Wanabodi,
Lakini kwa mwenendo na matamshi ya Tundu Lissu ya hivi karibuni kumhusu Magufuli, kwa maoni yangu, kwa hapa tulipo, ukimuondoa Zitto ambaye he looks a bit compromised, Tundu Lissu ndie mwanasiasa pekee wa upinzani aliyeonyesha angalau uwezo wa kuweza kumkabili mgombea wa CCM kwa Uchanguzi Mkuu wa 2020, Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwenye Uchaguzi huo wa 2020 na Magufuli ukapata pata angalau kaji joto joto cha uchaguzi, vinginevyo wapinzani wakimsimamisha mgombea mwingine yoyote, mgombea wa CCM, Dr John Pombe Joseph Magufuli, hahitaji kufanya kampeni yoyote, ni ushindi wa kishindo straight forward kwa kwenda mbele kama ameokota embe dodo bivu chini ya mti wa mwambe!.
Kwa jinsi nilivyomsikia Tundu Lissu na namna anavyoongea, then huyu Tundu Lissu ni typical yuko kama Magufuli type tena yeye ni zaidi ya Magufuli!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali