Tunavyosema mkataba una dosari muelewe, oneni ufafanuzi wa CCM hapa na ndio wamesema wanaelimisha watu

Tunavyosema mkataba una dosari muelewe, oneni ufafanuzi wa CCM hapa na ndio wamesema wanaelimisha watu

Duh! Mayala mbona unajiaibisha hivi? Yaani umesomea sheria lakini huelewi hata maana ya contract? Tatizo la kusomea kitu halafu hujawahi ku-practice.

Nikusaidie Mayala, contracts zote ni agreements. Lakini siyo agreements zote ni contracts. Kinachotofautisha kati ya agreement ambayo ni contract na agreement ambayo siyo contract, ni kitu kimoja tu: Agreement ambayo ni contract ina nguvu ya kisheria. Hivyo hii agreement ya kishenzi aliyosaini Mbarawa, kwa sababu ina nguvu ya kisheria, ni contract.

Lakini wajinga kwa vile IGA ina neno Agreement basi wanasema ule mkataba wa kishenzi wa DP ni agreement kwa sababu kuna neno Agreement. Lakini hawajiulizi kama IGA ni agreement kwa sababu ya neno Agreement, itakuwaje HGA iwe contract, wakati na yenyewe ina neno agreement.

CCM ni kaburi la akili. Mtu, katika hali ya kawaida anaweza kuwa na akili, angalao hata ile ya kawaida, lakini akienda CCM na labda akapewa na kacheo kidogo tu, akili yote kwisha, anabakia anabwabwaja vitu vya ajabu mpaka unashangaa.
Asante kwa elimu mkuu
 
Duh! Mayala mbona unajiaibisha hivi? Yaani umesomea sheria lakini huelewi hata maana ya contract? Tatizo la kusomea kitu halafu hujawahi ku-practice.
Duh...!, naomba niheshimu mawazo yako, maana ni kweli nimesoma sheria lakini sija practice.
Nikusaidie Mayala,
Asante sana kunisaidia,
contracts zote ni agreements. Lakini siyo agreements zote ni contracts. Kinachotofautisha kati ya agreement ambayo ni contract na agreement ambayo siyo contract, ni kitu kimoja tu: Agreement ambayo ni contract ina nguvu ya kisheria. Hivyo hii agreement ya kishenzi aliyosaini Mbarawa, kwa sababu ina nguvu ya kisheria, ni contract.
Asante sana kwa elimu hii.
Lakini wajinga kwa vile IGA ina neno Agreement basi wanasema ule mkataba wa kishenzi wa DP ni agreement kwa sababu kuna neno Agreement. Lakini hawajiulizi kama IGA ni agreement kwa sababu ya neno Agreement, itakuwaje HGA iwe contract, wakati na yenyewe ina neno agreement.
Naomba kukiri mimi ni miongoni mwao.
CCM ni kaburi la akili. Mtu, katika hali ya kawaida⁰ anaweza kuwa na akili, angalao hata ile ya kawaida, lakini akienda CCM na labda akapewa na kacheo kidogo tu, akili yote kwisha, anabakia anabwabwaja vitu vya ajabu mpaka unashangaa.
Duh...!.
P
 
Yes CCM wanasema kweli, na huu ndio uelimishaji umma wenyewe kuhusu hii IGA. IGA sio mkataba, ni makubaliano tuu, mkataba ni HGA bado, utakuwa ni mkataba mzuri.
P
Ume-time travel na kugundua kwamba utakuwa mzuri au huo uzuri wake upo based kwenye wishful thinking ?

Binafsi naweza kusema mkataba huu utakuwa mbaya (kwanini) sababu kuanzia mwanzo hata makubaliano ni ya ajabu hata makubaliano yangekuwa mazuri historia inatwambia kwamba katika suala la mikataba huwa tunaboronga....
 
Yes CCM wanasema kweli, na huu ndio uelimishaji umma wenyewe kuhusu hii IGA. IGA sio mkataba, ni makubaliano tuu, mkataba ni HGA bado, utakuwa ni mkataba mzuri.
P
Acha kupotosha umma. Makubaliano yoyote yakiwa kwenye maandishi yanaitwa mkataba. Yasipokuwepo kwenye maandishi ndiyo makubaliano. Anagalia kamusi ya kiswahili kitukuzwe. Yeyote anayesema haya ni makubaliano hana akili, arudi shule ya msingi akasome upya misamiati ya kiswahili.
 

Attachments

  • Screenshot_20230724_170324.jpg
    Screenshot_20230724_170324.jpg
    126.5 KB · Views: 3
Yes CCM wanasema kweli, na huu ndio uelimishaji umma wenyewe kuhusu hii IGA. IGA sio mkataba, ni makubaliano tuu, mkataba ni HGA bado, utakuwa ni mkataba mzuri.
P
Pascal bado unaleta uchawa Ili upate uDC?
 

Attachments

  • 20230710_203844.jpg
    20230710_203844.jpg
    82.8 KB · Views: 3
tumefanya mikataba mingi mikubwa kama SGR na JNHEP why huko kote hatukua na IGA?? pia kwanini tuingie IGA na Dubai na Sio UAE??
Kuna mikataba ya kimataifa ya makampuni haina IGA, ila mikataba ya nchi na nchi ina IGA, mkataba wa bomba la mafuta la Uganda, Hoima-Chongoleani una IGA na HGA zake. Mkataba wa LNG una IGA na iliisha ridhiwa na Bunge, HGA yake bado.

Ni kweli hii IGA ilipaswa kuwa kati ya Tanzania na UAE and not Dubai.
P
 
Kuna mikataba ya kimataifa ya makampuni haina IGA, ila mikataba ya nchi na nchi ina IGA, mkataba wa bomba la mafuta la Uganda, Hoima-Chongoleani una IGA na HGA zake. Mkataba wa LNG una IGA na iliisha ridhiwa na Bunge, HGA yake bado.

Ni kweli hii IGA ilipaswa kuwa kati ya Tanzania na UAE and not Dubai.
P

Tuendelee mdogo mdogo tutaelewana huko mbele.
Pia makubaliano hayo yanaonyesha Haki zote ni za DP na wajibu wote ni wa TZ hii imekaaje kwako??
Kwamba Duties zote ni zetu na obligation zote ni DP.
hii imekaaje kwako?
 
Yes CCM wanasema kweli, na huu ndio uelimishaji umma wenyewe kuhusu hii IGA. IGA sio mkataba, ni makubaliano tuu, mkataba ni HGA bado, utakuwa ni mkataba mzuri.
P
Je, makubaliano ndio yanatakiwa kua mabovu?

Je, kama wameweza kuingia makubaliano yenye vipengele vya hovyo, wataweza kulinda maslahi ya taifa kwenye mkataba?

Je, kama wanao uweledi, kwanini maslahi ya taifa yasingeanza kuangaliwa kuanzia kwenye hayo makubaliano mpaka kwenye mkataba wenyewe?

Je, unaweza kujenga nyumba yenye msingi mbovu, alafu ukasema "huu ni msingi tu jamani, kila kitu kitakaa sawa wakati wa kuezeka"?

Mkuu Pascal, a penny for your thoughts!

[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Tuendelee mdogo mdogo tutaelewana huko mbele.
Pia makubaliano hayo yanaonyesha Haki zote ni za DP na wajibu wote ni wa TZ hii imekaaje kwako??
Kwamba Duties zote ni zetu na obligation zote ni DP.
hii imekaaje kwako?
Nimesema karibu kila kitu kuhusu huu hii IGA
Katiba mbovu, sheria mbovu, mikataba mibovu. Leo tumetozwa zaidi ya Tsh. Bilioni 260. Kufanywa kichwa cha Mwendawazimu hadi lini? kwenye hili nimesema
Wanabodi,

Kwenye hii IGA, hoja za Prof. Shivji zina mashiko, kuwa mkataba umeegemea upande mmoja, serikali yetu ndio yenye wajibu, na sio DPW!. Tumeingia makubaliano na Dubai, ambayo sio sovereign, kukitokea mgogoro wa kushitaki kimataifa, Tanzania tunaweza kushitakiwa kwa international instruments, kwasababu Tanzania ni member wa Geneva Convention, Vienna Convention of the law of treaties lakini Dubai sio member, haipo kwasababu Dubai sio nchi. Kama DPW ndio watatukosea, Tanzania tutawashitaki wapi wakati Dubai sio member wa Geneva Convention, sio signatories wa international treaties?!. Member kule ni UAE!. Kwenye ile IGA, hakuna popote UAE, imetoa Power of Attorney kwa Dubai!, hivyo Tanzania kama nchi, tumeingia mkataba na an entity which has no capacity to contract an international treaty!. DPW wangesainiana tuu na TPA na kumalizana juu kwa juu!.
P
 
Wanaendelea kupotosha kwamba mkataba huu hauna ukumo, sio kweli! Mkataba huu una ukomo; ibara ya 23 ibara ndogo ya 1 inasema wazi ukomo wa mkataba huu; itakapotokea moja katika haya mambo mawili, kule kwenye mradi wa utekelezaji (ambao haujaanza) mradi ukaisha basi na mkataba huu utakuwa umefika mwisho lakini ikitokea ile mikataba mingine miwili ikisainiwa (HGA na mkataba wa mradi) na utekelezaji wake umeisha basi mkataba huu utakuwa umefika ukomo.
View attachment 2697503
Kamba 2 Kamba 😀
 
Back
Top Bottom