Tundu Lissu anaponda maridhiano kwa nia njema au anahofia nafasi yake ya ugombea urais 2025?

Lissu ni typical Magufuli katika kusema hovyo sema tofauti Lissu yuko upinzani na hajawahi kuwa Rais. Wote wawili ni hatari kuwapa madaraka ya juu kabisa ya kuongoza nchi. Tumejifunza kwa Magufuli tusirudie makosa hata kama upinzani watachukua nchi lakini LISSU hafai kuwa Rais.

Post zangu za nyuma nimemtetea sana Lissu kwa umahiri wake kwenye sheria za madini na mazingira, nimemtetea wakati Magufuli ananyima haki zake baada ya kumpiga risasi 16
 
Kwanini miaka yote mlishindwa kuitetea hiyo haki ya katiba kwa njia mnaodhani ni sahihi kwenu ?
Chama kilipoitisha maandamano nani alijitokeza zaidi ya kujificha kwenye mitandao na I'd fake,
Wakati mwingine tuwe wa kweli tuache unafiki

..wakosaji ni wale wanaovunja na kukiuka haki za wananchi.

..wahanga wa uvunjwaji wa haki hawastahili lawama kwa kushindwa kujitetea.
 
..wakosaji ni wale wanaovunja na kukiuka haki za wananchi.

..wahanga wa uvunjwaji wa haki hawastahili lawama kwa kushindwa kujitetea.
Mkuu ni jukumu na wajibu wa wananchi na haswa chama Cha siasa hususani vya upinzani kutetea haki za kikatiba wanapoona Zinakiukwa

Suala linabaki ni mbinu Gani watakayotumia kutetea haki zao za kikatiba
Hoja yangu ni kwamba
Kwa upande wa viongozi wa vyama vya upinzani walijaribu mbinu mbalimbali hazikuleta matunda
ikiwemo kuitisha maandamo kupiga kelele bungeni vyombo vya habari na wakaishia kupata madhara makubwa
Lakini kwa wa wafuasi wao hawakuwapa sapoti ya kutosha

Baada ya hapo viongozi wamekuja na mbinu mpya ya kutetea haki kupitia mariadhiano
Chakushangaza Kuna viongoazi wanapinga na baadhi ya wafuasi wakitaka zitumike mbinu zile zile za kizamani ambazo hazikuzaa matunda
 

..hakuna anayepinga maridhiano na mapatano.

..kinachopingwa ni danadana na janjanja ya watawala kuhusu maridhiano.

..matendo ya watawala yanaonyesha hawana nia ya dhati ya kufikia maridhiano.


..kuna ucheleweshaji ambao unaelekea ni wa makusudi ktk utekelezwaji wa madai ya kuandikwa kwa katiba mpya, na kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

..pia maamuzi ya Raisi kuteua baadhi ya watendaji wa serikali wanaohusishwa na ukiukwaji wa haki za wananchi yanatia mashaka kama ana nia ya kweli na maridhiano.

...kutokuzungumziwa kabisa kuhusu kuundwa kwa TUME YA UKWELI, HAKI, NA UPATANISHI, ni jambo ambalo linakatisha tamaa na kutia mashaka kama maridhiano haya ni ya kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…