Hoja zake zina mashiko.
Chadema wanapaswa kujikita kwenye Kutetea Haki, Kupigania mabadiliko katika mchakato mzima wa Maendeleo ya Watu na Demokrasia hapa nchini.
Wakumbuke kwamba: Chama Cha ANC cha Afrika Kusini enzi za Utawala wa Ubaguzi wa rangi kwenye nchi hiyo walikuwa hawana hata Mbunge mmoja na pia Chama hicho kilitangazwa na Makaburu kuwa eti lilikuwa ni 'Kundi la Kigaidi.'
Kwa kuwa ANC ilikuwa inapigania HAKI za Watu weusi wa nchi hiyo, Wananchi wengi sana waliwaunga mkono. Pia Wananchi hao Walijitolea kwa hali na Mali, na wakati mwingine Wananchi hao walikuwa tayari kujitolea mhanga kwa maisha na uhai wao ili kuitetea ANC hadi hapo Chama hicho kiliposhika hatamu katika Utawala wa nchi hiyo.