Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aanza kuwaletea maendeleo na haki Watanzania hata kabla ya Uchaguzi

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aanza kuwaletea maendeleo na haki Watanzania hata kabla ya Uchaguzi

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka, kazi ni msingi wa maisha. Akunyimaye kazi amekupa adhabu ya kifo.

Serikali ya awamu ya 5 imefanya jitihada kubwa sana ya kuwanyima kazi Watanzania. Yaani imefanya jitihada kubwa ya kuwapa Watanzania adhabu ya kifo

Awamu ya 5 iliwaondoa maelfu ya wafanyakazi kwa kisingizio cha vyeti fake licha ya Watanzania hao, walio wengi wakiwa na vyeti halisia vya umahiri wa weledi wao kwenye ngazi za juu za elimu zao. Wengi waliondolewa kwa kukosa vyeti halali vya kidato cha 4 wakati ukweli ni kuwa miaka hiyo nyuma fursa za elimu zilikuwa finyu sana kama hukuchaguliwa kuingia shule za serikali hata kama ulikuwa umefaulu vizuri masomo yako.

Kuna madaktari na manesi wengi ambao wameokoa maisha ya maelfu ya Watanzania, waliondolewa na kufukuzwa kama mbwa koko bila hata ya kulipwa mafao yao. Kuna walimu, wahasibu, n.k. Hawa wote walipewa adhabu ya kifo na utawala wa awamu ya 5, kwa tafsiri ya Baba wa Taifa.

Utawala wa Rais Magufuli uliua biashara na uwekezaji kwenye sekta karibu zote. Maelfu ya Watanzania wakakosa kazi. Hao nao, kwa tafsiri ya Mwalimu, utawala wa awamu ya 5 aliwapa adhabu ya kifo.

Rais Magufuli aliamuru kuvunjwa maelfu ya nyumba ambazo Watanzania walikuwa wakiendesha biashara mbalimbali kwenye nyumba hizo, tena nyumba zilizokuwa na hati, na kukiwa na zuio la mahakama. Hawa nao, kwa tafsiri ya Baba wa Taifa, Rais Magufuli aliwapa adhabu ya kifo.

Kutokana na uwekezaji kudondoka toka ukuaji wa 28% mpaka 4%, maelfu ya wahitimu wa vyuo walikosa kazi. Hawa nao wamepewa adhabu ya kifo, kwa tafsiri ya Baba wa Taifa.

TUNDU LISU AWAOKOA WATANZANIA KUTOKA ADHABU YA KIFO
Kutokana na Tundu Lisu kurejea nchini, na kugombea nafasi ya Urais kupitia CHADEMA, amekuwa akiibua wazi udhaifu wa utawala wa awamu ya tano, hasa kuhusu kupuuza haki za raia, uhuru na maendeleo ya watu.

Kampeni zikiwa zinaendelea, Serikali ya awamu ya 5, imetangaza ajira 13,000 za walimu. Bila Lisu, nina hakika kwa 100%, serikali ya awamu ya 5 isingetangaza hizi ajira. Watakaoajiriwa, wautambue kwa namna ya pekee mchango wa Lisu na upinzani katika ustawi wa Taifa, ustawi wao binafsi na familia zao.

Kwa zaidi ya miaka 3, wakulima wa pamba, walinyimwa malipo yao. Baada ya Tundu Lisu kueleza wazi kuwa Serikali inawaonea na kuwaibia wakulima wa pamba kwa kutowalipa fedha za mauzo ya pamba yao, Serikali ya awamu ya 5 imetangaza kuwa itaanza kuwalipa madeni wakulima wa pamba. Wakulima hawa, bila Tundu Lisu, walikuwa wamepuuzwa na kusahaulika na Serikali ya awamu ya 5.

Sijui mpaka Kampeni kwisha, ni wananchi wangapi watafaidila kwa ujio wa Tundu Lisu.

Watanzania tuuenzi na kuulinda upinzani. Bila upinzani, ukiwa na uongozi kama huu wa awamu ya 5, tutajuta. Titakamatwa na kurundikwa magerezani, tutauawa hovyo, tutatekwa ovyo, tutapotezwa ovyo, tutaonewa hovyo, tutanyimwa uhuru na haki zetu hovyo, tutapuuzwa na kudhalilishwa utu wetu na hawa viongozi miunguwatu kwa namna isiyoelezeka.

Nina imani mpaka kwisha kwa kampeni, Watanzania wengi watanufaka na Tundu Lissu kugombea nafasi ya Urais. Watanzania tuupe nguvu kubwa upinzani, ili wanaoshika madaraka watutendee haki.
 
Ni mipango ndani ya miaka 5.. Mh. Magufuli bado ni Rais ambaye Serikali yake bado ipo kazini.

Lolote lifanywalo ni kutimiza ahadi na kujali wananchi kimaisha na kiuchumi.

Yajayo yanafurahisha, hadi mbili nane mtaomba pooo.. na kulala tu.. mukikodoa macho.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka, kazi ni msingi wa maisha. Akunyimaye kazi amekupa adhabu ya kifo.

Serikali ya awamu ya 5 imefanya jitihada kubwa sana ya kuwanyima kazi Watanzania. Yaani imefanya jitihada kubwa ya kuwapa Watanzania adhabu ya kifo....
Kuhusu ajira. Ulikuwa ni mpango wa serikali kitambo tangu July.
 
Kuna watu wanatamani upinzani ufe,ila hawa ni walioshiba na kubweteka ambao kwao maisha yanaishia kwenye matumbo yao tu!
Walimu 13000 mtakaopata ajira nitawashangaa kama nanyi mtakuwa na mawazo kama hayo kuwa upinzani ufe wakati bila upinzani imara unaotishia kushika dola,hizo ajira mngezisikia kwenye bomba!Mtu mawazo yake ni kuongeza ndege,sasa imekuwa dharura tu kutokana na kukabwa koo akaone apunguze kidogo kwa kuachia ajira!
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka, kazi ni msingi wa maisha. Akunyimaye kazi amekupa adhabu ya kifo.

Serikali ya awamu ya 5 imefanya jitihada kubwa sana ya kuwanyima kazi Watanzania. Yaani imefanya jitihada kubwa ya kuwapa Watanzania adhabu ya kifo...
Huyo mwalimu nyerere anatawala kutokea kaburini ,siku hizi ishu za nyerere nani anazitaka
 
Safi sana Rais Tundu Lissu kwa kuendesha nchi kwa muda wa mwezi mmoja tu. Hakika Ww ndo unastahili kua Rais maana unajua vipaumbele vya Watanzania.
 
Hata hizo ajira bado Nina mashaka nazo.

Mtu mwenye 'nia'' nzuri na watanzania huwezi kutoa ajira kipindi Cha kampeni.

Serikali ya Jiwe iache kumanipulate Hawa watoto wa masikini wenzetu waliosoma ualimu.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka, kazi ni msingi wa maisha. Akunyimaye kazi amekupa adhabu ya kifo.

Serikali ya awamu ya 5 imefanya jitihada kubwa sana ya kuwanyima kazi Watanzania. Yaani imefanya jitihada kubwa ya kuwapa Watanzania adhabu ya kifo...
Asante lissu. Sisi tuliokuwa tumetia nia kugombea ubunge majimboni kupitia vyama mbalimbali tulishafukuzwa makazini kwa kulazimishwa kuandika barua ya kuomba likizo bila malipo na kwamba kurudi kwetu kazini kulitegemea huruma ya mwajiri kama atakuwa bado anatuhitaji. Hii ilikuwa kabla lissu hajaanza kampeni zake.

Mungu si athumani lissu kaanza kampeni na mwitikio wa watu ukawa ni mkubwa sana. Hotuba yake lissu ya kanda ya ziwa kwamba serikali yake haitawanyanyasa wafanyakazi kwani wana haki ya kuchagua na kuchaguliwa ikamshitua magu na kuagiza turudishwe kazini. Na sasa tumerudi kazini. Kwa kweli kipindi changu hiki cha utumishi kilichobaki kabla ya kustaafu nakiita ni cha "asante lissu".
 
Lissu tutakuenzi daima Tanzania haitakusahau bila wewe wanyonge tungekuwa wapi!!
 
Ni mipango ndani ya miaka 5.. Mh. Magufuli bado ni Rais ambaye Serikali yake bado ipo kazini.

Lolote lifanywalo ni kutimiza ahadi na kujali wananchi kimaisha na kiuchumi.

Yajayo yanafurahisha, hadi mbili nane mtaomba pooo.. na kulala tu.. mukikodoa macho.
Huoni aibu kuandika huu utopolo .?
 
Asante lissu. Sisi tuliokuwa tumetia nia kugombea ubunge majimboni kupitia vyama mbalimbali tulishafukuzwa makazini kwa kulazimishwa kuandika barua ya kuomba likizo bila malipo na kwamba kurudi kwetu kazini kulitegemea huruma ya mwajiri kama atakuwa bado anatuhitaji. Hii ilikuwa kabla lissu hajaanza kampeni zake.

Mungu si athumani lissu kaanza kampeni na mwitikio wa watu ukawa ni mkubwa sana. Hotuba yake lissu ya kanda ya ziwa kwamba serikali yake haitawanyanyasa wafanyakazi kwani wana haki ya kuchagua na kuchaguliwa ikamshitua magu na kuagiza turudishwe kazini. Na sasa tumerudi kazini. Kwa kweli kipindi changu hiki cha utumishi kilichobaki kabla ya kustaafu nakiita ni cha "asante lissu".

Malipo yako ni kuwapigia kampeni wapinzani, maana bila hivyo, jiwe akipita tena anaweza watenda tena, huyo jamaa hana utu kabisa, ni ibilisi mwenye madaraka.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka, kazi ni msingi wa maisha. Akunyimaye kazi amekupa adhabu ya kifo.

Serikali ya awamu ya 5 imefanya jitihada kubwa sana ya kuwanyima kazi Watanzania. Yaani imefanya jitihada kubwa ya kuwapa Watanzania adhabu ya kifo.

Awamu ya 5 iliwaondoa maelfu ya wafanyakazi kwa kisingizio cha vyeti fake licha ya Watanzania hao, walio wengi wakiwa na vyeti halisia vya umahiri wa weledi wao kwenye ngazi za juu za elimu zao. Wengi waliondolewa kwa kukosa vyeti halali vya kidato cha 4 wakati ukweli ni kuwa miaka hiyo nyuma fursa za elimu zilikuwa finyu sana kama hukuchaguliwa kuingia shule za serikali hata kama ulikuwa umefaulu vizuri masomo yako.

Kuna madaktari na manesi wengi ambao wameokoa maisha ya maelfu ya Watanzania, waliondolewa na kufukuzwa kama mbwa koko bila hata ya kulipwa mafao yao. Kuna walimu, wahasibu, n.k. Hawa wote walipewa adhabu ya kifo na utawala wa awamu ya 5, kwa tafsiri ya Baba wa Taifa.

Utawala wa Rais Magufuli uliua biashara na uwekezaji kwenye sekta karibu zote. Maelfu ya Watanzania wakakosa kazi. Hao nao, kwa tafsiri ya Mwalimu, utawala wa awamu ya 5 aliwapa adhabu ya kifo.

Rais Magufuli aliamuru kuvunjwa maelfu ya nyumba ambazo Watanzania walikuwa wakiendesha biashara mbalimbali kwenye nyumba hizo, tena nyumba zilizokuwa na hati, na kukiwa na zuio la mahakama. Hawa nao, kwa tafsiri ya Baba wa Taifa, Rais Magufuli aliwapa adhabu ya kifo.

Kutokana na uwekezaji kudondoka toka ukuaji wa 28% mpaka 4%, maelfu ya wahitimu wa vyuo walikosa kazi. Hawa nao wamepewa adhabu ya kifo, kwa tafsiri ya Baba wa Taifa.

TUNDU LISU AWAOKOA WATANZANIA KUTOKA ADHABU YA KIFO
Kutokana na Tundu Lisu kurejea nchini, na kugombea nafasi ya Urais kupitia CHADEMA, amekuwa akiibua wazi udhaifu wa utawala wa awamu ya tano, hasa kuhusu kupuuza haki za raia, uhuru na maendeleo ya watu.

Kampeni zikiwa zinaendelea, Serikali ya awamu ya 5, imetangaza ajira 13,000 za walimu. Bila Lisu, nina hakika kwa 100%, serikali ya awamu ya 5 isingetangaza hizi ajira. Watakaoajiriwa, wautambue kwa namna ya pekee mchango wa Lisu na upinzani katika ustawi wa Taifa, ustawi wao binafsi na familia zao.

Kwa zaidi ya miaka 3, wakulima wa pamba, walinyimwa malipo yao. Baada ya Tundu Lisu kueleza wazi kuwa Serikali inawaonea na kuwaibia wakulima wa pamba kwa kutowalipa fedha za mauzo ya pamba yao, Serikali ya awamu ya 5 imetangaza kuwa itaanza kuwalipa madeni wakulima wa pamba. Wakulima hawa, bila Tundu Lisu, walikuwa wamepuuzwa na kusahaulika na Serikali ya awamu ya 5.

Sijui mpaka Kampeni kwisha, ni wananchi wangapi watafaidila kwa ujio wa Tundu Lisu.

Watanzania tuuenzi na kuulinda upinzani. Bila upinzani, ukiwa na uongozi kama huu wa awamu ya 5, tutajuta. Titakamatwa na kurundikwa magerezani, tutauawa hovyo, tutatekwa ovyo, tutapotezwa ovyo, tutaonewa hovyo, tutanyimwa uhuru na haki zetu hovyo, tutapuuzwa na kudhalilishwa utu wetu na hawa viongozi miunguwatu kwa namna isiyoelezeka.

Nina imani mpaka kwisha kwa kampeni, Watanzania wengi watanufaka na Tundu Lissu kugombea nafasi ya Urais. Watanzania tuupe nguvu kubwa upinzani, ili wanaoshika madaraka watutendee haki.
AMEN
1599559347132.png
 
Back
Top Bottom