Elections 2015 Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

Elections 2015 Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

Haiwezekani eti kwakuwa magufuli ameshinda kwa zaidi ya kura laki tano ndio aapishwe,kura zinatakiwa kuthibitishwa kuwa ni za jimbo flani ndio maana hairuhusiwi kupiga kura sehemu yoyote ila tu ulipojiandikisha
 
Naomba kujua vipi kuhusu Yale matokeo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano kule Zanzibar... .. Je yale nayo yamefutwa?? Kama ndivyo Au sivyo ina maanisha nini kwa Rais wa Muungano kule Zanzibar
 
basi na tanzania bara wafute uchaguzi maana january alishatangaza kabla ya nec na nec ilisema ni tume peke yake ndio ina mamlaka ya kutangaza.

yani ccm ni majanga kwa kweli
 
Nakamwe zisilinganishwe kura za majimbo naza upande mmoja wa muungano,nafikiri sasa tutapata katiba mpya
 
Mkuu hapo kwenye kuiregard Zenji km kajimbo ka uchaguzi ni matusi makubwa kwa wanavisiwani na ni kebehi kwa washirika wote wa Muungano.
Uchaguzi wote urudiwe si zenj wala Bara, na kiranja wa uchaguzi awe huru!

SIO TUSI, acha kukuza mambo ukasababisha vurugu, wewe Kisima wewe. Bara na Visiwani wanaunda serikali kuu ya MUUNGANO. bara wangekosea tungerudi bara tu, kama Visiwani wamekosea, watarudia visiwani tu. HAUWEZI mmoja akakosea kila mtu akarudia.. what kind of logic is that? wewe mguu mmoja ukileta matatizo unakata yote?
 
..........................
Hapa ndipo tuone itavyokuwa ni vipi; maana:-

1. Ikiwa ni kweli uchaguzi wa rais wa JMT unasimamiwa na NEC na si ZEC, tuelezwe kulikuwa na daftari tofauti la wapiga kura wa kura za urais wa JMT?

2. Je, kulikuwa na wasimamizi wawili tofauti katika kila kituo na jimbo mmoja kwa ajili ya kura za rais wa JMT na mwingine rais wa SMZ?

3. Je, kulikuwa na vituo tofauti kabisa kwa ajili kupigia kura za rais wa JMT na rais wa SMZ?,

4. Je, kura hizi zilipigwa siku tofauti kwa kura za rais wa JMT siku yake na rais wa SMZ siku yake?

Kama jibu ni HAPANA kwa angalau swali moja katika hayo; ni wazi kwamba "uchaguzi huu na matokeo yake yote" yafutwe (kama nilivyonukuu katika taarifa ya ZEC si mimi)

Mkuu hata mimi nimeelewa ZEC imefuta uchaguzi wote na si wa Urais wa Zenji peke yake, kwani wasismamizi wa uchaguzi wa Zenji ni ZEC.....kama ilivyo hapa chini!

Katika hali ya kushtua Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar(ZEC) imetangaza kuyafuta Matokeo ya urais wa Zanzibar.

Yadaiwa Uchaguzi uligubikwa na kasoro nyingi.

Imeahidi kutangaza tarehe rasmi ya kurudiwa uchaguzi.

====
Statement:

vU05dG9.jpg

EdIidYV.jpg

BLhdlD9.jpg


VIDEO:

Chanzo: ZBC TV
 
Last edited by a moderator:
wana jf ninaiyona rasimu ya katiba ya warioba ikirejea taratibu ccm walikwepa mambo mengi leo rais kikwete mambo yanakudodea kwa mara ya kwanza tangu tupate uhuru matokeo ya urais zanzibar yanafutwa kweli unatuacha na historia kubwa ila kwa rais ajae nafuu yake ni kurejea rasimu ya warioba la sivyo nae ataondoka kwa aibu
 
...Seif jipange vizuri,ma ccm yanajipanga upya na mbinu mpya za wizi...you should outsmart them again, coz you are intelligent enough..!!
 
matokeo ya urais wa jamhuri ya muungano Tz.walipata toka Zanzibar nayo inafutwa?
na wakifuta inakuwaje
 
Mfano: Tanzania bara Jimbo la ubungo, unapewa karatasi TATU (Raisi muungano, Mbunge na Diwani) . kwa ZANZIBAR unapewa 4 (Raisi wa Muungano, Raisi wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani) tatizo liko kwenye hizi tatu za mwisho sio ile ya TANZANIA yote!!! TANZANIA BARA Hawana karatasi ya nne ya URAISI ZANZIBAR kwahiyo HAWARUDII.

Zilikua tano... kasoro ilikua picha hazionekani vizuri ama???
Hujasema bado tatizo nn
 
Hapa ndipo tuone itavyokuwa ni vipi; maana:-

1. Ikiwa ni kweli uchaguzi wa rais wa JMT unasimamiwa na NEC na si ZEC, tuelezwe kulikuwa na daftari tofauti la wapiga kura wa kura za urais wa JMT?

2. Je, kulikuwa na wasimamizi wawili tofauti katika kila kituo na jimbo mmoja kwa ajili ya kura za rais wa JMT na mwingine rais wa SMZ?

3. Je, kulikuwa na vituo tofauti kabisa kwa ajili kupigia kura za rais wa JMT na rais wa SMZ?,

4. Je, kura hizi zilipigwa siku tofauti kwa kura za rais wa JMT siku yake na rais wa SMZ siku yake?

Kama jibu ni HAPANA kwa angalau swali moja katika hayo; ni wazi kwamba "uchaguzi huu na matokeo yake yote" yafutwe (kama nilivyonukuu katika taarifa ya ZEC si mimi)
Yes mkuu ndivyo ilivyokua.
Kulikua na meza mbili, ulikua unaanza kupiga kura za Zanzibar kwanza na ukishatumbukiza unaenda upande wa pili kuchukua karatasi mbili za wabunge wa jamuhuri na karatasi ya rais kisha unaenda kutumbukiza kwenye masanduku mengine.
 
mkuu hiyo taarifa ya ZEC ni ya kama 30 minutes ago, vituo vyote vimeishiwa pozi vionyeshe nini tena maana hakuna cha kuripoti tena kila kitu kimesimama, utampata rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania bila kura za zaznibar???

Kituo kama AZAM TWO walijitoa kuripoti kila kitu ila wameona haya mazingaombwe huko zenji wamekosa hata kipindi cha kuweka, wako na vimatangazo vyao... CCM HUKO MAMBO MAGUMU BALAAA..... WALISEMA WATASHINDA KWA BAO LA MKONO, KUMBE UKAWA NAO WALIKUWA WANAJIANDAAA PIA..


MUNGU NI MWEMA
Hizi ni tetesi au ukweli? Vituo vya TV na radio vyote mbona kimya kuhusu habari hii?
 
Zimefutwa Kura Za Urais tu na Sio mengine

Uchaguzi umefutwa wote wa Rais wa Zanzibar, Rais wa Muungano, ubunge na uwakilishi. Hizi ni mbinu za viongozi wetu kupenda kuendelea kukaa madarakani.

Viongozi wanajua kuwa kukiharibika Zanzibar na huku ni lazima uchaguzi utakuwa haufai kwaiyo wataendelea kutawala na kula bata.
 
Back
Top Bottom