Lissu na ateue wake; Raisi ameteua kwasababu wanasifa zinazotakiwa hata leo hii Lissu akiteuliwa wapo watu watasema Lissu hana sifa; sasa kama huyu mwanaharakati wenu Lissu na atue jopo lake la majaji.
Kama madai ya Lissu ni sahihi basi hatuko salama!
mkuu umesema vyema unakumbuka mh.joseph mbilinyi alishawahi uliza BUNGENI rais anatumia kigezo gani anapoteua???mh.b.membe akasema rais anamteua mtu kama ikimpendeza hapa ndipo vilaza wanapopenyea!!!!!! Pamoja na kwenye sakata hili la majaji!!!!!!!!!!!tuwe na tume safi za kitaaluma. Watu waombe kazi hizi. Ifanyike vetting ya hali ya juu. Interview ziwe wazi kabisa. Wenzetu hapa kenya sasa hata jajimkuu anaomba kazi kwa uwazi kabisa hadi tv zinaonyesha "live" mahojiano. Kenya wanatuacha sana.
Ujinga ni mzigo. Bado hujajua, kinachokusumbua ni mbolea nyingi ya ujinga uliyowekewa ambayo bado inarutubisha ujinga kichwani mwako. Siku mbolea ujinga itakapokwisha, ufahamu utakuijia na utajua kuwa yu uchi. Kende zako zi nje zinaonekana, lakini kwa sasa sentesi hii kwako ni kichina.
Kamanda Lissu anasimamia katiba aliyoahidi kuilinda kwenye kiapo cha ubunge sasa akipeleka hoja ya kumchunguza rais mibunge mingi ya ccm itakwamisha hoja na pia mkwamo mwingine utaanza kwa Bi Kiroboto!
Tundu na zito hawatofautiani kitu katika kujitafutia umaarufu binafsi,tofauti yao ni kuwa tundu anabebwa na dini yake mbele ya pro chadema,wanampenda na ujinga wake
Kwa hiyo wakati huyu dada akiwa hakimu na baadae hakimu mkazi hakuwa hata lawyer! Achana na ujaji for a second, maana majority ya kesi za Mtanzania zinasikilizwa na mahakimu. Hakimu ni muhimu kuliko jaji kwa Tanzania, it is eerily funny in Tanzania eti kesi ya mauaji inaenda Kisutu kwa hakimu mkazi halafu kesi ya madai ya Manji anamdai Mengi shilingi moja kwa kumchafulia jina lake maarufu inaanzia Mahakama Kuu!Fatuma Masengi, ambaye kwa mujibu wa Lissu alikuwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Singida na baadaye akawa Hakimu Mkazi kisha akaanza kujisomea Chuo Kikuu Huria na kuhitimu mwaka 2003 na kuteuliwa kuwa jaji mwaka 2006.
Kuna nyingin nimeipata leo hii hapa:
- '' Ndesamburo na mtoto wake na mkwe wake, Lissu na Dada yake Christina, Zitto na Mchumba wake, Mtei na Mkwe wake, Slaa na mke wake!! HEBU ONDOA BORITI KWENYE JICHO LAKO KWANZA NDIO UNAWEZA KUTUFUNDISHA CCM!! quoted W.J. Malecela
Inawezekana ikawa ni siasa za mgongano wa kimaslahi hizi! Wanatuzuga wote hawa CCM na CDM mlengo wao ni mmoja. Inawezekanaje chama kinahodhiwa na familia?
Kwa wale wanaofuatilia mambo,inamaana tundu lisu ndie anaejua sheria kuliko watz wote?kama jibu ni hapana kwanini kama kuna ukweli na hao wengine mbona hawatoi ufafanuzi?tundu atakuwa ana wivu tu hana jipya.
Kama madai ya Lissu ni sahihi basi hatuko salama!
ndo maana magamba wanaipenda sana hii katiba mbovu, wateue vihiyo!Nimepitia vipengele vyenye red katika katiba nimeona viko sahihi kabisa. LAKINI KIPENGELE CHA 9 KATIKA IBARA HIYO YA 109 INASEMA HIVI"(9) Iwapo Rais atatosheka kwamba ijapokuwa mtu mwenye
sifa mojawapo ya hizo sifa maalum hakuwa nayo sifa hiyo kwa
muda usiopungua miaka mitano, lakini mtu huyo ana uwezo, ujuzi
na kwa kila hali anafaa kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa
Mahakama Kuu na kuna sababu za kumfanya mtu huyo astahili
kukabidhiwa madaraka hayo, basi Rais aweza kutangua lile sharti
la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano, na
baada ya kushauriana na Tume ya Kuajiri ya Mahakama, Rais
aweza kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu."
KWA MANTIKI HIYO BASI, RAIS YUKO SAHIHI KABISA KUWATEUA ALIOONA WANAFAA.
HIVI NDIVYO KATIBA INAVYOSEMA KUHUSU UTEUZI WA MAJAJI:
Ibara ya 109 kifungu cha 6:Bila kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (8) ya ibara hii, mtu aweza tu kuteuliwa kuwa jaji wa mahakama ya kuu ikiwa ana sifa maalumu, kama ilivyofafanuliwa katika ibara ndogo ya (7) ya ibara hii, na awe mtu ambaye amekuwa na mojawapo ya sifa maalum kwa muda usiopungua miaka kumi.
Kifungu cha 7: Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa ibara ndogo za (6), (8) na (10) ya ibara hii, sifa maalum maana yake ni mtu aliye na shahada ya sheria kutoka chuo kikuu kinachotambuliwa na mamlaka ya ithibati Tanzania na -
(a) amekuwa hakimu.
(b) amefanya kazi katika utumishi wa umma akiwa na sifa za kufanya kazi ya uwakili au ni wakili wa kujitegemea.
(c) ana sifa ya kusajiliwa kuwa wakili, na amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi.
Kifungu cha 8: Iwapo Rais atatosheka kwamba ijapokuwa mtu mwenye sifa mojawapo ya hizo maalum hakuwa nayo sifa hiyo kwa muda usiopungua miaka kumi, lakini mtu huyo anauwezo, ujuzi na kwa kila hali anafaa kukabidhiwa madaraka ya jaji wa mahakama kuu na kuu na kuna sababu za kumfanya mtu huyo astahili kukabidhiwa madaraka hayo, basi Rais aweza kutengua lile sharti la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka kumi na baada ya kushauriana na Tume ya Utumishi wa Mahakama, Rais aweza kumteua mtu huyo kuwa jaji wa Mahakama kuu.