Tundu Lissu is talk of the Town au kwa lugha yetu Tundu Lissu ndiye Habari ya Mjini kwa Sasa.
Mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu ameteka nyoyo za Watanzania na ukweli kabisa bila kuongeza chumvi Tundu Lissu ndiye mgombea wa Urais mwenye mvuto kuliko mgombea mwingine yeyote katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kiliomba kibali Cha kutumia Chopa kwa mgombea wake wa Urais ili iwe rahisi kuweza kufika maeneo yote ya kampeni kwa wakati.
Hata hivyo kwa makusudi Mgombea huyo wa Chadema amewekewa vigingi na mamlaka ili kumkwamisha kutumia Chopa hiyo kwa malengo yasiyofahamika.
Tundu Lissu na wasaidizi wake walishushwa pale Airport ya Dar na mamlaka ya Anga wakiwa wameshapanda helikopta hiyo kuelekea kwenye Mkutano wa Kampeni mkoa wa Pwani.Mpaka Leo takriban mwezi Sasa bado mgombea huyo hajaruhusiwa kutumia Chopa hiyo.
Hata hivyo Mungu ana makusudi yake Pamoja na njama za kumzuia Tundu Lissu kutumia Anga bado ameweza kuhutubia mikutano yote Kama inavyoonyesha kwenye ratiba.
Pili Lissu amekuwa akikutana na watu wengi zaidi anapotumia usafiri wa Barabara kwa kusimama njiani kusalimiana na Maelfu ya watu na kuwaachia ujumbe wa kuchagua #UhuruHakiNaMaendekeoYaWatu#
Lissu amekuwa akikaribishwa kwa maandamano makubwa ya Malaki kwa maelfu ya watu kilometa 10 mpaka 20 kabla ya kuingia viwanja vya mikutano na kusindikizwa umbali huo huo baada ya mikutano kitu kinacholeta hamasa kubwa kwani Ingekuwa anatumia Chopa isingewezekana.
Wachunguzi wa siasa wanasema hata Kama Watawala watamruhusu kutumia helikopta kwa siku zilizobaki asikubali Tena kwani kutumia gari Kuna manufaa zaidi na ujumbe wa mabadiliko unafika sehemu kubwa zaidi.
Mara baada ya Tundu Lissu kuzuiwa kutumia helikopta harakaharaka CCM walileta helikopta yao na kujigamba wao wataitumia chopa kwa sababu hakuna wa kuwazuia.
CCM walidhani kwa kula njama na CDM kuzuiwa kutumia Chopa Basi ilikuwa ni pigo kubwa kwa Lissu lakini imeonekana kinyume chake na Sasa wanatamani mgombea huyo wa CDM aruhusiwe kutumia Chopa ili asiweze kukutana na Malaki kwa mamilioni ya watu anaokutana nao mabarabarani wakati akisafiri kwa gari
Mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu ameteka nyoyo za Watanzania na ukweli kabisa bila kuongeza chumvi Tundu Lissu ndiye mgombea wa Urais mwenye mvuto kuliko mgombea mwingine yeyote katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kiliomba kibali Cha kutumia Chopa kwa mgombea wake wa Urais ili iwe rahisi kuweza kufika maeneo yote ya kampeni kwa wakati.
Hata hivyo kwa makusudi Mgombea huyo wa Chadema amewekewa vigingi na mamlaka ili kumkwamisha kutumia Chopa hiyo kwa malengo yasiyofahamika.
Tundu Lissu na wasaidizi wake walishushwa pale Airport ya Dar na mamlaka ya Anga wakiwa wameshapanda helikopta hiyo kuelekea kwenye Mkutano wa Kampeni mkoa wa Pwani.Mpaka Leo takriban mwezi Sasa bado mgombea huyo hajaruhusiwa kutumia Chopa hiyo.
Hata hivyo Mungu ana makusudi yake Pamoja na njama za kumzuia Tundu Lissu kutumia Anga bado ameweza kuhutubia mikutano yote Kama inavyoonyesha kwenye ratiba.
Pili Lissu amekuwa akikutana na watu wengi zaidi anapotumia usafiri wa Barabara kwa kusimama njiani kusalimiana na Maelfu ya watu na kuwaachia ujumbe wa kuchagua #UhuruHakiNaMaendekeoYaWatu#
Lissu amekuwa akikaribishwa kwa maandamano makubwa ya Malaki kwa maelfu ya watu kilometa 10 mpaka 20 kabla ya kuingia viwanja vya mikutano na kusindikizwa umbali huo huo baada ya mikutano kitu kinacholeta hamasa kubwa kwani Ingekuwa anatumia Chopa isingewezekana.
Wachunguzi wa siasa wanasema hata Kama Watawala watamruhusu kutumia helikopta kwa siku zilizobaki asikubali Tena kwani kutumia gari Kuna manufaa zaidi na ujumbe wa mabadiliko unafika sehemu kubwa zaidi.
Mara baada ya Tundu Lissu kuzuiwa kutumia helikopta harakaharaka CCM walileta helikopta yao na kujigamba wao wataitumia chopa kwa sababu hakuna wa kuwazuia.
CCM walidhani kwa kula njama na CDM kuzuiwa kutumia Chopa Basi ilikuwa ni pigo kubwa kwa Lissu lakini imeonekana kinyume chake na Sasa wanatamani mgombea huyo wa CDM aruhusiwe kutumia Chopa ili asiweze kukutana na Malaki kwa mamilioni ya watu anaokutana nao mabarabarani wakati akisafiri kwa gari