Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu


Duuh! Leo kweli hapa kimenuka!?

Mkuu mpaka weye umeamua kushirikiana na Tundu Lissu kuivua nguo maiti ya Baba wa Taifa!¿ Daah¡

Tafadhali kipata fursa Mkuu...tuwekee picha/vivuli hapa vya kumbukumbu za Baba wa Taifa na pia Muheshimiwa Tundu Lissu!

Ahsanta.
 
mi naona Ni vizur kila mtu ajibebe mzigo wake,,,, hawa wa Zanzibar so watu wazuri kabisa wala,,, he mnamfahamu john okello,, mganda aliyepigania mapinduzi ya Zanzibar,,, yeye ndiye chanzo had Zanzibar walisucceed revolution but after revolution,,,,,,,,
 
Nyerere na mapungufu yake yote bado anabaki LEGEND mbele ya macho ya Wabongo hata kama Tundu lisu au Faiza Fozzy wakichonga hadi pumzi yao ya mwisho.
 

Ninakubaliana na wewe 100% kwamba Nyerere alikuwa Rais mbovu lakini lazima ukubali jamaa alikuwa mjanja kwenye ku manipulate watu. Hamna mtu/kiongozi hapa TZ hadi leo amefanikiwa ku influence watu kama Nyerere naamini angekuwepo sasa hata huyo (Mtundu) Lisu hizo hoja zake angezifanya zionekane carbage.
 

Nimeuliza maswali mawili humu JF sijapata jibu.

1) Kwanini muda mfupi tu kabla ya Nyerere kung'atuka Benki Kuu ya Tanzania ilichomwa moto?

Mzee Mwinyi alipochukuwa madaraka hakukuta senti tano ya kigeni, peupe peee. Rejea hotuba ya Mzee Mwinyi ya "Mikuki Miwili", nimeitafuta mtandaoni sijaipata, imefichwa kama ilivyofichwa hati ya Muungano wa Karume na Nyerere.

2) Kwanini muda mfupi tu kabla ya Nyerere kung'atuka Wizara ya Mambo ya ndani ilichomwa moto?
 

Hakuwa na ujanja, alikuwa ni dikteta katili na haambiliki, ukimpinga amma unapotea amma unashughulikiwa kama alivyofanyiwa Aboud Jumbe, Kassim Hanga, Wolfgan Dourado, Abeid Karume na wengine wengi. Ukiwa salama labda uikimbie nchi, kama Kambona na wengine wengi.
 
ndio maana tunasemaga CCM ni mazuzu tu! LiSSU aliongea facts na ushahidi juu ss mnakuja mazuzu wa ccm mnaanza kusema LISU alimtukana Nyerere! embu mfungulieni mashtaka basi muone km mtashinda hiyo kesi!?
 
Najua watu wanaandika tu kumdiss Lissu sababu ya mkate wa siku lakini moyoni wanakubali he is smart. Bravo Lissu keep going ulielimika ili uelimishe sio walioelimika kupotosha:frusty::frusty:

adi sasa vijana wengi sana waliokuwa wamenyeshwa maji ya bendera ya magamba sasa wametapika na wamejivua magamba lissu amewaelimisha sana 😛eace:
 
ndio maana tunasemaga CCM ni mazuzu tu! LiSSU aliongea facts na ushahidi juu ss mnakuja mazuzu wa ccm mnaanza kusema LISU alimtukana Nyerere! embu mfungulieni mashtaka basi muone km mtashinda hiyo kesi!?

Mkuu,

Mbona shughuli ndo kwanza inaanza, khalaf weye wataka watu wakimbilie mahakamani!? Duuh!

Sasa,huo ushauri wako nafikiri utamfaa zaidi yule kilaza wa Kihehe...yaani mtoto wa nje ya ndoa wa Baba wa Taifa aka Yericko Nyerere!

Ahsanta.
 
Ng'wamapalala,

Uko wapi Mkuu!?

Au na weye waogopa kuitwa "mdini"!? Daah! Usijali hiyo Title imewekwa tu kwa ajili ya watu kama sisi,ambao wenye imani/dini tafauti na yule Baba wa Taifa!?

Acha kungia mitini Mkuu...umelianzisha njoo tuendelee kutoa dose hapa! Tumechoka kuishi na hawa misukule ya Nyerere ndani ya Taifa letu...wanatugharimu sana hawa vilaza!

Rudi jamvini Msukuma mtani wangu wa Usukumani!

Ahsanta sana.
 
Zipapa nani kakupa mamlaka ya kuzungumza kwaniaba ya watanzania.
 
adi sasa vijana wengi sana waliokuwa wamenyeshwa maji ya bendera ya magamba sasa wametapika na wamejivua magamba lissu amewaelimisha sana 😛eace:

Mkuu,

Kwa kifupi yule Tundu Lissu hajasema lolote/chochote kipya! Yaani aluchosema ni marejeo tu ya yaliyosemwa na Watanzania wengi mno tangia enzi zile za Nyerere na mpaka kesho!

Tafauti labda iliyopo....ni kwamba yule Lissu amewavua nguo vijana wake wa Bavicha na Chadema yoote...ambao wao ndo walokua wamejipa wajibu wa ufia Unyerere!

Kijana pekee wa Chadema, ambae labda kiduchu alikua na mitazamo/fikra tafauti na zile sera/siasa za kinyama ni yule ajiiate Ben Saanane!?

Kwahiyo kama pana somo unakhis labda limetolewa na huyo Lissu...basi ni kwa hao vilaza wa Ufipa aka Bavicha...kama vile msukule wa Kihehe Yericko Nyerere,Mag3 na wachovu wangine wa fikra!

Ahsanta.
 
Zipapa nani kakupa mamlaka ya kuzungumza kwaniaba ya watanzania.

Suali hili ndo nilomuuliza yule mfia Unyerere na mdini alokubuhu aka Mwanakijiji...weeks kadhaa zilopita, na akangia mitini mpaka kesho!? Daah!
 
Umepunguza CV ya Judge Joseph Sinde Warioba ongeza Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, Judge wa International Tribunal of Lawa of Sea Humburg Germany, Judge of East African Community, chairman of the Presidential Commission Against Government Corruption aka Warioba Commission

 
“Baada tu ya Nyerere kung`atuka Benki na Wizara zilivyochomwa moto“ Let say tunaachana na akili ya darasani na kuamua kutumia ya kuzaliwa. Kwa akili yako ya kuzaliwa unadhani ni kwanini alisubiri ang`atuke ndio aagize zichomwe moto?! Alikuwa na mamlaka gani tena juu ya mambo aliyokwisha kabidhi? Na kwanza una uhakika gani? Kama kweli ni yeye alifanya hivyo? Don't assume things, na pia try to feed us with something better and not these Pumbas of yours. You are really good kumpambania umtakaye aonekane yupo sahihi, ila Pambana kwa kutumia njia iliyosahihi. Usituchafulie wazee wetu maana hata wewe hutatufaa ikiwa hujali Feelings zetu WaTz kwa Ropoka Ropoka yako hii Ovyo.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Dah! kweli Ng'wamapalala nadhani upo sawa kwa kiasi fulani...

cc gombesugu
Mkuu, vipi tena!. Ukweli umekufikia!.

Itabidi unirudishie angalau heshima yangu kiduchu kwa kunipiga madongo bila kuuelewa ukweli ndani ya hoja!.

Kama ujuavyo, huu ni ukumbi la kupashana habari, kuelimishana na kulijenga taifa but remember Moliere once said, "A wise man is superior to any insults which can be put upon him, and the best reply to unseemly behavior is patience and moderation."
 
Mkuu wangu ndiyo ninaingia kwa sasa. Kama unavyofahamu tena, watoto lazima wavae na wapate chakula mezani. Nilikuwa niko kwenye shughuri za kutafuta visenti ili watoto waishi.

Kwa sasa najaribu kuyapitia mawazo na maoni ya wachangiaji.

Tuko wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…