Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Nimesikia kauli za hatari katika harakati za kampeni za urais zinazotumiwa na Mh Tundu Lisu kwenye mikutano ya CDM. Hoja za kikabila! Oh eti JM kabila lake ni Mzinza, Msubi na siyo Msukuma kwa hiyo watu wa Mwanza wasimhesabu kama mwenzao!

Kweli tumefika huko? Wanataka kuturudisha kwenye ukabila? Wasukuma wa Mwanza hawana ukabila, ndiyo maana wabunge wao ni Wachaga na Wajaluo - hawa walichaguliwa kwa sababu ya uchapa kazi wao, wakawaacha wasukuma wenzao akina Dialo,Masha, Cheyo n.k. Wao huchagua mchapakazi, JM watamchagua kama wataamini ni mchapakazi hodari na wala siyo kwa sababu ya kabila lake. Watanzania wote watafanya hivyo.

Kama tunalitakia mema Taifa letu, tuache kabisa kuingiza masuala ya ukabila katika hizi kampeni. Afadhali hata yule Prof Safari aliyejaribu kutumia tuhuma dhidi ya JM ya ufisadi sijui wa mahindi, kugoma kuwa shahidi wa kesi ya RA, watumishi wa serikali kuuziwa kwa mkopo nyumba walizokuwa wamepangishiwa na serikali.

Mambo ya kupakana matope kwenye kampeni zinakubalika na tumezizoea. Endeleeni kupakana matope - kila upande, lakini tafadhali sana sana tusitaje mambo ya makabila.

Waelimisheni na wale Yeloo wa Arusha watulize mnkali - tunatafuta rais wa Taifa na siyo Laigwan wa Tanzania!
 
CCM imeingiwa hofu, Magufuli kuwa shughuli

KUNA hofu imetanda ndani ya CCM; hofu ambayo inajaribu kufichwa mapema kwani kama mambo hayatobadilika ndani ya miezi hii mitatu hivi iliyobakia kabla ya Uchaguzi Mkuu basi chama hiki kikongwe zaidi nchini kinaweza kujikuta kikipumzishwa kutoka madarakani kwa nguvu. Dalili ya hofu hii imeonekana baada ya kutangazwa kwa mgombea wao wa kiti cha Urais Dk. John Pombe Magufuli.

Mojawapo ya mambo ambayo yametokea baada ya Magufuli kutangazwa ni kauli za kuwa yeye “anakubalika na anachagulika”. CCM imetaka kuliaminisha taifa kuwa Magufuli siyo tu anajulikana kwa utendaji kazi wake, na kuwa wananchi wengi wanampenda na wanaweza kumchagua. Kiasi kwamba wametaka watu waamini kuwa Magufuli ni Rais anayesubiria (President in waiting). Kwamba, upinzani hauna nafasi hata kidogo ya kumnyang’anya uwezekano huo.

Ukweli ni kuwa matendo ya CCM hayaoneshi kujiamini huku. Kama kweli CCM inaamini Magufuli anajulikana na kazi zake zinakubalika nchi nzima kwa nini juhudi kubwa sana inajaribu kufanywa ya “kumtambulisha”. Unamtambulisha vipi mtu ambaye tayari unaamini anajulikana, kufahamika na kukubalika? Ukiangalia utaona kuwa CCM inataka kumtumia Magufuli kukibeba chama; tatizo ni kuwa Magufuli mwenyewe – ukiondoa kukariri kwake takwimu mbalimbali – utendaji kazi wake una shaka. Tayari wizara ambayo amekalia imeshagubikwa na kashfa lukuki na hili peke yake lingetosha hata kumchafua. Akija mgombea mzuri kutoka upinzani na akajizibu hizi takwimu za Magufuli, basi Magufuli na CCM iko matatani. Yote haya yanatosha kufanya watu wajiulize mara mbili kama kweli Magufuli hatokuwa shughuli kweli kweli.

CCM imepasuka, rekodi yake mbovu, na upinzani ukimsimamisha mgombea makini, Magufuli ataweza vipi kushinda? Njia pekee ya kushinda katika mazingira ya namna hiyo ni matumizi makubwa ya nguvu, vyombo vya dola na hata kuliingiza jeshi katika siasa kama walivyofanya chini ya Jenerali Shimbo mwaka 2010. Vyovyote vile ilivyo hata hivyo kuna hofu imetanda kwa CCM; hofu kama vile wingu zito la mvua lenye dalili ya radi na ngurumo. CCM hawajui sasa wafanye nini zaidi ya kuombea Magufuli aweze kuwaokoa. Akishindwa je Hili ndilo swali la kuogopesha zaidi kwa kila mwana CCM

Chanzo: Raia Mwema (22, July 2015)
 
Dr Akili kampeni za urais zimeshaanza?Ni Magufuli na nani wanapambana kwenye kiti cha Urais?
 
CCM ndio wanatumua hizo propaganda za ukabila na ukanda wa ziwa ili kurubuni Wananchi. Wewe ulikuwa unasikiliza mkutano wako chumbani au? Mbona watu wa magamba mnakuwa wahuni?

Lissu alichokifanya ni kukemea na kueleza kuwa Dr.Magufuli sio mtu wa kabila lolote, bali kabila lake ni CCM. Hata Mwenyekiti Mbowe mwishoni amekuja kukemea kuwa CCM waache tabia za kuwagawa Watanzania kwa kutumia makabila. Akasema sisi hatuchagui mtu kwa sbb ya kabila lake.

Sasa unachofanya hapa JF, na wewe mwenyewe unaleta hizo hizo propaganda na upuuzi wenu, ambazo kimsingi viongozi wote walikuwa wanazikemea leo.

Upuuzi kama huu hatutauacha uendelee, lazima tujibu. Lengo letu kubwa ni kuhakikisha kuwa tunaling'oa hili dubwasha la huyu mkoloni mweusi CCM pmj na vibaraka wake
 
Km ulifuatilia alisema magufuli hajasimama km mmoja wa hayo makabila bali kasimama kama ni miongoni mwa kabila la ccm na si kama ulivyotoa maada. Usipotoshe umma kama hukuelewa ungeuliza nini alichosema kwa walioelewa wangekusaidia kuliko kudakia kutoa maana ukiwa hujui ata kipi kilichosemwa.
 
Acha kudaganya watu,hata mimi ni msukuma lakini hakuna tusi wala lugha ya ubaguzi. Amesema kabila la Magufuri si usukuma wake, msubi wala mzinza isipokuwa kabila la Magufuri ni CCM. Nyie ndo Madaktari wanaopasua kichwa badala ya mguu kama kweli ni Dr. kutokana na title yako.
 
kikwete,mkapa,mwinyi na hata magufuli kabila lao ni moja nalo ni CCM. kabila hili tuliogope kama ukoma.
 
Acha kudaganya watu,hata mimi ni msukuma lakini hakuna tusi wala lugha ya ubaguzi. Amesema kabila la Magufuri si usukuma wake, msubi wala mzinza isipokuwa kabila la Magufuri ni CCM. Nyie ndo Madaktari wanaopasua kichwa badala ya mguu kama kweli ni Dr. kutokana na title yako.

Lisu nilimsikiliza mwanzo mwisho ni kejeli tu,na kuonyesha hofu aliyo nayo kwa Magufuli muda wote aliopewa hakuzungumza nini chama chake kinataka kuwafanyia Watanzania kuelekea uchaguzi mkuu! Alijikita kumtaja mara nyingi sana tena akimtambulisha kwa wanachadema na kutumia Air time kumnadi mgombea wa CCM bila kujijua kweli Lisu kwa mara ya kapote njia!
 
Muda bado Mwakaboko subiria filimbi itakapopulizwa

Unasubiri Filimbi wakati wenzenu walishaanza
Dodoma na bado wanaendelea kupasua anga! Magufuli alishakaa kwenye vichwa vya watu mpaka watoto!nyie mgombea tu kawashinda kumpata!
 
Lisu nilimsikiliza mwanzo mwisho ni kejeli tu,na kuonyesha hofu aliyo nayo kwa Magufuli muda wote aliopewa hakuzungumza nini chama chake kinataka kuwafanyia Watanzania kuelekea uchaguzi mkuu! Alijikita kumtaja mara nyingi sana tena akimtambulisha kwa wanachadema na kutumia Air time kumnadi mgombea wa CCM bila kujijua kweli Lisu kwa mara ya kapote njia!

Kama una akili ndogo huwezi mwelewa lissu kamwe...
 
Ratiba ya chama ilitoka mapema kabisa inaonyesha mchakato wa kuchukua form ndani ya Chadema , kurudisha na kura za maoni kwa nafasi za udiwani, ubunge na Rais.Hawawezi kwenda kinyume na utaratibu wa chama.Watu wasubirie wakati ukifika mgombea atajulikana kwa kila mtu.Magufuli atawatoka tu kichwani na uzuri kila anakopita baada ya siku mbili minds za watu zinabadilika kwa sababu ya ugumu wa maisha.

Unasubiri Filimbi wakati wenzenu walishaanza
Dodoma na bado wanaendelea kupasua anga! Magufuli alishakaa kwenye vichwa vya watu mpaka watoto!nyie mgombea tu kawashinda kumpata!
 
Back
Top Bottom