Tundu Lissu awataja Majaji wa Kikwete wasio na Sifa (Kazi ndio inaanza)

Tundu Lissu awataja Majaji wa Kikwete wasio na Sifa (Kazi ndio inaanza)

Mimi ningependa hao watumishi wa serikali kuanzia naibu waziri wa katiba na sheria pamoja na waziri wake, katibu mkuu kiongozi, jaji kiongozi na jaji mkuu na hata raisi kikwete mwenyewe wajitokeze na utetezi wenye kueleweka.

Kwakuwa Lissu amewataja kwa majina majaji wasio na sifa ya kuwa majaji basi nao wawataje kwa majina na kuthibitisha kwamba wana sifa za kuwastahili kuwa majaji.
Kimsingi ulichokitaja hapa kiongozi hata wanaojibu hizo hoja kwa ujumla jumla nadhan wanajua ndicho wanachopaswa kufanya. Na kama hawajui ka hivyo ndivyo wanavyopaswa kufanya basi inabidi tuwe na wasiwasi na utumishi wao. Kinachoonekana hapa kwa huu ukwepajikwepaji wa hoja kwa kutoa majibu ya jumla jumla (Esther Wassira referred to Cheap Answers) ni kushindwa kujibu hoja ambayo ipo very specific mana Lissu kataja majina. Suluhisho ni kuwavua vyeo hao majaji wasio na sifa na sio kuleta majibu ya kijinga kwa wananchi!!!
 
Huu udhuru wa Mh. Rais kuteua majaji wasio na sifa unatokana na sababu gani? Maana Mwl. JK Nyerere wakati Tanganyika inapata uhuru mwaka 1961 angeweza kuwa na sababu ya kufanya uteuzi wa namna hii kwa vile 'wasomi' wazawa walikuwa wachache.

Sasa hivi kuna wasomi-wanasheria kibao wenye shahada za sheria na utumishi uliotukuka wa angalau miaka 10 kama katiba isemavyo.

Ni vizuri kuwa na wabunge na chama makini kama CHADEMA ambacho kwa niaba ya wananchi wasio na sauti kuuliza hizi teuzi za 'kasi' za Mh. Rais Jakaya Kiwete bila kuzingatia taratibu, sheria, katiba na utumishi uliotukuka.
 
I hate this president.What is this kind of leadership?Is he really knows what he is doing there at state house?

If these allegations are true,then definitely, there is something wrong with our president.

I think he should resign.
 
Kwa wale wanaofuatilia mambo,inamaana tundu lisu ndie anaejua sheria kuliko watz wote?kama jibu ni hapana kwanini kama kuna ukweli na hao wengine mbona hawatoi ufafanuzi?tundu atakuwa ana wivu tu hana jipya.

Huyo Tindu Lissu ni Mdini tu.Amewalenga waislamu ili awachafue.Christian Democratic Movement in Action
Wakuu jibuni hoja kwa hoja.

Katiba inatoa sifa za majaji. Watu walioteuliwa kuwa majaji bila sifa hizo wametajwa na sababu zimewekwa wazi. Kujibu hoja ya Lissu: ama uoneshe kuwa Lissu amepotosha vigezo vilivyowekwa na katiba (uvitaje hivyo ambavyo ni sahihi), au uoneshe kuwa waliotajwa wanakidhi vigezo vilivyowekwa na katiba alivyovitaja Lissu.

Tunataka kujua vigezo gani vimetumiwa kuwateua hao majaji.

Ni hoja dhaifu kuhoji kuwa "ina maana Tundu Lissu ndie anaejua sheria kuliko watz wote?" au kukimbilia single iliyozoeleka ya udini. Hoja za namna hii nashangaa zinafikaje kwenye jamvi hili, linalopaswa kuwa jamvi la Great thinkers.

Yawezekana kuna wengi wanaoona hilo, lakini ni waoga au wanatanguliza maslahi ya chama chao kwanza au ni wavivu wa kuhoji au wachumia tumbo wanaoogopa kupoteza nafasi zao.

Watanzania tumezoea kuhongwa kwenye chaguzi na tunaishia kuchagua kwa vigezo vya fedha zao watu wasioweza kujenga hoja na kusimamia serikali ilinde na kufuata katiba. Wabunge wenye ujasiri kama Lissu ni wachache, lakini ndio wanafaa kuwakilisha wananchi, kwani kwenye ukweli hawaogopi yeyote bali wanaisimamia serikali kikamilifu, ambayo ndiyo kazi ya msingi ya bunge.
 
Mwenye kuweza kupata CV za hao waliotajwa naomba atuwekee hapa jamvini....
 
JK alikosa Waislam wenye sifa za kuwa majaji kwa hiyo akaamua kuwateua hata wasio na sifa ili ku-balance dini za majaji. JK ni mdini sana.

..yeah, rais DHAIFU from chama na serikali DHAIFU
 
Ingekuwa serikali makini, hii ni sababu tosha kumshtaki rais! Amevinja katiba aliyoapa kuilinda na kuifuata!!

Chama, maslahi ya cham ndo yako mbele zaidi!!
 
Fatuma Masengi, ambaye kwa mujibu wa Lissu alikuwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Singida na baadaye akawa Hakimu Mkazi kisha akaanza kujisomea Chuo Kikuu Huria na kuhitimu mwaka 2003 na kuteuliwa kuwa jaji mwaka 2006.

INAWEZEKANA NI JINIASI????
 
Hatuko salama kabisa Tundu Lissu sio mwehu na ushahidi anao kazi ni kwa hao walioguswa!
 
ndugu yangu hawawezi kufanya hivyo. Nchi yetu imekuwa ya kuendeleza upoendeleo badala yakufuata sheria
Mimi ningependa hao watumishi wa serikali kuanzia naibu waziri wa katiba na sheria pamoja na waziri wake, katibu mkuu kiongozi, jaji kiongozi na jaji mkuu na hata raisi kikwete mwenyewe wajitokeze na utetezi wenye kueleweka.

Kwakuwa Lissu amewataja kwa majina majaji wasio na sifa ya kuwa majaji basi nao wawataje kwa majina na kuthibitisha kwamba wana sifa za kuwastahili kuwa majaji.
 
Isije ikawa hao majaji walichakachua vyeti na cv zao, maana JK anapenda sana vitu vilivyochakachuliwa!
 
Kwa wale wanaofuatilia mambo,inamaana tundu lisu ndie anaejua sheria kuliko watz wote?kama jibu ni hapana kwanini kama kuna ukweli na hao wengine mbona hawatoi ufafanuzi?tundu atakuwa ana wivu tu hana jipya.

...Acha uvivu wa kutumia akili yako japo ya kuzaliwa tu ndugu. Jibu hoja na sio kutoa majibu rahisi rahisi tu kwa maswali magumu. Sio tu Tundu Lissu anajua sheria, bali pia ni mjasiri wa kutetea na kusimamia anachokijua
 
Kwakweli sasa ukweli hupo hadharani sijui na hapa atasema alikuwa hajui! Yani hapa kaidharirisha katiba!

Kujuana kwingi uharibu kazi na haya ndio yanayo mkuta jk!

Daa tatizo wanao ambiwa hawataki kukubali japo ukweli wana uona!
 
Isije ikawa hao majaji walichakachua vyeti na cv zao, maana JK anapenda sana vitu vilivyochakachuliwa!

By the way, hata Mh. Mulugo, Naibu waziri wa Elimu aliajiriwa ualimu kwa cheti cha Diploma ya Ualimu cha Dr. Dick Mulungu. Dr. Mulungu kwa sasa ni mwalimu wa chuo kikuu Mkwawa. Na kazi hiyo ya ualimu ndio imekuwa mwanzo wa safari yake kwenda Unaibu waziri.

Hii hata Usalama wa Taifa wanajua. Na JK anajua bila shaka.
 
Back
Top Bottom