Walio kufa kwa amri ya Nyerere{hapa wakuu namaanisha yeye kama amiri jeshi mkuu msinihukumu} labda ni wale wa vita ya Kagera nasikia watu walikufa sana kuliko inavyo tangazwa na ilivyo andikwa....wazee wa huko wanajua nini kilicho tokea enzi hizo.
watajeni basi jamani hatakama ni wafununu watajeni tuu
Moja Ameuwa Ufahamu Wako Only Have Now Is Highly Claiming Capasity Wisdom And Understanding Zero.pili Jamaa Kakujibu Hapo Juu
Baba Wangapi Waliliwa Na Fisi Wakati Wa Vijiji Vya Ujamaa?kasimu Hanga,twala,sokoine,karume. Sasa Jaza
Pezzo,
Labda Wengine Wanakuelewa - Mimi Nimeshindwa, Duh. Hata Hivyo Kwa Ufahamisho Wako Aliyeongoza Mapinduzi Ya Zanzibar Si Mwingine Bali field Marshall Okelo Na Ndiye Alikuwa Mwenyekiti Wa Kwanza Wa Baraza La Mapinduzi 1964. Wakati Huo Akina Karume, Babu Na Wengineo Waliikimbia Zanzibar Na Kupata Hifadhi Tanganyika. Ni Nyerere Huyo Huyo Aliyeweza Kuhakikisha Kuwa Mamluki Okelo Hatwai Uraisi Wa Zanzibar Na Hivyo karume Kuukwaa Uongozi On A Silver Platter.
Sokoine Alikuwa Kipenzi Wa Nyerere Na Kama Kuna Kilichomfanya Mwalimu Kusalimu Amri Na Kukubali Kung'atuka Ni Hicho Kifo. Matumaini Ya Mwalimu Kwa Tanzania Kupata Kiongozi Bora Baada Yake Yalikufa Siku Hiyo. Kusema Alihusika Na Kifo Cha Sokoine Ni Kuonyesha Utaahira Mkubwa Wa Akili.
Mimi napingana na hoja hii kwa sababu hizi:
1. Nyerere alikuwa anamuandaa Sokoine achukue nchi baada yake kwa hiyo hakukukuwa na sabau ya kutishika kwa umashuhuri wa Sokoine. Sokoine aliuawa 1984 na Nyerere aling'atuka 1985 na akamuachia Mwinyi kwa hiyo utaona ni kweli Nyerere alikuwa anajiandaa kuondoka hivyo Sokoine si tishio
2. Sokoine hakuwahi kupingana na sera za ujamaa na kujitegemea wala hakuwahi kutofautiana na sera za Nyerere. Kwanini basi Nyerere amuue? Hakuna sababu
3. Sokoine aliuawa na wahujumu uchumu ambao kwao Sokoine alikuwa tishio
Baba Wangapi Waliliwa Na Fisi Wakati Wa Vijiji Vya Ujamaa?kasimu Hanga,twala,sokoine,karume. Sasa Jaza
Sio Pope tu; nimejaribu kuisoma hiyo thread na kurudia sijaielewa. Kiswahili sio na kiingereza sio.
Baba Wangapi Waliliwa Na Fisi Wakati Wa Vijiji Vya Ujamaa?kasimu Hanga,twala,sokoine,karume. Sasa Jaza
Sorry Sir Kwa Kuweka Jina La Sokoine Kwenye Wale Elfu Waliokufa Wakati Wa Callya Nyerere,lakini Wakatiti Nyerere Akiwa Raisi Wa Jamuhuri Ndipo Kassim Hanga,sarehe Twala,idrissa, Na Wengine Wengi Waliuwawa,naluda Tena Jina La Sokoine Niliteleza.
wenzio walijaribu hiyo gear ya "vijiji vya ujamaa"; hadi leo hajajitokeza mtu hata mmoja ambaye ameweza kutoa madai au uthibitisho kuwa:
a. Ndugu yake aliliwa na fisa au simba
b. Huyo ndugu yake aliwahi kuwepo!
c. Hakuna mtu mwenye idadi ya kusema ni wangapi waliliwa na wanyama na wapi.
Nimesikia habari hizi siku nyingi kweli lakini hadi leo hakuna ushahidi wa kuonesha kama kuna mtu aliliwa na simba au fisa ni sababu ya vijiji vya ujamaa kwani hadi leo hii kuna maeneo bado watu wanaliwa na fisi, simba na sungura!! na hakuna harakati za vijiji vya ujamaa. So, kama una ushahidi angalau wa mtu, kijiji, au mahali ambapo watu "maelfu" waliliwa na wanyama useme au nipe contacts mimi nitafuatilia.
...
Mada ya Nyerere na idadi ya watu alioua ni rahisi kuijibu na ndio maana hata Papa anasita kumpa "Utakatifu". 1) Akiwa Kamanda anawajibika moja kwa moja kwa mauaji yanayofanywa na Wanajeshi wake. Yeye ndiye ALIYEIDHINISHA UVAMIZI WA UGANDA (bila idhini ya OAU), NIGERIA KWA KUISAIDIA BIAFRA, NA SHELISHELI (ndege za ATC zilibeba Wanajeshi na silaha kinyume cha sheria za ICAO/IATA) - mote humo walikufa Watanzania na "maadui".
Hawa wanatosha hata bila ya kuwataja waliofia "kizuizini" (detention) bila kushitakiwa au wengine walioozea jela kwa MAJARIBIO MAWILI YA KUMPINDUA (Army mutiny aliyo-msave Kambona na Mapinduzi ya "Kamandoo wa Mkwajuni", akina Roderick Roberts na MacGhee!! AU MMESAHAU??
Mjadala wa kilichomuua Edward Sokoine ni wa siku nyingi ila mimi naona ni katika mwendelezo wa "nasikia eti" za Watanzania. My suspiciuos minds tends to believe:
1: Kama wana-nadharia wa kundi la kwanza wanavyosema... kama mwalimu J. K. Nyerere alikuwa anamchukia na akaona anakuwa tishio; Nyerere akiwa kama rais alikuwa na njia nyingi tu za kumdhooofisha bila kumuua.
2. Kama wana-nadharia wa kundi la pili wanavyosema... kama Cleopa Msuya na Rashidi Kawawa (and/or others) walikuwa wanamchukia na wakaona anakuwa tishio... na WAKAHAKIKISHA AMEUAWA.... mwalimu Nyerere lazima angefahamu... Na asingenyamaza... lazima kungekuwa na some sort of displinary action kwa hao wahusika.
Assignment:
1.Naomba mnieleze kwa nini Nyerere aliamua kuuchuna (kama kweli Sokoine aliuawa na kina Kawawa/Others???
unakumbuka Akina Kadego,macgee Na Wengine Walipo Kimbilia Nairobi, Nyerere Ali -trade Na Moi Maisha Ya Akina Ochuku Wale Makamanda Toka Jeshi La Anga Kenya ,nyerere Akawapa Akina Ochuku Na Moi Akampa Akina Macgee Jamaa Walipo Fika Tu Kenya Mzee Nyao Akawauwa Jamaa1. Charles Taylor Yuko Hague Kwa Mauaji Ya Sierra Leone Ambako Wala "hakushiriki Yeye Binafsi" - Ni Amri Yake Tu Kwa Vikosi Vyake.
2. Nyerere Mbona Alimsamehe Mwalimu Wa Kike Aliyeua Watoto Wake Watatu (akabaki Mmoja - Mtangazaji Kijana Maarufu, Jina Ninalo) Baada Ya Kuombwa Na Uwt (akina Ms Mongela) Mwaka 1977?
3. Nimezungumzia Uvamizi An Sio Vita. Nyerere Aliyaingiza Majeshi Yetu Uganda Na Wla Hakumfukuza Idi Amini Mpakani Tu Ila Alihakikisha Anmng'oa Kabisa Atawale Rafiki Yake Obote. Hivi Hamkumbuki Alivyowachezea Akina Lukle Na Binaisa Kama Watoto Wadogo Amri Zikitoka Msasani?
Hebu Wee Tuache Tu .... Ukimpenda Mtu Madhambi Yake Huyaoni!!