Pre GE2025 Tundu Lissu: Bila Katiba Mpya, Bila Tume Huru ya Uchaguzi CHADEMA haitashiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025

Pre GE2025 Tundu Lissu: Bila Katiba Mpya, Bila Tume Huru ya Uchaguzi CHADEMA haitashiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huyu jamaa hana jipya,je huo ndo msimamo wa chama,vipi kama chama kina maoni tofauti,na vipi kama chama kikiamua kusimamisha ntu tofauti la huyu Lissu,!!? Je chadema mtu mwenye sifa za kugombea urais ni mmoja tu!?, Poor chadema jipangeni mje na hoja za kumshawishi mwananchi wa Nanjilinji ambaye hajui hata maaana ya katiba ili awape kura!
 
Wameshagundua watu hawawaungi mkono wanataka kutafuta sababu, wao kila kukicha ni kumuandama JPM sasa madhara yake ni kuwa wanaanchi wanawapoteza. Wanataka tume huru ili wakigaragazwa kwenye uchafuzi waende kupinga mahakamani kusema wameibiwa.
 
Nashukuru mkuu kwa kuliona Hilo la upatinanaji wa katiba Kwa sasa mpaka 2025 ni ngumu,
Linahitaji mchakato mrefu kidogo,
Tukumbuke mwakani uchaguzi serikali za mitaa then 2025 ni uchaguzi mkuu,
So maybe lifanyike mwaka huu huu lipitishwe kwanza kwenye bunge la bajeti then mchakato uanze,
Kitu ambacho Bado ni ngumu
Ninachowaambia CHADEMA ni lazima wawe wakweli kwa wananchi wakati wote ili kuaminiwa katika wanayoyasimamia, kuliko kuendelea kuvungavunga huku wakiiujua ukweli wenyewe ulivyo.

Katiba Mpya, ni muhimu sana, na inatakiwa waendelee kuishikia bango; lakini wakati huo huo kutokana na hali halisi ilivyo, hasa kutokana na ufinyu wa wakati, ni dhahiri wanajuwa katiba mpya haiwezi kuwepo kabla ya uchaguzi.

Kwa hiyo hili ni jambo linaloeleweka vizuri kwa wananchi.

Kinachotakiwa sasa wakitilie mkazo kabisa kabisa, ni kuhakikisha kwamba mazingira ya uchaguzi utakaokuja, ambao hata hivyo utafanyika chini ya katiba hiyo mbovu, ni lazima uwe wa HAKI, HURU na wa WAZI kabisa, ili matokeo yake yasiwe ya kutilia mashaka.

Hili linawezekana kabisa, na ndilo lililobaki kulifanyia mipango jinsi gani litatekelezwa.

Hii ndiyo kazi wanayotakiwa kuisimamia sasa hivi CHADEMA, kuliko kuendelea kutishia kutoshiriki uchaguzi kama hakuna katiba mpya.

Akina Mahera na wengine wote, kama hao wakurugenzi kusimamia uchaguzi, ni mambo yanayowezekana kuyarekebisha sasa hivi.

Hata huyo Rais, mwenye mamlaka yote dhidi ya Katiba iliyopo sasa, atatambua kwamba kufanya maamuzi yanayovuruga uchaguzi ni njia iliyo wazi kumwondoa madarakani kwa nguvu, kama siyo kumpeleka ICC kabisa.

Kwa hiyo hatakuwa na uthubutu wowote wa kuingilia maamuzi ya wananchi watakayofanya wenyewe kuhusu viongozi wanaotaka wawaongoze.

Hii ndiyo kazi inayowasubiri CHADEMA tangia sasa hadi baada ya uchaguzi 2025. Wasianze kutafuta visababu pembeni.
 
Kati ya kosa ambalo Chadema itakosea ni kutoshiriki Uchaguzi.
Uhalisia ni kuwa hakuna muda wa kupata hiyo katiba mpya kwa sasa na huo ndio ukweli wenyewe.

Ili wapate katiba nzuri inabidi wawe na wawakilishi bungeni, nje ya hapo ni kupoteza.
Watakiwa upigane ukiwa ndani
Mkuu mbona unafunua siri kwenye vita.
 
Ninachowaambia CHADEMA ni lazima wawe wakweli kwa wananchi wakati wote ili kuaminiwa katika wanayoyasimamia, kuliko kuendelea kuvungavunga huku wakiiujua ukweli wenyewe ulivyo.

Katiba Mpya, ni muhimu sana, na inatakiwa waendelee kuishikia bango; lakini wakati huo huo kutokana na hali halisi ilivyo, hasa kutokana na ufinyu wa wakati, ni dhahiri wanajuwa katiba mpya haiwezi kuwepo kabla ya uchaguzi.

Kwa hiyo hili ni jambo linaloeleweka vizuri kwa wananchi.

Kinachotakiwa sasa wakitilie mkazo kabisa kabisa, ni kuhakikisha kwamba mazingira ya uchaguzi utakaokuja, ambao hata hivyo utafanyika chini ya katiba hiyo mbovu, ni lazima uwe wa HAKI, HURU na wa WAZI kabisa, ili matokeo yake yasiwe ya kutilia mashaka.

Hili linawezekana kabisa, na ndilo lililobaki kulifanyia mipango jinsi gani litatekelezwa.

Hii ndiyo kazi wanayotakiwa kuisimamia sasa hivi CHADEMA, kuliko kuendelea kutishia kutoshiriki uchaguzi kama hakuna katiba mpya.

Akina Mahera na wengine wote, kama hao wakurugenzi kusimamia uchaguzi, ni mambo yanayowezekana kuyarekebisha sasa hivi.

Hata huyo Rais, mwenye mamlaka yote dhidi ya Katiba iliyopo sasa, atatambua kwamba kufanya maamuzi yanayovuruga uchaguzi ni njia iliyo wazi kumwondoa madarakani kwa nguvu, kama siyo kumpeleka ICC kabisa.

Kwa hiyo hatakuwa na uthubutu wowote wa kuingilia maamuzi ya wananchi watakayofanya wenyewe kuhusu viongozi wanaotaka wawaongoze.

Hii ndiyo kazi inayowasubiri CHADEMA tangia sasa hadi baada ya uchaguzi 2025. Wasianze kutafuta visababu pembeni.
Haya yote Chadema wanayajua. Yako kwenye Maridhiano. Mazungumzo hayajaisha...kumbuka Kauli ya Rais siku akiruhusu mikutano.
 
Makamu mwenyekiti wa CHADEMA mh Tundu Antipas Lissu amesema yeye kugombea Urais wa JMT ni hadi ipatikane Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Kimsingi CHADEMA tutaonekana Watu wa ajabu sana kama tutashiriki Uchaguzi mkuu wa 2025 kwa Katiba hii na Tume hii ya Uchaguzi amesema Lissu.

Lissu amesema CHADEMA ndio Chama pekee cha Upinzani nchini ndio sababu walipokataa kujumuishwa Kwenye Kikosi Kazi cha Prof Mkandalla na Kikosi chenyewe kikafa ganzi hapo hapo na hakisikiki tena popote.

Chanzo: ITV


Sometimes uwa nahisi tundu lissu ni wakala wa CCM ambae anatumika kuwapa ccm ushindi mwepesi tena wa bure kabisa

Coz hata wakigoma sio kama uchaguzi hautofanyika hapana,

Uchaguzi utakuwepo na viongozi wataapishwa na Maisha yataendelea then yy anapata faida gani?

Ningemwelewa ishu yake kama angekuwa na uwezo wa kusimamisha uchaguzi, au kuandamana uchaguzi usifanyike, but hakuna kitu anaweza kufanya zaidi ya kutoroka na kwenda ulaya


Huyu jamaa Mwangalieni vizuri

Hata kwenye mambo ya viti maalumu, ni yy ndio alileta siasa zake za majitaka na akaondoka zake eeeh what happen? Wakina mdee si wapo bungeni?
 
Nashukuru mkuu kwa kuliona Hilo la upatinanaji wa katiba Kwa sasa mpaka 2025 ni ngumu,
Linahitaji mchakato mrefu kidogo,
Tukumbuke mwakani uchaguzi serikali za mitaa then 2025 ni uchaguzi mkuu,
So maybe lifanyike mwaka huu huu lipitishwe kwanza kwenye bunge la bajeti then mchakato uanze,
Kitu ambacho Bado ni ngumu
Hakuna kitu kigumu. Rasimu ya Warioba iko tayari. Rais akiamua hata mwaka huu huu inapatikana. Kwani marekebisho ya Rasimu inachukua miezi mingapi? Ikienda mingi ni 3months only.
 
Sometimes uwa nahisi tundu lissu ni wakala wa CCM ambae anatumika kuwapa ccm ushindi mwepesi tena wa bure kabisa

Coz hata wakigoma sio kama uchaguzi hautofanyika hapana,

Uchaguzi utakuwepo na viongozi wataapishwa na Maisha yataendelea then yy anapata faida gani?

Ningemwelewa ishu yake kama angekuwa na uwezo wa kusimamisha uchaguzi, au kuandamana uchaguzi usifanyike, but hakuna kitu anaweza kufanya zaidi ya kutoroka na kwenda ulaya


Huyu jamaa Mwangalieni vizuri

Hata kwenye mambo ya viti maalumu, ni yy ndio alileta siasa zake za majitaka na akaondoka zake eeeh what happen? Wakina mdee si wapo bungeni?
Wewe ni mwana ccm mambo ya chadema achana nayo
Mwaka 2019 na 2020 Chadema ilishiriki.

Ilichoambulia ni watu kupiga marisasi, kuchomwa visu( mdogo wake Wenje na Heche). Kuvunjwa miguu na kufungwa.

Kuna watu mpaka walichomwa moto na mwisho wa siku chadema ikaambulia Zero.

Je unataka warudie hayo hayo?

Msiwe wa rahisi kusahau mambo ya juzi tu.

Yaani kukaa miaka mitatu tu tayari mmeshasahau? Ni uroho wa madaraka bila kujali athari??

Chadema inatambua hasara na maafa yaliyowakuta wanachama wake wakati wa uchaguzi walipojarbu kulinda haki za uchaguzi haiwezi ku- risk tena.

Chadema ikirudisha wanachama wake kwenye mazingira kama yale maana yake inajali madaraka tu haiangalii madhara wanayopata wafuasi wake.

That can be very radiculous.

Huo uchaguzi fanyeni wenyewe mshinde 100% lakini msiue mtu wala kuvunja mtu miguu
 
Makamu mwenyekiti wa CHADEMA mh Tundu Antipas Lissu amesema yeye kugombea Urais wa JMT ni hadi ipatikane Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Kimsingi CHADEMA tutaonekana Watu wa ajabu sana kama tutashiriki Uchaguzi mkuu wa 2025 kwa Katiba hii na Tume hii ya Uchaguzi amesema Lissu.

Lissu amesema CHADEMA ndio Chama pekee cha Upinzani nchini ndio sababu walipokataa kujumuishwa Kwenye Kikosi Kazi cha Prof Mkandalla na Kikosi chenyewe kikafa ganzi hapo hapo na hakisikiki tena popote.

Chanzo: ITV
Hivi hizi taarifa nyingine huwa mnazitowa wapi?wakati kipindi kimerushwa wote tumekifuatiria hakuna kauli kama hiyo aliyoisema,tena ni kwa kiswahili kabisa,hayo maneno huwa mnayatoa wapi na kwa faida gani??!
 
Haya yote Chadema wanayajua. Yako kwenye Maridhiano. Mazungumzo hayajaisha...kumbuka Kauli ya Rais siku akiruhusu mikutano.
Mkuu, mimi hayo ya mazungumzo ya "maridhiano", sina ufahamu nayo, na kama wewe unataarifa zake, basi jaribu kutudokeza nasi tuwe na ufahamu juu yake.

Kwa nini nayasema haya.

Viongozi wa CCM wameonyesha kwa muda mrefu sana kuwa wasiokuwa na uaminifu; kuwa watu wanaolinda maslahi yao zaidi kuliko maslahi ya nchi. Kwa hiyo, binafsi siwaamini. Wawe wale waliokuwa wakitumia miguvu mingi na kuumiza watu ambao hawakukubaliana nao, au hawa sasa hivi wanaotumia mbinu za kulainisha, bila kuumiza, lakini wakijuwa matokeo yatakuwa ni yale yale ya wao kuendelea kubaki madarakani wakifanya madudu yale yale wanayofanya miaka yote.

Kwa hiyo, mimi ninawatahadharishahawa CHADEMA, wasilazwe usingizi kabisa, na kuja kustuka wakati umepita kwamba wamekwishaachwa kwenye mataa.

Hata hivyo, kama kweli CHADEMA wanayafahamu hayo maridhiano kama unavyodai wewe hapa, iweje sasa wawe wanasikika tena kwamba "hawatashiriki uchaguzi kama hapatakuwepo na katiba mpya"?

Au umesahau yanayozungumziwa kwenye mada hii?
 
Mkuu, mimi hayo ya mazungumzo ya "maridhiano", sina ufahamu nayo, na kama wewe unataarifa zake, basi jaribu kutudokeza nasi tuwe na ufahamu juu yake.

Kwa nini nayasema haya.

Viongozi wa CCM wameonyesha kwa muda mrefu sana kuwa wasiokuwa na uaminifu; kuwa watu wanaolinda maslahi yao zaidi kuliko maslahi ya nchi. Kwa hiyo, binafsi siwaamini. Wawe wale waliokuwa wakitumia miguvu mingi na kuumiza watu ambao hawakukubaliana nao, au hawa sasa hivi wanaotumia mbinu za kulainisha, bila kuumiza, lakini wakijuwa matokeo yatakuwa ni yale yale ya wao kuendelea kubaki madarakani wakifanya madudu yale yale wanayofanya miaka yote.

Kwa hiyo, mimi ninawatahadharishahawa CHADEMA, wasilazwe usingizi kabisa, na kuja kustuka wakati umepita kwamba wamekwishaachwa kwenye mataa.

Hata hivyo, kama kweli CHADEMA wanayafahamu hayo maridhiano kama unavyodai wewe hapa, iweje sasa wawe wanasikika tena kwamba "hawatashiriki uchaguzi kama hapatakuwepo na katiba mpya"?

Au umesahau yanayozungumziwa kwenye mada hii?
Wait and see
 
Back
Top Bottom