Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

mkuu utawapata wajinga tu kwa kumlisha maneno tundu lissu na kugeuza hoja zake ziwe za kumtusi mwalimu ukweli sisi twaujua alikuwa anawaambia hawa vilaza wanao geukageuka kwa ajili ya matumbo yao na familia zao hawa maccm wa sasa.
 
siku zote Tundu Lisu ni mlopokaji na asieweza kudhibiti hisia zake anaposhangiliwa anaondoa kabisa hadhi ya upinzani nchini. Na hili ndio tatiizo la upinzani, hawa jamaa hawana uzalendo, heshma wala miiko.

...hahahaaa mkuu umenichekesha kweli,kaa utulie alafu usome ulichoandika,unamaanisha uzalendo upo wapi sasa ? ..kwa ccm,na uadilifu ?..heshima..kama za mwigulu na nape za kusema wazee wafe..miiko, ?...usinikumbushe azimio la zanzibar...jipange upya,wenzako jasho linawatoka bungeni hoja zimewaishia...
 
Msimtumie Nyerere kama hirizi, hizo zilikuwa zama zake, kila utawala una mambo yake, siku hizi kuna semi zinadadilishwa kutokana na mazingira, samaki mmoja kioza wote wanaoza, samaki mmoja akioza mtoe mtupe wengine wakaushe. Aliyejuu mgoje chini siku hizi unamwekea ngazi au unatumia hata helikopta.
 
JULIUS NYERERE-Humanist,Politician ,and Thinker.-POLE SANA TUNDU LISU,HUNA HADHI YA KUMKEJELI BABA WA TAIFA,JIKITE KATIKA KUJENGA HOJA ZAKO TU,UTAELEWEKA.

Tuwe wakweli, je Mwl J.K Nyerere hakuzungumza/ kuandika kwenye gazeti tajwa 1968? Je mzee Jumbe hayakumkuta yaliyosemwa 1984? Ukweli utabaki ukweli tu. Kila mtu akiwa kama binadam anamapungufu yake. Halafu hata level ya ufaham na uchokonozi ni mkubwa enzi hizi kuliko zamani. Hivyo watu na viongozi wetu wanatakiwa wajitune kisaikolojia, kwani kadri siku zinavyoenda kizaz cha udadis kinaongezeka. Tutarajie udadis zaidi 10 years to come!
 
Huyu mganga njaa anaropoka kuwafurahisha MABWANA, lakini akumbuke kuna leo na kesho..........atapata hizo helkopta na nini.......lakini mwisho wake ni nini ?

Hapo tu alipo amebakiza muda mfupi sana ataanza kubeba makopo......sijui ni wangapi wanadhani jamaa yupo timamu upstairs.

Haya ni maneno ya kipuuzi puuzi. jitenge nayo tafadhali.
 
Kati ya wanasiasa ambao wanatakiwa kufungwa gavana ni Tundu lisu. Kwenye Bunge hili la katiba wajumbe wako pale Kujenga ni kubomoa. Kama kuna makosa na dosari katika muundo wa muungano huu ndo wakati wake na si kupokea waasisi wa muungano. Bila hao waasisi ambao waliusimamia muungano ambao hadi leo miaka 50 upo, si wa kubezwa hata Kidogo. Mchango wao ni mkubwa mno kulinganisha na Lisu ambao kazi yake ni kuponda na katika nchi mchango wake katika Kujenga umoja, mshikamano, kudumisha amani hatujauona zaidi ya siasa za uhasama na utengano

hivi kusema hati haipo na kama ni kweli haipo ni kutukana!,kwahiyo ndugu wewe ulitaka tuendelee kuongozwa kisanii mpaka lini?,au wewe ni mmoja wa wafaidika wa mfumo huu mbovu.hayo ndio malezi tuliyopewa na nchi yetu ukiwa mdadisi na kuhoji mambo unachukiwa na kupewa majina lukuki.
 
Alitukanwa Yesu, akatemewa mate adhabu yetu ikawa juu yake, sembuse Nyerere aliyeoza! Safi sana Lisu....
 
Hivi kwani Mwl Nyerere ni mungu mtu???sifa ya ukamilifu katika namna na hali zote ni Mungu mmoja pekee...alishawahi kusema yeye mwenyewe amefanya mema na ya kijinga ila cha ajabu mema yanaachwa na yanakumbatiwa ya kijinga....miongoni mwa ya kijinga ni kuiuwa Tanganyika na hili la muungano wa nchi mbili serikali mbili.....
 
sijapenda kauli ya lissu na kama hakuwa na hoja ya kushauri juu ya serikali tatu ajuwe amepoteza yeye na wenzake wote waliokuwa wanatoa ufafanuzi juu ya hoja ya serikali tatu, na kama wanafikiri kupigiwa makofi ndio kukubalika kwa hoja yao watambue kuwa wamejifunga goli.
 
sijapenda kauli ya lissu na kama hakuwa na hoja ya kushauri juu ya serikali tatu ajuwe amepoteza yeye na wenzake wote waliokuwa wanatoa ufafanuzi juu ya hoja ya serikali tatu, na kama wanafikiri kupigiwa makofi ndio kukubalika kwa hoja yao watambue kuwa wamejifunga goli.

mwenye akili timamu kama zako ndio anaweza kubaliana na ulichoandika.
 
Punguza udini utaeleweka. Lissu hajachambua mambo kidini bali kisiasa na ameeleweka vizuri sana. Sasa wewe na makuwadi wenzio mnapoanza kutuletea habari za Kariakoo na misikitini hamueleweki. Mnafiki mkubwa wewe.
would've been "shocked" had you spoken something different!
 
Nafikiri kilichopo sasa kwa haya tunayoyaona ni viini macho, Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika iliyoamua kujitenga na sasa inataka inataka mamlaka kamili, Hiyo ndiyo tafsiri itakayoondoa chokochoko maana aibu inakuja kwa wenye nchi. Sasa tutasema je kama hati za muungano hamna na miaka yote tupo pamoja?
 
Bwa mdogo hatofika mbali.Huyu kilaza hajui yeye asingekuwa bungeni kama sio kazi. Ya Mwalimu

Kivp ndugu?
Nyerere alikuta nchi ikiwa mikononi mwa Malkia ikiwa ktk kpindi cha mpito kusubiri uhuru kamili.
Haya tuliyonayo ni matunda ya kina Kinjekitile Ngwale, Chief Mkwawa, Mtemi Mirambo, Mangi Meli,Mangi Sina,Zumbe Minja na Machifu wengi waliopambana na Wakoloni na kusababisha harakati zilizosababisha Wakoloni kushindwa kutawala baada ya vita kuu ya pili.
Nyerere alitengeneza mifumo na kuunganisha watu.
Ukisema Elimu hata mwalimu Nyerere aliipata kwa wamisionary kama ilivyokuwa wakushukuriwa ni wamisionary walioelimisha baadhi ya watu.
Ndiyo maana Nyerere hakuweka rangi nyekundu kwenye bendera ya Tanganyika ilihali watu waliuwawa na kujinyonga pia.
 
Ona sasa, wakati wa Sheikh Hemed Bin Jumaa Bin Hemed Bakwata yake ilikuwa sio iliyoundwa na Nyerere, au hamkujua kuwa waislam wote hawako chini ya Bakwata hadi mtu wa Shinyanga alipochaguliwa kwa haki kuiongoza?

Bibi yako Faiza Foxy ndio ameenda mbali zaidi kwa kuweka dharau kuwa Mh Sitta hajakutana na kiongozi wa Waislam, anadai Sitta alikutana na Pengo peke yake, kukutana na Sheikh Simba ni sawa na kutokutana na mtu. Acheni dharau zenu nyie watu wa pwani. Ni sawa na mzee wenu mwingine Mohamed Said anayedai kuwa uhuru wa Tanganyika uliletwa na kikundi fulani cha ma Alwatan wa pale Kariakoo,,, watu wa pwani mnajiskia sana nyie...
Nani kakwambia Waislam walikuwa wanaikubali Bakwata sababu ya Mufti Hemed Bin Jumaa?
Tarehe 19 Desemba, 1968 serikali kama vile imegutushwa na taarifa ya Kwikima, iliipa BAKWATA Cerificate of Exemption na kuifungia EAMWS.[SUP]72[/SUP] Waziri wa Mambo ya Ndani Said Ali Maswanya kwa niaba ya serikali alitoa taarifa fupi:
Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kuamriwa na Rais anatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[SUP]73[/SUP]
Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Julus Nyerere, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao. Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo hilo.
Viongozi wa EAMWS waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS. Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama. Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza. Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali ya Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam. Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA. Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe. Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu. BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa. Hivi ndivyo halikadhalika moto wa Waislam uliowashwa kwa kupatikana kwa uhuru waliopigania hadi ukapatikana ulivyokufa. Moto huu ulikuja ukawaka tena, lakini hiki ni kisa kingine. Insha Allah Mwenyezi Mungu akipenda tutakuja kukieleza.

Huu ndiyo ukawa mwisho wa kile kilichokuwa kikijulikana kama mgogoro wa Waislam ulivyomalizika. Mgogoro ambao ulianza pale mwalimu wa shule ya msingi asiyefahamika na yeyote alipofanya maandamano katika mitaa ya Bukoba akimuunga mkono Julius Nyerere na Azimio lake la Arusha na ukaishia kwa mwalimu huyu akiwa na nafasi juu katika jumuiya ya Kiislam ambayo ilikuwa ikichukiza machoni mwa Waislam. Mwalimu huyu ambae sasa amekuwa Makamu Katibu Mkuu wa BAKWATA alianza kazi yake kwa kuwashutua Waislam. Katika mkutano wa waandishi wa habari Adam Nasibu aliiomba TANU na ASP kujikinga na watu wanaohujumu umoja wa nchi kupitia dini. Akaendelea na kusema kuwa BAKWATA ni sawa na Baraza la Kikristo la Tanzania. [SUP]74[/SUP] Kwa kuwa Waislam walinyimwa fursa ya kujadili "mgogoro' hivi sasa kilichobaki na dhana tu, kuwa nini kingelitokea endapo wangeliruhusiwa kufanya mkutano ule ulioitishwa na EAMWS. Waislam wa Bukoba ambao ilitaarifiwa kuwa walifanya maandamano kuunga mkono Azimio la Arusha hawakutayarisha maandamano ya kuunga mkono BAKWATA. Dar es Salaam na katika miji mingi ya Tanzania, neno BAKWATA halina tofauti na tusi. Kumuita Muislam kuwa yeye ni mwanachama wa BAKWATA ni sawa na kumuita Mkristo mfuasi wa Yuda Iscariot, aliyemsaliti Yesu kwa vipande thelathini vya fedha.
 
Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost
He's so naive. Anapaswa kufahamu kwenye siasa hakuna `ukweli' udumuo na hali kadhalika uongo.
 
Back
Top Bottom