Pre GE2025 Tundu Lissu: Pesa za jana zilitoka wapi?, alizodakwa nazo mjumbe Uchaguzi wa BAVICHA

Pre GE2025 Tundu Lissu: Pesa za jana zilitoka wapi?, alizodakwa nazo mjumbe Uchaguzi wa BAVICHA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Yericko Nyerere ametoa tuhuma kuwa Dola na CCM wanaingilia uchaguzi na wanamtaka Lissu kwa nguvu.

Wamejificha weeee hatimaye wamejitokeza hadharani!

Halafu mwanachama halisi anainuka anasema Lissu anafaa kuwa mwenyekiti bila kujua nyuma yake kuna agenda gani? Wajumbe wa Mkutano Mkuu msifanye makosa yatakayokigharimu Chama chetu!

Dola na CCM yake wanaingilia uchaguzi wanamtaka Lissu kwa nguvu kubwa wametoa pesa na wanafanya kampeni za Wazi kabisa, Malengo yao ni kuwa Lissu ni mropokaji tu asiyeweza kuongoza taasisi ya Kisiasa inayohitaji hekima, busara na USIRI mkubwa, Kwamba Lissu hana uwezo wa kutafuta pesa ya kuendeshea chama, Kwamba Lissu akiwa Mwenyekiti hakuna Taasisi wala Watu wa Heshima nchini na nje ya Nchi watakaoshirikiana na Chadema kwakuwa Mwenyekiti wake Lissu HANA SIRI, ni Mropokaji kwa chochote watakachoshirikiana nae! Na hivyo Chama kitamfia ndani ya miezi michache tu baada ya kuchaguliwa na CCM itabaki salama dhidi ya Chadema ya Lissu.

CCM inaamini akina Lema ni wahuni tu wasioweza hata kujitafutia pesa ya kulisha familia zao badala yake wao na Familia zao wanalishwa na Serikali za Canada na Ubelgiji kama wakimbizi wa Kisiasa. Kwavyovyote vile, hawawezi kuongoza chama cha siasa Tanzania ambacho kukiongoza unatakiwa kuwa na Maarifa, misuli ya uchumi, busara na hekima.

Wajumbe epukeni mihemko, Lindeni Chama chenu, Mchagueni Mh Freeman Mbowe aendelee kuwa Mwenyekiti. Freeman Mbowe ana hekima, ana busara, msikivu, ana uthubutu na anaeleweka kwa kila mtu!
Inahitaji akili ya maiti kumuamini kibwengo kama huyu
 

Attachments

  • GfMNLpyXYAA8ucg.jpeg
    GfMNLpyXYAA8ucg.jpeg
    58.9 KB · Views: 3
Hili jamaa linasura ya porini hata mawazo yake yapo kipori pori 😄😄😄
 
Huyu jamaa nilikuwaga namheshimu ila kumbe ni empty set🚮🚮
 
Makamu Mwenyekiti CHADEMA, Tundu Lissu akizungumza kwenye Kikao amehoji;

"Wananisema kuwa sina Pesa, siwezi kuendesha Chama, hebu watueleze pesa za Jana usiku zilitoka kwa nani? Tumeshuhudia vitendo vya rushwa kwenye Uchaguzi wa BAVICHA"
View attachment 3201902
Soma, Pia:

Kimeumana! mjumbe adakwa akidaiwa kugawa nauli uchaguzi Bavicha

BAVICHA watoa ufafanuzi mazingira ya rushwa kwenye uchaguzi wao

Uzi maalumu wa matokeo Uchaguzi wa Baraza la Vijana (BAVICHA) na Baraza la Wazee (BAZECHA) CHADEMA Taifa 2025
 
Aka kajamaaa Kwa hakika ni kajinga.


Mara Pesa,.mara Mlopaki, mara chama kinataka Hekima na Busara .


Kati ya LISSU na Mbowe nani anaweza kuleta mamilioni ya Dola ya wafadhili ?.

Hivi humu JF Huwa kamo pia??
 
Back
Top Bottom