Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Dr Akili

Nimeshasema sana kuhusu huyu Jamaa yetu sii mwanasiasa kabisa sijui kwa nini Chadema wanampa jukwaa. Huyu abakie katika mambo ya sheria mahakamani tu..
 
Last edited by a moderator:
Nimeshasema sana kuhusu huyu Jamaa yetu sii mwanasiasa kabisa sijui kwa nini Chadema wanampa jukwaa. Huyu abakie katika mambo ya sheria mahakamani tu..

..mambo mengi anayoyasema Tundu Lissu ni yale ambayo wengi wanatamani kuyasema lakini wanashindwa kwa sababu ya kukosa ujasiri.

..huyu Magufuli ndiye waziri wa kwanza maishani mwangu kumsikia akihutubia kwa kilugha.

..nashukuru Tundu Lissu ameamua kumlipua mchana kweupe.

cc Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Siasa dhaifu, mnaongelea makabila? Mtanzania yupi asiyejua kuwa JPM ni mwana CCM? Toka lini chama likawa Kabila la mtu? Tatizo mnojiita wapinzani mnatuona wote Mandaza tu. Mabadiliko hayawezi letwa na ubaguzi wala kauli zenye kuzua sintofahamu.
Zamani kulikuwa na utaratibu wa kuandaa hotuba, kiongozi akiyapima maneno yake kabla hajayaleta kwa umma, siku hizi hamna tena. Wote wanaropoka tu, halafu wala hawaji kutetea kauli zao, sie ndo tunafanya kazi za kuwasafisha. Tuwakumbushe viongozi wa vyama vyote kuandaa hotuba zao. Wayapime watayowaambia watu na kuwashirikisha viongozi wenzao wa karibu ili wawasaidie kuyaangalia kwa jicho la pili, wazipime athari zake kwa jamii.
Siasa sio maigizo, kuficha script ukiamini mwenzako atawahi kuitengenezea movie kabla yako.
 
Lisu nilimsikiliza mwanzo mwisho ni kejeli tu,na kuonyesha hofu aliyo nayo kwa Magufuli muda wote aliopewa hakuzungumza nini chama chake kinataka kuwafanyia Watanzania kuelekea uchaguzi mkuu! Alijikita kumtaja mara


nyingi sana tena akimtambulisha kwa wanachadema na kutumia Air time kumnadi mgombea wa CCM bila kujijua kweli Lisu kwa mara ya kapote njia!

Ok sawa na huyu wen u huwa akihutubia anasema nini
ASANTE lisu kwa kuwaonyesha Magufuli ni nani poleni sana Inawaa sana
 
Amesema kabila la magufuli ni ccm na ndo ukweli

umesema exactly alosema Lisu na ni ukweli mtupu.CCM ni kabila la mafisadi ili uwe mwana CCM lazima uwe fisadi.Magufuli ni mmoja wao amewekwa kuendelea kulinda mafisadi.
 
umesema exactly alosema Lisu na ni ukweli mtupu.CCM ni kabila la mafisadi ili uwe mwana CCM lazima uwe fisadi.Magufuli ni mmoja wao amewekwa kuendelea kulinda mafisadi.

Hayo akayaseme jimboni kwake, boss wake mbowe keshajengewa barabara ya lami roho kwatu na JP, yeye ahangaike kurudi bungeni tu haya ya urais awachie wengine.
 
Simple minded people discuss people. Tangazeni sera zenu achaneni na Rais Magufuli
 
Nimesikia kauli za hatari katika harakati za kampeni za urais zinazotumiwa na Mh Tundu Lisu kwenye mikutano ya CDM. Hoja za kikabila! Oh eti JM kabila lake ni Mzinza, Msubi na siyo Msukuma kwa hiyo watu wa Mwanza wasimhesabu kama mwenzao!

Kweli tumefika huko? Wanataka kuturudisha kwenye ukabila? Wasukuma wa Mwanza hawana ukabila, ndiyo maana wabunge wao ni Wachaga na Wajaluo - hawa walichaguliwa kwa sababu ya uchapa kazi wao, wakawaacha wasukuma wenzao akina Dialo,Masha, Cheyo n.k. Wao huchagua mchapakazi, JM watamchagua kama wataamini ni mchapakazi hodari na wala siyo kwa sababu ya kabila lake. Watanzania wote watafanya hivyo.

Kama tunalitakia mema Taifa letu, tuache kabisa kuingiza masuala ya ukabila katika hizi kampeni. Afadhali hata yule Prof Safari aliyejaribu kutumia tuhuma dhidi ya JM ya ufisadi sijui wa mahindi, kugoma kuwa shahidi wa kesi ya RA, watumishi wa serikali kuuziwa kwa mkopo nyumba walizokuwa wamepangishiwa na serikali.

Mambo ya kupakana matope kwenye kampeni zinakubalika na tumezizoea. Endeleeni kupakana matope - kila upande, lakini tafadhali sana sana tusitaje mambo ya makabila.

Waelimisheni na wale Yeloo wa Arusha watulize mnkali - tunatafuta rais wa Taifa na siyo Laigwan wa Tanzania!

Chadema bana mara ohh chadema kama kanisa mara mgombea huyu sio msukuma dah ndio wanataka nchi hii
 
Dr Akili

CCM ndiyo wanataka kutumia hoja ya ukabila, Tundu lissu alichosema ,kama ulimwelewa ni kwamba ,Magufuli hata awe kabila gani, ni ccm yule yule with all Tabia za kiccm kama, Wizi, ufisadi Rushwa pamoja na kuwakandamiza wananchi kwa manufaa ya wachache. TUMIA UBONGO KUFIKIRI Ndugu ile ni kauli za kifasihi.....

kwanini umeandika hoja niliyotaka kutoa ? mi niandike nini sasa? basi andika kwa niaba yangu kila kitu.
 
Jiandaeni kuandamana mnaenda Ikulu kwa Mh. Magufuli.....maneno mengi hayatafanya kazi jamaa mtamsoma namba tu.
 
Wanaosifia utendaji wa magufuli wanampima kwa barabara za lami. Lakini ndiyo hizi barabara zinazojengwa chini ya kiwango kila iitwapo leo.

Kwa sababu ya kujengwa chini ya kiwango tumepoteza ndugu zetu wengi kwa ubovu wa barabara. Kwa mfano, ajali ya pale Mafinga iliyoangamiza wengi ni kwa sababu ya ubovu wa barabara ambazo zimejengwa hivi karibuni.

Sifa ambazo ni za kijinga anazopata Magufuli ni barabara ikiishajengwa kufoka kwamba ipo chini ya kiwango. Swali ni anakuwa wapi mpaka asubiri zimalizike ndipo atafute TBC kwenda kututangazia kwamba jamani barabara hii chini ya kiwango, na nyingine nanyingine???.


kwa hiyo Barabara nyingne ambazo hazijatengenzwa kwa kpnd cha Magufuli na ajari n kama kawa inakuwaje? All in all unamaanisha kabla ya Magufuli hakukuwepo na ajari ama nn? try to think beyond the scope sio mnaleta hzo mambo bwana....tangazeni Sera.

Tena jarbu kuwa makini na watu wanaokosa kuteuliwa at one side wanakimbilia pengne....waangalie Mara mbili mbili.
 
Lissu na ukabila, Msigwa na kanisa...viongozi wa CHADEMA hawana sifa za kutuongoza watanzania.
 
Dr Akili

Hivi huku ndani ni kwanini watu wanatabia ya kujiita vitu wasivyo??? Yaani opposite kabisa. Huyu ni doctor BRAINLESS.

Nani BRAINLESS, ni yule anayeijua Brain au ni yule ambaye haijui Brain? Nina wasi wasi kuwa wewe huijui hiyo brain.
Unajua caudate nucleus, claustrum, corpus callosum, putamen, globus pallidus na amygdala zinakaa wapi kwenye brain yako na kazi zake ni zipi? Unajua kuwa wengi wa wanasiasa wanaoshabikiwa sana wana kasoro kwenye basal ganglia kwenye brain zao? Kasoro hizi za ganglia zinaweza zikawa za kimaumbile (agenesis) au ziliathiriwa na ajali (post head injury) au maambukizi ya virus kama vya coxa viruses, retroviruses including vile vya HIV etc etc.

Kasoro hizi za basal ganglia husababisha clinical syndromes (magonjwa) mbali mbali kama: Parkinsonism (globus pallidus), Wilson's Disease (putamen), Huntingtone's chorea, Sydenham's chorea, Athetosis etc etc. Ndiyo maana tunasisitiza kuwa Katiba ya nchi iwatake wagombea wa nafasi nyeti kama ya Urais wakapimwe brains zao kwenye Neuro Centres za Kimataifa - ili kuepusha majanga ambayo taifa linaweza kuyapata kama waathirika hawa wakifanikiwa kuwa Marais!

Nadhani somo umelielewa na kuwa humu ndani (JF) kuna watu wa namna gani kama suala lako lilivyouliza.
 
Nimesikia kauli za hatari katika harakati za kampeni za urais zinazotumiwa na Mh Tundu Lisu kwenye mikutano ya CDM. Hoja za kikabila! Oh eti JM kabila lake ni Mzinza, Msubi na siyo Msukuma kwa hiyo watu wa Mwanza wasimhesabu kama mwenzao!

Kweli tumefika huko? Wanataka kuturudisha kwenye ukabila? Wasukuma wa Mwanza hawana ukabila, ndiyo maana wabunge wao ni Wachaga na Wajaluo - hawa walichaguliwa kwa sababu ya uchapa kazi wao, wakawaacha wasukuma wenzao akina Dialo,Masha, Cheyo n.k. Wao huchagua mchapakazi, JM watamchagua kama wataamini ni mchapakazi hodari na wala siyo kwa sababu ya kabila lake. Watanzania wote watafanya hivyo.

Kama tunalitakia mema Taifa letu, tuache kabisa kuingiza masuala ya ukabila katika hizi kampeni. Afadhali hata yule Prof Safari aliyejaribu kutumia tuhuma dhidi ya JM ya ufisadi sijui wa mahindi, kugoma kuwa shahidi wa kesi ya RA, watumishi wa serikali kuuziwa kwa mkopo nyumba walizokuwa wamepangishiwa na serikali.

Mambo ya kupakana matope kwenye kampeni zinakubalika na tumezizoea. Endeleeni kupakana matope - kila upande, lakini tafadhali sana sana tusitaje mambo ya makabila.

Waelimisheni na wale Yeloo wa Arusha watulize mnkali - tunatafuta rais wa Taifa na siyo Laigwan wa Tanzania!

Dr. Hukumuelewa Tundu Lissu,. Toa hiyo Dr. Unajidhalilisha
 
Kwani mkuu hujui hata chama chao ni cha kikabila ndio maana hawaoni hatari kuwagawa watu kwa misingi ya ukabila
 
Back
Top Bottom