Tunawashukuru sana Marekani kwa kukikata meno kikosi cha Wasiojulikana!

Tunawashukuru sana Marekani kwa kukikata meno kikosi cha Wasiojulikana!

Mleta mada anajenga hoja kama vile Marekani ndio kila kitu, wakati wamefanya uchafu mwingine tangu miaka ya 1960 hata kabla ya hapo.

Tafuta sababu hasa ya Kennedy kuuawa 1963 na mauaji mengine mengi tu ya kinyama yaliyofanywa kwa ruhusa ya CIA.
Sawa lakini kwa hili LA kuwapiga pin wasiojulikana tunawapongeza
 
Hamna tunae mtetea zaidi ya kumpongeza Mh.POMPEO kwa Upendo wake kwetu tusio na vyombo vya moto,madaraka wala mtetezi.
GOD BLESS HON.POMPEO
Basi sie tuna bahati maana wenzetu weusi huko marekani hawajapata upendo huo wa Pompeo dhidi ya wanaojulikana(polisi wazungu) tusiwe wachoyo tuwaombee na wenzetu ili Pompeo aweze kuwaonesha upendo kama alionesha kwetu maana hali si shwari.
 
Mleta mada anajenga hoja kama vile Marekani ndio kila kitu, wakati wamefanya uchafu mwingine tangu miaka ya 1960 hata kabla ya hapo.

Tafuta sababu hasa ya Kennedy kuuawa 1963 na mauaji mengine mengi tu ya kinyama yaliyofanywa kwa ruhusa ya CIA.
Marekani alikuwa anafanya jambo jema kwa ustaarabu wa dunia, alikuwa anapambana na ucomunist mfumo wa kilaghai na kitapeli hatimaye miaka ya mwanzo ya 90 alishinda, miaka ya 2000 amepambana na ugaidi,
Miaka hii anapambana na viserekall uchwara vya kidikteta
 
Basi sie tuna bahati maana wenzetu weusi huko marekani hawajapata upendo huo wa Pompeo dhidi ya wanaojulikana(polisi wazungu) tusiwe wachoyo tuwaombee na wenzetu ili Pompeo aweze kuwaonesha upendo kama alionesha kwetu maana hali si shwari.
Lakini tusitumie hao weusi kuwakandamiza,kuwapoteza au kuwateka wabongo wenzetu ingawa sikuwai kusikia mtanzania ananyanyaswa huko Marekani.AHSANTE SANA MH.POMPEO
 
Jambo moja ambalo linanisikitisha sana ni kwamba viongozi wakuu wastaafu walielewa nini kilikuwa kinatokea, lakini waliamua kukaaa kimya wakiona kila tunda na msimu wake. Huo ulikuwa ni usaliti mkubwa sana kwa Watanzania, na wao pia wanastahili kila aina ya lawama. Walikuwa na uwezo wa kukutana pamoja na kuamuru jambo hili likomeshwe mara moja.

Lakini pia, watu kama Membe, ambaye amesema wazi kwamba ana source zake zinamjulisha kila kitu, ni wazi sana walijua kinachoendelea. Je hawakuwa na uwezo wa kuingilia kati, hata kama ni kwa njia ya ki-covert? Labda juu ya Membe tusiseme mengi, lakini yeyote atakaepata fursa kuongea na Membe amuulize hili suala - je, hukujua kilichokuwa kinaendelea, na kama ulijua ulifanya nini?
 
Mleta mada anajenga hoja kama vile Marekani ndio kila kitu, wakati wamefanya uchafu mwingine tangu miaka ya 1960 hata kabla ya hapo.Tafuta sababu hasa ya Kennedy kuuawa 1963 na mauaji mengine mengi tu ya kinyama yaliyofanywa kwa ruhusa ya CIA.
Hakuna sehemu nimesema Marekani ni msafi, usinilishe maneno. Ongelea nilichoandika sio kile unachohisi nafikiria.
 
Mauaji yapo dunia nzima na sababu hutofautiana kati ya nchi moja na nyingine.Wanaoishi ni binadamu wenye udhaifu wa kibinadamu.
Kwa hiyo sio tatizo kuwa na kikosi cha mauaji cha Wasiojulikana nchini? Mbaya zaidi kikosi ambacho kina target wapinzani na wakosoaji wa kisiasa kwa serikali?

Hata kama kikosi cha Wasiojulikana kingekuwa kina target majambazi na majangiri bado kingekuwa ni cha kishetani na waote wanaohusika wanapasa kukamatwa na kuchukuliwa hatua. Hizo zilikuwa ni extrajudicial killings, period.
 
Marekani alikuwa anafanya jambo jema kwa ustaarabu wa dunia, alikuwa anapambana na ucomunist mfumo wa kilaghai na kitapeli hatimaye miaka ya mwanzo ya 90 alishinda, miaka ya 2000 amepambana na ugaidi,
Miaka hii anapambana na viserekall uchwara vya kidikteta
Humo humo katika mifumo ya upashanaji wa habari ndipo Marekani anapowapata watu wa kuwaongopea juu ya umalaika wake.
Marekani hawezi kukwambia kwamba Osama Bin Laden alifundishwa huo ugaidi na taifa lake mwenyewe, Osama alipowageuka ndipo wakatengeneza mazingira kutumia media yake ii kumdanganya mliberali kwamba yeye ni malaika mwema kabisa.

Marekani kamuua Gaddaffi, Obama alikiri kuhusika kwa unyama huo. Yeye Obama na familia yake wanapomzika kivulini wakila maisha wakati raia wa Libya wanauana kama wanyama.
 
Usipotoshe watu
Marekani walijua kabisa kwamba kulikuwa na kikosi kilichobatizwa jina la "Wasiojulikana" hapa nchini, kikosi ambacho kilijikita katika kuteka watu na hata kuua. Na Marekani waliona wazi kwamba wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani pamoja na waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla walioikosoa serikali. Pia kulikuwa na wafanya biashara wakubwa ambao walionekana kutenda kinyume na matakwa ya serikali,

Na jambo jingine Marekani waliloona wazi ni kwamba siku zote Polisi hawakuonyesha nia ya dhati ya kushughulikia na kupepeleza kesi au matukio yaliyofanywa na hiki kikosi cha Wasiojulikana. Mara nyingone Polisi walitoa matamko ya kuwalaghai na kuwapoteza lengo wananchi pale ilipohusu matukio ya Wasiojulikana.

Ndipo Marekani wakaamua kuingilia na kuwaokoa watanzania walioendelea kuwa wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana. Wakatuma ujumbe. Wakatoa onyo.

Tunawashukuru sana Marekani kwa jambo hili. Ni wazi kuingilia kwenu kumeokoa maisha ya Watanzania wengi na kutoa ahueni kubwa. Tunajua watu wegi walikuwa kwenye "hit list" ya hiki kikosi cha Wasiojulikana na kama sio kuingilia kwenu wengi wangeumizwa au kutoweshwa. Lakini bado tunaomba mwende mbali zaidi na kufunua wazi nani waliohusika na kikosi cha Wasiojulikana, na kiliundwa kwa amri ya nani. Damu za waliopota zinatulilia tuwafanyie hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo sio tatizo kuwa na kikosi cha mauaji cha Wasiojulikana nchini? Mbaya zaidi kikosi ambacho kina target wapinzani na wakosoaji wa kisiasa kwa serikali?

Hata kama kikosi cha Wasiojulikana kingekuwa kina target majambazi na majangiri bado kingekuwa ni cha kishetani na waote wanaohusika wanapasa kukamatwa na kuchukuliwa hatua. Hizo zilikuwa ni extrajudicial killings, period.
Wasiojulikana wamekuwepo nchini tangu enzi za Nyerere, wakati huo JPM alikuwa mwanafunzi wa sekondari.

Wasiojulikana wa hatari zaidi walikuwepo enzi za Idd Amin kule Uganda, kulikuwa na mtu anaitwa Maliyamungu aifanya unyama kuliko huu wa hapa TZ.

Wasiojulikana mwalimu wao ni CIA ya Marekani, wameteka watu na kuua kila kona ya dunia. Bora hawa wasiojulikana kuliko Trump na marais wa Marekani wanaoua watu na kujisifu bila ya kuogopa mtu yoyote yule.
 
Lakini tusitumie hao weusi kuwakandamiza,kuwapoteza au kuwateka wabongo wenzetu ingawa sikuwai kusikia mtanzania ananyanyaswa huko Marekani.AHSANTE SANA MH.POMPEO
Kutokusikia mbongo kunyanyaswa huko marekani ni sawa na huku bongo kutosikia wazungu kunyanyaswa,ila muhimu mkuu ni kuwaombea tu ili Pompeo aweze kuwaonesha upendo wa dhati kama alionao kwetu. Naamini kama Pompeo ameweza kutuona sisi huku wa mbali na akaona jinsi tunavyofanyiwa na akapatwa na huruma na kuamua kutusaidia kwa upendo basi ni wazi atawaona na wale wenzetu ambao wapo karibu yake.
 
Wasiojulikana wamekuwepo nchini tangu enzi za Nyerere, wakati huo JPM alikuwa mwanafunzi wa sekondari.

Wasiojulikana wa hatari zaidi walikuwepo enzi za Idd Amin kule Uganda, kulikuwa na mtu anaitwa Maliyamungu aifanya unyama kuliko huu wa hapa TZ.

Wasiojulikana mwalimu wao ni CIA ya Marekani, wameteka watu na kuua kila kona ya dunia. Bora hawa wasiojulikana kuliko Trump na marais wa Marekani wanaoua watu na kujisifu bila ya kuogopa mtu yoyote yule.
Mkuu, are you for real? Tutajie viongozi wa upinzani na waandishi wa habari waliotekwa au kuuwawa na Wasiojulikana unaosema walikuwapo enzi za viongozi wengine hapa Tanzania
 
Mkuu, are you for real? Tutajie viongozi wa upinzani na waandishi wa habari waliotekwa au kuuwawa na Wasiojulikana unaosema walikuwapo enzi za viongozi wengine hapa Tanzania
Enzi za Nyerere kulikuwa na upinzani unaojulikana kikatiba?. Walikuwepo wanasiasa walioteswa, kumbuka magazeti yalikuwa ni ya serikali, hakukuwa na free media kama leo hii.

Kina Ulimboka waliofanyiwa ukatili ilikuwa ni awamu ya JPM?.

Kombe aliyepigwa risasi licha ya kunyoosha mikono kusalimu amri ya kukamatwa, ilikuwa ni awamu ya JPM?.

Kambona aliyelazimika kuishi uhamishoni Uingereza, ilikuwa ni awamu ya tano?.
 
Enzi za Nyerere kulikuwa na upinzani unaojulikana kikatiba?. Walikuwepo wanasiasa walioteswa, kumbuka magazeti yalikuwa ni ya serikali, hakukuwa na free media kama leo hii.

Kina Ulimboka waliofanyiwa ukatili ilikuwa ni awamu ya JPM?.

Kombe aliyepigwa risasi licha ya kunyoosha mikono kusalimu amri ya kukamatwa, ilikuwa ni awamu ya JPM?.

Kambona aliyelazimika kuishi uhamishoni Uingereza, ilikuwa ni awamu ya tano?.
Hivi akina Ulimboka ni wangapi? Hivi kuwepo kwa hivyo vitendo awamu hizo ni kuhalalisha ata awamu hii hivyo vitendo viwepo?
 
Jambo moja ambalo linanisikitisha sana ni kwamba viongozi wakuu wastaafu walielewa nini kilikuwa kinatokea, lakini waliamua kukaaa kimya wakiona kila tunda na msimu wake. Huo ulikuwa ni usaliti mkubwa sana kwa Watanzania, na wao pia wanastahili kila aina ya lawama. Walikuwa na uwezo wa kukutana pamoja na kuamuru jambo hili likomeshwe mara moja.

Lakini pia, watu kama Membe, ambaye amesema wazi kwamba ana source zake zinamjulisha kila kitu, ni wazi sana walijua kinachoendelea. Je hawakuwa na uwezo wa kuingilia kati, hata kama ni kwa njia ya ki-covert? Labda juu ya Membe tusiseme mengi, lakini yeyote atakaepata fursa kuongea na Membe amuulize hili suala - je, hukujua kilichokuwa kinaendelea, na kama ulijua ulifanya nini?
Ngoja niwataje ambao wanasubiri hukumu ya Umma
Kikwete
Mkapa
Makonda
Mwamunyange
Warioba
Malecela
Kawambwa
Augustine
Mrema
 
Back
Top Bottom