Pre GE2025 Tundu Lissu: Chama hakitaokolewa na mtu ambaye ameshakiongoza kwa miaka 21. Namuokoa Mbowe asiwe 'Mugabe'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Akishinda Lisu, utauona mwamko mpya wa CHADEMA na wa watu wote wasioridhishwa na jinsi nchi inavyoongozwa. LAKINI kama atashinda MBOWE, nchi itakuwa kama vile ipo kwenye msiba, na hakuna mtu atakayepoteza muda wake kwa sababu ya CHADEMA.
Hakika
 
Itakuwa vizuri ili wananchi wawe wanaangalia taasisi badala ya mtu. Mtu anaweza akaondoka mda wowote lakini taasisi itaishi.
taasisi imara ya siasa ni CCM, wananyukana kimyakimya ndani kwa ndani wakitofautiana
 
Akishinda Lisu, utauona mwamko mpya wa CHADEMA na wa watu wote wasioridhishwa na jinsi nchi inavyoongozwa. LAKINI kama atashinda MBOWE, nchi itakuwa kama vile ipo kwenye msiba, na hakuna mtu atakayepoteza muda wake kwa sababu ya CHADEMA.
Loyalists wa Ayatollah Mbowe hawatakubali yaishe. Huo mpasuko utatibika vipi?
 
Haya mahojiano yalifanyika lini?
 
taasisi imara ya siasa ni CCM, wananyukana kimyakimya ndani kwa ndani wakitofautiana
Sasa huyo wanayempigia chapuo awe kiongozi mkuu halafu fridge haligandishi atajenga taasisi au kitakuwa kikundi cha kutuhumiana kila siku.
 
Tarehe 21.01.2025 naiona mbali sana!
Mungu akinipa neema ya kuishi maisha marefu kama Mzee mwinyi ntakuja kuwasimulia wajukuu zangu hizi mambo!
 
Hata aseme nini lkn hapati uenyekiti
 
Kama wanaangakia Taasisi hawahitaji mtu wa kuwaongoza, Wakenya hawategemei kiongozi yoyote wa siasa wao kuingia Barabarani.
Ndio nawashangaa hawa wanaharakati uchwara wanaohangaika na mtu. Kama wameona chama hakisimami na hao wananchi wanaoqasema kwa nini wasianzishe movement zao wafanye mambo kama Kenya?
Oh TAL anakubalika sana na wananchi, sasa natamani akose iongozi ili tuone hao wafuasi wake kama wataweza kuwamobilise waendelee na harakati zao.
Taasisi (chama) kibakie kama chama na hao wenye harakati zao wabakie na harakati zao.
Mfano mzuri ni Malema wa Afrika Kusini, ana kaliba ya TAL lakini anagalia kwenye uchaguzi alivuna nini.
Taasisi ikiwa imara wafuasi watapatikana tu, wenye mihemuko na wasaka tonge (kama mchungaji wa Iringa) ndio watakuwa wanatangatanga kutafusa green pastures.
 
Sahihi kabsa, MABADILIKO NI MUHIMU SANA NDANI YA CHADEMA! Wasipofanya hivyo basi CCM ataendelea kutawala milele na milele
 
Lissu anataka kukiuka katiba ya chama, Mbowe ana haki ya kikatiba ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti taifa, yeye atangaze sera zake halafu wajumbe wa kamati kuu wataamua wanaenda na nani, kutumia muda wote kulalamika kuhusu Mbowe kugombea ni kama ameshakubali matokeo🐼
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…