Zanzibar 2020 Tunakubaliana na maridhiano, lakini Maalimu Seif na ACT Wazalendo lazima muwajibu Watanzania haya

Bwana Mnyika ndio kabisa hakuna kitu pale
 
Perfect.
Kabla ya jambo lolote lile, ACT walipaswa waseme kwanza wameridhiana na CCM kwa lipi hasa, msingi wa maridhiano yao ni upi, na kipi tukitegemee kitazaliwa na maridhiano yao?

Kuhusu kuwa wanachama wa ACT walipiga kura kuamua kuingia kwenye SUK, hilo nalo siliamini kwa 100% kwa sababu mbili.
(i)Wanachama wa ACT hawakujulishwa mantiki ya kile ambacho chama chao kimepanga kukifanya.
(ii)Hatukuona mchakato wowote wa ndani ya ACT wa kupiga hizo kura.
 

 
Shukrani sana mkuu
 
Katiba huwa mwamvuli kwa yale yanayowafurahisha tu. Wanapoivunja hawaikumbuki kabisa.
 
Mngekuwa mnahoji pia kuhusu mishahara ya wafanyakazi wa ACT na pango za majengo zinalipwaje bila nyie kushirikishwa ingekuwa poa sana
 
Kaka,Yerico kabla hatujaisimanga ACT Wazalendo Hata nyie CDM mna maswali ya Kujibu Kwann madiwani wenu wameapa na watakuwa madiwani wakat uchaguz hamuutambui?..

Pili kwann ishu ya maridhiano ya wazanzbar Nyie wabara ndo mmekua mna uchungu nayo?

Tatu Maalim hakuingia serikalin 2015--2020 je Chuki,hasama ziliongezeka au Kupungua?..
Achen unafiki kama mnajiona Mpo sahihi mngemfukuza Aidan wa nkasi ma madiwan wenu woote nchi nzma waloapa
 
Wanachgua vipengele vinavyo wa fauvor wanasiasa na ulaji kuliko vyenye maslahi kwa wananchi

Mfano sisi wananchi tunaumizwa na mfumo wa Kodi

Hakuna mwanasiasa anayelipa Kodi

Nani atusemee

Seif na act wameuuza mechi
 

KILICHOFANYWA NA ACT NA MAALIM SIO MARIDHIANO
Kumekuwa na maoni mengi hasa baada ya ACT Wazalendo na MAALIM kukubali yaishe kwa Serikali ya mapinduzi Zanzibar, kumekuwa na na majibu hasa kutoka kwa ACT Wazalendo wakitetea walichokifanya kwamba ni kukidhi takwa la katiba ya Zanzibar juu serikali ya umoja wa kitaifa.

Watetezi kutoka ACT Wazalendo wanaita ni maridhiano,kwa mtizamo wangu haya si maridhiano bali ni kukimbilia madaraka kwa masilai ya chama chao zipo sababu nyingi.

1:Maalimu sio mara ya kwanza kufanya maridhiano na CCM zaidi mara nne yote yalizingatia masilai ya umma ndo maana hitimisho ilikuwa 2010 walipofanya mabadiliko ya katiba ili kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa,na wakati wote kilichofanywa ni kila upande kuleta mapendekezo yake na mwishowe mnakubaliana ndio maana maalimu hakulaumiwa.

2:Tofauti ya uchaguzi wa 2015 na 2020 hakuna yote ilikuwa uporaji na wengi kuumizwa na wengine kufa kama ACT Wazalendo walipodhibitisha na imewapelekea kufungua case icc japo kwa hatua hii ya sasa watafifisha kwa kitendo cha kujiunga na waliowapora uchaguzi ili wahalalishe uchafuzi waliofanya

3:Maalim 2015 alifanya mazungumzo ya maridhiano na CCM wakashindwa kufikia muafaka sasa leo anakwenda bila maridhiano yaani ukiwauliza wanakuambia tunatimiza takwa la kikatiba ambalo lilikuwepo 2015 alioshindwa kuafikiana

Mwisho tulitaraji kuwe na mazungumzo ya maridhiano ya kuponya majera ya Zanzibar kuliko kumponya maalimu kisiasa watu wamekufa, wameteswa wamefilisiwa ilitakiwa waliokamatwa kwa sababu ya uchaguzi waachiwe waliokufa familia zao ziangaliwe pia kuwepo kwa usawa haki na wajibu wa vyama kufanya kazi za kisiasa ,lakini maalim na ACT Wazalendo wameangalia masilai ya chama chao kuliko umma

Maridhiano huwaweka maasimu wawili kwa pamoja ili kutatua maswaibu yaliyowakuta na Zanzibar ina makovu mengi yanayopaswa kuponywa
 
Tupo wengi sana kwa hili halikubaliki kabisa,lkn siku zote nimekuwa nikisema kuwa upinzani wa Zitto unatia mashaka sana hapa Tanzania.
Mmawia
Ukitaka kujua maana yake nakushauri anzisha chama chako ambacho kitakuwa cha kipinzani kwa upinzani huo unaouona kwako.
 
Mmawia
Ukitaka kujua maana yake nakushauri anzisha chama chako ambacho kitakuwa cha kipinzani kwa upinzani huo unaouona kwako.
Mimi nipo cdm chama ambacho naamini ni cha upinzani wa kweli kabisa ,kwa sasa tunaendelea kuwaondoa makapi, wale wasiyo na moyo wa subira.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…