SYLLOGIST!
JF-Expert Member
- Dec 28, 2007
- 8,189
- 7,853
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tafuta hela bro ukalipe mahari,Tatizo ulilo nalo unadhani kila aliye kinyume na mfumo huu hana pesa
Swali kwako. Kwa nini wazungu walipiga marufuku kununua waafrika karne ya 19 ? Unadhani walikuwa hawana pesa za kuendelea kuwa nunua.
Kumbuka pia huko enzi za mababu hakukuwa na feministsSubiri kwanza unijuze kitu.
Huko enzi za mababu hapakuwa na mahari? Mama zetu, bibi zetu hawakutolewa mahari?
Mahari ni utamaduni.
Ng’ombe watakuja kwetu na mie nitaenda kwa kina ng’ombe.
Cha ajabu kuwa wale walioona tohara kwa wanawake kuwa ni ukatili hawakuona ni Ukatili kutenganisha Familia za Kiafrika, hawakuona ni ukatili kuwachapa viboko Waafrika, wanawake na wanaume, wa 'toto' na wakubwa hawakuona ukatili wao mpaka pale waumini wa dini, tena baadhi, kuingilia kati biashara za watu zilizoakisiwa na kudhaminiwa na Serikali zao ambazo ndizo hizo hizo zilizowatumia-waumini wa dini- kuja kufanya mabadiliko ya kile walichokiita mabadiliko ya kiroho. Mabadiliko ya Tamaduni zilizopitwa na wakati.Kwa nini wazungu walipiga marufuku kununua waafrika karne ya 19
Mahari ni Utamaduni wetu. It is our Custom and should be respected as is. Tatizo mnataka kuunganisha mambo mengi ya Haki kwa kuangamiza Tamaduni zetu za Kiafrika.Mahari ni sawa kuendelea kuwepo au sio sawa isitishwe ?
Swali kwako
Una maanisha nini TPP? Sina tofauti ya Kivipi, fafanua nikuelewe.Hauna tofauti na hao wazungu na waarabu waliokuwa wana nunua na kuuza waafrika
Utoaji wa mahari ni utamaduni ambao umekuwepo kwa muda mrefu katika jamii nyingi za Afrika na sehemu nyingine duniani. Hata hivyo, kuna sababu kadhaa ambazo zinaweza kufanya utoaji wa mahari kuonekana kuwa ni utamaduni uliopitwa na wakati.
Kwanza, utoaji wa mahari unaweza kuchukuliwa kama aina fulani ya biashara ya watu, ambayo inaweza kusababisha mawazo ya ubaguzi wa kijinsia na kudhalilisha wanawake. Katika baadhi ya jamii, mahari inaweza kuwa ya kiwango kikubwa sana, na hii inaweza kuzuia wanawake kuolewa na wanaume ambao hawana uwezo wa kulipa mahari hiyo.
Pili, utoaji wa mahari unaweza kuathiri haki za wanawake. Katika baadhi ya jamii, mahari inaweza kutafsiriwa kama kifuta jasho cha wazazi wa msichana, na hii inaweza kuwa na maana ya kwamba mwanamke anaweza kutazamwa kama mali au kitu cha biashara. Hii inaweza kusababisha wanawake kupata ubaguzi na kukosa haki ya kuchagua wenza wao.
Tatu, utoaji wa mahari unaweza kuchukua nafasi ya upendo na uhusiano wa kimapenzi kati ya wapenzi au wanandoa. Badala yake, mahari inaweza kuonekana kama kiwango cha thamani ya mwanamke, badala ya upendo na kujali. Hii inaweza kuathiri uhusiano wa ndoa, na kusababisha matatizo ya kifamilia na ndoa zenye shida.
Kwa hiyo, utoaji wa mahari unaweza kuonekana kuwa utamaduni uliopitwa na wakati kwa sababu ya athari zake hasi kwa haki za wanawake, uhusiano wa kimapenzi na familia. Ni muhimu kuhamasisha jamii kuondokana na utamaduni huu na badala yake kukuza haki sawa kwa wanawake na wanaume na uhusiano wa kimapenzi ambao unategemea upendo na kujali bila kuangalia thamani ya mahari
Haya sasa, mnaanza matusi na madharau. Ati ni Ushenzi.Fikra zako kuhusu tamaduni za kishenzi( mahari ) hazina tofauti na wale wazungu na waarabu wa kale walio kuwa na fikra za kishenzi kuhusu tamaduni za kununua na kuuza watu( utumwa )
Zingatia sio kila tamaduni mlizonazo zinapaswa kukumbatiwa kwa kigezo kuwa ni tamaduni zenu na muachwe na tamaduni zenu
Huo ni mtazamo wa kigeni. Hakuna mohari iliyopewa thamani ya kifedha. Hilo hallikuwepo. Hayo ya milioni au mamilioni waliyoleta ni wageni. Hatahivyo nahisi lugha ya dhihaki.Mahari hata ukiambia utoe milioni 10 unachotakiwa kutoa hakizidi hata milioni.
Sasa tatizo lipo wapi kama ni mila na desturi za kiafrika?Halafu mahari ni mila na desturi za kiafrika, kila jamii ya kiafrika wanayoprocess ya mahari, South Africa hapo wazulu wanaita LOBOLA.
Hayo yote yangepungua mahari ingefutwaUkitaka kupinga mahari na kupata picha mahusiano yatakuwaje pigia picha hali ya sasa ya mabinti kuzalishwa hovyo halafu kijana aliyezalisha anakuja kujulikana baadae sana mtoto ameshaanza kutembea.
Wazazi wanakubali tu maana watafanyaje maana binti yao kishazalishwa na huyo kijana ndie baba wa mjukuu wao na wameshaunganisha damu.
Sasa pigia picha mahari ikikataliwa tutakuwa katika hali gani kama jamii ya mwafrika. Kijana anayekataa mahari hofu yake sio pesa ya kulipia ile process yote ya posa bali hofu yake ni kurasimisha mahusiano yake na kutambulika ukweni kama mume wa fulani.
Vijana wengi wa sasa courtships hawaziwezi yaani hawawezi ile kitu inaitwa kufuata utaratibu wa mila na desturi zetu waafrika.
Kijana muhuni atataka akutane na binti wapelekane huko kwake walane hadi atosheke na ikibidi ampe na ujauzito kabisa huyo binti halafu akimbie kwa binti mwingine.
Ndio maana miaka hii kuna hizi story za kusikia binti anataka kuolewa na kijana mpya ila ana mtoto au watoto sasa anaomba ushauri afanyaje, au kijana anataka kuoa ila ana mtoto na mwanamke mwingine.
Haya yangepungua sana endapo utaratibu wa mahari ungeheshimiwa na kuboreshwa.
Iv si kuna wengne mahari ni msaafu tu?Tafuta Pesa ulipe mahari,
Mwanaume hakimbii majukumu, anayakabili
Wanawake Wa kuwapa thamani ndio hawa ma feminist uchwara?Kwa aina ya wanaume tuliopo hii nchi mahari ni muhimu sana kuwepo,kwasababu inampa mwanamke thamani mbele ya mwanaume.ukiondoa mahari thamani ya mwanamke itaondoka kwasababu wanaume wakiafrika hawajali sana umuhimu wa mwanamke nje ya mapenzi na kuzaa.Kwahiyo wacha iwepo ili wanaume tuangaikie kile chenye thamani kwa nafsi yako.Ukioa bila mahari ata ndoa yenyewe inakua haina thamani.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Feminist hawa hawa wanaotaka 50/50 kwenye maslahi yao Ila kwenye kwenye ishu zinazotaka majukumu na uwajibikaji wanalamba chocho.Hakuna mwanamke mwenye thamani kama feminist
Kwa aina ya wanaume tuliopo hii nchi mahari ni muhimu sana kuwepo,kwasababu inampa mwanamke thamani mbele ya mwanaume.ukiondoa mahari thamani ya mwanamke itaondoka kwasababu wanaume wakiafrika hawajali sana umuhimu wa mwanamke nje ya mapenzi na kuzaa.Kwahiyo wacha iwepo ili wanaume tuangaikie kile chenye thamani kwa nafsi yako.Ukioa bila mahari ata ndoa yenyewe inakua haina thamani.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Mahari inawapandisha thamani hamjui tu.
Tatizo lenu nyie feminist huwa mnapigania kujimaliza wenyewe.
Bila mahari mtaolewa na kuachika hovyo.
Kwani wanawake wakizungu huwa na thamani tofauti na wanawake weusi/wakiafrika?Watanzania wanaooa wanawake wazungu wanawalipia mahari?
Thamani ya wanawake wazungu huwa inashuka kwa kutolipiwa mahari?