Tunaosimama na Sabaya hatuipingi Serikali, tunapambana dhidi ya dhuluma na uonevu kwa waliojitolea kupambania Taifa

Naona wafuasi wa Bashite wnajificha sana nyuma ya Issue ya Sabaya, saa yake bado ila ikifika hakuna wamkusaidia
 
Kesho Bashite anaweza kuwa mkubwa zaidi kuliko wewe na Gwajima wako
Aaah wapi laws of nature hairuhusu.
Alishafutwa kwenye ulimwengu wa roho,atarudia Kazi yake ya awali kukataa mkaa mbezi.
Uliona wapi gunia la misumari likabebeka
 
Ngoja nikuonyeshe "UNYAMA" angalau huu tu wa Ole Sabaya kisha utasema ni wangapi wengine wameshauriwa kujitokeza kueleza walivyotendwa.
 
Hii ndiyo 255 ukifinya nawe unafinywa mwisho wa siku unakuwa mfinyano tu.
 
Hivi kumbe Ole sabaya alikua anapamba ia Taifa🙄
 
Crap.

Una uhuru wa kusimama na watu wema au na jambazi Sabaya.
 
Mleta mada hivi uhujumu uchumi, kutakatisha fedha na kuongoza genge la uhalifu/ujambazi ni kupambania taifa?
Tuwe serious kidogo akikutwa na hatia, sheria ichukue mkondo wake tu.
 
Nenda kamtetee mahakamani. Hii setikali iliyomuweka ndio inamshitaki wewe ni nani uone anaonewa. Hukosi kuwa ni mnufaika wa matendo ya Sabaya. Hata Hitler na Id Amini walikuwa na mashabiki wao pia haishangazi.
 
Mimi sijui mengi kuhusu uhalifu wake,!! Ila ninachojua, huyu ni mwana ccm, kijana, aliyehudumu kipindi cha magu(marehem).

Ambaye ndo alikua ni mtaji wa kisiasa kwa ccm kwa walio wanyonge
 
Hakuna kesi hapo kwa maslahi mapana ya chama pendwa
 
Kuna clip nyingi zinatokea kwenye mitandao zikimuonyesha Sabaya kama mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama akichukua hatua za kutetea umma kwa kuwakamata wahujumu uchumumi na watu dhulumati kwa wanyonge.

Binafsi naamini hatua za kumsimamisha kazi na baadae kumburuza mahakamani sabaya mara baada ya kifo cha Magufuli ni hatua ya mwanzo tu ya kuwarejeshea fisadi na watu dhulumati furaha na ni ishara samia hakuja kwa wanyonge kama alivyokua Magufuli.

Haiwezekani kiongozi aliyekua anatetea maslahi ya umma kama Sabaya aondolewe na kuburuzwa hapohapo mahakamani kwa uzushi tu wa watu wenye kisasi kutokana na utumishi wake.

Picha iliyotokea ni furaha kwa mabwanyenye na watumishi wala rushwa waliyokua wanadhulumu haki za raia wa kawaida. Pia watu hao wanaonekana wanaamini samia ni mtu wao yeye na CCM yake sio tena ya kutetea umma wa wananchi ila wafanyabiashara na fisadi wapenda rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma.

Anyway time will tell 2025 wanaccm wataamua tena nani awaongoze maana kura za wananchi kwa magufuli zimeenda naye. So sad.
 
Pole wewe ndio yule baunsa wake mmoja ambaye hatujakukamata. Mpelekee Hennesy Kisongo.
 
Kuna clip nyingi zinatokea kwenye mitandao zikimuonyesha sabaya kama mkuu wa wilaya na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama akichukua hatua za kutetea umma kwa kuwakamata wahujumu uchumumi na watu dhulumati kwa wanyonge...
Tapeli, jambazi, mbakaji, muuaji, mtesi mahali pake pa kuishi ni gerezani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…