Pre GE2025 Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kuanza mchakato wa kugawa na kubadili Majina ya Majimbo kuanzia Februari 27, 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nimeona watu wa Tume ya Uchaguzi eti wamefungua mchakato wa kuongeza na kugawa majimbo mengine.

Kwanza hakuna sababu za msingi za kuongeza idadi ya majimbo ya uwakilishi ikiwa tayari tuna Wabunge wa Viti Maalumu karibu 1/3 ya Wabunge Wote.Aisha Tanzania ni Kati ya Nchi yenye Wabunge wengi.

Kuongeza Majimbo ni kielelezo Cha ubinfsi wa Hali ya Juu wa Wanasiasa ambao wanajali matumbo Yao.

Kama Rais amekuwa anakataa kuongeza maeneo ya Utawala iweje Tume ya Uchaguzi itake kuongeza Wabunge wengine?

Mbunge ana kazi gani hiyo inayomtagiza Kuwafikia Wananchi? Haya ni matumizi mabaya ya Rasilimali za Nchi katika mazingira ambayo Vijana wanahangaika na Ajira,ongezeko kubwa la watu wanahitaji Huduma za jamii na kiuchumi sanjali na Changamoto zingine za Nchi kimiundombinu.

View: https://www.instagram.com/p/DGiMOcXt_wB/?igsh=a2pzZ205ZW1oNnZr
My Take
Kuongeza Majimbo ya Uchaguzi ni kumuongezea mzigo wa Kodi mwananchi.

Napinga hili Kwa Nguvu zote,Naomba Serikali ilitazame upya jambo hili.
 
Hili halikubaliki kabisa na ni ibinafsi wa Hali ya Juu ndio maana nawachukia Wanasiasa na siasa kasoro SSH.

Nita mtag akatae jambo hili.Wabunge wanatosha.
Dunia ya Sayansi na Teknolojia Kila mkoa ungetoa Wabunge wawili tu πŸ˜‚

Pale DOGE USA Watumishi ni 20 tu wanafuatilia utendaji wa Majimbo yote na kutoa Ripoti Kila Wiki
 
Napinga huu upuuzi Kwa Nguvu zote
 
Hiyo inaitwa tume huru ya ccm ya Uchaguzi.
 
Hakuna jipya majimbo ya uchaguzi yanatakiwa kuwa ya kimikoa tu, mbona wakuu wa mikoa wanafika kona zote za mikoa yao, hao wabunge wananshindwa nini?
Wabunge wabaki wawili tu kila mkoa, inatosha mno.
 
Huu ni muda wa akina Lissu kutoa maoni sasa sio kusubiri mchakato upite waanze kutikisa matumbo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…