Tunaposema Diamond ni mnyonyaji muwe mnaelewa. Inasemekana kipindi cha Bartender kimepigwa ''stop''

Tunaposema Diamond ni mnyonyaji muwe mnaelewa. Inasemekana kipindi cha Bartender kimepigwa ''stop''

Robidinyo

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
4,043
Reaction score
8,686
Msanii Baghdad aliwahi kusema kuwa wazo la kipindi cha The Bartender lilikuwa ni lake na mwanzo wazo lilikuwa TheCounter au The Bartender na alilisajili COSOTA na kubaki na hatimiliki yake. Alishangaa kuona kipindi kinatangazwa wakati makubaliano hayakuwa yametimizwa na kukubaliana. Baghdad anasema kuwa makubaliano yalikuwa ni apate 13% ya mapato yatokanayo na show na idea zote ambazo ataziweka pale Wasafi kuliko kuajiriwa, yaani awe na life-time contract na Wasafi Media.

Baghdad anaendelea kusema kuwa wakiwa katika mchakato wa kusaini mkataba ambao ilionekana kuwa 13% ni kubwa na ishuke hadi 5% ghafla akashangaa kuona promo ya The Bartender, anasema aliamua kuwasiliana na Diamond, cha ajabu Diamond hakuwahi kupokea simu wala kujibu meseji zake. Anasema ilimstua na kuamua kumtafuta Babu Tale, Tale alimsihi sana Baghdad kuwa mtulivu wakati anaongea na Diamond juu ya hili. Alimsihi pia kutofanya chochote mathalani interview popote. Baada ya siku kadhaa Tale na Baghdad walichekiana na kumchana kuwa Diamond kasema fanya chocote unachoweza.

Baghdad aliamua kwenda COSOTA kutafuta haki yake kwa maana hata wazo la Jogoo ni miongoni mwa madini aliyoyatoa Wasafi. Anazidi kusema kuwa, COSOTA waliwaita ili kuwasuruhisha japo Diamond alikuwa akituma wawakilishi, mazungumzo yalifanyika kwa siku kadhaa bila mafanikio na Baghdad kuamua kwenda Mahakamani ili tu haki yake ipatikane.

Kwakeli huu ni utapeli wa kuaminika. Jamaa hawana ubunifu wowote ni wazee wa Kucopy na ku-paste. Walimsema sana Ruge hawa; sasa yule mtoto aliyekua analialia kuonewa kawa mtoto mbaya.
 
Tatizo la usafini ni ubunifu na ile tabia ya kukwapua watangazaji vituo tofauti wasio na mawazo bunifu, mfano Zembwela iv yule ana ubunifu upi aliiua Uswazi ya EATV baada ya Mussa Hussein kutoka. Maulid Kitenge naona alpoishia ndo hapo hana ubongo mpya wa kutanua ubunifu, Lil Ommy yuko vizuri ila naona kapwaya The Switch maana hajaja pale na ubunifu mpya. Pale watu wenye maono ni Ambangile na nahisi akimtumia vizuri anaweza leta impact kubwa, Aaliyah, na Edo Kumwembe ingawa yupo kimasilahi zaidi lakini akibadili mindset Edo ana akili kichwani.
 
Uzuri wa Kiba hapendi maujiko. The good, the bad and the ugly.
 
Baghdad mbona naye kacopy, au paka waje wamshitaki wenye startup yao ndio aseme ukweli?
 
Mbona hizi Thread za 'Diamond Mnyonyaji' zimekuwa nyingi kipindi hiki kulikoni? Mna ajenda gani? Ni lini wewe Robidinyo umemuandika Diamond kwa mazuri? Je ni kweli hajawahi kufanya lolote zuri? Wewe ni jinsia gani? Una familia? Asubuhi,mchana,jioni,usiku unamuwaza Diamond. Just imagine mtoto wa kiume (kama ndivyo) saa 8 usiku unawaza uandike nini ili watanzania wamuone mbaya kijana Diamond aliyekulia kwenye maisha ya kimaskini ambaye anaendelea kupambana kujikwamua na ukata na kuwasaidia pia vijana wengi wanaomzunguka, hii roho mbaya inakusaidia nini? Hivi inakuwaje mtu unakuwa na chuki mbaya kiasi hiki? Sidhani kama hata wakina Tanasha wanamchukia kiasi hiki...
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Robidinyo,

Domo ni mwizi na kila mwenye akili timamu analiona hilo.

Kaiba na anaendeleakuiba nyimbo za watu.

Anakopi na kupaste kuanzia kweny Nyimbo, watangazaji mpaka vipindi vya media.

Aisee wazee shule MUhimuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Mleta uzi jitihada unazozifanya za kumchafua huyo kijana wa tandale ni za kipuuzi na za kubezwa na kila mpenda maendeleo! Wewe pia anzisha kituo chako ili utende hiyo haki unayoipigania, huyo dogo mpk alipofikia mafanikio hayo kakwepa mishale mingi si wa kuangushwa na mende kama wewe.
 
Moderator uzi wa hivi upo tayari huyu sijui kafufukia wapi kipindi kilisimama kwa muda na kikarudi hewani unganisheni.
 
Baghdad mbona naye kacopy, au paka waje wamshitaki wenye startup yao ndio aseme ukweli?
Kwanini wakiuke Makubaliano hauni kama ni utapeli.. Msiwe mnatetea kila kitu ebu vaa viatu vya baghdad uone maumivu yake..
 
Mbona hizi Thread za 'Diamond Mnyonyaji' zimekuwa nyingi kipindi hiki kulikoni? Mna ajenda gani? Ni lini wewe Robidinyo umemuandika Diamond kwa mazuri? Je ni kweli hajawahi kufanya lolote zuri? Wewe ni jinsia gani? Una familia? Asubuhi,mchana,jioni,usiku unamuwaza Diamond. Just imagine mtoto wa kiume (kama ndivyo) saa 8 usiku unawaza uandike nini ili watanzania wamuone mbaya kijana Diamond aliyekulia kwenye maisha ya kimaskini ambaye anaendelea kupambana kujikwamua na ukata na kuwasaidia pia vijana wengi wanaomzunguka, hii roho mbaya inakusaidia nini? Hivi inakuwaje mtu unakuwa na chuki mbaya kiasi hiki? Sidhani hata kama wakina Tanasha wanamchukia kiasi hiki...
Sent using Jamii Forums mobile app
We ni jinsia gani mkuu au ndo Juma lokole. Inakuuma sana huyo mzazi mwenzenu mnataka aongelewe kwa mazuri tu wakati kuna mabaya kibao anafanya..

Usinipangie cha kupost wala usinipangie mda wa kupost,. Wewe andika mazuri ya huyo mzazi mwenzako, mi ntaandika ambayo nyie hamwezi kuyaandika kisa ushabiki maandazi, Imekuuma utapeli wake kuwekwa wazi,.

Nyie ndo wale hata jamaa akipost sink la choo Mnaenda kukoment viemoj vya moto huku mkibana pua Chibu akee, simbaa akee, hizo pigo peleka huko hapa tunaongea mambo ya kiume, Utapeli haukubaliki
 
Back
Top Bottom