LGE2024 Tuna mtaji wa imani ya Watanzania: Dkt. Nchimbi

LGE2024 Tuna mtaji wa imani ya Watanzania: Dkt. Nchimbi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Hamduni

Senior Member
Joined
Apr 25, 2020
Posts
172
Reaction score
118
TUNA MTAJI WA IMANI YA WATANZANIA: NCHIMBI

Azindua kampeni Mwanza akitamba na takwimu za kura za uhakika

Awasihi wanaCCM kila mmoja kutafuta kura 10 kwa ajili ya ushindi wa kishindo


Ahamasisha kampeni za nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu, isiachwe kura hata moja, wakiwemo wapinzani

Awataka washindi kuwatumikia Watanzania kwa kupinga dhuluma na rushwa

IMG-20241120-WA0057.jpg

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema CCM inaingia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kikiwa na imani kubwa ya Watanzania kutokana na uimara wa chama na uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa uimara wa CCM unatokana na wingi na umakini wa wanachama wake, akitoa takwimu jinsi wanachama wapatao milioni 8 wa CCM walivyojitokeza kupiga kura wakati wa mchakato wa ndani ya chama hicho kupata wagombea wa nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

IMG-20241120-WA0050.jpg

Balozi Nchimbi amesema mtaji wa imani ya Watanzania, utumishi wa CCM kupitia sera zake, na uongozi makini unakipatia chama hicho uhakika wa ushindi mkubwa wa kishindo katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024.

Katibu Mkuu huyo wa CCM aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za CCM kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Mkoa wa Mwanza, uliofanyika katika Viwanja vya Furahisha, jijini Mwanza, leo tarehe 27 Novemba 2024.

IMG-20241120-WA0053.jpg

Katika kujihakikishia ushindi huo wa kishindo, Balozi Nchimbi alisisitiza kampeni za kuomba kura ziwalenge hata wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani, ili kuhakikisha kila kura inapatikana kwa ajili ya CCM, akiwahamasisha kupiga kampeni “nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu” nchi nzima.

“Pamoja na uhakika wa kura, msiridhike na ushindi. Twendeni nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu. Tusiache kura hata moja. Kila mwanachama atafute kura 10. Hata wa vyama vya upinzani, wawe ACT, NCCR, Chadema, na wote, watatupigia kura. Tumalizeni huu mchezo kwa kuipatia CCM ushindi mkubwa wa kishindo.

Soma Pia: Dkt. Nchimbi kuzindua kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mkoani Mwanza

IMG-20241120-WA0059.jpg

“Wajibu wetu ni kuwakumbusha tu Watanzania kazi kubwa ambayo CCM imeendelea kufanya katika kutoa uongozi wa nchi hii. Uhakika wa kesho ya Tanzania uko CCM. Watanzania wana imani kubwa na CCM kila wanapofikiria maendeleo, umoja wa nchi yetu, utaifa wetu, amani na utulivu. Tunataka wagombea wetu mtakapochaguliwa mkalinde heshima na imani hii ya Watanzania kwa kuwatumikia vizuri, mkijiepusha na dhuluma na rushwa,” alisema Balozi Nchimbi.

Aidha, akisisitiza kuhusu uimara wa CCM, Balozi Nchimbi alisema CCM ndiyo chama pekee ambacho wanachama wake, kwa mamilioni, walijitokeza kushiriki mchakato wa ndani wa kupata wagombea, hasa kupitia kura za maoni. Hii ndiyo sababu kimesimamisha wagombea maeneo yote nchi nzima katika uchaguzi huo, kwa kuwa kimeenea nchi nzima, tofauti na vyama vingine vya upinzani.

#Ends
 

Attachments

  • IMG-20241120-WA0055.jpg
    IMG-20241120-WA0055.jpg
    667.4 KB · Views: 6
Chama cha kutangazwa washindi kwa kuwahujumu wapinzani wa kweli. Chama kilichofanya box la kura kuwa maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
CCM hakina ushawishi tena kwa wapiga kura ndiyo maana wameengua wagombea wa upinzani ili kukwepa aibu ya kushindwa vibaya.
 
TUNA MTAJI WA IMANI YA WATANZANIA: NCHIMBI

Azindua kampeni Mwanza akitamba na takwimu za kura za uhakika

Awasihi wanaCCM kila mmoja kutafuta kura 10 kwa ajili ya ushindi wa kishindo


Ahamasisha kampeni za nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu, isiachwe kura hata moja, wakiwemo wapinzani

Awataka washindi kuwatumikia Watanzania kwa kupinga dhuluma na rushwa


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema CCM inaingia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kikiwa na imani kubwa ya Watanzania kutokana na uimara wa chama na uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa uimara wa CCM unatokana na wingi na umakini wa wanachama wake, akitoa takwimu jinsi wanachama wapatao milioni 8 wa CCM walivyojitokeza kupiga kura wakati wa mchakato wa ndani ya chama hicho kupata wagombea wa nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.


Balozi Nchimbi amesema mtaji wa imani ya Watanzania, utumishi wa CCM kupitia sera zake, na uongozi makini unakipatia chama hicho uhakika wa ushindi mkubwa wa kishindo katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024.

Katibu Mkuu huyo wa CCM aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za CCM kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Mkoa wa Mwanza, uliofanyika katika Viwanja vya Furahisha, jijini Mwanza, leo tarehe 27 Novemba 2024.


Katika kujihakikishia ushindi huo wa kishindo, Balozi Nchimbi alisisitiza kampeni za kuomba kura ziwalenge hata wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani, ili kuhakikisha kila kura inapatikana kwa ajili ya CCM, akiwahamasisha kupiga kampeni “nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu” nchi nzima.

“Pamoja na uhakika wa kura, msiridhike na ushindi. Twendeni nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu. Tusiache kura hata moja. Kila mwanachama atafute kura 10. Hata wa vyama vya upinzani, wawe ACT, NCCR, Chadema, na wote, watatupigia kura. Tumalizeni huu mchezo kwa kuipatia CCM ushindi mkubwa wa kishindo.

Soma Pia: Dkt. Nchimbi kuzindua kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mkoani Mwanza


“Wajibu wetu ni kuwakumbusha tu Watanzania kazi kubwa ambayo CCM imeendelea kufanya katika kutoa uongozi wa nchi hii. Uhakika wa kesho ya Tanzania uko CCM. Watanzania wana imani kubwa na CCM kila wanapofikiria maendeleo, umoja wa nchi yetu, utaifa wetu, amani na utulivu. Tunataka wagombea wetu mtakapochaguliwa mkalinde heshima na imani hii ya Watanzania kwa kuwatumikia vizuri, mkijiepusha na dhuluma na rushwa,” alisema Balozi Nchimbi.

Aidha, akisisitiza kuhusu uimara wa CCM, Balozi Nchimbi alisema CCM ndiyo chama pekee ambacho wanachama wake, kwa mamilioni, walijitokeza kushiriki mchakato wa ndani wa kupata wagombea, hasa kupitia kura za maoni. Hii ndiyo sababu kimesimamisha wagombea maeneo yote nchi nzima katika uchaguzi huo, kwa kuwa kimeenea nchi nzima, tofauti na vyama vingine vya upinzani.

#Ends
kwa umoja wetu na imani ya waTanzania kwa CCM, ushindi wa uhakika wa kishindo kikuu ni Lazima.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi 🐒

Mungu Ibariki Tanzania 🌹
 
Hivi una akili timamu kweli wewe?😀😀Kwa hiyo ulitaka waachwe tu hata kama hawajakidhi vigezo?
Wewe ndiye huna akili kushabikia ubakaji wa demokrasia. Bila upuuzi aliofanya huyu gaidi Mchengerwa CCM ingeaibika vibaya mno.
 

TUNA MTAJI WA IMANI YA WATANZANIA: NCHIMBI

Azindua kampeni Mwanza akitamba na takwimu za kura za uhakika

Awasihi wanaCCM kila mmoja kutafuta kura 10 kwa ajili ya ushindi wa kishindo

Ahamasisha kampeni za nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu, isiachwe kura hata moja, wakiwemo wapinzani

Awataka washindi kuwatumikia Watanzania kwa kupinga dhuluma na rushwa

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema CCM inaingia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kikiwa na imani kubwa ya Watanzania kutokana na uimara wa chama na uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa uimara wa CCM unatokana na wingi na umakini wa wanachama wake, akitoa takwimu jinsi wanachama wapatao milioni 8 wa CCM walivyojitokeza kupiga kura wakati wa mchakato wa ndani ya chama hicho kupata wagombea wa nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Balozi Nchimbi amesema mtaji wa imani ya Watanzania, utumishi wa CCM kupitia sera zake, na uongozi makini unakipatia chama hicho uhakika wa ushindi mkubwa wa kishindo katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024.

Katibu Mkuu huyo wa CCM aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za CCM kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Mkoa wa Mwanza, uliofanyika katika Viwanja vya Furahisha, jijini Mwanza, leo tarehe 27 Novemba 2024.

Katika kujihakikishia ushindi huo wa kishindo, Balozi Nchimbi alisisitiza kampeni za kuomba kura ziwalenge hata wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani, ili kuhakikisha kila kura inapatikana kwa ajili ya CCM, akiwahamasisha kupiga kampeni “nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu” nchi nzima.

“Pamoja na uhakika wa kura, msiridhike na ushindi. Twendeni nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu. Tusiache kura hata moja. Kila mwanachama atafute kura 10. Hata wa vyama vya upinzani, wawe ACT, NCCR, Chadema, na wote, watatupigia kura. Tumalizeni huu mchezo kwa kuipatia CCM ushindi mkubwa wa kishindo.

“Wajibu wetu ni kuwakumbusha tu Watanzania kazi kubwa ambayo CCM imeendelea kufanya katika kutoa uongozi wa nchi hii. Uhakika wa kesho ya Tanzania uko CCM. Watanzania wana imani kubwa na CCM kila wanapofikiria maendeleo, umoja wa nchi yetu, utaifa wetu, amani na utulivu. Tunataka wagombea wetu mtakapochaguliwa mkalinde heshima na imani hii ya Watanzania kwa kuwatumikia vizuri, mkijiepusha na dhuluma na rushwa,” alisema Balozi Nchimbi.

Aidha, akisisitiza kuhusu uimara wa CCM, Balozi Nchimbi alisema CCM ndiyo chama pekee ambacho wanachama wake, kwa mamilioni, walijitokeza kushiriki mchakato wa ndani wa kupata wagombea, hasa kupitia kura za maoni. Hii ndiyo sababu kimesimamisha wagombea maeneo yote nchi nzima katika uchaguzi huo, kwa kuwa kimeenea nchi nzima, tofauti na vyama vingine vya upinzani.

#Ends
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-11-20 at 23.17.57.mp4
    27.4 MB
  • WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.29.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.29.jpeg
    1.3 MB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.31.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.31.jpeg
    627.1 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.36.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.36.jpeg
    1 MB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.35 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.35 (1).jpeg
    1.1 MB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.34.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-20 at 19.30.34.jpeg
    539.1 KB · Views: 4
Kuna shida kubwa sana huko ccm.. Wanaishi maisha ya kufikirika mno hawa viongozi wake! Na ni watu na elimu zao
Kweli nimeamini kusoma sio kuelimika
 
Back
Top Bottom