Pre GE2025 Tundu Lissu: Kuongoza Watu Wajinga ni rahisi sana, tumekuwa Taifa la kuogopa miungu Watu badala ya kumtegemea Mungu wa Mbinguni!

Pre GE2025 Tundu Lissu: Kuongoza Watu Wajinga ni rahisi sana, tumekuwa Taifa la kuogopa miungu Watu badala ya kumtegemea Mungu wa Mbinguni!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa logic ya Lissu, Fisadi akishajiuzulu basi anafaa kupokelewa , kupigiwa kampeni ili awe rais wa nchi!.

Kwenye Ishu ya Lowasa kuwekwa na CHADEMA katika list of shame na huyuhuyu Lissu, halafu baadae kuja kumpigia kampeni ili awe rais, Lissu inabidi auombe msamaha umma au aiombe msamaha familia ya Lowasa kama alimuingiza ktk hiyo list kwa hila!
Lowassa alituhumiwa tu lakini baadae Tume ya Dr Mwakyembe ikaogopa kwenda kumhoji na Edward Lowassa akatangaza Kujiuzulu na kumtaja mwenye Richmond huku Dr Mwakyembe mwenyewe akiwa na Kampuni ya kufua Umeme wa Upepo Singida

Na Lowassa hakuwahi kushtakiwa popote 😂
 
Makamu Mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Lisu amesema Jukumu kubwa lililo mbele ya Watanzania wote wakati huu tunapoisaka Katiba Mpya ni Kufuta Ujinga, kwa sababu Ujinga wa Taifa unawarahisishia Watawala kutenda wapendavyo

Lisu anasema Tanzania imegeuka kuwa Taifa linaloabudu miungu Watu ambao ndio huwapangia wengine maisha yao yaweje

Akihutubia maelfu ya Wananchi kwenye Viwanja Vya Mwembeyanga Tundu Lisu amesema miaka 17 iliyopita walitangaza orodha ya Mafisadi Uwanjani Hapo wakiwemo Marais wawili na Waziri mkuu mmoja ambaye alijiuzulu baadae, lakini Ufisadi uliopo sasa unazidi mara mia ya Ule

Lisu ametoa mfano wa vifo vya Watu waliokufa Rufiji kwa Mafuriko na kuhoji ni nani aliyeruhusu bwawa lifunguliwe?

Aidha Lisu amesema kuna Wizi wa kutisha kwenye Halmashauri zetu lakini kwa sababu Taifa limemwacha Mungu wa Mbinguni na Kuabudu miungu Watu hakuna anayehoji na badala yake wanajinyenyekeza kwa Wezi Ili nao waonekane wa maana mtaani

Katika mkutano huo Wananchi wameazimia Tundu Lisu anunuliwe Gari Imara litakalomwezesha kuzunguka Nchi nzima kuwafuta Tongotongo Wananchi Ili macho yao yaweze kuona tena kama ilivyokuwa wakati wa Nyerere

Tundu Lisu amezungumza mambo mengi lakini kama mjuavyo mimi siyo Mwandishi wa Gazeti kama Lucas

Ahsanteni na Pokeeni Baraka za Mungu wa Mbinguni 😀😀

Kwako Erythrocyte pale Kajunjumele - Kyela 😂😂🔥
Hii ni kweli kabisa mkuu mtoa mada. CCM ndio wametufikisha hapa tulipo kwa kutujaxa ujinga na undondocha ili waendelee kutafuna rasilimali za taifa.
 
Nini kigumu nisichoweza kuelewa kuwa Lissu alipigwa risasi na wakala wa serikali hii. Kwa mwovu kama wewe ndiye unafumbia macho ukweli huu.
Serikali ingemtaka mabeki 3 wangeshughulika naye

Ni beki 3 wa Serikali Ndiye alimuwahisha Tundu Lisu hospital na kuokoa maisha yake kama ulikuwa hujui 😂😂😂

Sema nyie watoto Wadogo mnaongeaga tu mkishakunywa hayo maenergy
 
Kifupi mifumo imeparalyze na hakuna anayejali tena zaidi ya watu kuendelea kusosomola.
 
Serikali ingemtaka mabeki 3 wangeshughulika naye

Ni beki 3 wa Serikali Ndiye alimuwahisha Tundu Lisu hospital na kuokoa maisha yake kama ulikuwa hujui 😂😂😂

Sema nyie watoto Wadogo mnaongeaga tu mkishakunywa hayo maenergy
Ukifikiri mipango hiyo angeshirikishwa huyo beki 3? Yeye alifanya hivyo kwa wema wake kuokoa maisha ya mtu anayekaribia kutokwa na uhai. Reasoning yako ni ya kitoto sana kuwa kwa vile beki tatu anayelipwa na serikali alihusika kutoa msaada basi serikali haikuhusika. Wale askari FFU waliokuwa wanalinda pale nani aliwaondoa? Cctv camera zilizochukuliwa na polisi baada ya tukio leo hii ziko wapi? Usifikiri unajadili na walevi wenzako wa ulanzi hapa.
 
Lowassa alituhumiwa tu lakini baadae Tume ya Dr Mwakyembe ikaogopa kwenda kumhoji na Edward Lowassa akatangaza Kujiuzulu na kumtaja mwenye Richmond huku Dr Mwakyembe mwenyewe akiwa na Kampuni ya kufua Umeme wa Upepo Singida

Na Lowassa hakuwahi kushtakiwa popote 😂

Sawa, lakini ni CHADEMA ndiyo waliomuweka katika listi ya mafisadi iliyosomwa Mwembeyanga, na wakamuita fisadi kila kukicha kwa zaidi ya miaka 8 hata baada ya kujiuzulu kwake!. Waliacha kumuita fisadi alipogombea uraisi kupitia chama chao!

Mwakyembe hajawahi kumuita Lowasa fisadi!
 
Sawa, lakini ni CHADEMA ndiyo waliomuweka katika listi ya mafisadi iliyosomwa Mwembeyanga, na wakamuita fisadi kila kukicha kwa zaidi ya miaka 8 hata baada ya kujiuzulu kwake!. Waliacha kumuita fisadi alipogombea uraisi kupitia chama chao!

Mwakyembe hajawahi kumuita Lowasa fisadi!
Unaelewa maana ya Tuhuma bwashee?
 
Wewe kweli hamnazo. Yawezekana hujitambui kuwa umgonjwa wa akili. Wenzako wanaleta hoja, wewe unaleta porojo.

Hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuleta uthibitisho wa Lisu kupokea rushwa au kudai rushwa kutoka kwa mtu yeyote katika maisha yake.

Katika masuala ya rushwa, ufisadi na unafiki, Lisu ni mtu anayeweza kusimama mahali popote Duniani kuthibitisha kuwa ni mtu safi.
lisu ni kichaa full stop
 
Back
Top Bottom