Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Kweli cdm wanatapa tapa. Mi ningeshauri watulie kuimarisha majimbo ya ubunge urais waachane nao. Magufuli hana doa. Kila anaye mlaani anajilaani kwani jamaa ni mkeeli na muwazi sana.

haa haaa magufuli hana doa eeh? subir madoa yake yawekwehadharani. ndani ya ccm kila mtu ni fisadi isipokuwa kiwango...
 
Dr Akili

Asa sisi hayo ya chini chini sisi hatukuyasikia km wananchi, tulichokisikia lissu pale jukwaani ni kwamba pindi wafugaji wanauliwa magufuli hakusimama km msukuma kuwatetea bali alisimama km kabila la ccm n kweli hakupanua kinywa chake kukemea huu unyama, pia kwny opareshen kimbunga magufuli hakusimama kutetea waliokuwa wakiaangamizwa.

Hivyo usitake kuibua mambo ambayo hayapo kwny uelewa wa umma kwa kulazimisha kimejikita kwny kambi ya upinzani ingali tumesikia wakikemea ukabila hadharani? Tuweni wamoja usitoe maada kutaka kututenganisha watanzania. Mi msukuma lakin cjawahi kusimama au kuandika juu ya hujuma zinazotolewa kwa magufuli, je mimi sio mkereketwa wa kabila langu? Tusijnge hoja kwa kutumia ukabila ata ukiongea vingne vikiwa na tija tutakusikiliza tu!
 
Last edited by a moderator:
Kweli cdm wanatapa tapa. Mi ningeshauri watulie kuimarisha majimbo ya ubunge urais waachane nao. Magufuli hana doa. Kila anaye mlaani anajilaani kwani jamaa ni mkeeli na muwazi sana.

Ambacho watu wa ccm mnashindwa kuelewa ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi wa nchi hii ikiwamo mimi hatujafungamana na wala si wanachama wa chama chochote, mtu akisimama kukemea mabaya ya ccm mwaanza kuwaka cdm watakoma mara hii, mbona mwatuvika vyeo ambavyo hatuna?

Naomba uelewe watanzania wengi hatuna vyama ila huunga mkono wale wanaoonesha njia na neema ya kuleta matumaini na pia uelewe kuwa zile fikra za kwamba ccm watatawala milele kwny kizazi changu tuliofumbuliwa macho na shul za kata japo elimu yetu sio bora ni ngumu, tarajia mabadiliko na uwe tayari kuyapokea ata km sio sasa inaweza kuwa badae ndani ya leo.
 
Mkuu Paschal hao wanaoeneza habari kuwa Tundu Lissu katika hotuba yake ya Mwanza ameendekeza ukabila, hao ni Propagandists wakubwa ambao humu JF huwa 'tumewabatiza' kama Buku 7 Lumumba Sports Club.

Kwa hiyo hao wasikutie hofu, kwa kuwa kwao wao kuweza ku-attend 'msalani' ni lazima wapost vitu humu jamvini vya kuukandia upinzani hata kama vitu hivyo vitakuwa ni fabricated stories.

Lengo kuu ni kupata per day yao pale Lumumba ili mkono uweze kwenda kinywani.

Asa watakuwa hawajielewe hicho wakipatacho lumumba hajuia ndo kinasababisha kuleta uongozi ambao sukari haikawii kupanda madukani na kuzidi kudumaza huduma takribani zote zinazomlenga mwananchi?

Tanzania cjui nani alofunga mboni na bongo zetu na maskio yetu tukashindwa kuona yale yanayotendeka huku tukisahau kila tunachosikia na kuona huku tukiendelea kutamani mabadiliko kwa wale wale walotutuo kwny chai ya bure mahotelini.
 
CCM ni kama mshipa mkuu wa fahamu ( SPINAL CORD)ktk taifa hili ikidhurika tu taifa hili linakoelekea Mungu atusaidie.

Upinzani bado sana wajifunze kwa ccm kuongoza

MTANZANIA WALEO SIO WAJANA.
TANZANIA YALEO SIO JUZI.
TUNAELEWA NA TUNAUFAHAMU.
 
Dr Akili

Hivi huku ndani ni kwanini watu wanatabia ya kujiita vitu wasivyo??? Yaani opposite kabisa. Huyu ni doctor BRAINLESS. Hakuna sehemu yeyote TUNDU LISSU alisema statement yenye maana hiyo, let me re-iterate, HAKUNA SEHEMU YEYOTE TUNDU LISSU ALISEMA STATEMENT YENYE MAANA HIYO!!!! Alichosema ni kwamba, alipokuwa akitembelea maeneo tofauti kagera, chato na kadhalika, watu wakawa wanachanganya kabila ya JOHN MAGUFULI, Wengine wanasema mzinza, wengine msubi, wengine msukuma, yeye akawasahihisha na kuwaambia KABILA LA MAGUFULI SIYO MFIPA, SIYO MSUKUMA, SIYO MSUBI ILA NI M-CCM, KWASABABU HATA WAKATI WA UWIZI WA EPA, ESCROW, RICHMOND YEYE HAKUSIMAMA KUTETEA WASUKUMA ,WAFIPA WALA WA SUBI DHIDI YA UWIZI HUO ILA ALINYUTI KWA MAANA HIYO AKITETEA KABILA LAKE WACCM. Acha kupotosha uma, kweli kuna watu wabaya duniani,wewe ungepewa sura inayofanana na ubaya wako ungekuwa makalio ya nyani. Ukabila kwa political leader ni very serious offense huwezi kumsingizia mtu kitu kama hicho kwasababu wa afrika tumeona first hand madhara ya ukabila. The Rwanda genocide and what note. Acha huo ujinga wewe a.k.a dr akili, itumie akili yako kufikiri mara mbili haitaisha betrii
 
Last edited by a moderator:
Ambaye hakuelewa ana shida zake.

Lissu alieleza vizuri sana kuwa haijalishi Magufuli kuwa kabila lolote lile, haijalishi awe Mzinza, Msubi, Msukuma au kabila jingine. Muhimu zaidi ni matendo yake.

Akasema 'kabila' la Magufuli ni CCM ambayo serikali yake ikihusika na kashfa za kudidimiza uchumi kama EPA, Buzwagi, Richmond, uchotwaji pesa za Escrow, viongozi kuuziana nyumba za umma kwa bei chee.

Akasema kuwa 'kabila' la Magufuli ni sawa na la Kikwete, Chenge, Sitta, Makinda.
 
kabila la Magufuli ni Mccm , tena ukoo wake ni wa uuzwaji wa nyumba za Serikali.
Samia Suluhu kabila lake ni Mccm, ukoo wa bunge la katiba.
 
Kabila lao ni uzalendo

kabila la ccm lina koo kuu zifiatazo.
1. EPA
2. BUZWAGI
3. KAGODA
4. MEREMETA
5. OPERESHENI TOKOMEZA
6. UTOROSHWAJI WA TWIGA
7. RICHMOND
8. UUZWAJI NYUMBA ZA SERIKALI( HUU NI UKOO WA MAGUFULI)
9. BUNGE LA KATIBA( UKOO WA SAMIA SULUHU)
10. UKOO WA PEMBE ZA NDOVU aka UJANGILI( HUU NI UKOO WA KATIBU WAO MKUU KINANA)
10. KUNA UKOO MKUBWA SANA TENA MPYAAA UNAOITWA ESCROW.

koo zingine ongezea wewe.
 
Kabila la Magufuli ni ccm, hiki ndicho tulichokielewa Na wala hakina ubishi
 
kabila la ccm lina koo kuu zifiatazo.
1. EPA
2. BUZWAGI
3. KAGODA
4. MEREMETA
5. OPERESHENI TOKOMEZA
6. UTOROSHWAJI WA TWIGA
7. RICHMOND
8. UUZWAJI NYUMBA ZA SERIKALI( HUU NI UKOO WA MAGUFULI)
9. BUNGE LA KATIBA( UKOO WA SAMIA SULUHU)
10. UKOO WA PEMBE ZA NDOVU aka UJANGILI( HUU NI UKOO WA KATIBU WAO MKUU KINANA)
10. KUNA UKOO MKUBWA SANA TENA MPYAAA UNAOITWA ESCROW.

koo zingine ongezea wewe.

Hahahaaa...hatare
 
Dr Akili

Wewe ni kati ya watu wenye uelewa mdogo sana wa kupambanua mambo. Lissu anaposema Magufuli kabila lake siyo Msukuma, mzinza wala Msubi ila kabila lake ni CCM. Watu waelewa nanaelewa kuwa CCM ni kabila mmoja na ukabila wao ni ufisadi. Hivyo watu wa mwanza wasimchague kwa sababu ya mahali anapotokea bali waangalie Chama anachotokea yaani CCM. Mfumo w CCM ni ufisadi na kulindana
 
Last edited by a moderator:
Wanaosifia utendaji wa magufuli wanampima kwa barabara za lami. Lakini ndiyo hizi barabara zinazojengwa chini ya kiwango kila iitwapo leo.

Kwa sababu ya kujengwa chini ya kiwango tumepoteza ndugu zetu wengi kwa ubovu wa barabara. Kwa mfano, ajali ya pale Mafinga iliyoangamiza wengi ni kwa sababu ya ubovu wa barabara ambazo zimejengwa hivi karibuni.

Sifa ambazo ni za kijinga anazopata Magufuli ni barabara ikiishajengwa kufoka kwamba ipo chini ya kiwango. Swali ni anakuwa wapi mpaka asubiri zimalizike ndipo atafute TBC kwenda kututangazia kwamba jamani barabara hii chini ya kiwango, na nyingine nanyingine???.
kanda ya ziwa hakuna mchaga atakae shinda ubunge.
 
RATIBA%2BYA%2BUCHUKUAJI%2BFOMO%2B2015-page-001%2B(1).jpg

HII ITAKUSAIDIA DR AKILI

Wote wenye akili zao wanajua fika kuwa kampeni za urais zilishaanza tangia ndani ya bunge la bajeti, kwenye utia nia, utambulisho na kadhalika. Wewe unasubili kipenga cha NEC? Ikalaga baho! CUF walishatangaza mgombea wao, CDM walikuwa wamtangaze mgombea wao pale kwenye mkutano wa Mwanza wakasita kwa sababu/taarifa wanazozijua wao - kuna tetesi yule mkubwa wa akina Lembeli wanamsubili atoe maamuzi magumu, na vyama vingi tu vya upinzani vilishatoa wagombea wao ngazi za Urais. Tanzania ina vyama vya upinzani zaidi ya ishirini kama ulikuwa hujui.
 
Tundu lisu anajalibu kutumia hoja za ukabila ili Magufuli asikubalike. Lakini ukweli ni kwamba sisi tunao mjua Magufuli ndio tusema. Magufuli ni mwenzetu na ni mtanzania halisi. Hoja zao hàziwezi kutubabaisha hata kidogo. Mbona wenyewe mambo yao ya kujikopesha hela ndani ya chama na kukigeuza kuwa saccos hawayasemi? Au taratibu zao za chama zinaruhusu hivo?
 
Ambacho watu wa ccm mnashindwa kuelewa ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi wa nchi hii ikiwamo mimi hatujafungamana na wala si wanachama wa chama chochote, mtu akisimama kukemea mabaya ya ccm mwaanza kuwaka cdm watakoma mara hii, mbona mwatuvika vyeo ambavyo hatuna?

Naomba uelewe watanzania wengi hatuna vyama ila huunga mkono wale wanaoonesha njia na neema ya kuleta matumaini na pia uelewe kuwa zile fikra za kwamba ccm watatawala milele kwny kizazi changu tuliofumbuliwa macho na shul za kata japo elimu yetu sio bora ni ngumu, tarajia mabadiliko na uwe tayari kuyapokea ata km sio sasa inaweza kuwa badae ndani ya leo.
Niahidi kuwa utampigia kura ya ndiyo Mh. Dr. Magufuli!
 
Back
Top Bottom