Tundu Lissu aendelea kushambuliwa mitaani kwa kauli zake za kibaguzi na chuki

Tundu Lissu aendelea kushambuliwa mitaani kwa kauli zake za kibaguzi na chuki

Hana hoja zaidi ya kujipofusha akili yake.
kama hana hoja kipi kinakuumiza mpk muanzise mashambuliz ? Ccmu ni jamii ya watu wajinga sana , nashukuru nlistuka mapema maana wapo watu wanazeeka na ujinga wa ccmu
 
watu weusi sijui nan kawaloga , nyinyi ndo lile kundi serikali inawalipa ili kupindisha madai ya watu huku mitandaoni , siez dharau utanganyika wangu kisa hongo ya buku 2 , muda ukifika utafuta post zenu hata wapigania uhuru waliitwa kila aina ya majina na waafrika wenzao ambao walikuwa wanatumikia matumbo yao kwa wakoloni , wewe ni mmoja wa wale wachumia tumbo

HOJA ZA LISSU ZIPO WAZI , JIBUNI HOJA ZAKE NA SIO KUMSHAMBULIA YEYE , KAMA HAMUEZ JIBU HOJA ZAKE INAMAANA NI ZA KWEL
Ninyi ni aina ya watu ambao bado mna mawazo ya kikoloni vichwani mwenu licha ya kuwa ukoloni ulishafutwa. Jina Tanzania ni fahari yetu,ni akili zetu na utashi wetu na siyo jina la kurithishwa na wakoloni. Kwanini mnataka kuturudisha kwenye fikira za kikoloni?
 
kama hana hoja kipi kinakuumiza mpk muanzise mashambuliz ? Ccmu ni jamii ya watu wajinga sana , nashukuru nlistuka mapema maana wapo watu wanazeeka na ujinga wa ccmu
Tunashambulia maneno yake yanayohamasisha na kuchochea ubaguzi na chuki kwa watu.
 
Hata akizungumza vipi bado hatapata uungwaji mkono kutoka kwa watanzania,maana hakuna mtanzania mzalendo aliyetayari kuona Taifa letu likipandikizwa chuki na ubaguzi kwa maslahi ya mtu mmoja na chama chake kwa uchu na uroho wao wa madaraka.ambayo wameshindwa kuyapata kwa njia za kushawishi watu kuwaunga mkono.
Sema hatopata uungwaji mkono toka CCM wasiojitambua na sio watanzania, unajipa cheo cha kunisemea. Kingine punguza kuandika migazeti, ni dalili kuwa uwezo wako wa akili mdogo.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kauli za kibaguzi ambazo zimetolewa na zimekuwa zikitolewa kupitia mdomo wa Lissu zimeendelea kulaaniwa na kukemewa sana na watanzania maeneo mbalimbali nchini. Ambapo watanzania wengi wameonyesha kuchukizwa na kauli za Lissu ambazo zinatokana na uchu na uroho wake wa madaraka.

Watanzania wanapinga na kukemea sana ubaguzi na chuki inayopandikizwa na Lissu ,ambapo hata hivyo watanzania wamekataa na kugoma kabisa kuingia katika mtego huo wa kutaka kuwagawa. ikumbukwe ya kuwa Lissu hana uchungu wa aina yoyote ile na Taifa letu pale litakapogawanyika na kupasuka vipande vipande au kutokea machafuko hapa nchini.

Hii ni kwa kuwa watoto wa Lissu wana Uraia wa Marekani ,kauli ambayo amewahi kuitoa na kukili kwa mdomo wake mwenyewe lissu .kwa mantiki hiyo mnaweza kutambua kwa nini Lissu hana habari wala uoga wala hofu wala aibu ya kupandikiza chuki na ubaguzi hapa nchini. Yeye hata yakitokea machafuko leo ,basi yeye kesho yake anapanda zake ndege na kwenda ulaya au Marekani kutulia na familia yake akiwa ameshika kinywaji mkononi mwake kupeleka mdomoni mwake, huku akiangalia kupitia Tvs namna watanzania wanavyohangaika na kuteseka,huku akina mama wakiwa na watoto migongoni na wengine wajawazito wakilia kwa uchungu pasipo msaada.

Mtakumbuka hata 2020 alipotaka watanzania waandamane halafu yeye akaenda kujificha ubalozini huku akiwa na tiketi ya ndege mkononi mwake kwa ajili ya kwenda ulaya kula upepo. Sasa hamjiulizi kwanini alikwenda kujificha ubalozini? Kama alikuwa anakiogopa kifo ,je alitaka mtoto wa nani ndio afe kwa ajili ya maslahi yake binafsi? Kwanini asingetoka hadharani aongoze maandamano kama walivyokuwa wakifanya akina Dkt Martin Luther King junior kule Marekani?

Kwanini alitaka awarubini watanzania wakati yeye tayari anayo tiketi ya ndege mfukoni na mipango ya kusindikizwa hadi uwanja wa ndege kupanda ndege kwenda ulaya? Uzalendo wake ulikuwa wapi? Alitaka nani aongoze hayo maandamano ikiwa muanzisha maandamano alikuwa msitari wa mbele kutimua mbio? Je siyo kwamba alikuwa anataka awalaghai watanzania na kusababisha machafuko hapa nchini kwa maslahi yake binafsi?

Sasa Lissu baada ya kuona watanzania wamekuwa wakimgomea kuandamana,ameamua kuanza kutumia njia nyingine ya kutaka kupandikiza mbegu ya ubaguzi,chuki,uhasama pamoja na kuleta nyufa na mpasuko kwa Taifa letu. Hii ni baada ya kuishiwa hoja ,sera na ajenda zenye kugusa maisha ya watu na kupata uungwaji mkono. lakini bado watanzania wamesimama kidete kupinga kauli zake za kibaguzi na zenye lengo la kujenga chuki na uhasama miongoni mwa watanzania.

Hayati Baba wa Taifa amewahi kutuasa na kutumbia kuwa kuna watu wakikosa hoja na sera za kuwashawishi watanzania kuwapigia kura ,huanza kutumia hoja za ubaguzi kwa misingi ya Udini au ukabila. Sasa ndio haya tunayo yaona kwa Lissu leo hii akitumia katika kutaka kupata uungwaji mkono kwa njia ya kuwagawa na kulisambaratisha Taifa letu ,baada ya kuwa amefirisika kisera.

Watanzania tumuogope na kuwaogopa kama ukoma watu aina ya Lissu wanaotaka kutugawa watanzania na kulisambaratisha na kulipasua Taifa letu kwa kauli za kibaguzi. Tumkemee na tuungane kumkataa Lissu na CHADEMA yake dhidi ya kauli zao chafu za kibaguzi. Tuwakatae kuanzia mitaani hadi katika sanduku la kura lolote lile watakaloweka wagombea wao.

Tuwaambie kuwa tunahitaji siasa safi,siasa za hoja,ajenda,sera na ushindani wa mbinu bora za kutatua kero zilizopo pamoja na kulipeleka mbele Taifa letu likiwa moja,lenye amani,upendo, utulivu na mshikamano. Kama siyo amani na utulivu huu uliotamalika hapa Nchini, hao akina Lissu wasingepata nafasi ya kutoa maneno yao hayo machafu ya kibaguzi.tuulinde Muungano wetu na Taifa letu na umoja wake. Lissu kama amechoka kuishi hapa nchini basi ni bora aondoke haraka sana Nchini na siyo kupandikiza chuki ambazo haziwezi kamwe mpatia hata kura moja tu kwenye sanduku la kura.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Wakati wa zile kauli za "Tuna raisi mshamba kuwahi kutokea"....."Magufuli ni Dikteta uchwara"...."Kama imewauma mkazikwe nae" Hawa wapinzani walikuwa heroes kwenu ila sahizi imeanza kula kwenu mmewageuka tena😂
 
Tunashambulia maneno yake yanayohamasisha na kuchochea ubaguzi na chuki kwa watu.
mnashambulia maneno ya ubaguz au mnatetea ubaguz wa Zanzibar kwa watanganyika ?kwamba mtanganyika hana haki Zenji hii kwenu sw ila si sw mtangany kuidai hii haki ? ni sw Samia kuuza Ngorongoro nyumban kwa wamasai hii ni sw kwenu ila si sw mtu kuwapigania wamasai kurudishwa kwenye ardhi mama ya Ngorongoro

Nina mashaka ccmu inakutumia vibaya , hizi sio zama za 1900s watu tumeelimika hatudanganywi tena , taarifa zote tunazipata hata mzuie media kuonyesha

CCMU NI MKOLONI MWEUSI , KEMEA CCMU NDO ADUI WA NCHI
 
Naunga mkono hoja zako.
kwamba ni sahihi mzenji kumiliki ardhi huku bara hata kuhodhi madaraka huku bara kuanzia ubalozi wa nyumba 10 ila sio sahihi mbara kumiliki ardhi kule zenji au hata kuwa mwenyekiti mtaani , JE KUKOSOA HILI NDO MTU AITWE MBAGUZI ?


KUNA MSTARI MWEMBAMBA KBS UNATENGENISHA UJINGA NA UCCMU
 
Ninyi ni aina ya watu ambao bado mna mawazo ya kikoloni vichwani mwenu licha ya kuwa ukoloni ulishafutwa. Jina Tanzania ni fahari yetu,ni akili zetu na utashi wetu na siyo jina la kurithishwa na wakoloni. Kwanini mnataka kuturudisha kwenye fikira za kikoloni?
Sifa ya nchi moja ni kila raia awe huru popote pale ndani ya nchi hiyo kwanini mtanganyika haez kwenda kumilik ardhi kule zenj ? kwann mkristo wa bara haez kwenda zenji na kujenga kanisa akaabudu ?

Ccmu mnamezeshwaga ujinga pale Lumumba , neno ukoloni sijui linaingiaje kwenye madai ya hapo juu ? kwamba sisi tunaotetea muungano wa kwel wakoloni ila nyiny mnalinda ukandamizwaj wa mtanganyika ndo wapenda haki ?

ENDELEA KUCHUMIA TUMBO MUDA SI MREFU MTALIPA KWA UBAYA WENU KWA WATANGANYIKA
 
mnashambulia maneno ya ubaguz au mnatetea ubaguz wa Zanzibar kwa watanganyika ?kwamba mtanganyika hana haki Zenji hii kwenu sw ila si sw mtangany kuidai hii haki ? ni sw Samia kuuza Ngorongoro nyumban kwa wamasai hii ni sw kwenu ila si sw mtu kuwapigania wamasai kurudishwa kwenye ardhi mama ya Ngorongoro

Nina mashaka ccmu inakutumia vibaya , hizi sio zama za 1900s watu tumeelimika hatudanganywi tena , taarifa zote tunazipata hata mzuie media kuonyesha

CCMU NI MKOLONI MWEUSI , KEMEA CCMU NDO ADUI WA NCHI
Weka ushahidi wa kuuzwa kwa Ngorongoro. Kwa hiyo ulitaka mazingira ya ngorongoro yaendelea kuharibiwa na idadi kubwa ya watu na mifugo iliyokuwa inakua kwa kasi kuliko wanyama ambao ndio kivutio cha utalii?
 
Sifa ya nchi moja ni kila raia awe huru popote pale ndani ya nchi hiyo kwanini mtanganyika haez kwenda kumilik ardhi kule zenj ? kwann mkristo wa bara haez kwenda zenji na kujenga kanisa akaabudu ?

Ccmu mnamezeshwaga ujinga pale Lumumba , neno ukoloni sijui linaingiaje kwenye madai ya hapo juu ? kwamba sisi tunaotetea muungano wa kwel wakoloni ila nyiny mnalinda ukandamizwaj wa mtanganyika ndo wapenda haki ?

ENDELEA KUCHUMIA TUMBO MUDA SI MREFU MTALIPA KWA UBAYA WENU KWA WATANGANYIKA
Kulilia Tanganyika Ni sawa na kuulilia ukoloni na matendo yake maovu ikiwepo ya kutugawa kwa kutucholea mistari ya mipaka wakiwa Ujerumani
 
Jitahidi uwe unaandika mambo kwa mtiririko mzuri wa mawazo na kimantiki , Unaandika mambo mengi Sana with zero evidence .
 
Jitahidi uwe unaandika mambo kwa mtiririko mzuri wa mawazo na kimantiki , Unaandika mambo mengi Sana with zero evidence .
Unahitaji ushahidi gani juu ya kauli za kibaguzi na chuki zinazotolewa katika mdomo wa Lissu? Kwamba wewe huzisikii au hujazisikia?
 
Back
Top Bottom