Tunda gani la asili umelikumbuka na halipatikani ulipo kwa sasa?

Tunda gani la asili umelikumbuka na halipatikani ulipo kwa sasa?

Kuna matunda ya asili mengine yanapatikana kwenye maeneo fulani tu, unakuta umekua ukiyala na baada ya kuondoka hapo kwenda sehemu nyingine huyaoni tena.

Leo nimekaa nimeyakumbuka matunda ya kwetu yanaitwa ndati, sema siwezi yapata hadi nirudi kwetu, ila ili kupoza moyo nitaenda sokoni kutafuta mengine ambayo nilikuwa nakula utotoni yanaitwa ntalali au sungwi kama wengi wanavyoyaita maana huku nilipo yanapatikana.

Kwa bahati mbaya picha ya ndati sina ningewaonesha.

View attachment 2790027
Picha ya sungwi au ntalali kwa msaada wa mtandao
Unatoka unyamwezini nini?. Jina la ntalali linatumika sana Tabora na nsungwi ni Usukumani huko lkn hizo ndati Tabora manispaa zipo nyingi vibaya mno vitunda vidogo vidogo hivi ukubwa wa karanga na Nadhani Tabora ndio sehemu pekee ambapo kila aina ya tunda utalikuta.
 
View attachment 2790098
Kwetu kule tunayaita MASUKU, lakini kwa watani zangu wa kujinyonga yanaitwa MAKUSU

Ni mengi mm yalinishinda kula Yani yametapakaa chini nilivosogea Njombe mjini nikakuta yanauzwa nikatamni ningebeba kiroba😂😂😂
 
Piches and suse, zilikuwa zinapatikana sana Moshi Marangu huko
 
Ule ukwaju ulikua unaota kwenye michongoma ndani una vitunda vyeusi... Maeneo ya msasani na mikocheni yalikua mengi sana miaka ya 90 mpaka 2000...View attachment 2790121
haya mikoa mingi yapo, shinyanga wanayaita matunda kunigwa, dar yanaitwa matunda mifensi pia nimeyaona mwaka jana chunya mbeya, haya ayajapotea, hapa kuna matunda yamepotea kabisa sikuizi ndio yanatakiwa kupata hata mbegu kuotesha kwani ni matunda asili
 
Kuna tunda wakazi wa kanda ya ziwa victoria wanaita limbe, kama bado yanapatikana tufahamishane nije ninunue hata mbagu maana sijui kama yana jina jingine niyatafute maana ilo jina hata mtandaoni sipati picha
 
Back
Top Bottom