Tumeudharau ugonjwa wa Corona kwa kukosa Maarifa na itakuwa inaondoa mmoja mmoja?

Tumeudharau ugonjwa wa Corona kwa kukosa Maarifa na itakuwa inaondoa mmoja mmoja?

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Amani iwe kwenu wapendwa katika bwana.

Wakati tukiendelea kuomboleza msiba wa Jemedari wetu Dkt Magufuli, tuna kila sababu ya kutafakari sana kama taifa. Haiwezekani tupoteze watu maarufu na wakubwa hapa nchini kwa kipindi kimoja, sababu ya kupoteza hawa viongozi zinatajwa kuwa ni chronic illnesses. Je, tunasahu kua huyu Kovidi ndio anawaondoa wenye Chronic illnesses? Kuna hata mmoja tuliyeambiwa kafa kwa Covid-19? Tutajuaje wakati halisemwi hili ni siri?

Ni kweli Mungu hupanga vifo lakini kwanza vifo hutangulia na sababu ndipo Mungu atume malaika wake kuja kubeba roho zetu. Tulipewa maarifa tuyatumie kupambana na mazingira lakini sasa huenda mazingira ndio yanatuzidi maarifa tunabaki na vilio kila kukicha.

Hivi tungekuwa strict kujikinga na COVID-19 100% tukachukua tahadhari katika kila kipengele kwa mujibu wa maelekezo ya wataalam na WHO mnafikiri leo hii tungekua na hamaki kila mitaa tunakopita au taifa sasahivi lingekuwa na utulivu wa aina gani?

Kuchukua tahadhari siyo lazima Lockdown wala si chanjo ya Mabeberu. Tahadhari tuliyokuwa nayo mwaka jana ilitosha sana kupunguza maambukizi na wala leo tusingekua na hamaki mitaani.
Tumepuuzia hili, timekimbizana kwenye njia za kienyeji au asili ambazo ni njia za pata potea kuliko za kitaalam. Tumeshindwa kuyatumia maarifa ipasavyo hii hali itatutesa sana.


Mwisho nawatakieni mwisho mwema wa wiki, tuchukue tahadhari binafsi kwa kujali afya zetu na familia zetu. Apumzike kwa amani Jemedari wetu JPM.[emoji120][emoji120]
 
Corona hapa kwetu inatazamwa katika mlengo wa kisiasa kuliko ulivyo uhalisia wenyewe........

Wapinzani wanautumia kama kete ya kisiasa dhidi ya watawala na watawala wameingia katika mtego wa wapinzani......kuupinga kisiasa.......

Shida inaanzia hapo.......
Waende hivo hivo,atakae umia ana tundika gloves
 
Ni kweli, lakini mimi nadhani ni muhimu kujifunza kwanza kwa wenzetu wa mataifa ya nje ili tuone, wao wanatumia njia zipi na zinawasaidia kwa kiwango gani?
Mimi nadhani hata wewe ungekuja na njia mbadala unazofikiri zitatusaidia kujikinga na ugonjwa huu.
 
20210326_122734.jpg

Bi Samia Suluhu Vaa Barakoa
 
Kwahiyo tuendelee kusubiri mwezi wa ngapi ndio Corona itatufagia? Tulibiwa tutadondoka kama kuku wewe kideri....muda hujafika tu?
Corona inafyeka Wamarekani wenye chanjo na barakoa na social distance kuliko changanyikeni ya tz...
Nashauri wewe vaa barakoa
 
Hivi tungekuwa strict kujikinga na COVID-19 100% tukachukua tahadhari katika kila kipengele kwa mujibu wa maelekezo ya wataalam na WHO mnafikiri leo hii tungekua na hamaki kila mitaa tunakopita au taifa sasahivi lingekuwa na utulivu wa aina gani?
Hebu nambie tu tangu walipoanza kuchukua hizo tahadhari, ni nchi gani angalau moja tu duniani imefanikiwa kudhibiti kusambaa kwa maambukizi na vifo vya UVIKO_19 na sasa wako salama kabisa. Ahsante
 
Sikatai na hoja zako lakini nikukumbushe tuu hata hizo nchi bado watu wanaangaia hivyo kwa huku kwetu acha tutumie head immunity system kutokana na hali yetu, kikubwa wale wenye hizo changamoto wachukue tahadhari maani inaonesha kwa kiasi kikubwa wao ndio wahanga wakubwa
 
Umeshauri jambo muhimu, naona hasa kipindi hiki cha msiba ni kama tumejisahau kama ugonjwa upo, hata Wizara husika ni kama haipo

Siku zote Watanzania tulikua tunaishi hivyo na hamna hata hivyo vifo ... kama huko Ulaya na kwengineko watu wanajazana masokoni siku zote kwenye ma daladala lipi sasa lililobadilika !
 
Back
Top Bottom