Tunda gani la asili umelikumbuka na halipatikani ulipo kwa sasa?

Tunda gani la asili umelikumbuka na halipatikani ulipo kwa sasa?

Kuna matunda ya asili mengine yanapatikana kwenye maeneo fulani tu, unakuta umekua ukiyala na baada ya kuondoka hapo kwenda sehemu nyingine huyaoni tena.

Leo nimekaa nimeyakumbuka matunda ya kwetu yanaitwa ndati, sema siwezi yapata hadi nirudi kwetu, ila ili kupoza moyo nitaenda sokoni kutafuta mengine ambayo nilikuwa nakula utotoni yanaitwa ntalali au sungwi kama wengi wanavyoyaita maana huku nilipo yanapatikana.

Kwa bahati mbaya picha ya ndati sina ningewaonesha.

View attachment 2790027
Picha ya sungwi au ntalali kwa msaada wa mtandao
Furu na nduwau
 
Kuna matunda ya asili mengine yanapatikana kwenye maeneo fulani tu, unakuta umekua ukiyala na baada ya kuondoka hapo kwenda sehemu nyingine huyaoni tena.

Leo nimekaa nimeyakumbuka matunda ya kwetu yanaitwa ndati, sema siwezi yapata hadi nirudi kwetu, ila ili kupoza moyo nitaenda sokoni kutafuta mengine ambayo nilikuwa nakula utotoni yanaitwa ntalali au sungwi kama wengi wanavyoyaita maana huku nilipo yanapatikana.

Kwa bahati mbaya picha ya ndati sina ningewaonesha.

View attachment 2790027
Picha ya sungwi au ntalali kwa msaada wa mtandao
1698049671928.png

Kwetu kule tunayaita MASUKU, lakini kwa watani zangu wa kujinyonga yanaitwa MAKUSU

 
Makende ya nyau siyaoni kabisa siku hizi

Mazingafuli nayo yamepotea sana
 
Maviru, Sambia na mafyoksi haya matumda nime ya miss sana yapo huko milimani kwa wasambaa, ( mafyoksi nadhani ndio cherry ila sina uhakika)
 
NDILOLO hili tunda sijaona sehemu nyingine zaidi ya kyela na hilo jina lake sidhani kama na kiswahili linatamkwa hivyo.Kuna mtu aliwahi kuniambia ni mzaituni kwa kiswahili lkn nikagundua sio kweli, lingine ni KOKOA japo yapo morogoro ila ni adimu sana sehemu nyingine.
 
Back
Top Bottom