Tundu Lissu nenda taratibu, tumia hekima na busara kumaliza tofauti zako na Freeman Mbowe. Vinginevyo mnaiua CHADEMA

Tundu Lissu nenda taratibu, tumia hekima na busara kumaliza tofauti zako na Freeman Mbowe. Vinginevyo mnaiua CHADEMA

Mbona tofauti ziko kwenye mitandao tu!

Hapana ni tofauti ktk uhalisia wake kabisa japo Tundu Lissu huwa yuko very technical kila anapojaribu kueleza mambo yasiyo sawa ndani ya chama chao....

Na kwa wenye akili kupitia maelezo yake huweza kugundua moja kwa moja kuwa kuna makundi kinzani mawili ndani ya chama hicho, moja likienda na msimamo wa M/Kiti na jingine likiunga mkono msimamo wa M/M/kiti...

Hata hivyo, mimi tofauti kubwa ninayoiona kati ya hii miamba miwili ya siasa za vyama vilivyo nje ya serikali - opposition parties (i.e Freeman Mbowe & Tundu Lissu) ndani ya CHADEMA ni kuwa mmoja (TL) hana kifua cha mtu wa kufichaficha na kulealea mambo yasiyoenda sawa ndani ya taasisi...

Huyu nyeusi huisema ni nyeusi na sio bluu na koleo hulisema ni koleo na sio Kijiko kikubwa hadharani na popote...

Kwa mwenzie wa upande wa pili (FM), yeye ni aina ya wanasiasa wale wa kuuma na kupuliza huku waki - pet - peti na kubembeleza mbembeleza watu wakiamini kuwa "chama ni watu..."

Mara nyingi wanasiasa wa aina ya Freeman Mbowe huwa ni wanasiasa opportunists. Unaweza kuwa mbaya ndani ya chama lakini kama una maslahi fulani, hata ufanyeje utapetiwa petiwa tu. Lakini ukiwa mwanasiasa mzuri na ukaonekana uko kinyume na maslahi ya wanasiasa dizaini ya Freeman Mbowe, wanaweza kukufurusha asubuhi na mapema kabisa...!
 
Hapana ni tofauti ktk uhalisia wake kabisa japo Tundu Lissu huwa yuko very technical kila anapojaribu kueleza mambo yasiyo sawa ndani ya chama chao....

Na kwa wenye akili kupitia maelezo yake huweza kugundua moja kwa moja kuwa kuna makundi kinzani mawili ndani ya chama hicho, moja likienda na msimamo wa M/Kiti na jingine likiunga mkono msimamo wa M/M/kiti...

Hata hivyo, mimi tofauti kubwa ninayoiona kati ya hii miamba miwili ya siasa za vyama vilivyo nje ya serikali - opposition parties (i.e Freeman Mbowe & Tundu Lissu) ndani ya CHADEMA ni kuwa mmoja (TL) hana kifua cha mtu wa kufichaficha na kulealea mambo yasiyoenda sawa ndani ya taasisi...

Huyu nyeusi huisema ni nyeusi na sio bluu na koleo hulisema ni koleo na sio Kijiko kikubwa hadharani na popote...

Kwa mwenzie wa upande wa pili (FM), yeye ni aina ya wanasiasa wale wa kuuma na kupuliza huku waki - pet - peti na kubembeleza mbembeleza watu wakiamini kuwa "chama ni watu..."

Mara nyingi wanasiasa wa aina ya Freeman Mbowe huwa ni wanasiasa opportunists. Unaweza kuwa mbaya ndani ya chama lakini kama una maslahi fulani, hata ufanyeje utapetiwa petiwa tu. Lakini ukiwa mwanasiasa mzuri na ukaonekana uko kinyume na maslahi ya wanasiasa dizaini ya Freeman Mbowe, wanaweza kukufurusha asubuhi na mapema kabisa...!

Naona unaelezea tofauti za personality sio sera. Watu kutofautiana personality ni sawa kabisa hamuwezi kukubaliana kila kitu
 
Naona unaelezea tofauti za personality sio sera. Watu kutofautiana personality ni sawa kabisa hamuwezi kukubaliana kila kitu
Unaongelea kitu kimoja kilekile, yaani tofauti za kimitizamo inayotokana na kutokubaliana juu utekekezaji na uelekeo wa sera fulani ya chama ba inavyotendewa kazi...

Mfano sera za fedha za chama; zinavyopatikana na namna zinavyotoka na kutumika jambo ambalo linailetea shida kidogo CHADEMA na hii hutumiwa na wapinzani wao kama nyundo ya kuwapondea..

Kwa tofauti hizi za kimitizamo ya kisera ndani ya chama, obviously watu (wakiwemo viongozi) watatofautiana tu. Na namna kiongozi anavyozi - handle tofauti hizi na kuzielezea akiwa nje ya mifumo ya kichama ikiwemo vikao, moja kwa moja zita - expose personality ya mtu/kiongozi huyu huku nje....

Huu ndiyo msingi wa maelezo yangu hapo juu. Na ofcoz ndiyo msingi wa ushauri wangu kwa Tundu Lissu...

Na ndugu Kamundu, viongozi wanaongoza taasisi fulani huwa Kuna kitu kinaitwa "uwajibikaji wa pamoja (collective responsibility) bila kujali yamefanyika maamuzi sahihi au siyo sahihi..

Na kama kuna kiongozi anayeona kuwa hawezi kushiriki maamuzi ya namna fulani na wenzake, busara huelekeza kujitoa ktk maamuzi hayo kwa kuachia ngazi au kuachana na taasisi hiyo..

I know hiki anachokifanya TL ni kujaribu kuhakikisha taasisi hii (CHADEMA) inafanya maamuzi sahihi...

Lakini I know pia kuwa, kama hali hii itaendelea hivi, kuna hatari ya hawa watu kutengana na ikitokea na kwa hali ilivyo CHADEMA yaweza kukumbwa na msukosuko ambao haujawahi kutokea. Tundu Lissu si Dr Slaa wala Zito Kabwe wala Peter Msigwa...

CCM wako chobiz wanachochea mgogoro kwa nguvu sana. Hii colabo ya CHADEMA & Tundu Lissu & Freeman Mbowe hawaitaki na mataminio yao siku zote ni kuivuruga....

Wanasubiri uive kisha wapasue nazi...
 
Ukishaona imefika mahari watu ni wakubwa kuliko chama, ujue hapo hakuna chama kuna kikundi tu cha watu
 
Mimi The Palm Beach si mwanachama wa CHADEMA ila ni mpenzi na mfuasi wake na nakiunga mkono kwelikweli chama hiki...

Ni wazi kuwa Kuna mgogoro mkubwa kati ya Mwenyekiti Freeman Mbowe na Makamu Mwenyekiti wake Tundu Lissu ndani ya CHADEMA

Nitasikitika na kuumia sana kama chama hiki cha siasa kilicho tegemeo pekee la Watanganyika nacho kitafuata njia ya CUF, TLP na NCCR - MAGEUZI kujidhoofisha na kisha kwenda kujifia zake huko.

Na naona wazi kabisa, kazi hii ya kukisambaratisha chama hiki inafanywa na viongozi wenyewe kwa kujua au kutojua.

Mpaka hatua hii, haina shaka kuwa iko shida ndani ya CHADEMA hususani kwa viongozi wakuu wa chama. Ili kukiokoa chama hiki na kuhifadhi moto wake uliowashwa kwa miaka takribani 30 sasa usizimike ni lazima ifanyike intervention ya haraka kuzuia hali hii isifikie point of no return.

Press Conference ya Tundu Lissu huko Singida leo imethibitisha shaka yangu hii.

Kila alichoki - address kule Singida mbele ya waandishi wa habari kuhusu uchaguzi wa serikali za vijiji na mitaa hakina shida, ni kizuri na ni kweli hali ndivyo ilivyo

Lakini mwishoni alipoulizwa swali na waandishi wa habari kama hiyo ni kauli ya chama ama la na yeye kujibu kuwa, kila alichokisema hapo ni cha yeye Tundu Lissu na sio kauli ya chama na kwamba baadaye ndio atapeleka hoja hizo ndani ya chama na kushinikiza ziwe ni kauli rasmi ya chama, nikawa shocked kidogo na kuliona tatizo hili ninalolisema hapa kwa uwazi kabisa...

Hii ya Singida ni mwendelezo wa tukio na kauli nyingine aliyoitoa kule Same - Kilimanjaro. Hii ya Same ilimshambulia Mwenyekiti wake Freeman Mbowe moja kwa moja bila kificho....

Kauli ya Tundu Lissu kule Same - Kilimanjaro aliitoa baada ya kusambaa kwa tuhuma kuwa, ule mkutano uliokuwa uhututubiwe na yeye huko Same, eti ulizuiliwa na Mwenyekiti wake Freeman Mbowe kwa kushirikiana na CCM kwa kutumia Polisi...

Ieleweke kuwa hoja hapa si kuzuiliwa kwa mkutano huo iwe ni kwa sababu hiy kweli au nyingine....

Tatizo ni namna Tundu Lissu alivyoshughulikia tuhuma hizo zilizomuhusisha Mwenyekiti wake...

Kauli yake kule Same Kilimanjaro ilikuwa hii, nanukuu;

"........Kama ni kweli, basi nyie ndiyo wenye chama, ndio wanachama wa chama hiki. mnapaswa kujiuliza Je, kila anayevaa makombati haya ni mwenzetu kwa kiasi gani kama anaweza kushirikiana na wabaya wetu kutuhujumu. Ila kama tuhuma hizi sio za kweli, basi mtanisamehe.."

Hii statement ni tata sana. Ni kama vile Makamu Mwenyekiti alishajiridhisha kuwa ni kweli Mwenyekiti wake ametenda hivyo na akaisema indirectly ili kupeleka ujumbe mahususi kwake...

Kwa kawaida, mimi nilifikiri kuwa, kabla ya kusema lolote, basi Makamu Mwenyekiti alipaswa kutumia hekima kidogo ya kuwasiliana na Mwenyekiti wake na kupata kauli yake juu ya tuhuma hizo zilizoelekezwa kwake. Na majibu ya Mwenyekiti ndiyo yalipaswa kuwa mwongozo wake kujibu hoja hiyo hadharani mbele ya umma...

Lakini kwa kauli yake hii, moja kwa moja inaonesha kuwa hakuwa amewasiliana na Mwenyekiti wake.

Na kama ni hivyo, napata shaka kuelewa kama hata Mwenyekiti na ofisi kuu ya chama (katibu mkuu na mtendaji mkuu wa chama) kama walikuwa wanajua kuwa Makamu Mwenyekiti wao atakuwa ziarani Same - Kilimanjaro siku hizo.

USHAURI:

CHADEMA kaeni chini, malizeni tofauti zenu amicably. Na kama kuna mambo yanayokwanza wengine, basi yashughulikiwe haraka ndani ya chama kwa taratibu za wazi za kichama....

Kuonesha tofauti zenu waziwazi huku nje ni hatari sana na wapinzani wenu wakuu CCM watatumia mwanya na udhaifu huu kuwamaliza kabisa na kusambaratika Moja kwa moja...

Hiki (Anguko la CHADEMA) ndicho CCM wanachokisubiri kukiona kikitokea Ili waweze kupumua....

Na hili la kuisambaratisha CHADEMA likitokea mikononi mwenu wewe Freeman Mbowe, Tundu Lissu, John Mnyika na Kamati kuu kwa ujumla fahamuni leo kuwa, mtalipa gharama kubwa sana Ili Watanganyika wawasamehe...!!!

CC: Erythrocyte
Mmawia aione hii
 
Tatizo la Chadema ni Mbowe,

Shida yenu tukianza kumsema humu kinazuka kile kikundi chake cha kikabila kumtetea...

Mbowe ni pro maslahi sana, hua namshauri Lissu atengeneze Chama kipya...

Najua kitachukua mda mrefu, lakini by 2030 kitakua tishio na tunaweza kuchukua nchi...

Kuendelea kuing'ang'ania Chadema, kuna siku watamshinda nguvu na kumzushia propaganda itakayochukua mda kuisafisha.
Waendelee kukaza kiwakute cha boss wake na Marim seif
 
Back
Top Bottom