Tunatamani uwepo wao lakini haiwezekani kuwa nao

Na sio wote wanalia..
Kingine till now hakuna mtu aisiyejua kuwa kifo kipo...

Tunarudi pale pale ukijua mechanism za hormonal response mwilini sizani kama utakua unabisha bisha kuhusu watu kulia na kujiandaa na hayo unayosema..
Hukatazwi kulia.

Mimi Point yangu kuu ipo hapa, Hata ukilia bado uhalisia wa kifo upo palepale.

Ulie, ucheke, usikitike, unyamaze hakubadilishi uhalisia wa kifo.

Kifo kipo palepale.

Kwa hivyo kusikitika miaka nenda rudi hakusaidii kitu.
Ina elekea wee mwamba una roho mbaya sana aiseee..
Roho haipo.

Roho ni dhana ya kufikirika tu.
an wee licha ya kumkataa Mungu ila sasa naona unataka kukataa mpaka kuhusu kulia yaani umekaa kiukatili ukatili tuu
Sijakataa kuhusu kulia.

Nilikwambia na Ninakwambia hivi..👇

Kulia hakubadilishi chochote na wala hakusaidii chochote baada ya kifo kutokea.
 
Kwanini useme ni dhana tuu
Tena ya kufikilika
 
Yeah mimi nimemaliza. Unajua labda mtu ataona tu Hilo la mwanangu lakini Kuna jumbe mbili ndani yake.

1. Kuna watu wanaotupa watoto wakiwazaa.
Mtu mpaka anafikia hatua ya kutupa mtoto, kuna mambo mawili:

Moja, Ameshindwa kabisa kabisa kumhudumia huyo mtoto. Akaamua amtupe amtelekeze. Wasamaria wema waje wamsaidie.

Mbili, Hana mapenzi kwa huyo mtoto. Pengine hakutarajia kumpata. Hivyo ana amua kumtupa.

2. Kuna wale ambao watoto wanao lakini hawawajali.
Hawa wanakuwa hawana mapenzi kwa hao watoto. Pengine labda waliwapata wakiwa hawatarajii kulea, Hivyo wanalea hao watoto ili mradi tu.
Kwa hivyo lazima kuwepo sababu kwa baadhi ya watu wanao zaa watoto wao kabisa lakini hawana mapenzi ya kuwalea kwa dhati.
 
Kama amebakwa ni ishu nyingne lakini kama ni maridhiano kwanini ubebe mimba au uruhusu iingie ikiwa huna uwezo wa kulea!?.

Na kama umeamua uzae kwanini usimlee kwa mapenzi mwanao!?.
 
Kwa sababu hakuna uthibitisho wowote wa kuwepo roho.
Kwani uhai ni nini!?. Na inakuwaje mtu anakuwa hai!?.

Na kifo ni nini!? Inakuwaje tunasema huyu kafa!?.

Kwanini mtu akifa haiwezekani kumrudisha!?.

Yaani kwanini binadamu pamoja na teknolojia zilizopo sasa, hawezi kuzuia asife!?. Yaani lazima muda ukifika afe??.

Kwanini tunakufa!?.
 
Kama amebakwa ni ishu nyingne lakini kama ni maridhiano kwanini ubebe mimba au uruhusu iingie ikiwa huna uwezo wa kulea!?.
Hapo ndio tunasema mapenzi kwa huyo mtoto yameisha.
Na kama umeamua uzae kwanini usimlee kwa mapenzi mwanao!?.
Kuna baadhi ya watu huzaa watoto bila matarajio hivyo unakuta wanalea hao watoto ili mradi tu.
 
Kwani uhai ni nini!?.
Uhai ni hali ya kiumbe kuwa na uwezo wa kukua, kupumua, kuhisi, kuzaliana n.k

Kapitie sifa za viumbe hai.
Na inakuwaje mtu anakuwa hai!?.
Hii ni sayansi ya darasa la tatu kabisa.

Nenda kajifunze sifa za viumbe hai.
Na kifo ni nini!? Inakuwaje tunasema huyu kafa!?.
Kifo ni kutokuwa na uhai.

Mtu atasemwa kafa akiwa hana sifa za kiumbe uhai.

Hapumui, hakui, hazaliani, hahisi chochote kwenye mazingira n.k
Kwanini mtu akifa haiwezekani kumrudisha!?.
Kwa sababu bado hakuna teknolojia hiyo.

Kwa sasa bado teknolojia ya kurudisha uhai haijafikiwa.

Ila tafiti zinavyo endelea, inawezekana uhai ukaweza kurudishwa kwa kiumbe kilicho kufa au mtu aliyekufa.
Yaani kwanini binadamu pamoja na teknolojia zilizopo sasa, hawezi kuzuia asife!?. Yaani lazima muda ukifika afe??.
Teknolojia inakua sio kwamba imeshindwa au itashindwa forever kurudisha uhai.

Huenda huko mbeleni teknolojia ikafanikiwa kuzuia kifo au ikaweza kurudisha uhai.
Kwanini tunakufa!?.
Kuna sababu nyingi sana zinazo sababisha tufe.

Kuna magonjwa, ajali, majanga ya asili, vita, maamuzi binafsi ya mtu kuamua kujiua kwa kunywa sumu au kujinyonga n.k

Pia tunakufa kwa sababu kadiri muda unavyokwenda seli zetu za mwili nazo hufa na kuishiwa nguvu. Hivyo uzee pia unatuua.

Tukiweza kudhibiti factors zote hapo, Tutaweza kuzuia tusife kwa 100%
 
Eehh, haya sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…