Tunajua Mengi tunanyamaza, Lissu kudharau Mamlaka ya Ikulu kumefanya kufifisha juhudi zilizopangwa na Rais Samia kuleta maridhiano

Tunasubiri maandamano ya CDM kwa hamu kubwa, hakuna cha maridhiano wala nini, Mama mwenyewe tunamnyoa kwa wembe, CDM ndiyo chama kikuu cha Upinzani na ukombozi TZ, nguvu ya umma ipo nyuma yetu, tukiitisha maandamano leo watu mil 7 wanaingia barabarani, kwanza huyo Mbowe tukiamua hata leo hii tunamtoa Segerea!! Alisikika mlevi mmoja kutoka Ufipa!! Makamanda gani wakiona polisi hadi wanajikojolea
 
Hawa vijana wa ccm wanajitungia tu uozo ili wafurahishane
 
Who is Tundu Lissu to say our president is incapable?!!

Who is he by the way?!!!

Deluded chap?

Psychopath?!!!

How would one treat this guy nicely while he got bad tough.....

It is havoc......

SIEMPRE URT!
Come on!

Can you actually prove that Lissu said so?

When it comes to Lissu you believe any negativity raises against him,why?

B'se you have that 'Lissuphobia' in your mindset,take it easy.
 
Kama ni kweli uliyoyaandika, sasa mama analaumiwa nini wakati issue ni ujuaji wa jamaa.

Moja ya changamoto ya jamaa yetu ni ujuaji na kujiona anahaki kesho apewe nchi aiongoze kana kwamba kuna jambo kuubwa aliifanyia nchi na nchi inapaswa kumlipa....aka ujivuni...
 
Mzee acha Uwongo....mmekula za MABEBERU Mbowe mtamtoa tu.....
 
Umeandika nini sasa
 
Hawa vijana wa ccm wanajitungia tu uozo ili wafurahishane

..exactly.

..hawa vijana wanaamini Watz ni wajinga ndio maana wanatuletea maandiko kama haya.

..hakuna ulazima wa Rais SSH kukutana na Chadema, au hata vyama vingine vya upinzani.

..Raisi angeweza kuamua kwamba vyombo vya dola viheshimu sheria ya vyama vya siasa kwa kutovibugudhi wakati wa mikutano yao.

..Raisi na serikali yake wanaweza kupeleka mswada bungeni kuhusu kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

..Raisi na serikali wanaweza kufuta kesi zote za kisiasa na tukasonga mbele vyama vikiwa vimeridhiana.

..Raisi hajatekeleza yote hayo lakini mtoa mada anaelekeza lawama kwa Tundu Lissu.

..Binafsi naamini Rais na serikali hawajafanya kwasababu hawaamini ktk haki na usawa miongoni mwa vyama vya siasa. Pia hawaamini ktk Tume huru ya uchaguzi.
 
Mkuu acha propaganda za uongo. Kwahiyo mna mtesa Mbowe kwasababu alisema mams hana uwezo wa kuongoza?

Mmechagua njia haramu, endeleeni nayo. Lissu ni level nyingine. Uongo wenu mtaumbuka.
 
Nyie ni watu hovyo kabisa. Watu wanaoumizwa ndio mnawalaumu?

Mnaua biashara za watu ili wawapigie magoti?

Akili ya hovyo kabisa hii.
 
Lissu alianza kuongea sana na kumdharau Sa100, kibaya zaidi hata kama anahoja ila presentation yake hakuna anayeweza kuivumilia hasa huku kwetu Africa.
 
Ukishindwa kupigana nae basi join nae walitakiwa upinzani wafanye hivyo lkn kiburi chao sasa kinawaonyesha ndio Fatma Karume akamwambia Lissu Huna ADABU.
Kila siku nikisema huyu TL ni mpuuzi mnakataa. Huwa hajitambui, tatizo lake anafikiri ni yeye tu anaweza kuongoza hii nchi. Mbowe is an intelligent man ingawa ana kazi mbili
 

Mbona haueleweki? Unataka kutuaminisha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) alimpigia simu Lissu bila kupitia kwa wasaidizi wake? Halafu Lissu akamtolea nje, na kumtaka Rais wake afuate utaratibu ndio aweze kuongea nae? Au aliyeambiwa hivyo ni msaidizi wa Rais aliyepiga simu kwa niaba ya Rais? Halafu baada ya utovu huo wa nidhamu alio uonyesha Lissu, Rais wa JMT akampigia tena, lakini kwa kiburi Lissu hakupokea simu huku akijua inatoka kwa Rais? Na kuwa Mbowe ana kesi kwa sababu Rais wa JMT, Amiri Jeshi Mkuu wetu alikasirika alipoambiwa kuwa anadharauliwa kwa sababu ni mwanamke! Hilo tu ndio limemfanya aangalie tu wakati Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani akiwa ameswekwa ndani kwa mashtaka ambayo anajua hayana mashiko? Unataka kutuaminisha kuwa Rais wetu yuko so petty kuwa anakubali hali hii itokee kwa sababu kuna raia wake ana doubt uwezo wake wa kuongoza nchi? Yaani kwa kumtia ndani Mbowe ndio atamthibitishia Lissu kuwa pamoja na yeye kuwa mwanamke ana uwezo sana wa kuongoza nchi yake?

Mimi nadhani hapa lengo ni kumchafua Mheshimiwa Rais wa JMT kwa kuonyesha kuwa anatawaliwa na 'emotions' na kuwa ni rahisi kuyumbishwa ( kwanza wakina Warioba halafu sasa wakina Sirro). Kwa hili hamumtendei haki kabisa.

Kingine ni kuwa mnataka kuleta mpasuko katika uongozi wa Chadema kwa kuonyesha kuwa anayesababisha matatizo yao ni Lissu ambae amejaa kiburi na jeuri. Hilo nalo sio kweli kwa sababu Lissu alieleza kwa nini hakuweza kuongea na Ikulu alipopigiwa simu. Version yake ni kuwa alijaribu kuwapigia Ikulu alipokuwa na nafasi lakini hakufanikiwa.

Paragraph ya mwisho haiendani kabisa na yaliyotangulia. Kwa sababu hiyo itakuwa vyema kama utanisahihisha pale ambapo sikukuelewa ili nikuombe msamaha.

Amandla...
 
Samia ni rais dhaifu ka babake mwinyi, kujitutumua anakofanya ni kujaribu kuficha udhaifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…