Uchaguzi 2020 Tundu Lissu akiwasili nchini atakamatwa na kuwekwa mahabusu baada ya wadhamini wake kujitoa, atafanyaje kampeni?

Ndiyo mlichobaki nacho cha kutegemea mabeberu watz wamewakataa. Lissu ni ndoto kuongoza TZ anapoteza muda wake na familia yake tu.
Mbona mnatapatapa Sana si ndo vizuri ili aje mmgaragaze Kama kweli mnakubalika
 
Tundulisu mkumbuke kwanza Ana kesi ya uchochezi kabla ya yote pia atatakiwa aje athibitishe tuhuma zake alizokua akimtupia Rais wazi wazi na kumchafua Rais na serekal yake kwa mabeberu

Tunataka aje atuthibitishie Yale alio kua anaongea nje
Mnataka wewe na nani? Usitupotezee muda hapa, kaa pembeni ya computer yako au simu yako na hakikisha una bundle la kutosha usubiri hotuba ili uchangamshe akili.
Watumishi wa umma wanangoja kwa hamu uchaguzi wamchague atakaye hakikisha mishahara yao inaboreshwa. Haijapata kutokea, maana hata wakati wa vita Kagera Nyerere alikuwa anapandisha mishahara. Lakini huyu 5years Chweeee?
 
Lissu hahitaji kufanya campaign. Nawe Unajua .
Pengine wapinzani wake wanahitaji kufanya campaign zaidi, kwa vile wana cha kujibu
 
Kwema kabisa kamanda...
1. MAENDELEO HAYANA VYAMA
2. UDIKTETA UHAUNA VYAMA
 
Hao ni tishio kwa chama tawala? Vyama vyao vina wabunge na madiwani wangapi kwa ujumla wao?

Kwa hiyo kuna sifa kuwa tishio kwa watawala badara ya kuwa tishio kwa maendeleo ya nchi?
Basi kama ni tishio kwa watawala basi wacha wapate haki yao,
Hakuna binadam anayetaka kuishi kwa kutishiwa,
Nakama watataka kuendelea kuwa tishio,
Basi CCM bado ipoipo saana.
 
Hiyo ni kesi ina dhamana atapambana nayo.
Ila kurudi lazima ili aingie kwenye kinyanganyilo cha kampeini za Urais!!
Usiyempenda anakuja!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…