Tunawakosesha fursa wazawa kwa kuwekeza nguvu kwenye timu mbili za Kariakoo tu.

Tunawakosesha fursa wazawa kwa kuwekeza nguvu kwenye timu mbili za Kariakoo tu.

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Tangu nimsikie Mbwana Samatta katika jukwaa la kimataifa sijamsikia tena mzawa mwingine Mtanzania akiwa maarufu hapa Africa au duniani kwa ujumla katika sekta ya michezo.

Huenda sababu mojawapo kubwa ni serikali na raia kuelekeza nguvu zao na focus yao yote katika vilabu viwili zaidi vya Kariakoo vya Simba na Yanga. Sasa ukiangalia kwa sasa wanaowika zaidi katika hivi vilabu kwa sasa karibia wote ni wageni kutoka nje. Wazawa wamepoteana kabisa wamebaki kuwa wasindikizaji tu.

Tanzania ni kubwa sana, haiawezekani watu wote wenye vipaji wakapata nafasi ya kucheza katika vilabu viwili vya Kariakoo vya Simba na Yanga. Ni vyema serikali na wadau wakahakikisha angalau kila kanda inakuwa na timu imara za michezo au kutoa kipaumbele kwa michezo mingine kama riadha, rugby, tennis, golf n.k kama nchi nyingine majirani zetu walivyofanya na kuwapa wazawa wa nchi zao fursa kubwa zaidi ya michezo.
 
Wabongo tunapenda sana ubinafsi hadi kwenye vitu ambavyo viko nje ya uwezo wetu. Ukitaka soka likue hiyo lazima litokee kwa sababu utahitaji vipaji zaidi na sio upendeleo ndio mana wageni lazima waje na wachukue tuzo. Angalia ligi za wenzetu zilizoendele mfano laliga Messi na Ronaldo wametawala sana pale na sio raia wa spain ukija Epl kwa hivi karibuni KDB, Halland, Salah hao wote sio raia wa Uk. Kwa iyo acha mboyoyo zako wazawa wanatakiwa wajitume ili kushindana na wageni.
 
Wakati Samatta anacheza pale Simba hakukuwa na wageni kama Emmanuel Okwi, Patrick Ochan, na wengineo? Ikawaje Mbwana Samatta akaonekana? Hawa akina Mzize na Kibu wao wamekatazwa kuonekana?

Kikubwa hawa Wachezaji Mazwazwa Wazawa wakalishwe chini wapewe makavu labda watabadilika. Mojawapo ni;wajitume waache kuendekeza Uchawi.
 
Wabongo tunapenda sana ubinafsi hadi kwenye vitu ambavyo viko nje ya uwezo wetu. Ukitaka soka likue hiyo lazima litokee kwa sababu utahitaji vipaji zaidi na sio upendeleo ndio mana wageni lazima waje na wachukue tuzo. Angalia ligi za wenzetu zilizoendele mfano laliga Messi na Ronaldo wametawala sana pale na sio raia wa spain ukija Epl kwa hivi karibuni KDB, Halland, Salah hao wote sio raia wa Uk. Kwa iyo acha mboyoyo zako wazawa wanatakiwa wajitume ili kushindana na wageni.
Kwanza siongelei wachezaji wa mpira tu, naongelea wanamichezo wote kwa ujumla, pia Hispania imekuwa na wanamichezo wengi maarufu kimataifa kabla, wakati wa enzi za Messi na Ronaldo na hata baada ya wao kuondoka. Uingereza ina wananamichezo maarufu wa kimataifa wazawa wengi sana pia, kuwataja hapa huu uzi hautatosha.
 
Wakati Samatta anacheza pale Simba hakukuwa na wageni kama Emmanuel Okwi, Patrick Ochan, na wengineo? Ikawaje Mbwana Samatta akaonekana? Hawa akina Mzize na Kibu wao wamekatazwa kuonekana?

Kikubwa hawa Wachezaji Mazwazwa Wazawa wakalishwe chini wapewe makavu labda watabadilika. Mojawapo ni;wajitume waache kuendekeza Uchawi.
Huwezi kuwa na kina wazawa kama kina Samatta wengi kama una timu mbili tu kubwa zinazogombaniwa na kila mtu, halafu nafasi inakuwa finyu zaidi kama kuna wageni wanaoongeza ushindani kwa kuchukua hata hizo nafasi chache.
 
Back
Top Bottom