Tundu Lissu, huwezi kuongoza chama na kuleta mabadiliko kwa kususa na kutofanya chochote tu.

Tundu Lissu, huwezi kuongoza chama na kuleta mabadiliko kwa kususa na kutofanya chochote tu.

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Badala ya kujikita kushambulia maridhiano ni vyema Tundu Lissu aeleze sasa atafanya nini akichaguliwa kuwa mwenyekiti ikiwa aina ya chaguzi zilizofanyika 2019, 2020 na 2024 zinaendelea. Ikiwa wanachama wa chama chake wataendelea kupotea, kukamatwa na kufunguliwa kesi za kisiasa.

Tundu Lissu anajisifia kwamba alikataa mialiko yote ya CCM na serikali wakati Freeman Mbowe akiwa gerezani lakini hasemi alifanya nini zaidi ya hilo na kupiga kelele tu.

Tundu Lissu ana uwezo wa kuwashawishi Wanachadema wenzake au Watanzania kwa ujumla washinikize mabadiliko kwa njia yoyote? Mimi siamini kama huo uwezo anao. Angalau Mbowe alijaribu maridhiano.
 
Swali sahihi ni Mh Mbowe amejipanga na jambo gani jipya? Maana uwezekano kuwa atashinda ni mkubwa.
 
Badala ya kujikita kushambulia maridhiano ni vyema Tundu Lissu aeleze sasa atafanya nini akichaguliwa kuwa mwenyekiti ikiwa aina ya chaguzi zilizofanyika 2019, 2020 na 2024 zinaendelea. Ikiwa wanachama wa chama chake wataendelea kupotea, kukamatwa na kufunguliwa kesi za kisiasa.

Tundu Lissu anajisifia kwamba alikataa mialiko yote ya CCM na serikali wakati Freeman Mbowe akiwa gerezani lakini hasemi alifanya nini zaidi ya hilo na kupiga kelele tu.

Tundu Lissu ana uwezo wa kuwashawishi wanachadema au Watanzania washinikize mabadiliko kwa njia yoyote? Mimi siamini kama huo uwezo anao. Angalau Mbowe alijaribu maridhiano.
Maridhiano gani? Mbowe alijidhalilisha na akaonyesha hajui haki yake na hasimamii katiba ya nchi. Unapiga magoti na kuomba uruhusiwe kufanya mkutano wakati ni haki yako? Watu wako wamewekwa jela bila makosa, wewe badala ya kutaka waachiliwe bila masharti na kudai fidia unasujudu na kuomba waachiliwe? Huu siyo uongozi bali ni utumwa. Kiongozi shupavu ni yule anayejua haki na kuidai. Unadhani Mandela angetaka kutoka jela kwa kuonyesha unyenyekevu kwa makaburu angeshindwa? Hakutaka kuwalamba miguu na alisema bora aendelee kukaa jeli kuliko kukubali masharti yao ili atoke. Huu ndiyo kiongozi!
 
Kila mtu aje na mawazo mbadala sio kukosoa tu halafu hamna way foward

Lisu anatakiwa asema anataka afanye nini kwenye kila anachoona mtangulizi wake ameshindwa kufanya sawa sawa

Lakini mbowe ndio ataingia kwenye orodha ya wenyekiti wa vyama vya siasa walioshindwa wakati wamekalia viti vyao

Unajua haiingii akilini umshinde mwenyekiti mnaegombea nae. Anyway ngoja tuone
 
Badala ya kujikita kushambulia maridhiano ni vyema Tundu Lissu aeleze sasa atafanya nini???? akichaguliwa kuwa mwenyekiti ikiwa aina ya chaguzi zilizofanyika 2019, 2020 na 2024 zinaendelea. Ikiwa wanachama wa chama chake wataendelea kupotea, kukamatwa na kufunguliwa kesi za kisiasa.

Tundu Lissu anajisifia kwamba alikataa mialiko yote ya CCM na serikali wakati Freeman Mbowe akiwa gerezani lakini hasemi alifanya nini zaidi ya hilo na kupiga kelele tu.

Tundu Lissu ana uwezo wa kuwashawishi Wanachadema wenzake au Watanzania kwa ujumla washinikize mabadiliko kwa njia yoyote? Mimi siamini kama huo uwezo anao. Angalau Mbowe alijaribu maridhiano.

Mbona alishatoa mwelekeo mzima wa uenyekiti wake wakati anatangaza nia? Mnataka aseme nini kingine zaidi ya kusema anataka kuifanya chadema iwe taasisi ya umma badala ya ilivyo sasa hivi?? Kipi ambacho hakijaeleweka na alitoa lecture ya zaidi ya lisaa na akaulizwa na maswali akajibu pia??
 
Badala ya kujikita kushambulia maridhiano ni vyema Tundu Lissu aeleze sasa atafanya nini akichaguliwa kuwa mwenyekiti ikiwa aina ya chaguzi zilizofanyika 2019, 2020 na 2024 zinaendelea. Ikiwa wanachama wa chama chake wataendelea kupotea, kukamatwa na kufunguliwa kesi za kisiasa.

Tundu Lissu anajisifia kwamba alikataa mialiko yote ya CCM na serikali wakati Freeman Mbowe akiwa gerezani lakini hasemi alifanya nini zaidi ya hilo na kupiga kelele tu.

Tundu Lissu ana uwezo wa kuwashawishi Wanachadema wenzake au Watanzania kwa ujumla washinikize mabadiliko kwa njia yoyote? Mimi siamini kama huo uwezo anao. Angalau Mbowe alijaribu maridhiano.


Kama unaitaji Chama cha upinzani then go with lissu

Ila kama unaitaji Chama ambacho ni copy ya Chama tawala then Mbowe is the best

So chaguo ni lako

Unataka Chama cha Aina gani
 
Kila mtu aje na mawazo mbadala sio kukosoa tu halafu hamna way foward

Lisu anatakiwa asema anataka afanye nini kwenye kila anachoona mtangulizi wake ameshindwa kufanya sawa sawa

Lakini mbowe ndio ataingia kwenye orodha ya wenyekiti wa vyama vya siasa walioshindwa wakati wamekalia viti vyao

Unajua haiingii akilini umshinde mwenyekiti mnaegombea nae. Anyway ngoja tuone
Hukumsikia akisema atabadilisha katiba ya chama na kuvunja secretary ya chama iundwe upya?
 
Mbona alishatoa mwelekeo mzima wa uenyekiti wake wakati anatangaza nia? Mnataka aseme nini kingine zaidi ya kusema anataka kuifanya chadema iwe taasisi ya umma badala ya ilivyo sasa hivi?? Kipi ambacho hakijaeleweka na alitoa lecture ya zaidi ya lisaa na akaulizwa na maswali akajibu pia??
Una maana gani unaposema "taasisi ya umma"? Hembu fafanua ueleweka au aeleweke ina maana gani.
 
Badala ya kujikita kushambulia maridhiano ni vyema Tundu Lissu aeleze sasa atafanya nini akichaguliwa kuwa mwenyekiti ikiwa aina ya chaguzi zilizofanyika 2019, 2020 na 2024 zinaendelea. Ikiwa wanachama wa chama chake wataendelea kupotea, kukamatwa na kufunguliwa kesi za kisiasa.

Tundu Lissu anajisifia kwamba alikataa mialiko yote ya CCM na serikali wakati Freeman Mbowe akiwa gerezani lakini hasemi alifanya nini zaidi ya hilo na kupiga kelele tu.

Tundu Lissu ana uwezo wa kuwashawishi Wanachadema wenzake au Watanzania kwa ujumla washinikize mabadiliko kwa njia yoyote? Mimi siamini kama huo uwezo anao. Angalau Mbowe alijaribu maridhiano.
Nimegundua wewe ni FISADI kuu
 
Una maana gani unaposema "taasisi ya umma"? Hembu fafanua ueleweka au aeleweke ina maana gani.
Vyama vya siasa ni taasisi za umma kiongozi sio private institutions, hujui hili?
 
Back
Top Bottom