV ..kisa na mkazaa hr alisema mm na mzee mmoja tulimpiga majungu kwa kupenda kuajir wapare ndugu zao ambao baadhi. Hawajasom shule ..bas nayey katika sekeseke la vyeti vyeki magufuli akamla kichwa juu kwa juu

Nilirudi Tena kitaah na watu wengi walishajuwa Niko tanesco nilichukia sana ila nimewasamehe ...
Tatu nilifukuzwa kampuni ya Sola kinyemelaa pia kwakufitiniwa na ndugu yangu eti kaenda kuwaambia maboss kuwa portfolio imenishinda bas duh ach kbsa ...
Aisee pole Sana

Bora wali maharage kuliko walimwengu
 
KI ukweli mimi nilipewa kazi ya ushushu ndani ya idara nayo fanyakazi eti niwe nawachunguza wafanyakazi wenzangu nampelekea taarifa boss...

Ukweli nilikataa wazi wazi nikakwambia siwezi kufukuzisha watu kazi kwa maslahi ya ki shetani mimi.
 
pole sana Lugumya amin kuwa utafika ..ulimpambania sana mama ,amin Mungu atakulipa na baraka tele.
Kiongozi hii thread yako imenikumbusha machungu Makubwa sana.

Nilivomaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza bn, nikapiga kazi miezi mitatu tu nikapandishwa hadhi kidogo bana. Kazi ikaendelea, baada ya Mwaka mmoja kuisha, Kiongozi mmojawapo katika ofisi yetu akapa nafasi ya kuajiriwa serikalini, kampuni ikanipa nafasi yake. Kumbe ile hali wenzangu ambao tulikuwa tunafanya nao kazi walichukia sana. Why me?

Sijawa na hili wale like, mdogo wangu akauugua, wadogo zangu wengine walikuwa wanasoma bado secondary, so ikabidi nichukue likizo ya siku 14 kwanza nikamuuguze, bahati mbaya haikuwa riziki akafariki. Baada ya kumaliza matanga, nilirejea kazini, lakn haikuisha hata mwezi mama akaugua.

Akapelekwa hospital, akawa anakaa na dada yangu, kila wikend lazima niwe huko, nikalazimika kumhamishia kwangu (getho) pamoja na sista, afu Mimi nikawa nalala kwa mpangaji mwezangu msela. Uguza weee, hadi hela ikakata. Kazi nikiwa naendelea nayo lakini.

Basi bana nakumbuka ilikuwa Tarehe 1/10 tukaenda kuchukua mshahara, nilivyofika kwa mhasibu akanipa mshahara wangu na barua. Kuifungua, eti nimeachishwa kazi!

Kosa silijui. Basi ile hela yote nikamtibia mama, lakini haikufua dafu. Nikauza kabati la nguo laki 100,000/, nikauza sofa langu elfu 70, latop hp, 150,000,, uza king'amzi na TV, na dish lake 170,00, friji 70,000 nikaendelea kumtibia mama. Nilivyoishiwa kabisa, mama akapona!

Basi tukarejea kijijini, nikaanza kulima nyanya. Nikipeleka maombi ya ualimu hata shule za kata nakataliwa! Naambiwa nitaitwa lakn siitwi. Nyanya hakuna wanunuzi. Ikabidi nianze kuvua samaki, lkn wapi.

Wale watumishi wenzangu hata hawapokei simu yangu, kila surauali sasa hainitoshi, mwonekano umeshazidi umri wangu halisi. Nimezeeka balaa.

Sema ndo hivo siku hazifanani, nilikuja kupata pa kujishikiza na maisha yanaendelea. Lakn ukweli kuamka bila kujua pa kwenda ni shida.
 
Una matatizo wewe mengi Sana, report huwa siandiki na usinipangie Cha kuandika humu JF. Na naandika kusudi maana ni Mimi wewe baki na msimamo wako na nitazidi kuruka ruka nitakavyo na kuandika ninachojiskia usinipangie kabisa, hizo dictions waziona wewe pyeeeee
Hii comment imeonyesha we ni mtu wa namna gani? We ni wale watu mtu akipinga hoja yako una panick na kugeuza kuwa ugomvi. Unaandika vitu ambayo havijasemwa na havipo. Mdau hapo kapingana nawewe kimtazamo na ingetakiwa ukae chini na kutafakari kuwa labda kamaa yupo right na wewe upo wrong .that is maturity , hakuna maali jamaa kasema anakupangia cha kuandika huku kama unavyodai?

Unasema utazidi kuruka ruka utakavyo , huku ndani tu hatufaamiani uko nje ukiruka ruka na maisha yako who cares?

Critical thinking is free you should try it sometimes
 
Report huandiki,unaandikiwa?

Hujui kuandika

Hata kama ni CEO,reports za kwenda nazo kwenye bodi unaandikaje kama uandishi wako ni wa bata namna hii?

Achana na bodi,mbali sana huko,emails za biashara unaandikaje wewe mamalia mwenzangu?

Au pia huandiki?

Therefore what the fvck are you doing in this world?

Unawasiliana vipi na wanadamu wenzako professionally?

You are tiktoking bwana
Kuna baadhi ya wafanyakazi wao niwa kulaumu na kulalamika tu hata kwa vitu ambavyo wanatakiwa kuwa responsible based on their contractual terms.

Nilijifunza siku moja kwenye kikao jamaa mmoja anapinga kila kitu mabosi wanachosema for the sake yaku onekana hero kwa wafanyakazi wenzake, huwezi pinga kila policies za kampuni na ikakuacha kazini lazma ufukuzwe maana izo policies ndo wanazisimamia na unakuta wakati wa kuajiriwa mtu ali zi saini.

Tulipotoka kwenye kikao nilimwonyesha eneo flani la wazi nikamwambia "unaona pale, nenda kapanunue alafu fungua kampuni yako then hayo mawazo yako yote ya kwenye kikao kayafanye kwenye iyo kampuni yako mpya sio izi za watu".

Alikua mshkaji wangu na alichukulia positive sana. Ever since hakua mtu wa kuropoka since ali realize he was wrong .watu wa hivi niwachache pia.
 
Mi sikufukuzwa kazi.

Nilipiga chini tu hiyo kazi.

Mshahara mdogo sana. Unatoka tar 25 ikifika tar 1 ushaisha wote.

Nikarudi home kuanza moja.
Bora wewe uliondoka kwa upole,,,

Mimi nilimtandika yule gabachori masumbwi kadhaa na kusepa, siku nilipochukua mshahara wangu wa mwisho.

Nilifanya kazi kwa miezi mitatu tu.... Sitakagi ujinga kwenye madharau mbele ya maslahi duni
 
Kuna siku nilipata kazi kwenye kampuni kubwa sana hapa nchini, hii kampuni Ina makao makuu mjini na branch moja Chang'ombe Dar. Basi baada ya kupata Ile kazi nikaambiwa kituo changu Cha kazi itakua branch. Mimi nikachukua taxi mpaka branch kuripoti. Kufika nakuta meneja wa branch Ni jamaa tulisoma nae form five na six, pale nilitakiwa kua assistant wake. Jamaa wa IT Ni mshamba mmoja nilisoma nae UDSM course tofauti yeye computer science. Aisee mnajua fitna, hata Rage Ile fitna haifikii.
Kwanza meneja aliniambia sitapewa gari wakati magari pale yako mawili moja lake jingine la assistant.
Pili kaniambia ngoja akaongee na makaburu halafu atanipigia simu.
Sijui aliwaambia Nini makaburu mwisho wa siku hakunipigia na Mimi sikuhangaika nae. Kipindi kile kazi zinatafuta watu.
Na huyo ulisoma nae,,,,, hii ni hatari sana
 
Kati ya vitu vinavyouma katika maisha ni kufukuzwa kazi, nakumbuka miaka kadhaa nyuma baada ya kumaliza degree yangu nikabahatika kupata kazi kwenye kitaasisi kimoja hivi.

Nikapiga kazi kwa kujituma saana aliekua boss wangu akawa ananichukia mno visa kila siku kikianza hiki kinakuja hiki nikawa Nina stress saana na kazi.

Mara nikajikuta naambiwa nimewatukana staff mate wenzangu yaan balaa juu ya balaa, nakumbuka nlienda likizo ya kawaida kama ilivyo haki ya mfanyakazi yoyote nikiwa likizo watu wa kazini wakanitonya kua kuna mtu kaajiriwa anafanya majukumu yangu ni balaa.

Siku narudi kazini namkuta mfanyakazi mpya kakalia kiti changu na anatumia computer yangu nikashindwa nikae wapi na nifanye majukumu gani mzee nikashinda bench cku nzima, baada ya happy tukawa tunafanya kazi kwa kupokezana kwenye computer nlokua natumia Mimi shida hizi jamani.

Bas bhana aliekua msaidizi wa boss wangu akaniita kiutu uzima akanambia apa kazi hamna kama unaweza apply sehemu nyingine wenzio wanakusubiria uteleze kidogo tu wakule kichwa, nikabaki dilemma basi cku moja foleni za mjini apa nikachelewa kuingia kazini km dakika kumi ivi boss akawaandikia HR office kama hayupo tayari kufanya kazi na Mimi.

Hr mmoja akanambia kama naweza ni andike resignation letter au nisubirie kufukuzwa nikaona maji yamekua mengi nikaandika barua ya kuacha kazi kwa mwezi mmoja boss akaacha kunifatilia tangu siku nlipoandika barua nikawa naingia kazini kiubish mpk mwezi ukaishi nikalipwa mafao yangu mambo yakawa yanasonga

Ugumu wa kwanza baada ya kuacha kazi ni ile hali ya kuamka asbuhi hujui uende wapi, unajikuta unachukia sehemu ulokua unafanyia kazi hata kupapita hutaki tena marafiki wa kazini wanakutenga na wengine wanakupotezea kabisaa majirani na ndugu wanaanza kukusengenya usipojipanga unaweza kujiua.

Nashukuru Mungu nliweza kupambana na maisha bila kazi nimecmama tena nje ya ajira.
Pole sana, hawa mabosi wakati mwingine huwa ni changamoto sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi hadi nineisha zoea private nikifanya kazi najua kufukuzwa ni muda wowote tu.

Cha kwanza sinaga kumuogopa mtu awe boss awe nani yani hii hali inaniponza sometimes siwezi kunyenyekea..

Kazi za hospitali kupiga madili huwa kupo tu mala moja moja
Nimefanya kazi Zahanati nyingi sana sitoboi hata nusu mwaka nisha fukuzwa.

Ila nilipofukuzwa mala ya mwisho ndio inachekesha na kutia simanzi.
Nesi mmoja alikua ni mke wa mtu akawa ananitaka, shobo shobo kibao, mala akija job aseme amenimiss na kutaka kunikiss juu, mwamba nagoma.

Bwana hee nikapokeaga elfu 30 ya mgonjwa nikaichapa juu kwa juu.
Huyo nurse akajua, alinichoma kwa bosi live bila chenga.

Kilichoniuma sio kufukuzwa kazi, yani ni kuchomewa na demu ambae nilikua na uwezo wa kumla/ kuchapa mashine na tukashirikiana vizuri kila sector
Unakula 30k ya mgonjwa??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahaaaaa Ningemtia tu hata kwa kondom, kwanza ningetaka kumla peku ningempima tu kwanza.

Ila ni kusudi la Mungu najua alitaka nisiendelee kufanya kazi hapo, maana kuna sheikh alikua anataka kunipanda kichwani... kwenye Zahanati ya Bakwata.

Na mimi kipindi hizo nimezama kiroho balaa,,
Yani nilikua nataka kumuoneshea Jina la Yesu lilivo na nguvu na usheikh wake nilimwambia hunibabaishi kitu
Kama ulizama kiroho usingejisifia kula rushwa ya 30k kutoka kwa mgonjwa, seriously ulikuwa una-act tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom