Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Kanda2.... unajua kwanini Balozi Daraja alikwenda Houston na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Richmond Development Co. Hii ilikuwa ni Julai 2003 (wakati huo Rais alikuwa ni... )

Jamani tusimtafute Mchawi asiyekuwa ndiye Hili deal la Richmond ni mzigo wa KIKWETE na timu yake hapa mkapa muondoeni kabisa mimi binafsi nimemsikia Mh Rais akilitetea hili ktk mikutano miwili tofauti na akasema walifanya hivyo kwaajili ya kutaka kulitatua tatizo la umeme kwa HARAKA yaani kwa mtizamo ilikuwa Emergency,Sasa sijui ni emergency ya aina gani kwani mpaka mvua imejaza bwawa na umeme kurudi hawa jamaa hawakufanikisha kuzalisha umeme Kwanini wasiondolewe.

Mathalani, Hata kama deal lilianza enzi ya Mkapa (kitu ambacho kwenye hili si kweli) LAKINI MKATABA ULIKUWA HAUJASAINIWA HIVYO HAKUKUWA NA SHERIA YA KUIBANA AU KUILAZIMISHA SERIKALI MPYA KUSAINI MKATABA, HIVYO SERIKALI MPYA CHINI YA MH KIKWETE IMESAINI MKATABA KWA MATAKWA YAKE NA WANAHUSIKA.

HAPA muungwana anawajibika na makolokolo yote yaliyosababishwa na Richmond.
 
Kazi ndiyo kipimo cha utu,

Ndugu yangu hufahamu kwamba CXCM wana sera moja kubwa isemayo KULINDANA kwanza?... sasa kama hujatanguliza hilo sijui kama tutafika maanake hata lile la Rada umesikia JK akisema tumwache mzee wa watu...

Kyoma,
Niliposoma ile habari yako ya kwanza tu nilinyoosha mikono kwani penye ukweli ujinga wote hujitenga na ndio maana nikaliacha kumbi kimya kimya! Uliandika hivi:-

Mimi natofautiana na nadhalia ya kumfananisha Moringe Sokoine na Ngonyani Lowasa au Lyatonga Mrema. Sokoine alikuwa na sifa ya Uongozi, kwa maana ya kudhamilia kuonyesha njia. Pia, alikuwa ni mfanyakazi mwenye juhudi na maarifa. Dhamila ya Sokoine ilikuwa haimsuti katika utendaji wake wa kazi, ndio maana alifanikiwa kuthubutu kupunguza kero zilizowasibu watanzania. Mrema na Lowasa hawana sifa ya Uongozi, bali wana sifa ya kutawala.

Pia, Mrema na Lowasa hawana sifa ya kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, bali wana sifa ya kushughulika. Dhamila zao wote wawili zinawasuta katika utendaji wao wa kazi, ndio maana hawawezi kufanikiwa, sio tu kupunguza, bali hata kugusa kero zinazowasumbua watanzania.

What more should I say!...
 
Mkandara!

Swala la RADAR tunalielewa ni tofauti na Richmond,swala la Radar tayari mkataba ulisainiwa hivyo kulikuwa na nguvu ya kisheria.Tusitake kumuokoa JK katika hili la Richmond alikuwa madarakani na alitudanganya kwamba angepitia mikataba yote na mambo mengi yote yameshindikana sababu ni kwamba tayari kuna mikataba ya kisheria. Je, hili ambalo lilikuwa halina mkataba alishindwaje kulizuia lisilitie Taifa Hasara kwa kuacha kusaini mkataba?Kwanini alikubali serikali yake kusaini mkataba?

He has got no excuse, HE IS RESPONSIBLE!
 
Kazi ndio kipimo cha utu,
Did I say he is not responsible?....

Jamani, lini tutaweza kutambua chanzo cha maafa yetu bali tudakie nani alikuwa madarakani wakati kikifanyika. nacho jarivu kueleza hapa ni kuelewa mapana ya swala zima na kama kuna hoja ya kujenga tuanze toka kule kilipoundwa kama vile tukianza leo kuzungumzia swala la IPTL na uuzwaji wa wake hata kama siahihi ziliwekwa wakati wa Mkapa.

Hawa wahusika hua na hoja zimejengwa tayari na mtu kama rais si rahisi kuelewa mbinu zinazotumika.

Swala la Richmond ni swala zito zaidi ya huo mkataba mmoja kwani kuna akina Richmond wengi sana nchini ambao wanazidi kuliweka taifa ktk hali mbaya sana. Kwa hiyo kama alivyosema Kyoma kuna tofauti kubwa ya ya kingozi na Mtawala na bahati mbaya kila siku tunazidi kuchagua watawala.
 
Mwakjj

Sijui kilicho jadiliwa baina balozi Daraja la Richmond. Ninachojua ni Richmond waliomba kazi ya bomba la mafuta na wakakosa!

Hata hivyo kwa mujibu wa Mkandara deal la Richmond lilianzishwa na Mkapa miaka mitano iliyopita! kwa hesabu zangu za ngumbaru hizi inanipa kuwa ni 2002. Hivyo kwa mujibu wa Mkandara dili la Richmond lilianza 2002!.

Mkandara
Nakubali sera ya CCM ni kulindana, lakini katika hili inaonekana ni kinyume. Swali je 2002 Richmond na serikali walianzisha deal gani ambalo limeruka viunzi mpaka kaja kulikamata mzee Ngoyai June, 23, 2006! mmh kazi ipo.

KNCU

Richmond belongs to Kikwete, EL & Co only
 
Kazi ndio kipimo cha utu,
Did I say he is not responsible?....

Jamani, lini tutaweza kutambua chanzo cha maafa yetu bali tudakie nani alikuwa madarakani wakati kikifanyika. nacho jarivu kueleza hapa ni kuelewa mapana ya swala zima na kama kuna hoja ya kujenga tuanze toka kule kilipoundwa kama vile tukianza leo kuzungumzia swala la IPTL na uuzwaji wa wake hata kama siahihi ziliwekwa wakati wa Mkapa.

Hawa wahusika hua na hoja zimejengwa tayari na mtu kama rais si rahisi kuelewa mbinu zinazotumika.

Swala la Richmond ni swala zito zaidi ya huo mkataba mmoja kwani kuna akina Richmond wengi sana nchini ambao wanazidi kuliweka taifa ktk hali mbaya sana. Kwa hiyo kama alivyosema Kyoma kuna tofauti kubwa ya ya kingozi na Mtawala na bahati mbaya kila siku tunazidi kuchagua watawala.
Mkandara!

Hukusema kwamba hayuko responsible Lakini Hukusema vile vile kwamba yuko responsible,Chanzo tunakielewa na tulikuwa na nafasi ya kuzuia kile chanzo kisilete maafa LAKINI nafasi hiyo tuliipoteza.Na aliyeipoteza nafasi hiyo Muhimu ni Huyu Mh.JK na serikali yake tena alihuburi kingine na akatenda Lingine!
 
Kazi ndiyo kipimo cha utu,

Ndugu yangu hufahamu kwamba CXCM wana sera moja kubwa isemayo KULINDANA kwanza?... sasa kama hujatanguliza hilo sijui kama tutafika maanake hata lile la Rada umesikia JK akisema tumwache mzee wa watu...

Kyoma,
Niliposoma ile habari yako ya kwanza tu nilinyoosha mikono kwani penye ukweli ujinga wote hujitenga na ndio maana nikaliacha kumbi kimya kimya! Uliandika hivi:-

Mimi natofautiana na nadhalia ya kumfananisha Moringe Sokoine na Ngonyani Lowasa au Lyatonga Mrema. Sokoine alikuwa na sifa ya Uongozi, kwa maana ya kudhamilia kuonyesha njia. Pia, alikuwa ni mfanyakazi mwenye juhudi na maarifa. Dhamila ya Sokoine ilikuwa haimsuti katika utendaji wake wa kazi, ndio maana alifanikiwa kuthubutu kupunguza kero zilizowasibu watanzania. Mrema na Lowasa hawana sifa ya Uongozi, bali wana sifa ya kutawala.

Pia, Mrema na Lowasa hawana sifa ya kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, bali wana sifa ya kushughulika. Dhamila zao wote wawili zinawasuta katika utendaji wao wa kazi, ndio maana hawawezi kufanikiwa, sio tu kupunguza, bali hata kugusa kero zinazowasumbua watanzania.

What more should I say!...

Mzee Mkandara, heshima yako mkuu,

Duh!
Mbona unapigilia Msumari wa mwisho kwenye jeneza la hoja za Kyoma? Si ndo haya madongo ninayoyasema? Umelishwa matoke nini huko ulikotoka? Umesahau hadithi ya mgeni siku ya kwanza...? Hata zile busara za majirani zetu wa Kenya umezipiga teke? Manake Mkenya akiambiwa karibu anasema nimekaribia alafu madongo baadae.

Anyway, umeniacha bila chaguo zaidi ya kuazima busara za Bill Clinton za kujifedhehesha, kwa kuyakwepa madongo na kujificha ndani ya tafsiri za maneno. Mzee, hapo nilikuwa natofautiana na wale waliotaka kumfananisha Sokoine na Lowasa/Mrema. Kumfananisha kwa maana ya kushabihiana, kufanana katika sifa za uongozi na utendaji kazi. Kufanana kitabia na dhamila zinazowasukuma. Mfano mtu anapofananishwa na mtu mwingine kisura. Tunaweza kuwalinganisha hawa viongozi bila kuwafananisha.

Hakika nakubaliana na wewe kuwa hawafanani katika jambo lolote. Kujaribu kuwafananisha ni kupotosha ukweli au kupoteza muda. Infact, nilichofanya ni kuwalinganisha, kwa maana ya kuchambua urefu wa matendo yao, upana wa maamuzi yao, na uzito wa sifa zao za utendaji wa kazi/shughuli, pamoja na sera walizozisimamia kama vinaafikiana.

Kuhusu Richmond, nadhani nitaligusia katika ngwe ya Lowasa na Sokoine kwa kinagaubaga. Richmond ilikuwepo toka zamani wakati wa enzi za Mkapa. Hata hivyo, walikuwa wanajaribu kutafuta miradi ya Serikalini bila mafanikio. Hii ilitokana na kupigana vikumbo vya kimaslahi miongoni mwa viongozi wenyewe. Kumbuka hii kampuni iliwahi kuomba kuchapisha makablasha yote ya Serikali, kuanzia ngazi za Serikali za mitaa, madiwani, na mpaka Bunge. Mfano ukienda halmashauri ya mji wa Dar, au ofisi ya Meya wa mji, utakuta hata sample za majarida waliyotoa kama njia ya kushawishi. Walitaka kuchukua tenda ya kumbukumbu zote za Serikali na kuzichapisha katika majarida. Viongozi walitiliana mikono, na haikufanikiwa.

Hakika, miradi yao mingi ilipigwa nje. Hata hivyo, waliokuwa nyuma yao kupenyeza hayo makablasha, ni wale viongozi waliokuwa katika safu ya Mkapa, na sasa hivi ndio wanashikilia nchi. Walikuwa na mapafu wakati ule, lakini sio kama waliokuwa nayo sasa hivi. Hivyo basi, kwasababu hii kampuni walikuwa nayo muda mrefu, ndio maana waliposhika madaraka, wameweza kuikabidhi fedha kwa mtindo wa kulipana fadhila chini ya mikataba mibovu. Richmond kwa suala la mkataba wa Umeme peke yake, ni utawala wa Kikwete. Je? unataka kujua fedha zinazokopwa katika mabenki duniani lakini zinaishia kwenye makampuni uchwara? tega sikio
 
kyoma,sasa unanifanya hata prison break nisiangalie kwa kusubiri hizo nyeti,huwenda na kampuni yangu ikawepo (joke)
 
Kyoma,

Baba navua kofia data unazo na ndio maana sikupenda kujihusisha sana na hao jamaa zetu Richmond na wahindi wengine akina Manji kwani hawa jamaa wamekuwa wakitafuta tender kwa hali na mali. Hizo habari za Richmond nilizisikia siku nyingi sana na hasa wakati ule Daraja na meya walipokuwa na safari zisizokuwa na mwisho Houston....

Unajua pia kwamba Lowassa alivyotembelea Canada alialikwa rasmi na jumuiya ya hawa jamaa zetu ambao wanajiita Tanzanite!..Jumuiya yao kubwa na ina nguvu kishenzi wakitumia ngawila kama mti shamba wa maradhi ya mwafrika...

Baba shusha mashuzi!
 
Mkandara,

Meya (presumably Kleist) karudi tena kwenye Richmond?
 
Nafikiri tumalize huu mjadala wa Richmond kwa kusema hivi huu mkenge ulifanywa na serikali ya CCM!
 
Kanda2,
Weee mhuni sana yaani mitego yako ya kunasia Changu unaiweka kumnasa kamba?..niko deep bob hunikamati kwa nyavu hizo. hata hivyo meya Kreist alikuwa msindikizaji tu hakuwa na sauti kabisa!... deal la wahindi sii mchezo mdogo hawa jamaa wanajua nani wa kumkamata.
Hivi jiulize kwa nini ametolewa nje Umeya?....
 
Mkandara,
That's a good question. Meya wa sasa alikubali kucheza mchezo uliokuwa unatakiwa na wenye, Kleist akatemwa.
 
Mkandara.

Mie navua jalifye! au kama kule bara basi ni kokoro, lenyewe linakomba kila kitu!

Anyway Bro hii flip-flop yako inanifurahisha sana. It reminds me of John Edwards!.

In that kesi back to square one! Kleist hayumo and thats why wali mtema!.

Hapo ndipo ninapo ipenda JF, nyeti zote zipo hapa!
 
Kanda2,

Kuwepo madarakani na kuwa mhusika na deal la Richmond hivi ni vitu viwili tofauti. Kama nilivyosema toka mwanzo Richmond walianza madeal yao wakati wa Mkapa, sina maana Mkapa alikuwepo ktk deal hilo ama alihusika na kuwakataa Richmond wasipewe tender ya kwanza. Bado kipi mjomba?
 
Mkuu Mkandara,

Hapo umemaliza kila kitu! hakuna kingine, Mkapa na Kleist wote hawamo.

Thanx bro lets move on with Sokoine mtu wa wote
 
Mzee Kyoma,

Vipi babuuu mawazo yako yanatakiwa mkuu kwani tofauti zetu ktk kutazama swala MOJA haina maana kwamba hekima zako hazipokelewi. Darasa lako kubwa zaidi kwani unazungumzia msitu mzima na watu kama mimi tunachosema ni miti tu iliyopo msituni!..
Haujapoteza kabisa kura zangu!
 
Mzee Mkandara na Mzee Machumo, heshima zenu kwa mpigo

Mzee Machumo, sidhani kama naweza kunyamazishwa kwa mtindo huu usio na kichwa wala miguu. Ingawa sio jambo la busara kuwapuuza hawa watu, lakini ni vema kuwadhalau. Mzee Mkandara, acha utani! Sijuhi nisisitize vipi mpaka unielewe kuwa kutofautiana kihoja ndiko kunaniweka Jamii Forums. Usipoona mchango wangu, basi ujue kuna jambo la msingi. Hata hivyo, nitamalizia viporo vyangu vyote kama nilivyoahidi.

Labda kwa leo nikatishe mchango wangu katika hii mada ya Sokoine, ili nitoe masikitiko yangu kuhusu tathmini ya hali ya uchumi iliyotolewa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Daudi Balali, na kuwasilishwa kwenye kamati ya fedha na uchumi ya Bunge (Habari leo Mei 29, 2007). Tathmini ya Gavana imegusia jambo ambalo tumelijadili kwa ufasaha ndani ya mjadala huu wa Sokoine. Huu utakuwa ushahidi tosha kwa Mzee JokaKuu aliyechokonoa mjadala wa IMF na WB. Binafsi, nadhani Gavana Daudi amewapotosha wabunge kwa kutokuongea kiini cha sababu za kushuka kwa thamani ya shilingi na chanzo cha mfumuko wa bei.

Pia, siamini kuwa Gavana wetu ni mjinga kiasi cha kutokujua njia za kurekebisha tatizo la kushuka kwa thamani ya shilingi au kupunguza mfumuko wa bei. Naamini kuwa mapendekezo yake yanalenga katika upotoshaji na wala sio utatuzi wa tatizo lenyewe. Eti ili kuondoa mfumuko wa bei, anawashauri watanzania wathamini bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi. Eti ili shilingi isishuke thamani, watanzania waache kusomesha watoto wao nje ya nchi, hivyo kupunguza matumizi ya fedha za kigeni.

Gavana anawatoa kafara wananchi kwamba ndio wanasababisha mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi. Mbona hajawakumbusha watawala wetu kuthamini hospitali na madaktari wetu wanaozalishwa Muhimbili? Mbona hajawaambia viongozi waheshimiwa waache au wapunguze safari za nje zisizo na manufaa kwa nchi yetu? Au hizo hazipunguzi matumizi ya fedha za kigeni?

Lakini ni watanzania wangapi wanasomesha watoto wao nje ya nchi kwa kutumia fedha za kigeni? Ni kweli, kuna watoto wa kitanzania wanaosoma Kenya na Uganda. Hata hivyo, idadi yao ni ndogo sana kiasi kwamba haiwezi kulitikisa taifa kwa kushusha thamani ya shilingi. Pengine, wengi wao wanatumia fedha za madafu zinazobadilishwa mpakani kwa fedha ya Kenya na Uganda. Fedha ya Kenya na Uganda, haiwezi kutikisa fedha yetu kama zifanyazo Dola, Paundi au Euro. Hivi ni visingizio vyenye lengo la kulikimbia tatizo la kweli.

Gavana lazima atambue na amshukuru Mungu kuwa kuna watanzania wanaoishi katika nchi zinazotumia fedha yenye thamani kubwa duniani. Wengi kama sio karibu wote, hawasomeshwi na wazazi wao, bali wanajisomesha wenyewe kwa kuchakalika. Niliwahi kuandika mahala kuwa naheshimu sana watanzania walioshindwa darasa la saba na kidato cha nne, alafu wakaamua kutimua na kuchakarika katika nchi zinazoitwa tajiri duniani. Hawa kwangu mimi ni majemedari wa taifa letu. Wangekuwa pale nyumbani, ungekuwa ni msalaba mkubwa kwa wananchi. Wengi wao wangekuwa ni vibaka au mashine za kusambaza ukimwi.

Gavana lazima atambue kuwa idadi ya hawa majemedari ni kubwa na hawapati msaada wa fedha kutoka nyumbani bali wanachakarika kuzisaidia familia zao zilizoko nyumbani. Wanatuma dola au paundi ishirini, mia moja, miatano, mpaka elfu moja. Hizi fedha kutoka kwa kila mmoja wao, zikijumlishwa kwa ujumla wake kwa kipindi cha miaka michache, zinakuwa maelfu kama sio mamilioni ya dola au paundi.

Wakati viongozi wetu wanahujumu uchumi wa nchi yetu kwa kusaidia utoroshaji wa fedha za kigeni kwenda nje ya nchi, hawa majemedari wanasaidia uchumi wetu kwa kuingiza nchini fedha za kigeni. Vilevile, fedha wanazotuma zinawasaidia ndugu zao katika mapambano dhidi ya umasikini uliokithiri, zinasaidia kuanzisha miradi midogomidogo, kuwasomesha ndugu zao, kuajiri mafundi kwa ujenzi wa vibanda vyao vya kufikia, kununua bidhaa kwa ajili ya mahitaji mbalimbali ya familia zao n.k. Fedha inayotoka nje kwa mtindo huu, inazunguka ndani ya jamii ya watanzania. Mzunguko wa fedha ndani ya nchi, ni neema kwa taifa letu.

Mchango wa mtu mmoja katika uchumi wa namna hii hautoi taswira halisi ya umuhimu wa hawa majemedari katika kukuza uchumi wa nchi yetu. Hata hivyo, ujumla wa watanzania wote walioko nje wanaotoa mchango wa namna hii, unaweza kutoa picha nzuri kwa wale waliodhamilia kufanya tathmini ya kweli. Waswahili wanatukumbusha kuwa haba na haba ujaza kibaba.

Hoja za kiini cha kushuka kwa thamani ya shilingi na kinachosababisha mfumuko wa bei kwa nchi yetu tumezijadili kwa undani katika hii mada ya Sokoine. Kama Gavana wa Benki na wengi wa wabunge wetu wangekuwa washiriki wa mijadala ndani ya Jamii Forums, wasingethubutu kudanganyana kwa tathmini zisizokuwa na mbele wala nyuma. Wasiwasi wangu ni kuwa, hata Raisi wetu anapewa tathmini hizi za ubabaishaji.

Nimetoa kiambatanisho (pdf format) cha habari inayohusu tathmini ya Gavana wetu kama ilivyoandikwa na gazeti la habari leo. Nachukuwa fursa hii kutoa onyo kwa wote wanaotubeza kuwa Jamii Forums ni mahala pa gumzo au porojo. Kama wadau wanavyosema, hapa "tunakata issues". Tunatabiri mambo kabla hayajatokea. Utabiri wetu sio wa kutumia majini kama ule wa Profesa maji marefu au Yahaya. Utabiri wetu umelalia katika kuzichambua issues kama unavyochamabua karanga. Tuna-argue kwa logics, tuna evidenced evidence, na mifano tele.

Gavana wetu analipwa fedha kwa kazi yake. Amefanya tathmini ya hali ya uchumi ambayo ameipeleka kwenye kamati husika ya Bunge. Wabunge nao wanalipwa fedha (posho) kukaa vikao ili kuisoma hiyo tathmini. Lakini tathmini yenyewe ni ya upotoshaji, ubabaishaji, na uongo. Hailisaidii taifa letu.

Nimenukuu baadhi ya paragrafu kutoka katika mabandiko yangu ndani ya hii mada ya Sokoine zinazohusu vipengere vya tathmini ya Gavana kwa wabunge wetu. Hii inamaana kuwa Jamii Forums tulikwisha fanya tathmini yetu kwa njia ya mijadara na kujua kuwa fedha yetu itaendelea kushuka thamani. Pia, tulikwisha jua kuwa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi yetu zitaendelea kukumbwa na dhoruba ya mfumuko wa bei. Tulitoa sababu na mifano hai ya kwa nini mambo hayo yatatokea. Habari nzuri kwa wadau wote ni kuwa mambo yanatokea, na yataendelea kutokea kama tulivyotabiri. Habari mbaya ni kuwa, taifa letu linaendelea kuegemea katika ukingo wa shimo la giza.

Yafuatayo ni baadhi ya maelezo yangu niliyoyatoa wakati namjibu JokaKuu kuhusu majangiri wa IMF na WB. Ukimaliza kuyasoma, yachungulie maelezo mafupi yaliyotolewa na Gavana wa Benki Kuu katika kiambatanisho (pdf format). Nikipata ripoti nzima ya Gavana nitaituma pia.

Binafsi, naona kuna tofauti kubwa kati ya Masharti na Sera. Masharti si Sera, na wala Sera si Masharti. IMF na WB hawana Sera, bali wana Masharti ya mikopo. Nchi yoyote ikikubali na kuyatekeleza hayo masharti, inakuwa kama vile umeonja Ganja, au Cocaine. Itaendelee kuwa tegemezi wa ile mikopo. Nchi ikiwa "addicted" na kitanzi cha Cocaine ya mikopo, ni vigumu kujinasua kutoka katika hicho kitanzi. Ndio maana IMF na WB wanakuja na Cocaine, kwa maana ya masharti yatakayotudumaza na kuendelea kutufanya mafukara wa mawazo, au tegemezi wa fedha. Tutaendelea kukopa kwa kuamini kuwa bila Ganja, yaani fedha za mikopo, hatuwezi kutatua matatizo yetu. IMF na WB wataendelea kutukopesha fedha mpaka siku ya kiama chetu. (labda tuazime busara za Venezuela)

Kumbuka kinachotutia umasikini sio riba ya hiyo mikopo bali ni masharti yanayoambatana na hiyo mikopo. Mfano, masharti tunayopewa ni kwamba, tukitaka kuongeza kiwango cha bidhaa zinazouzwa nje (export), na kupunguza kiwango cha bidhaa tunazonunua kutoka nje (import), yatupasa kuifanya fedha ya nje iwe na thamani kuzidi fedha ya ndani ya nchi yetu. Tunaaminishwa kuwa hii nadharia itakatisha tamaa manunuzi ya bidhaa kutoka nje. Hivyo, tunatakiwa kushusha thamani ya fedha ya nchi yetu, mfano kama tulivyofanya kushusha thamani ya shilingi ya Tanzania, na thamani ya dola, paundi au euro inapanda.

Hata hivyo, kwasababu tunakwenda kichwakichwa, hatukumbuki kuwa viwango vya uzalishaji katika jamii zetu ni vya chini sana. Tunategemea malighafi kutoka nje ili tuweze kuzalisha. Mfano wa bidhaa za lazima zitokazo nje ni Mafuta, Vitabu, Madawa, na Mbolea. Bidhaa zote hizi zinanunuliwa kwa fedha za kigeni. Thamani ya fedha ya nchi yetu inaposhuka na ile ya fedha za kigeni kupanda, gharama za uzalishaji zinakuwa juu na kusababisha mfumuko wa bei kwa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi. (Tathmini ya Gavana imekwepa sababu hii ambayo ni ya msingi. Mfumuko wa bei haupo kwasababu watanzania hawathamini bidhaa zinazozalishwa ndani, bali kwasababu hizo bidhaa ni za ghari. Sababu za bidhaa kuwa ghari nimezitaja)

Mfano mwingine wa hayo masharti ni kwamba, fedha wanazotukopesha, kamwe, haziwezi kutumika kuwasaidia wakulima au wafugaji wetu ili kupunguza makali ya uzalishaji (subsidize). Hata hivyo, Serikali zao, zinawasaidia wakulima wao ili kupunguza makali ya uzalishaji. Wanataka tufungue milango kwa maana kuwa bidhaa za wakulima wao ambazo ziko subsidized, zishindane na bidhaa za wakulima wetu ambazo haziko subsidized katika mfumo wa kitu kinachoitwa soko huria. Mwalimu aliwahi kusema Kirimanjaro hotel 1995, kuwa bingwa wa ngumi wa uzito wa juu hawezi kuingizwa ulingo mmoja na yule wa uzito wa kati. Alisema Burkina Faso and German haziwezi kuwekwa kwenye ulingo mmoja. (Tahmini ya Gavana inasema mfumuko wa bei wa Tanzania umefikia asilimia 7 wakati mfumuko wa bei wa nchi ambazo Tanzania inafanyanazo biashara ni kati ya asilimia 2.5 na 3. Hakuzitaja hizo nchi. Wakati viongozi wetu wanasalimu amri kwa hayo masharti, walitubeza kuwa uchumi wa kisasa unaendeshwa kwa nguvu ya soko. Sasa hizi ghiliba zinatoka wapi? Leo Gavana anatuletea takwimu za kushindwa kwetu zinazoonyesha kuwa German na Burkina Faso haziwezi kuwa katika ulingo mmoja)


Ingawa hizo nchi hazikutajwa, lakini baadhi ya nchi anazozisema Gavana kuwa tunafanyanazo biashara, mojawapo ni Marekani. Serikali yetu iliwekewa masharti na IMF na WB kuwa isiwape fedha (subsidize) wakulima wa Pamba. Hata hivyo, nchi ya Marekani inasaidia kupunguza makali ya uzalishaji ya wakulima wake wa Pamba kwa kuwapa fedha (subsidize). Wakulima wetu wanatumia majembe ya mkono na wale wa Kimarekani wanatumia Mashine za kisasa. Hata hivyo, Pamba inayotoka Marekani na ile ya Tanzania inauzwa kwa mashindano katika soko la pamoja bila kuangalia upendeleo katika njia za uzalishaji. Haya ndio masharti ya IMF na WB, yaliyojumlishwa katika mfumo wa uchumi wa Soko huria au utandawazi, ambapo njia zote zinazoweza kuinua viwango vya maisha ya wakulima na wazalishaji wa watu wa nchi yetu zinapigwa mweleka na haya majinamizi. (Tathmini ya Gavana inaeleza kuwa mauzo ya bidhaa zetu kwa nje ni kidogo ukilinganisha na mahitaji yetu, lakini haelezi kwa nini. Hii ndio sababu kubwa).

Matokeo ya hizi ghiliba za IMF na WB, bidhaa zinazoingia nchini kwetu kutoka nje zinauzwa kwa bei ndogo kwa sababu mbili, mosi, njia za uzalishaji katika nchi zenye nguvu za kiuchumi ni za kisasa, kwa maana ya kutumia mashine, wakati sisi tunatumia majembe ya mpini. Pili, Uzalishaji wa bidhaa zao unapata msaada wa fedha kutoka katika serikali zao kwa lengo la kupunguza makali ya uzalishaji. Kitu wanachotukataza sisi tusifanye kwa wakulima na wazalishaji wetu. (Tathmini ya gavana inawatoa kafara wananchi kwamba hawapendi bidhaa zinazozalishwa ndani. Huo ni uongo wa mchana. Tatizo haliko kwenye mapenzi, bali ni liko katika umasikini wa mawazo wa viongozi wetu kukubali masharti ya soko huria na utandawazi. Kamwe tatizo la mfumuko wa bei haliwezi kutatuliwa kimapenzi, bali ama kubadili sera au kuwang'oa wote wanaotubebesha huu msalaba. Ikibidi, yatupasa kuanza upya na mawazo mapya).

Nasisitiza kuwa sikubaliani na nia ya mataifa yenye nguvu za kiuchumi duniani, ingawa kwa nje wanaonekana kuazima sera za utu za kutufutia madeni. Haya mataifa hayawezi kumpinga shetani upande mmoja kwa kutufutia madeni, alafu wakahalalisha shetani upande wa mwingine kwa kukataa kuondoa mifumo ya uchumi duniani isiyo ya haki. Tumefutiwa madeni, lakini mifumo iliyo ndani ya nchi yetu na nje ya nchi yetu ambayo ilituingiza kwenye madeni, bado iko palepale. Tunachokifanya ni kuzunguka duara, na mwishowe tunarudi palepale.

Ndio maana baada ya kifo cha Sokoine na Nyerere, uchumi wa nchi yetu unaendeshwa na mataifa ya nje kwa kutumia mitambo ya ukopeshaji inayoendeshwa na mashirika ya fedha ya kimataifa IMF na WB, hivyo kuondoa dhana nzima ya matumaini na ndoto za kujitegemea.

Bahati mbaya wabunge wetu nao ndivyo hivyo kama tunavyojua. Hawawezi kumwambia Gavana wetu kuwa takwimu ulizozitoa ni za kweli, lakini sababu na suluhisho ni vya uongo. (fungua attachement)
 

Attachments

Bajeti ya 2007 inaonyesha itilafu ambazo tumezijadili hapa Jamii Forums kwa undani zaidi, na hata tukapendekeza njia za kuondoa hiyo itilafu. Bado nasisitiza kuwa, nia ya WB na IMF ni kutuwekea masharti ya kututia umasikini ili tuendelee kukopa mpaka siku ya kiama chetu. Hivyo basi, kinachotutia umasikini, sio riba itokanayo na hiyo mikopo, bali ni masharti yanayoambatana na mikopo tunayopewa.

Ile "prescription" ya WB na IMF ya kutulazimisha kushusha thamani ya Shilingi kwa kisingizio kuwa, hilo zoezi litakatisha tamaa manunuzi ya bidhaa kutoka nje ya nchi (import), na badala yake, litaongeza mauzo ya bidhaa zinazouzwa nje (export), ni ya hatari na inabidi tuihepuke.

Sababu za msingi za kuikataa hiyo "dose" tulizitoa humu ndani ya JF tena katika mjadala huu. Tulisema kuwa: "viwango vya uzalishaji katika jamii zetu ni vya chini sana. Tunategemea malighafi kutoka nje ili tuweze kuzalisha. Mfano wa bidhaa za lazima zitokazo nje ni Mafuta, Vitabu, Madawa, na Mbolea. Bidhaa zote hizi zinanunuliwa kwa fedha za kigeni. Thamani ya fedha ya nchi yetu inaposhuka na fedha za kigeni kupanda, gharama za uzalishaji zinakuwa juu na kusababisha mfumuko wa bei kwa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi".

Lakini takwimu kutoka katika bajeti ya Serikali, kama zilivyofanyiwa uchambuzi na taasisi ya Price Water House Coopers (pdf file attached) zinaonyesha kuwa: (page 10 of the pdf file) "Exports increased by 6.4% from US $ 2,945.5 million in 2005 to US $ 3,135.6 million in 2006". ‘The value of imports increased by 28.9% from US $ 2,997.6 million in 2005, to US $ 3,864.4 million in 2006. This wa mainly due to an increase in fuel prices and raw materials needed for manufacturing".

Hizi takwimu kutoka katika bajeti ya Serikali ya 2007 zina maana gani kwetu? Kadili tunavyokubali masharti ya WB na IMF, ndivyo shilingi yetu inavyozidi kushuka thamani. Kwasababu tunahitaji mafuta na "raw materials" kutoka nje, bidhaa zinazozalishwa ndani zinapanda bei na hazinunuliki. Hii ina maana kuwa, kwa makusudi ya WB na IMF, tunakatisha tamaa uzalishaji ndani ya nchi yetu.

Uzalishaji wa ndani ukianza kuchechemea, Serikali inakosa fedha. Inalazimika kwenda kukopa kwa mataifa makubwa au WB na IMF. Serikali inawekewa masharti kuwa ile fedha ya mkopo au ‘msaada" wanayopewa, haiwezi kutumika kurekebisha itilafu ya ndani kwa kusaidia kupunguza makali ya uzalishaji. Lakini wanaambiwa kuwa, wanaweza kutumia hizo fedha kununua ‘raw materials' au mahitaji mengine ya lazima kutoka nje.

Kumbuka Gavana amewaambia wabunge kuwa Serikali inatumia fedha za "wafadhili" kununua mahitaji nje ya nchi. Lakini hakuwaambia wabunge kwa nini Serikali inafanya hivyo. Jibu ni kuwa wanalazimishwa na WB na IMF. Hapa kuna mantiki gani? Uzalishaji ndani ya nchi yetu unapokufa kifo kitulivu, Serikali inakosa fedha za kigeni, kwasababu hatuuzi bidhaa za kutosha nje ya nchi.

Je, bidhaa zinazozalishwa ndani zikiwa ghali, wananchi watakidhi vipi mahitaji yao ya kawaida bila kupanga foleni na kula unga wa njano? Tulishawekewa masharti ya kufungua milango kwa makampuni ya nje kuingiza nchini kwetu bidhaa zinazouzwa kwa bei rahisi. Je, Serikali itapata wapi fedha za kigeni kama hatuuzi bidhaa za kutosha nje ya nchi? Inabidi ikaemehe (ombaomba) nje ya nchi kama anavyosema Lowasa. Ikakope kutoka mataifa yenye fedha au Majangiri wa WB na IMF.

Je hii ina madhara gani kwa taifa letu? Katika kitanzi hiki, hakuna njia yoyote ya maana kwa Serikali kupata fedha kutosha za kigeni kwa ajili ya kununulia mahitaji muhimu kama mafuta. Njia moja tu ni kuomba nje na kukopa. Kitanzi cha pili ni kuwa, kwasababu uzalishaji nchini kwetu unapigwa kabari na kushindwa kupumua, tunategemea bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.

Kwa maana hiyo basi, nchi yetu inaandaliwa kuwa soko la bidhaa zinazozalishwa nje. Haiandaliwi kuzalisha bidhaa kwa ajili ya masoko ya nje. Serikali ikihitaji fedha za kigeni, inabidi ikakope nje. Hii hali inachukuwa sura ya mviringo kwa maana ya kujirudia rudia mpaka tutakapo anguka chini kama Zaire. Hili ndilo lengo la WB na IMF.

Ndio maana tuliandika huko nyuma katika huu mjadala kuwa "uchumi wa nchi yetu unaendeshwa na mataifa ya nje kwa kutumia mitambo ya ukopeshaji ya mashirika ya fedha ya kimataifa WB na IMF. Kuendelea kukubaliana na haya mashirika ni kuondoa dhana nzima ya matumaini na ndoto za kujitegemea".

Kilimo


Viongozi wetu wanatulaghai, tena kwa kejeli kuwa hizi ni zama za Soko Huria, Utandawazi, Ujasirimali, na ujinga mwingine. Wamepiga teke ukweli wa kwamba kilimo ndio uti wa mgongo wa taifa letu. Lazima viongozi wetu watambue kuwa, bila wakulima, wasingeendesha hayo mashangingi. Bila wakulima, wasingevaa tai. Bila wakulima wa vijijini, barabara za rami za mjini zisingejengwa. Kwa kifupi, mpaka sasa hivi, wakulima wa vijijini ndio wanatuweka mjini.

Takwimu kutoka katika bajeti ya Serikali 2007 (page 10 of the pdf file) zinaonyesha kuwa, mwaka 2006, sekta ya kilimo imekwisha changia pato la taifa (GDP) kwa asilimia 44.7. Hii ina maana kuwa, kilimo bado ni uti wa mgongo wa taifa letu. Sera za WB na IMF zenye lengo la kuwaumiza wakulima wetu, inabidi zipigwe vita kwa nguvu zetu zote. Tukiumiza sekta ya kilimo, tunakuwa tumeumiza nchi. Sekta nyingine zote ni za ubabaishaji.

Mfano, pamoja na kwamba Tanzania ni nchi ya tatu kwa kutoa dhahabu katika Afrika, lakini mpaka sasa hivi, sekta ya madini imechangia pato la taifa kwa asilimia 3.8. Sekta ya Nishati imechangia asilimia 1.4, sekta ya Viwanda asilimia 9.2, sekta ya Mawasiliano na uchukuzi asilimia 5.4, na sekta ya Ujenzi asilimia 5.4. Takwimu hizi zinatufundisha kuwa, tunaweza kusimamisha uchimbaji wa madini kwa kufukuza makampuni yote ya nje, na uchumi wetu ukabaki ulivyo. Lakini hatuwezi kufunga sekta ya kilimo, alafu tukabaki salama.

Takwimu hizi zinaonyesha kuwa, hakuna sekta nyingine yoyote yenye ubavu wa kulipa madeni ambayo Serikali inakopa. Ni sekta ya kilimo peke yake. Wakulima wa vijijini ndio wanalipia gharama za mafuta ya kuendesha umeme tunaotumia mjini. Gharama za mafuta ya kuweka kwenye Mashangingi ya Viongozi na Wabunge. Gharama za kulipia viyoyozi maofisini kwa waheshimiwa na ndani ya magari yao.

Tumeuza benki ya wananchi NBC ambayo ilikuwa inafungua matawi vijijini, tukaleta benki za kibeberu zinazoishia mijini. Wakulima hawawezi kupata tena mikopo yenye ahueni ili kupunguza makali ya uzalishaji. WB na IMF wanaiwekea Serikali yetu masharti ili isiwasaidie fedha (subsdize) wakulima wetu. Mfano, bajeti ya Serikali 2007 (page 9 of the pdf file) imetenga asilimia 6.2 kwa ajili ya sekta ya kilimo. Inakuwa je sekta ya kilimo inachangia pato la taifa kwa asilimia 44.7, lakini inatengewa asilimia 6.2?

Karibia nusu ya fedha ya bajeti ya Serikali 2007, yaani Shilingi bilioni 2,549 zitapatikana kwa mikopo na zawadi. Lakini zaidi ya nusu ya fedha ya bajeti ya Serikali 2007, yaani Shilingi bilioni 3,866 ni kwa ajili ya matumizi tu na sio mipango ya maendeleo. Mchanganuo huu kutoka katika bajeti ya Serikali unatukumbusha kuwa, kwa kila Shilingi 100 anayotumia Rais wetu kwenda nje kukopa fedha, shilingi 63.7 ni za mkopo. Hivyo, tunakopa nauli ya Rais wetu ili aende kukopa. (tunakopa ili tukope-circle)

Kati ya mashirika ambayo yamekwisha tukopesha fedha kwa ajili ya hii bajeti ya Serikali, mojawapo ni WB. Lakini haohao WB wanatushauri tutenge asilimia chache kwenye sekta ya kilimo (6.2). Hata hivyo, tumeona kuwa sekta ya kilimo kinachangia pato la taifa kwa asilimia 44.7. Hata kwa mtu mjinga kabisa, baada ya kuangalia michango kutoka katika sekta nyingine, atawekeza asilimia kubwa ya bajeti yake kwenye kilimo ili mchango wa hiyo sekta uongezeke. Je fedha ya kuwalipa hao WB itatoka wapi?

Let me be clear: corrective actions are needed to eliminate our country's indebtedness, restore national ownership, control of productive assets, and balance exports and imports. A key step would be to close the World Bank, IMF, and restore the right of economic self-determination to our people and in deed, to our government. Responsibilities for economic management should be transferred to the people of Tanzania.



 

Attachments

Back
Top Bottom