Tundu Lissu: Tutazipima kauli za Kikwete kwenye Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala!

Tundu Lissu: Tutazipima kauli za Kikwete kwenye Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala!

Tundu ni kamanda wa ukweli huwa anani inspire sana anaitendea haki masters degree yake ya law
hakuna kulala mpaka kieleweke
 
Hata Jaji mkuu wa Kenya amemtaja Mh Tundu Lissu kama mmoja wa Wanasheria vijana wanaoijua sheria Afrika mashariki. Nitaweka link soon. Big up Mh Tundu Antipass Mugwai Lissu, Jk hana ubavu wa ku argue na wewe.
 
Hata mzazi wako anaweza kuwa mzandiki lazima Useme ukweli! Mzandiki ni mzandiki tu! Lissu ni mzandiki aseme wajumbe wa kutoka TEC au CCT wapo au hawapo kwenye tume ya Jaji Warioba

wapo wasioteuliwa na TEC naCCT majina hayo Jk kayatoa anakojua mwenyewe yale matatu aliyopewa hakuteua.
 
mimi tangu mwanzo niliona hawa ma ccm , kuna mtu alitakiwa kudanganywa lakini hadanganyiki(tundu lisu)
 
Wakuu kamanda Lissu anafanya press, sasa hivi Makao Makuu ya Chadema na haya ndiyo amezungumza;

- Wadau wa Zanzibar hawajashirikishwa hata kidogo na hawakuwepo kwenye ratiba ya Kamati.
- Kamati ilipanga kwenda Zanzibar kutembea na sio kuonana na wadau, kwa sabab walitakiwa pkutembelea miradi ya TASAF, OFISI YA MAKAMU WA RAIS NA OFISI YA BUNGE.
- Wakakataa na kuomba kwa katibu wa Bunge kuwaona wadau wa Zanziba, Katibu wa Bunge alikubali.
- Walitengeneza orodha ya wadau.
- Yalianza maneno pembeni kuwa hakuna usalama Zanzibar wakati huohuo Kamati ya Ulinzi na Usalama ilikuwa Zanzibar.
- Wakazuiliwa kwenda na hivyo hakuna mdau wa Zanzibar aliyehusishwa.
- Kama haya ni makosa uzandiki na unafiki unatoka wapi wakati hoja ya kwenda Zanzibar yeye aliyeitoa?

Nitaendelea kuwapa update

- Kama hakuna ulazima kwa mujibu wa kanuni kwenda Zanzibar ofisi ndogo za Bunge Zanzibar zina maana gani, kwa hili rais amepotoka na hajui analolifanya.
- Hawajawahi kukutana na mjumbe wa Baraza la wawakilishi Zanzibar, na hata M/sheria amekiri.
UTEUZI KWENYE TUME YA KATIBA
- Hoja ni mamlaka ya Rais kuteua wajumbe 166
- Walipinga 2011 Ikaondolewa na wakairudisha tena kwenye muswada huu
- Uteuzi wa wajumbe wa Tume usilinganishwe na uteuzi wa wajumbe wa Bunge la Katiba. Ushahidi wa TEC , CCT na Shirikisho la walemavu kutoteuliwa pamoja na kupeleka majina kwa Rais ulitolewa kwenye Kamati ya Bunge, uongo wake unatoka wapi?
- Shirikisho la walemavu halikumpendekeza Al Shaimar Kwegir na hivyo Rais aliteua watu alkyewaona yeye wanafaa. Uongo unatoka wapi?

Maneno ya Rais,
- Hatamuita mzindiki, mnafiki wala mwongo ila ametoa hitimisho kwa maneno ya sikia sema (hearsay) kwa sababu ametumia maneno "nimeambiwa, nimesikia na nimejulishwa" mara tisa kwenye hotuba yake.

Kuhusu kuwa na mazungumzo ya pamoja;
- Kama ana nia njema basi asiusaini muswada na Katiba inamruhusu kufanya hivyo.
- Akiusaini ataendekeza mambo ya kiccm na hana haja ya kuaminiwa tena.
- Kamati ya Sheria na Utawala ya Bunge inakutana kuanzia kesho na hivyo anasubiri sheria husika iliyopitishwa kinyemela kurudishwa Bungeni.

Mwisho. Anakaribisha maswali;

- Ukiwa na mchakato mbovu yatatokea mambo kama ya Zimbabwa miaka 16 ndiyo ikapata Katiba na Kenya miaka 11 ndipo wakapata Katiba, kwa sababu mwanzoni hakukuwa na mchakato shirikishi.
- Wanachokifanya CCM sasa ndicho walichokifanya KANU kule Kenya
- Wananchi hawatanyamaza kamwe katika mchakato huu.

Tangu nimeanza kusikia hoja za Serikali sijapata kusikia Serikali mekili udhaifu wake hata pale ambapo kuna shida. Nani anieleze au aseme wazi lini serikali iliwahi kukiri mapungufu yake pale ilipokwenda kinyume hata cha sheria? Imetokea mauaji na mateso watu wamepanda vyeo baada hata ya wanaharakati kupiga kelele juu ya hayo mauaji.

Hata pale walipoona kuna mateso na ukatili wa aina mbalimbali hapa nchini jeshi limeendeleza aina fulani za senema tu bila kuwapata wahusika na kuwafikisha mahala panapohusika.

Wakati fulani kulitokea mauaji ya mbwa wa serikali/polisi wahusika walitafutwa hadi kupatikana na kushughulikiwa kikamilifu. Inakuwaje leo hili la katiba litendewe haki kama linavyohitajika kuwa? NITASHANGAA SANA KAMA ITAKUWA HIVYO....

HII NDO BONGO BWANA, THE WRONGS ARE ALWAYS RIGHT.... LABDA IPO SIKU MUNGU ATATUSIKIA....
 
Amemfundisha spika sheria,amemfundisha mwanasheria wa serikali sheria, amemfundisha waziri mkuu sheria, amewafundisha kina ndugai, wasira, lukuvi, nk. "na sasa anamfundisha rais wetu sheria. Jamani si aongezewe mshahara

naomba makamanda wamwongezee ulinzi maana magamba watamtaftia watu wa kumlimboka. Maana Akina ighondu ni balaa
 
haya ya kikwete na lisu,yana maslahi kwa taifa hili?kj kutumia hotuba kumshambulia raia mmoja kwa hoja alizozitoa tena ndani ya bunge hiyo ni busara?ni vema angewaachia akina lusinde,nkamia na komba waendelee kumsemea yale aliyoyataka kusema kwa lisu ila hayapaswi kutokea kwenye mdomo wa rais wa nchi
 
Mkuu Mbelwa umenena,japo CCM hawawezi kukiri hadharani lakini wakiwa vyumbani mwao wanajisemea kimoyo moyo.......Lissu ni mwalimu wao.
 
Back
Top Bottom