Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Hivi dumisan dube bado yupo hai ? Maana anajua baadhi ya siri .
 
Rejao amka kuna watu wanamsema EL ....

 
Sijui kama tutapata PM kama Sokoine.
 
OMG siamini kama watu hawajui matukio muhimu kama haya....naona mnataja watu wasio husika kabisa...EL was no boddy by then, kuna mtu anaitwa RK huyo ndo muhusika, JKN alijua kitu kama hicho kitatokea akamshauri sana ES aende nae dar kwa kutumia ndege, lakini by then ES alishakua amekasirika kutokana na ugomvi uliotokea dom kati yake na RK, sasa kama unavojua masai akikasirika inakuaje, so akawa anamwambia JKN wakutane dar wataongea lakini JKN, so anacholaumiwa JKN ni kutokana na yeye kushindwa kutafta njia ya kumuokoa nyingine baada ya hiyo ya kumwambia wapande ndege pamoja kushindikana.
 
Kesho tarehe 12 April inatimia miaka 28 tangu kiongozi shujaa na mzalendo wa kweli kuaga dunia katika ajali ya gari, tutakukumbuka kwa mengi Sokoine upumzike kwa amani.... Amen
 
Mi nilikuwa naangalia kama watu watakumbuka, what with all the Kanumbamania.

May all beings attain enlightenment.
 
Vijana wengi hawamjui, na historia yake haitiliwi maanani. Hakuna hata ka documentary kamoja juu ya maisha yake?
 
Kesho ni tar 12/04/ tunakumbuka siku ambayo waziri mkuu wetu mpendwa Sokoine alipoaga dunia kwa ajali ya gari.Mimi namkumbuka Sokoine kwa mambo yafuatayo Uzalendo,Ujasiri,Uadilifu,Uajibikaji na mtu asiyependa Uonevu na Ubaguzi.Je viongozi wetu wa sasa tunaweza kuwafananisha na Sokoine. Naomba kuwasilisha.
 
Vijana wengi hawamjui, na historia yake haitiliwi maanani. Hakuna hata ka documentary kamoja juu ya maisha yake?

Mimi huwa najiuliza, hivi kwanini hakunaga Public Holiday inayokwendaga kwa jina la "SOKOINE-DAY" kama vile "NYERERE-DAY" na "KARUME-DAY" ...
 
Palikuwepo kikundi cha maigizo UDSM enzi hizo chini ya Prof. Penina Mhando, walikuwa na igizo la sokoinne, binafsi nilipata bahati ya kuliangalia kundi hilo Pugu sec school siku hizo nikiwa dent nakumbuka yafuatayo

1. Sokoinne akiwa kazini ofisini huku akisikia na kuona vitu vya kishirikina / kiuchawi ofisini mwake
2. Njama za kumwangamiza Sokoinne aliyekuwa na dira ya nchi inapoelekea
3. Baada ya kifo chake palikuwepo na wasafiri waliofika njia panda wakaanza kubishana wachukue njia ipi ya kulia au kushoto
4. Sokoinne akiwa peponi huku akihuzunika kwa vile wasafiri wale waliokosa ufahamu wa kujua ni njia ipi inawapeleka waendako.
5. Hitimisho la igizo lilikuwa walimuua Sokoinne kwa hila wakati wauaji wake hawana fikra wala ufahamu wa kutosha wa kuingoza tanzania

Kila ninapokumbuka igizo lile na jinsi ninavyoiona ccm inavyotawala tanzania hakika Prof. Penina Mhando na kundi lake walikuwa ni manabii, yote waliyolitabiria taifa hili katika igizo lile yametimia na kupitiliza
 
Thanx Mshawa for such a sensible thread. This generation must know THE REAL HEROES OF THIS NATION! If we don't learn from history then what is the use of torrow? They will soon call him a "hero", somebody killing himself while fighting for a Harlot!


Requiascat In Pace Hn. Edward Moringe Sokoine!
 
Kifo chake kiliniuma kama vile cha kanumba steve. Wamarekani walimpoteza raisi wao kipenzi na sisi vile vile tuna majonzi kama wao wmarekani kwa kumpoteza kipenzi wetu Edward Moringe Sokoine!
 

duh walithubutu kuigiza enzi za chama kikiwa kimeshika hatamu na utamu?
 
Always gambas ni 0brain usishangae kuwepo Kanumba Day!!!!!!!!!!!!!
 
Naikumbuka kama vile ilikuwa jana ile Alhamisi ya Aprili 12, 1984 ambapo Taifa lilimpoteza Edward Moringe Sokoine - Waziri Mkuu. Alikuwa ni mtu wa kwanza ambaye alitambua kwa kina vita ambayo imekuja kujithibitisha miaka karibu thelathini baadaye - kwamba wapo watu ambao wanaweza kutumia umaskini wa wananchi wetu kama mtaji wao! Sisi tuliwaita "wahujumu uchumi" leo wanaitwa "mafisadi" kiukweli ni watu walewale!!! Alikuwa ni shujaa wa kwanza katika mioyo ya Watanzania aliyewapigania wananchi wanyonge hasa na hadi sasa ndani ya CCM bado hajatokea mtu wa namna hiyo!!! RIP Sokoine!!!!
 
Tunaye Sokoine aliye Hai- EL, kijana, mchapakazi, mmasai. Anajua kutoa maagizo na kufuatilia. Huchukia mambo yakienda vibaya. Si unaona anavyosimamia ujenzi wa madarasa?

Sokoine mpaka wakati anafariki alikuwa na pea mbili za viatu, EL anamiliki nini hivi sasa mpaka tumlinganishe na Sokoine?

Ninaungana na wapenda haki kukumbuka siku Tanzania ilipota msiba mkubwa sana kwa kuondokewa na E. M. Sokoine (R.I.P).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…