KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,187
- 17,167
Tundu Lissu anavyoshambulia utadhani ni jeshi lenye askari wengi kiasi cha kuunda batalioni nzima. Ndiyo, inaeleweka chama chake kimempa nyenzo za watu na rasilimali chini ya kampeni yake; lakini ukitizama upande wa jeshi analopambana nalo ni dhahiri kwamba jemedari huyu anaongoza vyema kundi lake katika vita hii.
Jukwaa la Tundu Lissu, anasimama mwenyewe, hategemei Mwenyekiti wa Chama au Katibu Mkuu awashe msisimko ndani ya mioyo ya wananchi wanaokusanyika kwenye mikutano yake.
Hakuna mabango barabarani, wala wapambe kila sehemu wakipigana waziwazi upande wake kama ilivyo kwa jeshi zoefu la CCM.
Jemedari huyu sasa ndio anasuka jeshi la wananchi chini yake, jeshi ambalo hakuna IGP au amiri jeshi mkuu anaweza kulikabili na akabaki salama.
Wakati televisheni zote na vyombo vingine vya habari vinalazimika kulinda maslahi yao binafsi kwa kutoonyesha mikutano yake, mwanajeshi huyu anavyokusanya watu kwenye mikutano yake ni alama kwamba vyombo hivyo havina nguvu tena za kupasha habari. Kuna njia bora zaidi wanazotumia wananchi kupashana habari kwenye kampeni hizi.
Sasa ni dhahiri kwamba, hata zile njia za wizi wa kura walizotegemea CCM ziwabebe hawana uhakika nazo tena kama zitafanya kazi kama walivyozoea kuzitumia.
Jambo kubwa linalojitokeza katika vita hili ni hili: miaka mitano ilitumika sana kutugawa waTanzania katika makundi mbalimbali kiasi cha kuhatarisha umoja wetu.
Jeshi la wananchi analojenga Tundu Lissu linadhihirisha kwamba juhudi hizi za kutugawa katika mafungu ya kikabila, kidini, n.k., zimeshindwa vibaya sana. Jeshi la Tundu Lissu sio la wasukuma, wala wachaga au waislam au wakristo. Ni jeshi la waTanzania. Full Stop.
Tuendelee kutafuta HAKI, AMANI YA KWELI na UHURU wa Kweli.
Watanzania hawawezi kuwa mali ya mtu binafsi.
Jukwaa la Tundu Lissu, anasimama mwenyewe, hategemei Mwenyekiti wa Chama au Katibu Mkuu awashe msisimko ndani ya mioyo ya wananchi wanaokusanyika kwenye mikutano yake.
Hakuna mabango barabarani, wala wapambe kila sehemu wakipigana waziwazi upande wake kama ilivyo kwa jeshi zoefu la CCM.
Jemedari huyu sasa ndio anasuka jeshi la wananchi chini yake, jeshi ambalo hakuna IGP au amiri jeshi mkuu anaweza kulikabili na akabaki salama.
Wakati televisheni zote na vyombo vingine vya habari vinalazimika kulinda maslahi yao binafsi kwa kutoonyesha mikutano yake, mwanajeshi huyu anavyokusanya watu kwenye mikutano yake ni alama kwamba vyombo hivyo havina nguvu tena za kupasha habari. Kuna njia bora zaidi wanazotumia wananchi kupashana habari kwenye kampeni hizi.
Sasa ni dhahiri kwamba, hata zile njia za wizi wa kura walizotegemea CCM ziwabebe hawana uhakika nazo tena kama zitafanya kazi kama walivyozoea kuzitumia.
Jambo kubwa linalojitokeza katika vita hili ni hili: miaka mitano ilitumika sana kutugawa waTanzania katika makundi mbalimbali kiasi cha kuhatarisha umoja wetu.
Jeshi la wananchi analojenga Tundu Lissu linadhihirisha kwamba juhudi hizi za kutugawa katika mafungu ya kikabila, kidini, n.k., zimeshindwa vibaya sana. Jeshi la Tundu Lissu sio la wasukuma, wala wachaga au waislam au wakristo. Ni jeshi la waTanzania. Full Stop.
Tuendelee kutafuta HAKI, AMANI YA KWELI na UHURU wa Kweli.
Watanzania hawawezi kuwa mali ya mtu binafsi.