Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu kutumia hoja za ukabila ktk kampeni za Urais ni halali?

Lisu nilimsikiliza mwanzo mwisho ni kejeli tu,na kuonyesha hofu aliyo nayo kwa Magufuli muda wote aliopewa hakuzungumza nini chama chake kinataka kuwafanyia Watanzania kuelekea uchaguzi mkuu! Alijikita kumtaja mara nyingi sana tena akimtambulisha kwa wanachadema na kutumia Air time kumnadi mgombea wa CCM bila kujijua kweli Lisu kwa mara ya kapote njia!

Umeongea ukweli mtupu,UKAWA wamekosa sehemu ya kumchafua Magufuri badala yake wanambambikia zigo la uchafu wote wa CCM😀😀😀😀
 
Wanaosifia utendaji wa magufuli wanampima kwa barabara za lami. Lakini ndiyo hizi barabara zinazojengwa chini ya kiwango kila iitwapo leo.

Kwa sababu ya kujengwa chini ya kiwango tumepoteza ndugu zetu wengi kwa ubovu wa barabara. Kwa mfano, ajali ya pale Mafinga iliyoangamiza wengi ni kwa sababu ya ubovu wa barabara ambazo zimejengwa hivi karibuni.

Sifa ambazo ni za kijinga anazopata Magufuli ni barabara ikiishajengwa kufoka kwamba ipo chini ya kiwango. Swali ni anakuwa wapi mpaka asubiri zimalizike ndipo atafute TBC kwenda kututangazia kwamba jamani barabara hii chini ya kiwango, na nyingine nanyingine???.
 
mtoa mada ni mnafiki mzandiki, ni mtu hatari usiefaa katika jamii yetu. mtu mwenye, kubuni mabaya, mwenye fikra potofu kila wakati, mwenye kutugombanisha watanzania tunaopendana wakati wote. mchochezi usie tumia akili hata kidogo, kafie mbali kule.
 
Magufuli hana maono ya mbali kabisa jamani, tuseme kweli. Miaka michache iliyopita ni Magufuli huyu huyu ambaye alikuwa anapanua barabara ya Morogoro Road Dar. Barabara imegharimu mabilioni ya pesa mpaka sasa tuna madeni. Hata miaka 10 haijapita ni yeye Magufuli amefumua hii barabara kwa mradi wa yaitwayo mabasi yaendayo kasi.

Mabilioni yamepotea kabisa jambo ambalo kama mtu wa kuona mbali miaka michache tu nyuma angekuwa ameona kwamba barabara zinazojengwa haziwezi kukidhi mahitaji.
 
Dr Akili

CCM ndiyo wanataka kutumia hoja ya ukabila, Tundu lissu alichosema ,kama ulimwelewa ni kwamba ,Magufuli hata awe kabila gani, ni ccm yule yule with all Tabia za kiccm kama, Wizi, ufisadi Rushwa pamoja na kuwakandamiza wananchi kwa manufaa ya wachache. TUMIA UBONGO KUFIKIRI Ndugu ile ni kauli za kifasihi.....
 
Last edited by a moderator:
Wanaosifia utendaji wa magufuli wanampima kwa barabara za lami. Lakini ndiyo hizi barabara zinazojengwa chini ya kiwango kila iitwapo leo.

Kwa sababu ya kujengwa chini ya kiwango tumepoteza ndugu zetu wengi kwa ubovu wa barabara. Kwa mfano, ajali ya pale Mafinga iliyoangamiza wengi ni kwa sababu ya ubovu wa barabara ambazo zimejengwa hivi karibuni.

Sifa ambazo ni za kijinga anazopata Magufuli ni barabara ikiishajengwa kufoka kwamba ipo chini ya kiwango. Swali ni anakuwa wapi mpaka asubiri zimalizike ndipo atafute TBC kwenda kututangazia kwamba jamani barabara hii chini ya kiwango, na nyingine nanyingine???.
 
Lisu nilimsikiliza mwanzo mwisho ni kejeli tu,na kuonyesha hofu aliyo nayo kwa Magufuli muda wote aliopewa hakuzungumza nini chama chake kinataka kuwafanyia Watanzania kuelekea uchaguzi mkuu! Alijikita kumtaja mara nyingi sana tena akimtambulisha kwa wanachadema na kutumia Air time kumnadi mgombea wa CCM bila kujijua kweli Lisu kwa mara ya kapote njia!

Sasa wewe na Lisu nani mwenye akili timamu?upotee njia wewe alafu useme lisu ndo kapotea!hao vibaraka wenzio wameshatwambia wanachotaka kutufanyia ss watanzania?au ndo mnataka kuendelea kufisadi hadi na viwiliwili vyetu?
 
Tundu si nasikia ana kale kagonjwa ka kupelekwa Milembe. Utatumiaje dakika 35 unazungumzia ukabila wa Magufuri mara si msukuma, si mzinza si msubi nani alitaka kujua upuuzi huo. Mbona wewe hujisemi ni mdudu gani toka msitu upi!!! Halafu kuna mburura humu wanatetea ujinga. Hata huyo sijui Prof gani amabaye kasoma wala hakuelewek, anakuja na ngonjela dhaifu hazina ushahidi na mburura kama kawaida wanakenua meno. Hii taabu hii.Lissu Unaleta hofu katikati ya kandamnasi ili uonewe huruma. KWISHA KWISHA KABISA. AKA KAJITU NI HATARI KATENGWE KAMA KALIVYO
 
CCM ndiyo wanataka kutumia hoja ya ukabila, Tundu lissu alichosema ,kama ulimwelewa ni kwamba ,Magufuli hata awe kabila gani, ni ccm yule yule with all Tabia za kiccm kama, Wizi, ufisadi Rushwa pamoja na kuwakandamiza wananchi kwa manufaa ya wachache. TUMIA UBONGO KUFIKIRI Ndugu ile ni kauli za kifasihi.....

Umetumia Akili Nyingi Kumwelimisha Japo Inachosha!
 
Dr Akili kampeni za urais zimeshaanza?Ni Magufuli na nani wanapambana kwenye kiti cha Urais?

Wote wenye akili zao wanajua fika kuwa kampeni za urais zilishaanza tangia ndani ya bunge la bajeti, kwenye utia nia, utambulisho na kadhalika. Wewe unasubili kipenga cha NEC? Ikalaga baho! CUF walishatangaza mgombea wao, CDM walikuwa wamtangaze mgombea wao pale kwenye mkutano wa Mwanza wakasita kwa sababu/taarifa wanazozijua wao - kuna tetesi yule mkubwa wa akina Lembeli wanamsubili atoe maamuzi magumu, na vyama vingi tu vya upinzani vilishatoa wagombea wao ngazi za Urais. Tanzania ina vyama vya upinzani zaidi ya ishirini kama ulikuwa hujui.
 
Mbowe, Slaa, Mnyika, Tundu, Sugu hawa kabila lao ni lipi?

kabila lao WABINAFSI.
Humu kikipostiwa chochote cha chadema hata kiwe kibaya kitakuwa kizuri, kikipostiwa cha ccm hata kama ni kizuri kitavurugwa kionekane kibaya, sasa huu ni ubinafsi na ndio kabila la wanachadema,
 
Tundu si nasikia ana kale kagonjwa ka kupelekwa Milembe. Utatumiaje dakika 35 unazungumzia ukabila wa Magufuri mara si msukuma, si mzinza si msubi nani alitaka kujua upuuzi huo. Mbona wewe hujisemi ni mdudu gani toka msitu upi!!! Halafu kuna mburura humu wanatetea ujinga. Hata huyo sijui Prof gani amabaye kasoma wala hakuelewek, anakuja na ngonjela dhaifu hazina ushahidi na mburura kama kawaida wanakenua meno. Hii taabu hii.Lissu Unaleta hofu katikati ya kandamnasi ili uonewe huruma. KWISHA KWISHA KABISA. AKA KAJITU NI HATARI KATENGWE KAMA KALIVYO

mie mwenyewe nimeshangaa, halafu jamaa wanahangaika magufuli,, magufuli............lenyewe hata halitaji mtu linasema maendeleo hayana chama
 
Km ulifuatilia alisema magufuli hajasimama km mmoja wa hayo makabila bali kasimama kama ni miongoni mwa kabila la ccm na si kama ulivyotoa maada. Usipotoshe umma kama hukuelewa ungeuliza nini alichosema kwa walioelewa wangekusaidia kuliko kudakia kutoa maana ukiwa hujui ata kipi kilichosemwa.
Mkuu Paschal hao wanaoeneza habari kuwa Tundu Lissu katika hotuba yake ya Mwanza ameendekeza ukabila, hao ni Propagandists wakubwa ambao humu JF huwa 'tumewabatiza' kama Buku 7 Lumumba Sports Club.

Kwa hiyo hao wasikutie hofu, kwa kuwa kwao wao kuweza ku-attend 'msalani' ni lazima wapost vitu humu jamvini vya kuukandia upinzani hata kama vitu hivyo vitakuwa ni fabricated stories.

Lengo kuu ni kupata per day yao pale Lumumba ili mkono uweze kwenda kinywani.
 
Km ulifuatilia alisema magufuli hajasimama km mmoja wa hayo makabila bali kasimama kama ni miongoni mwa kabila la ccm na si kama ulivyotoa maada. Usipotoshe umma kama hukuelewa ungeuliza nini alichosema kwa walioelewa wangekusaidia kuliko kudakia kutoa maana ukiwa hujui ata kipi kilichosemwa.

Nimefuatitilia mikutano yote ya Tundu Lisu aliyofanya huko Kahama, Geita, Katolo na Mwanza. Katika mikutano yake hiyo hoja yake kuu imekuwa Magufuli si Msukuma: mama yake ni Mzinza na baba yake ni Msubi, kwamba Wasukuma wasidanganyike kwamba Magufuli ni msukuma mwenzao. Baada ya wakubwa wake (Mbowe na Slaa) kumtaadhalisha madhara ya dhana yake hiyo ndipo kaongeza kabila la CCM. Kwa hiyo kwa akili yake sasa ni kwamba kuna makabila ya CCM, CHADEMA, CUF, UKAWA na kadhalika. Ninachosema ni kwamba kuleta dhana za ukabila (iwe wa CCM au CDM) ni kuleta / kuchochea janga la kitaifa na hatua kali za kisheria zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya mtu huyo.

Kila mtu amemsikia pale Mwanza (despite ITV kujitahidi kukatakata mawasiliano hayo): Alianza kuwasalimia watu wa Mwanza kikabila kwa broken kisukuma! Kwa akili yake hajui kwamba ni asilimia 50% tu ya wakazi wa Mwanza ni Wasukuma kama ilivyo Dar es Salaam ambayo nayo 50% ni Wasukuma/ Wanya- Mwezi! Hajui kwamba Wasukuma / Wanyamwezi siyo kabila bali ni zaidi ya kabila - it is a gene or species in the scientific language. Strains za hii species ni watu million 18 Tanzania. Wanajulikana kwa majina ya makabila mbali mbali kama: Wanyatuzu, Wanamweli, Wasubi, Wadakama, Wazinza, Bahehe, Bagika, Banyakyusa, Bagalu, Bapemba, Bakwere, Bagogo, Banguja, Bamakonde, Banyaramba, Bangazija, Bapare, Bazigua etc etc. Wako kila mahali Tanzania bara na visiwani. Huko Singiga kuna wakina Mwigulu Nchemba, Bagamoyo kuna wakina Kikwete, Pemba kuna akina Shalifu nk.
 
CCM imeingiwa hofu, Magufuli kuwa shughuli

KUNA hofu imetanda ndani ya CCM; hofu ambayo inajaribu kufichwa mapema kwani kama mambo hayatobadilika ndani ya miezi hii mitatu hivi iliyobakia kabla ya Uchaguzi Mkuu basi chama hiki kikongwe zaidi nchini kinaweza kujikuta kikipumzishwa kutoka madarakani kwa nguvu. Dalili ya hofu hii imeonekana baada ya kutangazwa kwa mgombea wao wa kiti cha Urais Dk. John Pombe Magufuli.

Mojawapo ya mambo ambayo yametokea baada ya Magufuli kutangazwa ni kauli za kuwa yeye “anakubalika na anachagulika”. CCM imetaka kuliaminisha taifa kuwa Magufuli siyo tu anajulikana kwa utendaji kazi wake, na kuwa wananchi wengi wanampenda na wanaweza kumchagua. Kiasi kwamba wametaka watu waamini kuwa Magufuli ni Rais anayesubiria (President in waiting). Kwamba, upinzani hauna nafasi hata kidogo ya kumnyang’anya uwezekano huo.

Ukweli ni kuwa matendo ya CCM hayaoneshi kujiamini huku. Kama kweli CCM inaamini Magufuli anajulikana na kazi zake zinakubalika nchi nzima kwa nini juhudi kubwa sana inajaribu kufanywa ya “kumtambulisha”. Unamtambulisha vipi mtu ambaye tayari unaamini anajulikana, kufahamika na kukubalika? Ukiangalia utaona kuwa CCM inataka kumtumia Magufuli kukibeba chama; tatizo ni kuwa Magufuli mwenyewe – ukiondoa kukariri kwake takwimu mbalimbali – utendaji kazi wake una shaka. Tayari wizara ambayo amekalia imeshagubikwa na kashfa lukuki na hili peke yake lingetosha hata kumchafua. Akija mgombea mzuri kutoka upinzani na akajizibu hizi takwimu za Magufuli, basi Magufuli na CCM iko matatani. Yote haya yanatosha kufanya watu wajiulize mara mbili kama kweli Magufuli hatokuwa shughuli kweli kweli.

CCM imepasuka, rekodi yake mbovu, na upinzani ukimsimamisha mgombea makini, Magufuli ataweza vipi kushinda? Njia pekee ya kushinda katika mazingira ya namna hiyo ni matumizi makubwa ya nguvu, vyombo vya dola na hata kuliingiza jeshi katika siasa kama walivyofanya chini ya Jenerali Shimbo mwaka 2010. Vyovyote vile ilivyo hata hivyo kuna hofu imetanda kwa CCM; hofu kama vile wingu zito la mvua lenye dalili ya radi na ngurumo. CCM hawajui sasa wafanye nini zaidi ya kuombea Magufuli aweze kuwaokoa. Akishindwa je Hili ndilo swali la kuogopesha zaidi kwa kila mwana CCM

Chanzo: Raia Mwema (22, July 2015)

Hilo gazeti ni la kipuuzi linachochea chuki miongoni mwa wananchi. Hivi mmiliki wake si ulimwengu? Ambaye alikosana na mkapa? Nadhani ulimwengu itabidi arudi kwao burundi soon
 
Dr Akili

Kweli cdm wanatapa tapa. Mi ningeshauri watulie kuimarisha majimbo ya ubunge urais waachane nao. Magufuli hana doa. Kila anaye mlaani anajilaani kwani jamaa ni mkeeli na muwazi sana.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom