JE CHADEMA INAFUATILIA MABORESHO YA UANDIKISHWAJI KATIKA DAFTARI LA WAPIGA KURA 2025 ? INEC YAMALIZA KAZI MKOA WA MBEYA NA KUFUNGA VIRAGO KUELEKEA RUVUMA
View: https://m.youtube.com/watch?v=wr1U7pSvihU
Timu ya Tundu Lissu na CHADEMA watupe mrejesho jinsi walivyoshiriki katika zoezi la uandikishaji ambalo tayari limemalizwa na Tume INEC mkoani Mbeya na sasa wapo mkoani Ruvuma.
Tumejifunza kuhusu rai ya wasimamizi kuwa na uaminifu vituo vya kupiga kura TAMISEMI 2024, na sasa INEC nayo inaendelea na mchakato kuelekea uchaguzi mkuu 2025 inasisitiza uaminifu :
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele amewataka waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa halmashauri ya Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wakati alipowatembelea katika mafunzo ya siku mbili yao ..
Kuelekea uchaguzi mkuu 2025 halmashauri ya Chunya mkoani Mbeya wasimamizi wakusanywa na kupewa mafunzo ili kazi infanyike vizuri .....
Nao washiriki wasimamizi watoa maoni yao kuhusu kazi ya uboreshaji taarifa za mpiga kura kama amehama kijiji, mkoa n.k kurekebisha taarifa zao na wale waliofikisha miaka 18 pia wale waliopoteza kadi au wale wanaobidi kutolewa katika daftari la mpiga kura kutokana na kifo au kurukwa na akili hivyo hawataweza kupiga kura ...
Kwa mambo yaliyofanyika serikali za MITAA, wapinzani wajipange.Kutegemea wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia uchaguzi itakula kwao.Lissu Yuko sahihi sana
Tumejifunza kuhusu rai ya wasimamizi kuwa na uaminifu vituo vya kupiga kura TAMISEMI 2024, na sasa INEC nayo inaendelea na mchakato kuelekea uchaguzi mkuu 2025 inasisitiza uaminifu :
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele amewataka waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa halmashauri ya Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wakati alipowatembelea katika mafunzo ya siku mbili yao ..
Kuelekea uchaguzi mkuu 2025 halmashauri ya Chunya mkoani Mbeya wasimamizi wakusanywa na kupewa mafunzo ili kazi infanyike vizuri .....
Nao washiriki wasimamizi watoa maoni yao kuhusu kazi ya uboreshaji taarifa za mpiga kura kama amehama kijiji, mkoa n.k kurekebisha taarifa zao na wale waliofikisha miaka 18 pia wale waliopoteza kadi au wale wanaobidi kutolewa katika daftari la mpiga kura kutokana na kifo au kurukwa na akili hivyo hawataweza kupiga kura ...
WaTanzania kwa sasa, wameridhia mfumo wa maisha waliyonayo, kazi iendelee chini ya chama dola kongwe CCM.
Hata aje mwanasiasa mwenye msimamo mkali zaidi ya Tundu Lissu, atashangaa akiitisha mgomo, maandamano, kusema sana katika X -Twitter, YouTube, Clubhouse, FB, Insta lakini watu hawamuelewi.
Sana sana watamuona ni mroho wa madaraka, anataka kuvuruga amani, mchochezi, mkimbizi, familia ipo uhamishoni, mwanadispora, mhaini n.k
Kwa mtanzania siasa mbadala yaani upinzani ni sawa na kumpigia song kali na gitaa mbuzi, lakini mbuzi huyo ataishia kukimbia au kuendelea na shughuli yake ya asili kutafuna majani
Kihistoria watanganyika wamezoe atokee mtu mmoja anayeweza kushawisi umma kwa mdomo huku dola ikimuachia uwanja wa kufanya siasa kama ule wa Julius Nyerere, Augustino Mrema, Edward Lowassa, Freeman Mbowe lakini siyo wa kimapambano wa msimamo mkali wa kina Mtemvu, Kingunge Ngombale Mwiru, Tundu Lissu nikipitia mafaili ya kihistoria ya siasa za ukombozi za Tanganyika hapa ndani ya maktaba chakavu ya mkoa na maktaba ya intaneti.
Tanzania 2025 kwenda mbele inasubiri mwokozi binadamu mwenye ushawishi ajitokeze tena kwa siasa laini siyo siasa ngumu kama za Kenya, Mozambique n.k. Siasa za kuomba haki, kumsema mtawala kistaarabu, kusubiri hisani, siasa za Yallah umeniumiza lakini naomba n.k
Kwa wanaofuatilia siasa za Mozambique, hali ni mbaya kwa chama tawala cha Frelimo pamoja na serikali iliyoko madarakani. Baada ya uchaguzi kuisha na serikali kujitangaza kushinda kwa wastani wa asilimia sabini, wananchi wameikata, wakiongozwa na kiongozi wa upinzani Venancio Mondlane...
Ukiona mtu anataka kugombana na mtu halafu anaweka masharti kibao; mara tuvue mashati yasichanike; mara tupiganie uwanjani kuna eneo la kutosha; mara asiingilie mtu, jua huyo mtu ni mwoga na anaitafuta sababu za kusepa! Ahahahahaha!!!
Hizi nguo nilizonazo ni safi kuliko hizo mpya sasa kwann nibadilishe halafu hii nchi huru kila mtu ana haki ya kupenda kule anakotaka ww umechagua kwa hyo Lissu mimi nabaki na Samia tukutane mwezi wa 10
Kuanzia sasa hatutashiriki tena kwenye chaguzi zijazo ukiwemo uchaguzi mkuu 2025 bila kuwa na Katiba mpya na mfumo mpya wa kidemokrasia wenye Tume huru ya uchaguzi na sheria mpya za uchaguzi tutashiriki huku tukijua kwamba Wapiga kura feki wataandikishwa, Wagombea wetu wataenguliwa, tutafanyiwa vurugu kwenye kampeni na siku ya uchaguzi, kura feki zitaingizwa na kura halali zitaibiwa, na Wagombea walioshindwa watatangazwa Washindi wa chaguzi hizo”
“Ukweli huu mchungu unatutaka tubadilishe mbinu za mapambano ya kidemokrasia, tumesubiri CCM na Serikali zake wabadilishe msimamo wao kuhusu Katiba mpya na Tume huru kwa miaka mingi, tumewabembeleza kwa muda mrefu wakubali Nchi yetu iondokane na Katiba ya sasa bila mafanikio”
“Kuhusu uchaguzi wa Chama chetu, Mwenyekiti wetu wa Chama na Mgombea mwenzangu wa Uenyekiti wa CHADEMA (Freeman Mbowe) amesema uchaguzi wetu wa Chama unatakiwa kuwa huru na haki nami naunga mkono maneno yake, bila uchaguzi huru Wanachama wetu hawatopata fursa ya kuonesha kuwa wao ndio wenye madaraka ya mwanzo na mwisho katika kuamua hatima ya Chama chetu, ili haya yatekelezwe tunahitaji kutafakari masuala yafuatayo”
“Napendekeza kuwa pamoja na Wazee Wastaafu wa Chama watakaopatikana kusimamia uchaguzi, Kamati Kuu iwaombe Viongozi wa Dini kuhudhuria mkutano mkuu kama Watazamaji ili kusaidia kuzuia mipango ya Waovu kuvuruga uchaguzi wetu, Kamati Kuu pia iwaite Wawakilishi wa Balozi mbalimbali nchini kushuhudia uchaguzi wetu” —— Mgombea wa Uenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu akiongea na Watanzania leo January 01,2025
Ameshriki kkfkisha CDM hapa klipo - kaz kubwa. Lkn xaxa yanayoxemwa juu yke ni mengi mengne machaf na mengne hatkutegmea. Tamaa ya ukubwa inafanya heshma aloipta na kjijengea muda wte kuyeyuka kma baraf. Mambo mengi anotaka yawekwe ktk katba mpya kumbe yy hayataki ktk katiba yake! Ingependza angejtoa - na wanotaka hili ni wengi, apumzike kw heshima yke, hajachelewa - itaonekna mnafiq ...au!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.