#COVID19 Tumsikilize mchungaji Gwajima, tusimbeze. Chanjo zote zina bechi tofauti na kuna nchi hukataa baadhi ya bechi na nyingine ni zile zilizobakia

Huwezi kuchagua baadhi tu ya hoja za Gwajima halafu ukasema ana mantiki kwenye hii ishu. Huyu jamaa anadai miaka 5 baadaye Wazungu watakuwa wanawasha laptop zao na kuwa control Waafrika waliochanjwa kama mazombi au misukule. Mtu kama huyu kweli atakuwa serious?
 
Mbona dna inaweza kua manipulated kwa njia nyingi ili kutuma msg kwa rna ili itengeneze proteins za aina tofauti, ndio sayansi ya sasa na kwenye dawa nyingi tu hata anticancers, hata hizo chanjo nyingine ndio ivo ivo
 
Tatizo la gwajima ni kupiga kelele tena kwenye jukwaa ambalo halita ufikisha ujumbe wake na kupatikana
Ufumbuzi!
Atafute jukwaa sahihi akatoe malalamiko hayo!
 
Pia usisahau kuwa wapo wale ambao wamechanjwa na bado wanaambukizwa tena na tena.

Tatizo likiwa na Variant.
 
Jifunze kutumia lugha ya kiungwana. Sie kila alie na maoni tofauti na weye hana akili.

Nimetoa maoni Mchungaji asikilizwe na si kubezwa.

Hayo pia ni maoni yangu haimaanishi kuwa naunga mkono ila nami pia nametoa maoni.
Asikilizwe Nini wakati anatoa lugha ya kebei...Kama time imeshaundwa na imelidhika anataka nini zaidi..
 
Na huyo ushaaaidi unaouonyesha ni maandishi ya wapinga chanjo Huko mwanzo...wenzenu wameachana nao nyie bado
 
Umechambua vizuri,umeongea kutatua matatizo kulingana na mazingira tuliyonayo ni kweli.
Tatizo viongozi kutojiamini hasa kipindi hiki.
JPM aliamua Kama taifa tutumie maombi,kuwatoa watu,hofu na kutumia njia za asili,na nchi ikasonga mbele.Mataifa mengine ndo walitakiwa wajifunze kwetu tumetumia njia zipi.
Sasa viongozi wanajikomba kuwafurahisha wazungu.


 
Pia usisahau kuwa wapo wale ambao wamechanjwa na bado wanaambukizwa tena na tena.

Tatizo likiwa na Variant.
Chanjo za COVID-19 pia husaidia kukuepusha na khali kuwa mbaya na kuzidiwa(seriously Ill), hata ikiwa utapata COVID-19, hali haiuwi mbaya kama wale ambao hawajaipata. Kupata chanjo mwenyewe pia kunaweza kuwalinda watu walio karibu nawe, haswa watu walio katika hatari ya kupata madhara makubwa yanayotokana na COVID-19. Haswa wale wenye magonjwa mengine(underlying medical issues), mfano watu wazima na wale wenye kisukari nk.
 
Na hatimaye alifariki Kwa Corona
 
Hizo ndizo kazi za idara ya ujasusi naamini wamefanya hivyo.

Kukusanya chanjo mbali mbali na kuzifanyia majaribio kabla ya kuzikubali.

Mungu ibariki Tanzania

Mungu atuepushe na mabalaa yeyote.
 
Na hatimaye alifariki Kwa Corona
Wewe na rais tumwamini Nani?
Je wewe mwenzetu utaishi milele?

Je watu karibu 4m.waliokufa huko kwenye mabara mengine ukiondoa Afrika hawajui kujikinga?.
 
Mchungaji Gwajima anahoji, je chanjo wanopewa huko duniani ni sawa na hizi chanjo zilotua jana Dar?

Vipi content yake ni ileile

Je, ni zipi bechi zake ni zilezile zinazosababisha blood clot?

Huoni kuwa huyu mtu auliza masuali ya msingi?
Maswali haya hayana msingi,hizi chanjo zimetoka america kupitia mpango wa who na serikali wenyewe na WHO wamejiridhisha ni salama na zile zile ,sasa kama ngwajima anaamini WHO na America wanafoji chanjo basi ni yeye wa kuleta ushahidi.
Kuhusu batch no. Na kuganda damu,lilikuwa tatizo la mda ambalo lilionekana ni nadra sana na halijaleta madhara kwenye utoaji wa chanjo,katika watu zaid ya million 2 walopewa chanjo kuganda damu lilitokea 8.ndo maana nchi zinakuwa na chanjo zaid ya moja ili kushusha namba hii.
Mi naoongea hapa nna chanjo, batch no. Sio lazima ziendane kama anvyosema mzee ngwaji sababu unaweza ukapewa chanjo ya kwanza mkoa huu na ya pili mkoa mwengine tena kwa dharura wakati mwengine ,sasa hayo mambo ya btch no kulingana wao watKuwa wanatembea na machanjo kila sehemu?.Najua ni vigumu kwa mazingira ya bongo kuelewa kuhusu utaoji wa chanjo na challenge za corona,sababu mitandaoni kumejaa kebehi na dharau,lakin Ngwajima kwa silimia kubwa anapotosha.
 
Naunga mkono.

Gwajima anatakiwa kujibiwa kwa HOJA sio VIROJA.

Kwenye CONTENTS na BATCH ni vitu muhimu sana wasitufanyie CHENJI KOTA na kutuletea nyingine tofauti na zile wanazotumia wao.
 
Kwanza sidhani gwajima kasema hayo kimwenyewe. Lazima atakuwa kesha fanya mazungumzo na madaktari na kumaoa maelezo. Gwajima sio mjinga .

Hizo dawa zinazotolewa na uingereza wanazo ziita left over kwani kwawo washapiga watu wote sikweli only 60%.

Ni sahihi zilitoka batch tafauti.
kwani batch za mwanzo zilikuwa na matatizo na wakaendelea kubadili kila mara kwa kufuata yanayo tokea.
Sasa sisi hatujuwi tunaletewa zipi.
pili hatuna nyenzo za kukabiliana na mtu ambaye akipata matatizo ya chanjo kama yupo kijijini
 
Unajua hii chanjo wengi tuna mashaka nayo kwa sababu shart mojawapo ni ukichanjwa halafu ukapata madhara serikali haitahusika na madhara hayo pambana na hali yako maana yake serikali inakwepa kushitakiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…