Tuliowahi kutuma SMS kimakosa kisha zikatutia aibu na kashikashi tuje hapa

Tuliowahi kutuma SMS kimakosa kisha zikatutia aibu na kashikashi tuje hapa

Mi nakumbuka nilipambana kutoa betrii nikasahau simu hata haina mfuniko,
batan ya power nayo haishikikiiii, message icon ni kama inatelezaa, sijakaa vizuri naambiwa "message delivered".

Nilichofanya ni kuendelea kujichatisha maneno kama yale yalee,
halafu mwishoni nikamwambia: "nijibu haraka hamna umeme nimeomba tuu simu nikaweka laini kwa rafiki yangu hapa anataka aichukue".

Ujinga mwingne ni WhatsApp, ile ku-set popup message, una-type unamjibu huyu kwenye ku-send ishaingia nyingnee inaunga.

Haya mambo hayaaa bana, waweza umuombe dingi yako papuchuu, tena unafanya kumbembelezaa, unamwambia:
"usiogopeee hawatajuaaa, nitakununulia chipsi na gauni"

Aloooo hiyo kesi hata hakimu haingilii, umnunulie dingi yako chipsi na gauni?

usiombee uwe unasubiria akutumie ada au pocket money, alooo mpk aje kukuelewa ushakula vyakula vyote vya mifugo.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dada yangu alikosea kutuma ikaja kwangu ilikua inasema (leo umenipa penzi tam ila dudu lako ni kubwa )
Na mimi nika mjibu ( [emoji23][emoji23][emoji23]kwahiyo leo tayari )kasema dogo kausha nikamwambia paka amesikia harufu ya samaki alafu ajifanye hajaisikia
Hadi leo haniangalii usoni
Na binam nishamla sababu ya kukosea sms nakomaa had na mimi anipe
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] wee kiboko khaaaaaah
 
Dada yangu alikua na boyfrind wake,story za kitaa ilikua inasemekana jamaa huwa anakujaga home kumgegeda kukiwa hakuna mtu,..daaa ilikua inaniuma kinoma' Siku hiyo mida kama ya saa 3 usiku nikaiba simu ya sister nikamtumia text jamaa' Baby kama unaweza njoo nyumbani nipo mwenyewe hakuna mtu wote wameenda kwenye harusi watarudi kwenye saa 7 usiku hivi', njoo nikupe cha fasta, jamaa akajibu nakuja, nikamwambia ukifika we zama tu ndani then nikafuta text zote nikarudisha simu nilipoitoa,,,ukwiru noma asee dk kama 15 hivi jamaa si akafungua mlango kazama ndani bila hodi akatukuta familia nzima tupo mezani tunakula' watu wote macho kwake ,jamaa akaduwaa na ukimya ukatawala kama nusu dakika hivi' hana cha kuongea ,mwisho akapata akili ya kutoka nduki"""" ahahha ilibidi nitoke nikachekee chooni,

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaaah hiv ulikuwa unawaza nn?
 
Na mshua kuna siku alinizingua nikamsave “ndezi” mwanzoni kabisa hizi apps zilikuwa zinakuletea option ya ku re commend kutuma kwa wengine wajiunge mimi nikaselect contact zote, kumbe ile app ina copy hadi jina kwenye simu linaunganisha kwenye text, mfano nimesave jina lako megapixel inakutumia meseji “megapixel flani invite you”. Daah siku ilikuwa ndefu maana mshua alinitext nani ndezi

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dem mpya alikuja kitaa. Kumbe ni kwangu ndio namuona mpya sababu sikua mwenyeji wa ule mtaa, katika dodosa dodosa nikajikuta naambiwa demu yule kitaa kizima wamemshindwa. Siku moja nikajitoa ufaham nikamuomba namba barabarani kumbe wana wanatucheki tu. Nafika kijiweni wadau wakaniambia picha lote wameliona na sitofanikiwa kwani wanamjua alivyo mgumu. SIKU DEM ANAUJA GHETO NDIO NILIPOUNGUZA PICHA KWANI KWA KUTAKA SIFA NILIWATUMIA WAHUNI SMS KIJIWENI KUA LEO NAMALIZA KAZI ILIOWASHINDA NYIE . HUEZI AMINI SMS NILIMTUMIA MHUSIKA AMBAYE NI DEMU MWENYEWE.NILIKULA SIKU HIO HIO ILA SIKUA NA UJASIRI KABISA KINYONGE SANA
 
Nilikuwa nampenda sanaa demu flanii nikawa nachat nae sasa ghafla akanitafuta demu mwingine yeye simpendi ila yeye ananipendaa wee kwenye kuchat bhana ikapoop up msg ya yule ninayempenda sasa ubaya wakati namjibu nikakosea nikaandika mwisho jina la demu nisiyempendaa alafu msg tamuu balaaa wee ile kubonyeza ikaendaaa mamaeee siji kusahau... niliumia balaaa😀😀😀 demu akawa ninampenda akazingua japo aliumia sana. Toka siku hiyo msg nafunua ndo najibu huwa sijibu pale kwenye screen inapo poop up NEVER.
 
Miaka kadhaa nilivyokuwa mvulana, jpili lazima twende church familia nzima, dingi akaenda kuoga akaacha simu yake dinning alipo kuwa anakunywa chai, koz najua passwords zake za mpesa, mjanja nikaenda kujihamishia credit Kama ya buku 8, daah hela imeshaingia kwenye simu yangu, naiskilizia sms irudi kwenye simu ya mzee ili nifute, twende sawa. Dah sms haikurudi Hadi nikasahau. Tuko kwenye gari tunaenda church mara sms ikaingia kuwa namba ya mzee imenitumia hela, baba kuusoma tu, yaliyo nikuta acheni tu, mpesa mungu anawaona
[emoji16][emoji16][emoji16]
 
R.I.P, Bi. mkubwa. Moja ya matukio ambayo maza aliniokoa ni hili kukosea message halafu ikaenda kwenda mzee bahati nzuri muda huo maza alikuwa na simu ya mumewe anacheza game akaisoma coz namba yangu ni nyepesi akawa na uhakika imetoka kwangu akaifuta bila mshua kujua. Huwezi amini ilikuwa nimetoka kupewa ada ya chuo usiku huo nikawa nampanga demu nyumba ya jirani twende Kigamboni eti niliyekuwa namdai kanilipa. Kwa ninavyomjua mzee wangu siku ile ndio ingekuwa mwisho wa chuo; nilipewa risala kali na asubuhi tukaongozana na Bi mkubwa hadi CRDB Azikiwe branch kuweka ile hela.

[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom