Tunavyosema mkataba una dosari muelewe, oneni ufafanuzi wa CCM hapa na ndio wamesema wanaelimisha watu

Tunavyosema mkataba una dosari muelewe, oneni ufafanuzi wa CCM hapa na ndio wamesema wanaelimisha watu

Exile

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2021
Posts
1,477
Reaction score
3,642
Wanaendelea kupotosha kwamba mkataba huu hauna ukumo, sio kweli! Mkataba huu una ukomo; ibara ya 23 ibara ndogo ya 1 inasema wazi ukomo wa mkataba huu; itakapotokea moja katika haya mambo mawili, kule kwenye mradi wa utekelezaji (ambao haujaanza) mradi ukaisha basi na mkataba huu utakuwa umefika mwisho lakini ikitokea ile mikataba mingine miwili ikisainiwa (HGA na mkataba wa mradi) na utekelezaji wake umeisha basi mkataba huu utakuwa umefika ukomo.
Screenshot_20230724-093044_Twitter.jpg
 
Yes CCM wanasema kweli, na huu ndio uelimishaji umma wenyewe kuhusu hii IGA. IGA sio mkataba, ni makubaliano tuu, mkataba ni HGA bado, utakuwa ni mkataba mzuri.
P
Pascal mzee wangu unatatizo sehemu, km sio ulevi basi ni uzee.
Tangu lini makubaliano mabovu yakaleta mkataba mzuri?
Mbona mnajitoa ufahamu kiasi hiki?
 
Tatizo la CCM anayetoa ufafanuzi yeye mwenyewe hajausoma
Nimekumbuka enzi za ufafanuzi wa JK... mnaitana wazee wa Dar es salaam, nje mnapitia kwanza vibahasha vya kaki na sambusa kwa soda kisha mnaingizwa ukumbini.

Mnaanza kusifia namna alivyopasuliwa tezi dume kisha mwenyekiti JK anatoa ufafanuzi uliojaa ghilba, vijembe kejeli na mipasho wazee wanapiga makofi ufafanuzi kwisha!!
 
Nimekumbuka enzi za ufafanuzi wa JK... mnaitana wazee wa Dar es salaam, nje mnapitia kwanza vibahasha vya kaki na sambusa kwa soda kisha mnaingizwa ukumbini.

Mnaanza kusifia namna alivyopasuliwa tezi dume kisha mwenyekiti JK anatoa ufafanuzi uliojaa ghilba, vijembe kejeli na mipasho wazee wanapiga makofi ufafanuzi kwisha!!
Tuna nchi ya kijinga sn
 
Yes CCM wanasema kweli, na huu ndio uelimishaji umma wenyewe kuhusu hii IGA. IGA sio mkataba, ni makubaliano tuu, mkataba ni HGA bado, utakuwa ni mkataba mzuri.
P
Mzee wa vuguvugu na kutegea upande... na vile vi mada vyako unavyotegeshea katikati ili uzito utakapoelemea nawe unaelekea huko.

Ila pasco kwa muundo wa kichwa chako ulivyokaa kaa huwa sikushangai ndio psychology yenu ilivyo! Huwa hamna msimamo wa muda wa kati achilia mbali mrefu. Akili zenu huwa na ka ukasuku flani hivi na huendeshwa zaidi na matukio si uhalisia na hupenda sana viujiko ujiko vilivyojaa tamaa na uroho mwingi.

Hovyo sana.
 
Mwenye taarifa anijuze kabla TICTS hajapewa mkataba pale bandarini ni nchi ipi iliingia makubaliano ya awali (IGA) na bongolala kabla huyo TICTS hajasaini HGA, maana tusiendelee kujazana ujinga..
 
Back
Top Bottom