Litro
JF-Expert Member
- Nov 18, 2018
- 1,080
- 2,248
Mmeamshwaje wakuu poleni na mvua zinazoendelea kutufikirisha.
Jana niliangalia interview ya Milad na baba wa Gadna nachelea kusema baba yule yupo kwenye mtikisiko na msikitiko mkubwa sana.
Kilichonifikirisha na kuniuma ni yeye kusema siku hiyo alimtafuta mwana akamkosa akaenda jumuiya akiwa hana raha kwa kumkosa mwana mbaye alitaka kumsomea neno kutoka kitabu kitakatifu. akapigiwa simu mbili ile ya pili ilikuwa ni pole direct kwamba "nimeona Gadna amefariki huko kwenye mitandao" can you imagine habari nzito inafika kwa mtu muhimu kwa njia nyepesi kabisa?!!.
Kwanini tumekuwa washamba na malimbukeni kiasi hiki maana ingekuwa ajali utasema mashuhuda walipost, ingekuaje kama baada ya kifo kutokea akatafutwa mtu wa familia akapewa muda kupeleka kwenye ngazi ya familia hii taarifa then ndo ipelekwe kazini?.
Ni nani alivujisha taarifa mitandaoni kabla ya watu muhimu ambae mmoja wapo kwa ukubwa ni mzazi? natamani kuwepo na mtu wa kuwajibishwa katika hili ili iwe mfano.
Tuliona mzee Zoro nae alipatia taarifa kutoka kwenye mitandao binti yake amefariki well angalau ilikua ajali mashuhuda walipostpost lakini bado sio sawa. Usiseme kuwa huo ni umaarufu na maisha yake hapana; Mfu anahitaji stara.
Jana niliangalia interview ya Milad na baba wa Gadna nachelea kusema baba yule yupo kwenye mtikisiko na msikitiko mkubwa sana.
Kilichonifikirisha na kuniuma ni yeye kusema siku hiyo alimtafuta mwana akamkosa akaenda jumuiya akiwa hana raha kwa kumkosa mwana mbaye alitaka kumsomea neno kutoka kitabu kitakatifu. akapigiwa simu mbili ile ya pili ilikuwa ni pole direct kwamba "nimeona Gadna amefariki huko kwenye mitandao" can you imagine habari nzito inafika kwa mtu muhimu kwa njia nyepesi kabisa?!!.
Kwanini tumekuwa washamba na malimbukeni kiasi hiki maana ingekuwa ajali utasema mashuhuda walipost, ingekuaje kama baada ya kifo kutokea akatafutwa mtu wa familia akapewa muda kupeleka kwenye ngazi ya familia hii taarifa then ndo ipelekwe kazini?.
Ni nani alivujisha taarifa mitandaoni kabla ya watu muhimu ambae mmoja wapo kwa ukubwa ni mzazi? natamani kuwepo na mtu wa kuwajibishwa katika hili ili iwe mfano.
Tuliona mzee Zoro nae alipatia taarifa kutoka kwenye mitandao binti yake amefariki well angalau ilikua ajali mashuhuda walipostpost lakini bado sio sawa. Usiseme kuwa huo ni umaarufu na maisha yake hapana; Mfu anahitaji stara.