Tunafikiri kwa kutumia lugha gani?

Tunafikiri kwa kutumia lugha gani?

Mkuu @Kram billz unaposema kiziwi na Kipofu wanatumia lugha zao za asili ya jamii waliyomo una maana kwamba Kipofu aliye kiziwi anawezaje kusikia na kuona yale yanayoendelea ktk jamii yake hadi afikie kuwa na uwezo wa kufikiri kwa lugha ya jamii yake?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ktk hili suala hapa labda kwa kipofu na bubu ndilo lilikuwa kwenye mada kuhusu hili suala la mtu kuwa kiziwi n kipofu hapa huyu mtu hawez kuzumzungumza kwa kutumia lugha kwasababu zifuatazo:-mbaka lugha iweze kutumika na mtu anapaswa kuwa na organs ambazo ni sense organs ndan yake kuna organs nyngne ambazo zinaweza kuproduce different sounds kwa upande wa spoken ila kwa hao watu kuna baadhi ya vitu wanamiss so kuna wawili kutoweza kutumia lugha kwa kuandika n kuzungumza au kuweza kimoja kati ya hvyo apo
So kwa kesi ya mtu ambae ni kipofu n kiziwi kiukwel ni vigumu kutumia lugha kwa kufikiria labda nahc Mungu amewapa uwezo wao binafsi wa kufikiria
 
Kwamba unafikiria kwa kuumia lugha gani sisi haina tja kwetu, tunachojali baada ya kufikiria kwa kihindin au kinyakyusa unatueleza maoni yako kwa kutmia lugha gani kwa ufasaha. Kuna wahinindi ambao hawajui kujieleza kwa ufasaha wakitumia kihindi bali wakitumia kinyakyusa utawaelewa vizuri zaidi. The converse s also true.
 
Mkuu Lekanjobe hapa hoja sio uwezo wa kutoa maoni kwani unaweza kutumia lugha yoyote hata ya ishara, ila hapa tunaangalia hatua ya kwanza ya kufikiri ambayo ndio hupelekea kuelezea hoja ama chochote kupitia lugha yoyote inayojulikana kwa mhusika.
 
Last edited by a moderator:
badilisha heading iwe kiziwi na bubu wanatumia lugha gani kufikiri naona maswali yako mengi yameegemea huko.
 
badilisha heading iwe kiziwi na bubu wanatumia lugha gani kufikiri naona maswali yako mengi yameegemea huko.

Hoja ni lugha inayotumika kufikiri, hayo ya vipofu na viziwi ni kama challenge tu ya kuwafanya watu wafikiri kwani mtu anaposema tunafikiri kwa kutumia lugha tunayoitumia vp kwa kiziwi asiyesikia chochote na kipofu asiyeoona chochote? kwa vyovyote vile hakuna anayeweza kusema kwamba hao watu hawafikiri, ndio maana nikawatumia hao ili kuwaongeza vision tu.
 
Mm naongea lugha tano, pamoja kwamba inategemea na kitu unachofanya japokuwa kunakuwa kama kuna in-situ translation kutoka lugha moja kwenda nyingine lakini mother tongue ndo inayotawala. Na usishangae wakati mwingine uko kwenye mazungumzo kwa mfano ya kiingereza ukajikuta umetumia neno la kifaransa bila kujua.
 
Mm naongea lugha tano, pamoja kwamba inategemea na kitu unachofanya japokuwa kunakuwa kama kuna in-situ translation kutoka lugha moja kwenda nyingine lakini mother tongue ndo inayotawala. Na usishangae wakati mwingine uko kwenye mazungumzo kwa mfano ya kiingereza ukajikuta umetumia neno la kifaransa bila kujua.

Hoja ni lugha ya kufikiri sio kuzungumza.
 
Hoja ni lugha ya kufikiri sio kuzungumza.

Hujaelewa context kwa ujumla, suala suala la kuwa unafikiri kwa lugha gani linaanza kama unazungumza lugha zaidi ya moja. Na nikasema pamoja na hizo lugha ninazozungumza ila mara nyingi nafikiri kwa kutumia lugha mama. Lakini wakati mwingine inategemea na kitu unachofikiri na ukiwa unafikiri kunaweza kukawa na in-situ translation. Au neno lugha tano ndo limekukwaza!!!?
 
Hujaelewa context kwa ujumla, suala suala la kuwa unafikiri kwa lugha gani linaanza kama unazungumza lugha zaidi ya moja. Na nikasema pamoja na hizo lugha ninazozungumza ila mara nyingi nafikiri kwa kutumia lugha mama. Lakini wakati mwingine inategemea na kitu unachofikiri na ukiwa unafikiri kunaweza kukawa na in-situ translation. Au neno lugha tano ndo limekukwaza!!!?

We ndo hujanielewa, naomba ujenge hoja yako huku ukilinganisha watu wasio na uwezo wa kuona na kusikia.
 
Ni lugha ipi ambayo mtu huitumia wakati anafikiri? binafsi nimeshindwa kujua lugha nnayotumia wakati wa kufikiri(sio kuzungumza),
Vipi kwa wale wanaotumia lugha zaidi ya moja ktk kuzungumza, je kabla ya kuamua kuzungumza anakuwa amefikiri kwa lugha ipi? kwani anaweza kuchagua ni lugha ipi aitumie, lakini lugha ya kufikiri ni moja tu, kufikia hapo ndipo nnapotaka kujua lugha ya kufikiri ni ipi?

Fikra huwa ni mfano wa picha ambayo mtu hutengeneza ndani ya akili yake na kwa kawaida picha huwa haina lugha!
 
Ni lugha ipi ambayo mtu huitumia wakati anafikiri? binafsi nimeshindwa kujua lugha nnayotumia wakati wa kufikiri(sio kuzungumza),
Vipi kwa wale wanaotumia lugha zaidi ya moja ktk kuzungumza, je kabla ya kuamua kuzungumza anakuwa amefikiri kwa lugha ipi? kwani anaweza kuchagua ni lugha ipi aitumie, lakini lugha ya kufikiri ni moja tu, kufikia hapo ndipo nnapotaka kujua lugha ya kufikiri ni ipi?

Lugha uliyozoea
 
Lugha uliyozoea

Kwa mfano, kiziwi asiyewahi kusikia sauti yoyote ya mtu au kitu, halafu pia ni kipofu kwa maana ya kwamba hajawahi kuona taswira ya kitu chochote, je huyo anafikiri kutumia lugha ipi?
 
Kwa mfano, kiziwi asiyewahi kusikia sauti yoyote ya mtu au kitu, halafu pia ni kipofu kwa maana ya kwamba hajawahi kuona taswira ya kitu chochote, je huyo anafikiri kutumia lugha ipi?

Lugha inamaana pana, yeye kwa jinsi anavyowasiliana hata kama ni kwa hisia kwa mfano harufu ndivyo atakavyofikiria, ndio lugha aliyozoea hiyo. Bubu anayeona atawaza kwa lugha yake, kiziwi na bubu ila anaona analugha yake, kipofu anayesikia na kunusa analugha yake atafikiri na kuwaza kwa kutumia lugha hiyo aliyozoea.
 
Lugha inamaana pana, yeye kwa jinsi anavyowasiliana hata kama ni kwa hisia kwa mfano harufu ndivyo atakavyofikiria, ndio lugha aliyozoea hiyo. Bubu anayeona atawaza kwa lugha yake, kiziwi na bubu ila anaona analugha yake, kipofu anayesikia na kunusa analugha yake atafikiri na kuwaza kwa kutumia lugha hiyo aliyozoea.

Unajua maana ya lugha?
 
Ni utaratibu rasmi wa kuwasiliana kati ya binaadamu na binaadamu au wanyama wowote mwenye akili.

Duh! kama ni utaratibu wa kuwasiliana, ina maana mtu anapofikiri kitu/jambo fulani ni lazima kuwe na haja ya kuwepo mtu mwingine wa kuwasiliana naye?
 
Back
Top Bottom