Tumsaidie Rais Samia atambue kuwa yuko kwenye junction muhimu sana ya mustakbali wa nchi hii

Tumsaidie Rais Samia atambue kuwa yuko kwenye junction muhimu sana ya mustakbali wa nchi hii

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Kama Samia atakuwa ni mtu wa kukaa chini na kufikiri kwa makini basi atagundua kuwa yeye kuwa hapo siyo accident, Bali Mwenyezi Mungu amemuweka hapo kwa sababu maalum.

Machozi na vilio ambavyo watanzania walipitia katika utawla wa Magufuli, Mwenyezi Mungu aliamua kuwafanyia wepesi kwa kumuondoa mtu ambaye kila mtu alishaona kuwa hashikiki tena, hawezekaniki tena, anachokitaka yeye anaweza kukifanya na asiwepo mtu wa kusema fyoko, na yeyote aliyethubutu basi alikiona cha mtema kuni.

Magufuli hakuanza hivihivi kuanza kubambika watu kesi, kufanya kazi na vikundi vya watu wasiojulikana, kupora korosho za watu, kuvunja nyumba za wananchi kikatili, kuonea wafanyabiashara, kuonea wapinzani, kufukuza watu kazi kwenye hadhara kinyume cha taratibu za utumishi wa umma, kuvumilia viongozi wahuni kama akina sabaya Ila alianza kwanza kwa kuvunja kiapo chake cha kuheshimu katiba na sheria za nchi.

Kinachonisikitisha kwa Samia ni kwamba hakuwa mwanafunzi mzuri kwa Magufuli kuweza kujifunza mwenzie alianzia wapi kwenye mserereko wake wa kuanguka. Magufuli alianza kuserereka kuelekea kwenye kufanya udhalimu nchini baada ya kuanza kuvunja sheria na katiba hasa zile zinazowapa wapinzani wake haki fulanifulani ambazo yeye alikuwa hazipendi!

Sasa hebu tazama kiapo cha raisi Samia huku ameshika Qur'an tukufu, anaapa kulinda katiba inayotoa haki kwa Wapinzani kufanya siasa nchi nzima halafu kwenye kiapo hicho anamalizia kwa maneno eeh Mwenyezi Mungu nisaidie, Kisha siku 100 baada ya kiapo hicho anasema vyama vya siasa hakuna kufanya mikutano ya wazi ila vikao vya ndani tu, hivi sheria ndivyo inavyosema?

Samia ameamua kufuata Umagufuli, Umagufuli huu hautomuacha salama, kwa sababu ni njia feki, si njia za haki hata kidogo. ni njia amabzo zimeshakuwa tested na zikafeli sana, na mwishowe aliyezijaribu akaishia kuwa muongo zaidi, muonevu zaidi, mnunua watu wamuunge mkono, mnyamazisha vyombo vya habari ili visikemee udhalimu wake.Kama si udhalimu wake kukema kupitia kifo chake yule mzee alikuwa anatupeleka shimoni.

Samia alikuwa na nafasi adhimu sana ya kufanya reforms za msingi katika nchi hii lkaini ameamua kuwa "caretaker" president kwa kuendeleza umagufuli, bila shaka amejikosesha nafasi adhimu ya kulifanyia mabadiliko ya msingi taifa hili ambayo yangempa heshima kubwa mbele ya umma.

Anasema eti anataka kujenga uchumi kwanza, kiukweli kabisa kutawala kwa mujibu wa sheria hakumzuii mtawala kujenga uchumi, bali ni kutafuta uchochoro wa kutowajibika mbele ya wananchi. Hatuhitaji kwenda mbali kupata mifano, tunaweza kuangalia hapahapa nchini. Hakuna utawala uliovutia Uwekezaji nchini kama utawala wa Kikwete, lakini Kikwete hakuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi.

Ni wakati wa Kikwete tulishuhudi uchumi ukikua kwa asilimia 7 lakini yote haya yalifanyika bila kuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi!. Sasa Samia inakuwaje atwambie eti shughuli za Kisiasa zifanyike kupitia vikao vya ndani tu, hiyo sasa ni siasa gani? Utawapataje wananchama wapya kwa vikao vya ndani?

Samia amewahi kuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba na mwaka 2015 alizunguuka nchi nzima kuinadi ilani ya CCM yenye kutaka tuwe na katiba mpya. Kama CCM imewahi kuataka tuwe na katiba mpya kabla ya kuwa na uchumi wa kati, Samia asitwambie eti tusubiri akuze kwanza uchumi ndo tuwe na katiba mpya wakati sasa hivi tayari tupo kwenye uchumi wa kati. Au anataka kwanza tuwe Donnor country ndo tuwe na katiba mpya?

Lugha aliyotumia ya kuwa ngoja kwanza akuze uchumi kimsingi anamaanisha kuwa Hataki katiba mpya. Ni sawa na mtu anayeaandika bango nje ya duka lake kuwa mkopo kesho, kesho yake ikifika bango bado linasoma vile vile kuwa mkopo kesho!, Sasa kukuza uchumi ni kazi isiyoisha, hakuna siku uchumi utatosha maana kuujenga ni kazi isiyoisha!

Kiukweli kabisa suala la Katiba mpya kamwe halikwepeki, ni kujitia upofu tu kukwepa suala hili. Kuna mahitaji ya utekelezaji wa sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012, Kuna mgongano wa katiba ya Muungano na ya Zanzibar kwenye amsuala ya muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, katiba ya sasa bado inatambua muundo wa zamani wa serikali ya SMZ, Kuna ukweli kuwa nchi sasa ikpo katika mfumo wa vyama vingi lakini katiba ya sasa ni ya mfumo wa chama kimoja. Kwa hiyo Katiba mpya haikwepeki.

Tangu zamani palipokuwa pakitokea tukio kubwa nchini, liliambatana na mabadiliko ya katiba
  • Tulipopata uhuru, muda mchache baadae tulikuwa na katiba ya Jamhuri
  • Tulipoungana na Zanzibar tuliingiza mambo ya muungano kwenye katiba
  • Mwaka 77 baada ya Muungano wa ASP na CCM kulizaliwa hii katiba ya sasa ya Chama kimoja
  • Miaka iliyofuata mabadiliko yalifanyika kuingiza muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya katiba

Sasa mwaka 2010 kulitokea mabadiliko ya muundo wa serikali ya Zanzibar, Kwa nini Katiba ya nchi haibadilishwi ili kuaccomodate jambo hili?

Samia aache kutafuta wepesiwepesi, asimame sasa kama mkuu wa nchi arekebisha discrepancy hii.

UCHUMI TUTAUJENGA TUTAENDELEA KUUJENGA, YEYE SIYO WA KWANZA AU WA MWISHO KUJENGA UCHUMI, SASA HIVI ANATKIWA AFANYE VYOTE YAANI REFORMS ZA MSINGI ZA NAMNA YA KUENDESHA NCHI HII PAMOJA NA UCHUMI
 
Samia anaendesha roli (nchi kubwa) Sio Altezza (nchi ndogo) ambayo unakata kona haraka. Roli inabidi kona yake uilie timing. Aung San Suu Kyi
alipokabidhiwa roli, alitaka kuliendesha kama Altezza. Mwishowe ameishia kugombana na majenerali.
 
Samia anaendesha roli. Sio Altezza ambayo unakata kona haraka. Roli inabidi kona yake uilie timing. Aung San Suu Kyi
alipokabidhiwa roli, alitaka kuliendesha kama Altezza. Mwishowe ameishia kugombana na majenerali.
Syukii alijisahau alipoingia madarakani, badala ya kutetea haki akaanza kuvumilia matendo ya kidhalimu dhidi ya Warohingya wa huko Myanmar
 
Kama Samia atakuwa ni mtu wa kukaa chini na kufikiri kwa makini basi atagundua kuwa yeye kuwa hapo siyo accident, Bali Mwenyezi Mungu amemuweka hapo kwa sababu maalum.

Machozi na vilio ambavyo watanzania walipitia katika utawla wa Magufuli, Mwenyezi Mungu aliamua kuwafanyia wepesi kwa kumuondoa mtu ambaye kila mtu alishaona kuwa hashikiki tena, hawezekaniki tena, anachokitaka yeye anaweza kukifanya na asiwepo mtu wa kusema fyoko, na yeyote aliyethubutu basi alikiona cha mtema kuni.

Magufuli hakuanza hivihivi kuanza kubambika watu kesi, kufanya kazi na vikundi vya watu wasiojulikana, kupora korosho za watu, kuvunja nyumba za wananchi kikatili, kuonea wafanyabiashara, kuonea wapinzani, kufukuza watu kazi kwenye hadhara kinyume cha taratibu za utumishi wa umma, kuvumilia viongozi wahuni kama akina sabaya Ila alianza kwanza kwa kuvunja kiapo chake cha kuheshimu katiba na sheria za nchi.

Kinachonisikitisha kwa Samia ni kwamba hakuwa mwanafunzi mzuri kwa Magufuli kujifunza mwenzie alianzia wapi kwenye mserereko wake wa kuanguka, Magufuli alianza kuserereka kuelekea kwenye kufanya udhalimu nchini baada ya kuanza kuvunja sheria na katiba hasa zile zinazowapa wapinzani wake haki fulanifulani ambazo yeye alikuwa hazipendi!

Sasa hebu tazama kiapo cha raisi Samia huku ameshika Qur'an tukufu, anaapa kulinda katiba inayotoa haki kwa Wapinzani kufanya siasa nchi nzima halafu kwenye kiapo hicho anamalizia kwa maneno eeh Mwenyezi Mungu nisaidie, Kisha siku 100 baada ya kiapo hicho anasema vyama vya siasa hakuna kufanya mikutano ya wazi ila vikao vya ndani tu, hivi sheria ndivyo inavyosema?.

Samia ameamua kufuata Umagufuli, Umagufuli huu hautomuacha salama, kwa sababu ni njia feki, si njia za haki hata kidogo. ni njia amabzo zimeshakuwa tested na zikafeli sana, na mwishowe aliyezijaribu akaishia kuwa muongo zaidi, muonevu zaidi, mnunua watu wamuunge mkono, mnyamazisha vyombo vya habari ili visikemee udhalimu wake, kama si udhalimu wake kukema kwa kifo chake yule mzee alikuwa anatupeleka shimoni!

Samia alikuwa na nafasi adhimu sana ya kufanya reforms za msingi katika nchi hii lkaini ameamua kuwa "caretaker" president kwa kuendeleza umagufuli, bila shaka amejikosesha nafasi adhimu ya kulifanyia mabadiliko ya msingi taifa hili ambayo yangempa heshima kubwa mbele ya umma.

Anasema eti anataka kujenga uchumi kwanza, kiukweli kabisa kutawala kwa mujibu wa sheria hakumzuii mtawala kujenga uchumi, bali ni kutafuta uchochoro wa kuwajibika mbele ya wananchi. Hatuhitaji kwenda mbali kupata mifano, tunaweza kuangalia hapahapa nchini. Hakuna utawala uliovutia Uwekezaji nchini kama utawala wa Kikwete, lakini Kikwete hakuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi.

Ni wakati wa Kikwete tulishuhudi uchumi ukikua kwa asilimia 7 lakini yote haya yalifanyika bila kuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi!. Sasa Samia inakuwaje atwambie eti shughuli za Kisiasa zifanyike kupitia vikao vya ndani tu, hiyo sasa ni siasa gani?----Utawapataje wananchama wapya kwa vikao vya ndani?

Samia amewahi kuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba na mwaka 2015 alizunguuka nchi nzima kuinadi ilani ya CCM yenye kutaka tuwe na katiba mpya. Kama CCM imewahi kuataka tuwe na katiba mpya kabla ya kuwa na uchumi wa kati, Samia asitwambie eti tusubiri akuze kwanza uchumi ndo tuwe na katiba mpya wakati sasa hivi tayari tupo kwenye uchumi wa kati. Au anataka kwanza tuwe Donnor country ndo tuwe na katiba mpya?.

Lugha aliyotumia ya kuwa ngoja kwanza akuze uchumi kimsingi anamaanisha kuwa Hataki katiba mpya. Ni sawa na mtu anayeaandika bango nje ya duka lake kuwa mkopo kesho, kesho yake ikifika bango bado linasoma vile vile kuwa mkopo kesho!, Sasa kukuza uchumi ni kazi isiyoisha, hakuna siku uchumi utatosha maana kuujenga ni kazi isiyoisha!

Kiukweli kabisa suala la Katiba mpya kamwe halikwepeki, ni kujitia upofu tu kukwepa suala hili. Kuna mahitaji ya utekelezaji wa sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012, Kuna mgongano wa katiba ya Muungano na ya Zanzibar kwenye amsuala ya muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, katiba ya sasa bado inatambua muundo wa zamani wa serikali ya SMZ, Kuna ukweli kuwa nchi sasa ikpo katika mfumo wa vyama vingi lakini katiba ya sasa ni ya mfumo wa chama kimoja. Kwa hiyo Katiba mpya haikwepeki.

Tangu zamani palipokuwa pakitokea tukio kubwa nchini, liliambatana na mabadiliko ya katiba
  • Tulipopata uhuru, muda mchache baadae tulikuwa na katiba ya Jamhuri
  • Tulipoungana na Zanzibar tuliingiza mambo ya muungano kwenye katiba
  • Mwaka 77 baada ya Muungano wa ASP na CCM kulizaliwa hii katiba ya sasa ya Chama kimoja
  • Miaka iliyofuata mabadiliko yalifanyika kuingiza muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya katiba

Sasa mwaka 2010 kulitokea mabadiliko ya muundo wa serikali ya Zanzibar, Kwa nini Katiba ya nchi haibadilishwi ili kuaccomodate jambo hili?
Samia aache kutafuta wepesiwepesi, asimame sasa kama mkuu wa nchi arekebisha discrepancy hii.

UCHUMI TUTAUJENGA TUTAENDELEA KUUJENGA, YEYE SIYO WA KWANZA AU WA MWISHO KUJENGA UCHUMI, SASA HIVI ANATKIWA AFANYE VYOTE YAANI REFORMS ZA MSINGI ZA NAMNA YA KUENDESHA NCHI HII PAMOJA NA UCHUMI
Excellently thought out!
 
Tutaanza kumlaumu Samia, kwa mizinguo hii anayofanya, ni haki yetu kufanya hivyo; lakini tusisahau, Samia sasa hivi ni mateka wa CCM.

Uhusiano wake na chama chake ni tofauti kubwa sana na uhusiano aliokuwa nao Magufuli na chama hicho. Magufuli aliamua kujibinafsishia chama, na hakuna yeyote ndani ya chama , kuhoji lolote afanyalo Magufuli, baada ya kuwashughulikia ipasavyo aliodhani wataleta ubishi ndani ya chama, akina Nape, Makamba wote wawili, Kinana na wengine.

Kwa hiyo CCM ilikuwa ni chombo cha Magufuli, kukitumia vyovyote atakavyo, bila ya kuhojiwa na yeyote.

Samia hana (hajawa) na uwezo huo ndani ya chama, na wala sidhani kwamba atakuwa nao uwezo wa namna hiyo.
Kwa hiyo Samia, atake asitake, ni lazima afuate chama kinataka nini; hasa katika kuhakikisha kwamba ni CCM pekee itaendelea kuwa na madaraka nchini.
Samia hawezi kuanzisha mchakato wa katiba bila ya kusikiliza CCM inataka nini.

Ninaloona litamuwia gumu kwake ni kuvizima hivi vyama vya upinzani kuweka madai yao , hasa ya kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi, hili huenda akalishughulikia kiaina,; hata kama CCM hawalikubali.

Lakini ukweli ni huu: CCM na Mwenyekiti wao kukataa madai ya vyama vya upinzani ni kujiondolea fursa tu na kutaka kujiweka katika hali ngumu isiyokuwa na sababu.
CCM kuwa na woga wa kuwepo na uchaguzi huru na wenye haki kwa nini kuwatie hofu huku wakijua hulka ya waTanzania ilivyo?

Ngoja hili niliachie hapa kwa sasa.
 
Kiufupi It seems mwanzoni Samia alikuwa anajua hii nchi inahitaji nini haswa ila sasa hivi kadri anavyozunguukwa na wahafidhina, ameanza kusahau hasa nini nchi hii inahitaji au amenogewa na madaraka kwa hiyo hataki vitu vinavyoweza kumchallenge ktk uongozi wake. Kiufupi anaogopa siasa za hoja, ameamua kuwafunga mikono wapinzani wake kama alivyofanya Magufuli akaishia kufanya mambo ya ajabuajabu
 
Kama Samia atakuwa ni mtu wa kukaa chini na kufikiri kwa makini basi atagundua kuwa yeye kuwa hapo siyo accident, Bali Mwenyezi Mungu amemuweka hapo kwa sababu maalum.

Machozi na vilio ambavyo watanzania walipitia katika utawla wa Magufuli, Mwenyezi Mungu aliamua kuwafanyia wepesi kwa kumuondoa mtu ambaye kila mtu alishaona kuwa hashikiki tena, hawezekaniki tena, anachokitaka yeye anaweza kukifanya na asiwepo mtu wa kusema fyoko, na yeyote aliyethubutu basi alikiona cha mtema kuni.

Magufuli hakuanza hivihivi kuanza kubambika watu kesi, kufanya kazi na vikundi vya watu wasiojulikana, kupora korosho za watu, kuvunja nyumba za wananchi kikatili, kuonea wafanyabiashara, kuonea wapinzani, kufukuza watu kazi kwenye hadhara kinyume cha taratibu za utumishi wa umma, kuvumilia viongozi wahuni kama akina sabaya Ila alianza kwanza kwa kuvunja kiapo chake cha kuheshimu katiba na sheria za nchi.

Kinachonisikitisha kwa Samia ni kwamba hakuwa mwanafunzi mzuri kwa Magufuli kuweza kujifunza mwenzie alianzia wapi kwenye mserereko wake wa kuanguka. Magufuli alianza kuserereka kuelekea kwenye kufanya udhalimu nchini baada ya kuanza kuvunja sheria na katiba hasa zile zinazowapa wapinzani wake haki fulanifulani ambazo yeye alikuwa hazipendi!

Sasa hebu tazama kiapo cha raisi Samia huku ameshika Qur'an tukufu, anaapa kulinda katiba inayotoa haki kwa Wapinzani kufanya siasa nchi nzima halafu kwenye kiapo hicho anamalizia kwa maneno eeh Mwenyezi Mungu nisaidie, Kisha siku 100 baada ya kiapo hicho anasema vyama vya siasa hakuna kufanya mikutano ya wazi ila vikao vya ndani tu, hivi sheria ndivyo inavyosema?

Samia ameamua kufuata Umagufuli, Umagufuli huu hautomuacha salama, kwa sababu ni njia feki, si njia za haki hata kidogo. ni njia amabzo zimeshakuwa tested na zikafeli sana, na mwishowe aliyezijaribu akaishia kuwa muongo zaidi, muonevu zaidi, mnunua watu wamuunge mkono, mnyamazisha vyombo vya habari ili visikemee udhalimu wake.Kama si udhalimu wake kukema kupitia kifo chake yule mzee alikuwa anatupeleka shimoni.

Samia alikuwa na nafasi adhimu sana ya kufanya reforms za msingi katika nchi hii lkaini ameamua kuwa "caretaker" president kwa kuendeleza umagufuli, bila shaka amejikosesha nafasi adhimu ya kulifanyia mabadiliko ya msingi taifa hili ambayo yangempa heshima kubwa mbele ya umma.

Anasema eti anataka kujenga uchumi kwanza, kiukweli kabisa kutawala kwa mujibu wa sheria hakumzuii mtawala kujenga uchumi, bali ni kutafuta uchochoro wa kutowajibika mbele ya wananchi. Hatuhitaji kwenda mbali kupata mifano, tunaweza kuangalia hapahapa nchini. Hakuna utawala uliovutia Uwekezaji nchini kama utawala wa Kikwete, lakini Kikwete hakuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi.

Ni wakati wa Kikwete tulishuhudi uchumi ukikua kwa asilimia 7 lakini yote haya yalifanyika bila kuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi!. Sasa Samia inakuwaje atwambie eti shughuli za Kisiasa zifanyike kupitia vikao vya ndani tu, hiyo sasa ni siasa gani? Utawapataje wananchama wapya kwa vikao vya ndani?

Samia amewahi kuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba na mwaka 2015 alizunguuka nchi nzima kuinadi ilani ya CCM yenye kutaka tuwe na katiba mpya. Kama CCM imewahi kuataka tuwe na katiba mpya kabla ya kuwa na uchumi wa kati, Samia asitwambie eti tusubiri akuze kwanza uchumi ndo tuwe na katiba mpya wakati sasa hivi tayari tupo kwenye uchumi wa kati. Au anataka kwanza tuwe Donnor country ndo tuwe na katiba mpya?

Lugha aliyotumia ya kuwa ngoja kwanza akuze uchumi kimsingi anamaanisha kuwa Hataki katiba mpya. Ni sawa na mtu anayeaandika bango nje ya duka lake kuwa mkopo kesho, kesho yake ikifika bango bado linasoma vile vile kuwa mkopo kesho!, Sasa kukuza uchumi ni kazi isiyoisha, hakuna siku uchumi utatosha maana kuujenga ni kazi isiyoisha!

Kiukweli kabisa suala la Katiba mpya kamwe halikwepeki, ni kujitia upofu tu kukwepa suala hili. Kuna mahitaji ya utekelezaji wa sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012, Kuna mgongano wa katiba ya Muungano na ya Zanzibar kwenye amsuala ya muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, katiba ya sasa bado inatambua muundo wa zamani wa serikali ya SMZ, Kuna ukweli kuwa nchi sasa ikpo katika mfumo wa vyama vingi lakini katiba ya sasa ni ya mfumo wa chama kimoja. Kwa hiyo Katiba mpya haikwepeki.

Tangu zamani palipokuwa pakitokea tukio kubwa nchini, liliambatana na mabadiliko ya katiba
  • Tulipopata uhuru, muda mchache baadae tulikuwa na katiba ya Jamhuri
  • Tulipoungana na Zanzibar tuliingiza mambo ya muungano kwenye katiba
  • Mwaka 77 baada ya Muungano wa ASP na CCM kulizaliwa hii katiba ya sasa ya Chama kimoja
  • Miaka iliyofuata mabadiliko yalifanyika kuingiza muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya katiba

Sasa mwaka 2010 kulitokea mabadiliko ya muundo wa serikali ya Zanzibar, Kwa nini Katiba ya nchi haibadilishwi ili kuaccomodate jambo hili?

Samia aache kutafuta wepesiwepesi, asimame sasa kama mkuu wa nchi arekebisha discrepancy hii.

UCHUMI TUTAUJENGA TUTAENDELEA KUUJENGA, YEYE SIYO WA KWANZA AU WA MWISHO KUJENGA UCHUMI, SASA HIVI ANATKIWA AFANYE VYOTE YAANI REFORMS ZA MSINGI ZA NAMNA YA KUENDESHA NCHI HII PAMOJA NA UCHUMI

Naunga mkono hoja ila nisiache kuchomokea haya:

1. Rais kaapa kuiheshimu na kuilinda katiba
2. Kwa mujibu wa katiba serikali ni ya wananchi
3. Zaidi sana ya kuwa mwenyekiti wa CCM yeye ni rais wa nchi.
4. Kama rais anawajibika kuwa rais wa wote ikiwamo kuwasikiliza wote
5. Asiwachekee wanaomsukuma kuwabagua wengine, asikilize hoja za wote:

 
Kiufupi It seems mwanzoni Samia alikuwa anajua hii nchi inahitaji nini haswa ila sasa hivi kadri anavyozunguukwa na wahafidhina, ameanza kusahau hasa nini nchi hii inahitaji au amenogewa na madaraka kwa hiyo hataki vitu vinavyoweza kumchallenge ktk uongozi wake. Kiufupi anaogopa siasa za hoja, ameamua kuwafunga mikono wapinzani wake kama alivyofanya Magufuli akaishia kufanya mambo ya ajabuajabu
Mungu kawalahisishia ccm kwa kumtoa Magufuli kilichobaki uamuzi ni wao, ila inaonekana kama ni sikio la kufa halisikii dawa, uzuri Magufuli ameshaonyesha njia, kwa uamuzi ni wao, ila wakishupaza shingo wataenda njia aliyopitia Magufuli.
 
endeleeni kumtibua,

siku akikaa na kutafakati kwanini magufuli alifanya yote hayo ndio siku ambayo mtaanza kulia upya.
 
endeleeni kumtibua,

siku akikaa na kutafakati kwanini magufuli alifanya yote hayo ndio siku ambayo mtaanza kulia upya.
Akifanya udhalimu anajifanyia udhalimu yeye mwenyewe nafsi yake maana hataishi milele na wala hatatawala milele
Alikuwepo mtu mmoja mbabe nchi hii anaitwa Magufuli, yuko wapi?
 
Ufe ukiwa umefanya mambo ya maana ya kukumbukwa siyo unakufa watu wanashukuru
hata kristo alikufa kuna watu walishukuru.

mambo ya maana ni mtambuka,kwako yanawezakuwa upuuzi tu kwa mwingine.

kwa taifa hili jpm atabaki kuwa kiongozi bora wa muda wote,pamoja na kutiwafaa watu wachache kwa ubinafsi wao.
 
Biashara ya utalii imeanza kudhorota, booking nyingi zimekua cancelled tokana na kuthibitisha Tanzania kuna wagonjwa wa corona, wanaotegemea utalii kupata ugali wao wa kila siku ni kufunga mkanda sasa, msoto unandelea, hakuna matumaini tena
 
Biashara ya utalii imeanza kudhorota, booking nyingi zimekua cancelled tokana na kuthibitisha Tanzania kuna wagonjwa wa corona, wanaotegemea utalii kupata ugali wao wa kila siku ni kufunga mkanda sasa, msoto unandelea, hakuna matumaini tena
kama taifa bado hatujui ukubwa wa matatizo tuliyo nayo.

wakati jpm anaonyesha misimamo yake,wapo wanaume lege lege walimdhihaki.
huyu atatuweka lockdown muda sio mrefu.
 
Hizo tuhuma zote kwa JPM unaweza kudhibitisha? Unaweza thibitisha Mungu alimuondoa kwa sababu ya mambo yake? Mkuu mimi naona sio busara kuongea hata mambo yasiyokuhusu na yasiyokua na kithibitisho.

By the way Tunayoyatafuta ni ya Duniani ya Mda mfupi tu.
 
Kama Samia atakuwa ni mtu wa kukaa chini na kufikiri kwa makini basi atagundua kuwa yeye kuwa hapo siyo accident, Bali Mwenyezi Mungu amemuweka hapo kwa sababu maalum.

Machozi na vilio ambavyo watanzania walipitia katika utawla wa Magufuli, Mwenyezi Mungu aliamua kuwafanyia wepesi kwa kumuondoa mtu ambaye kila mtu alishaona kuwa hashikiki tena, hawezekaniki tena, anachokitaka yeye anaweza kukifanya na asiwepo mtu wa kusema fyoko, na yeyote aliyethubutu basi alikiona cha mtema kuni.

Magufuli hakuanza hivihivi kuanza kubambika watu kesi, kufanya kazi na vikundi vya watu wasiojulikana, kupora korosho za watu, kuvunja nyumba za wananchi kikatili, kuonea wafanyabiashara, kuonea wapinzani, kufukuza watu kazi kwenye hadhara kinyume cha taratibu za utumishi wa umma, kuvumilia viongozi wahuni kama akina sabaya Ila alianza kwanza kwa kuvunja kiapo chake cha kuheshimu katiba na sheria za nchi.

Kinachonisikitisha kwa Samia ni kwamba hakuwa mwanafunzi mzuri kwa Magufuli kuweza kujifunza mwenzie alianzia wapi kwenye mserereko wake wa kuanguka. Magufuli alianza kuserereka kuelekea kwenye kufanya udhalimu nchini baada ya kuanza kuvunja sheria na katiba hasa zile zinazowapa wapinzani wake haki fulanifulani ambazo yeye alikuwa hazipendi!

Sasa hebu tazama kiapo cha raisi Samia huku ameshika Qur'an tukufu, anaapa kulinda katiba inayotoa haki kwa Wapinzani kufanya siasa nchi nzima halafu kwenye kiapo hicho anamalizia kwa maneno eeh Mwenyezi Mungu nisaidie, Kisha siku 100 baada ya kiapo hicho anasema vyama vya siasa hakuna kufanya mikutano ya wazi ila vikao vya ndani tu, hivi sheria ndivyo inavyosema?

Samia ameamua kufuata Umagufuli, Umagufuli huu hautomuacha salama, kwa sababu ni njia feki, si njia za haki hata kidogo. ni njia amabzo zimeshakuwa tested na zikafeli sana, na mwishowe aliyezijaribu akaishia kuwa muongo zaidi, muonevu zaidi, mnunua watu wamuunge mkono, mnyamazisha vyombo vya habari ili visikemee udhalimu wake.Kama si udhalimu wake kukema kupitia kifo chake yule mzee alikuwa anatupeleka shimoni.

Samia alikuwa na nafasi adhimu sana ya kufanya reforms za msingi katika nchi hii lkaini ameamua kuwa "caretaker" president kwa kuendeleza umagufuli, bila shaka amejikosesha nafasi adhimu ya kulifanyia mabadiliko ya msingi taifa hili ambayo yangempa heshima kubwa mbele ya umma.

Anasema eti anataka kujenga uchumi kwanza, kiukweli kabisa kutawala kwa mujibu wa sheria hakumzuii mtawala kujenga uchumi, bali ni kutafuta uchochoro wa kutowajibika mbele ya wananchi. Hatuhitaji kwenda mbali kupata mifano, tunaweza kuangalia hapahapa nchini. Hakuna utawala uliovutia Uwekezaji nchini kama utawala wa Kikwete, lakini Kikwete hakuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi.

Ni wakati wa Kikwete tulishuhudi uchumi ukikua kwa asilimia 7 lakini yote haya yalifanyika bila kuminya uhuru wa kisiasa wa wananchi!. Sasa Samia inakuwaje atwambie eti shughuli za Kisiasa zifanyike kupitia vikao vya ndani tu, hiyo sasa ni siasa gani? Utawapataje wananchama wapya kwa vikao vya ndani?

Samia amewahi kuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba na mwaka 2015 alizunguuka nchi nzima kuinadi ilani ya CCM yenye kutaka tuwe na katiba mpya. Kama CCM imewahi kuataka tuwe na katiba mpya kabla ya kuwa na uchumi wa kati, Samia asitwambie eti tusubiri akuze kwanza uchumi ndo tuwe na katiba mpya wakati sasa hivi tayari tupo kwenye uchumi wa kati. Au anataka kwanza tuwe Donnor country ndo tuwe na katiba mpya?

Lugha aliyotumia ya kuwa ngoja kwanza akuze uchumi kimsingi anamaanisha kuwa Hataki katiba mpya. Ni sawa na mtu anayeaandika bango nje ya duka lake kuwa mkopo kesho, kesho yake ikifika bango bado linasoma vile vile kuwa mkopo kesho!, Sasa kukuza uchumi ni kazi isiyoisha, hakuna siku uchumi utatosha maana kuujenga ni kazi isiyoisha!

Kiukweli kabisa suala la Katiba mpya kamwe halikwepeki, ni kujitia upofu tu kukwepa suala hili. Kuna mahitaji ya utekelezaji wa sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012, Kuna mgongano wa katiba ya Muungano na ya Zanzibar kwenye amsuala ya muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, katiba ya sasa bado inatambua muundo wa zamani wa serikali ya SMZ, Kuna ukweli kuwa nchi sasa ikpo katika mfumo wa vyama vingi lakini katiba ya sasa ni ya mfumo wa chama kimoja. Kwa hiyo Katiba mpya haikwepeki.

Tangu zamani palipokuwa pakitokea tukio kubwa nchini, liliambatana na mabadiliko ya katiba
  • Tulipopata uhuru, muda mchache baadae tulikuwa na katiba ya Jamhuri
  • Tulipoungana na Zanzibar tuliingiza mambo ya muungano kwenye katiba
  • Mwaka 77 baada ya Muungano wa ASP na CCM kulizaliwa hii katiba ya sasa ya Chama kimoja
  • Miaka iliyofuata mabadiliko yalifanyika kuingiza muundo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya katiba

Sasa mwaka 2010 kulitokea mabadiliko ya muundo wa serikali ya Zanzibar, Kwa nini Katiba ya nchi haibadilishwi ili kuaccomodate jambo hili?

Samia aache kutafuta wepesiwepesi, asimame sasa kama mkuu wa nchi arekebisha discrepancy hii.

UCHUMI TUTAUJENGA TUTAENDELEA KUUJENGA, YEYE SIYO WA KWANZA AU WA MWISHO KUJENGA UCHUMI, SASA HIVI ANATKIWA AFANYE VYOTE YAANI REFORMS ZA MSINGI ZA NAMNA YA KUENDESHA NCHI HII PAMOJA NA UCHUMI
Endeleea kujamba jamba tu humu jf..hauna loloteee...subir sindano iingine vizur..hakuna watz walio lia enzi za utawala wa jpm..kama wewe uliliaa bas ulikuwa mla rushwaa..cheti feki..mtu wa madawa ya kulevyaa..na mengineyoo..
 
Back
Top Bottom